< Luka 23 >
1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
And the whole multitude of them, rising up, led him to Pilate.
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
And they began to accuse him, saying, We have found this [man] perverting our nation, and forbidding to give tribute to Caesar, saying that he himself is Christ, a king.
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
And Pilate demanded of him saying, Art thou the king of the Jews? And he answering him said, Thou sayest.
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
And Pilate said to the chief priests and the crowds, I find no guilt in this man.
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they insisted, saying, He stirs up the people, teaching throughout all Judaea, beginning from Galilee even on to here.
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
But Pilate, having heard Galilee [named], demanded if the man were a Galilaean;
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
and having learned that he was of Herod's jurisdiction, remitted him to Herod, who himself also was at Jerusalem in those days.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
And when Herod saw Jesus he greatly rejoiced, for he had been a long while desirous of seeing him, because of hearing many things concerning him, and he hoped to see some sign done by him;
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
and he questioned him in many words, but he answered him nothing.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
And the chief priests and the scribes stood and accused him violently.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
And Herod with his troops having set him at nought and mocked him, having put a splendid robe upon him, sent him back to Pilate.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
And Pilate and Herod became friends with one another the same day, for they had been at enmity before between themselves.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
And Pilate, having called together the chief priests and the rulers and the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
said to them, Ye have brought to me this man as turning away the people [to rebellion], and behold, I, having examined him before you, have found nothing criminal in this man as to the things of which ye accuse him;
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
nor Herod either, for I remitted you to him, and behold, nothing worthy of death is done by him.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
Having chastised him therefore, I will release him.
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
(Now he was obliged to release one for them at the feast.)
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
But they cried out in a mass saying, Away with this [man] and release Barabbas to us;
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
who was one who, for a certain tumult which had taken place in the city, and [for] murder, had been cast into prison.
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Pilate therefore, desirous to release Jesus, again addressed [them].
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
But they cried out in reply saying, Crucify, crucify him.
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
And he said the third time to them, What evil then has this [man] done? I have found no cause of death in him: I will chastise him therefore and release him.
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they were urgent with loud voices, begging that he might be crucified. And their voices [and those of the chief priests] prevailed.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
And Pilate adjudged that what they begged should take place.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
And he released him who, for tumult and murder, had been cast into prison, whom they begged for, and Jesus he delivered up to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
And as they led him away, they laid hold on a certain Simon, a Cyrenian, coming from the field, and put the cross upon him to bear it behind Jesus.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
And a great multitude of the people, and of women who wailed and lamented him, followed him.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
And Jesus turning round to them said, Daughters of Jerusalem, do not weep over me, but weep over yourselves and over your children;
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
for behold, days are coming in which they will say, Blessed [are] the barren, and wombs that have not borne, and breasts that have not given suck.
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Then shall they begin to say to the mountains, Fall upon us; and to the hills, Cover us:
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
for if these things are done in the green tree, what shall take place in the dry?
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
Now two others also, malefactors, were led with him to be put to death.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
And when they came to the place which is called Skull, there they crucified him, and the malefactors, one on the right hand, the other on the left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
And Jesus said, Father, forgive them, for they know not what they do. And, parting out his garments, they cast lots.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
And the people stood beholding, and the rulers also [with them] sneered, saying, He has saved others; let him save himself if this is the Christ, the chosen one of God.
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
And the soldiers also made game of him, coming up offering him vinegar,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
and saying, If thou be the king of the Jews, save thyself.
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
And there was also an inscription [written] over him in Greek, and Roman, and Hebrew letters: This is the King of the Jews.
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
Now one of the malefactors who had been hanged spoke insultingly to him, saying, Art not thou the Christ? save thyself and us.
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
But the other answering rebuked him, saying, Dost thou too not fear God, thou that art under the same judgment?
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
and we indeed justly, for we receive the just recompense of what we have done; but this [man] has done nothing amiss.
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
And he said to Jesus, Remember me, [Lord, ] when thou comest in thy kingdom.
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
And Jesus said to him, Verily I say to thee, To-day shalt thou be with me in paradise.
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
And it was about [the] sixth hour, and there came darkness over the whole land until [the] ninth hour.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
And the sun was darkened, and the veil of the temple rent in the midst.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
And Jesus, having cried with a loud voice, said, Father, into thy hands I commit my spirit. And having said this, he expired.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
Now the centurion, seeing what took place, glorified God, saying, In very deed this man was just.
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
And all the crowds who had come together to that sight, having seen the things that took place, returned, beating [their] breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
And all those who knew him stood afar off, the women also who had followed him from Galilee, beholding these things.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
And behold, a man named Joseph, who was a councillor, a good man and a just
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
(this [man] had not assented to their counsel and deed), of Arimathaea, a city of the Jews, who also waited, [himself also, ] for the kingdom of God
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
— he having gone to Pilate begged the body of Jesus;
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
and having taken it down, wrapped it in fine linen and placed him in a tomb hewn in the rock, where no one had ever been laid.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
And it was preparation day, and [the] sabbath twilight was coming on.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
And women, who had come along with him out of Galilee, having followed, saw the sepulchre and how his body was placed.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
And having returned they prepared aromatic spices and ointments, and remained quiet on the sabbath, according to the commandment.