< Luka 23 >
1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
And the entire multitude of them, rising up, led him to Pilate.
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
Then they began to accuse him, saying, “We found this one subverting our nation, and prohibiting giving tribute to Caesar, and saying that he is Christ the king.”
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
And Pilate questioned him, saying: “You are the king of the Jews?” But in response, he said: “You are saying it.”
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
Then Pilate said to the leaders of the priests and to the crowds, “I find no case against this man.”
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they continued more intensely, saying: “He has stirred up the people, teaching throughout all of Judea, beginning from Galilee, even to this place.”
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
But Pilate, upon hearing Galilee, asked if the man were of Galilee.
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
And when he realized that he was under Herod’s jurisdiction, he sent him away to Herod, who was himself also at Jerusalem in those days.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
Then Herod, upon seeing Jesus, was very glad. For he had been wanting to see him for a long time, because he had heard so many things about him, and he was hoping to see some kind of sign wrought by him.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
Then he questioned him with many words. But he gave him no response at all.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
And the leaders of the priests, and the scribes, stood firm in persistently accusing him.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
Then Herod, with his soldiers, scorned him. And he ridiculed him, clothing him in a white garment. And he sent him back to Pilate.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
And Herod and Pilate became friends on that day. For previously they were enemies to one another.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
And Pilate, calling together the leaders of the priests, and the magistrates, and the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
said to them: “You have brought before me this man, as one who disturbs the people. And behold, having questioned him before you, I find no case against this man, in those things about which you accuse him.
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
And neither did Herod. For I sent you all to him, and behold, nothing deserving of death was recorded about him.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
Therefore, I will chastise him and release him.”
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
Now he was required to release one person for them on the feast day.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
But the entire crowd exclaimed together, saying: “Take this one, and release to us Barabbas!”
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
Now he had been cast into prison because of a certain sedition that occurred in the city and for murder.
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Then Pilate spoke to them again, wanting to release Jesus.
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
But they shouted in response, saying: “Crucify him! Crucify him!”
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
Then he said to them a third time: “Why? What evil has he done? I find no case against him for death. Therefore, I will chastise him and release him.”
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they persisted, with loud voices, in demanding that he be crucified. And their voices increased in intensity.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
And so Pilate issued a judgment granting their petition.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
Then he released for them the one who had been cast into prison for murder and sedition, whom they were requesting. Yet truly, Jesus he handed over to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
And as they were leading him away, they apprehended a certain one, Simon of Cyrene, as he was returning from the countryside. And they imposed the cross on him to carry after Jesus.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
Then a great crowd of people followed him, with women who were mourning and lamenting him.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
But Jesus, turning to them, said: “Daughters of Jerusalem, do not weep over me. Instead, weep over yourselves and over your children.
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
For behold, the days will arrive in which they will say, ‘Blessed are the barren, and the wombs that have not borne, and the breasts that have not nursed.’
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Then they will begin to say to the mountains, ‘Fall over us,’ and to the hills, ‘Cover us.’
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
For if they do these things with green wood, what will be done with the dry?”
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
Now they also led out two other criminals with him, in order to execute them.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
And when they arrived at the place that is called Calvary, they crucified him there, with the robbers, one to the right and the other to the left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
Then Jesus said, “Father, forgive them. For they know not what they do.” And truly, dividing his garments, they cast lots.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
And people were standing near, watching. And the leaders among them derided him, saying: “He saved others. Let him save himself, if this one is the Christ, the elect of God.”
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
And the soldiers also ridiculed him, approaching him and offering him vinegar,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
and saying, “If you are the king of the Jews, save yourself.”
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
Now there was also an inscription written over him in letters of Greek, and Latin, and Hebrew: This is the king of the Jews.
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
And one of those robbers who were hanging blasphemed him, saying, “If you are the Christ, save yourself and us.”
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
But the other responded by rebuking him, saying: “Do you have no fear of God, since you are under the same condemnation?
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
And indeed, it is just for us. For we are receiving what our deeds deserve. But truly, this one has done nothing wrong.”
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
And he said to Jesus, “Lord, remember me when you come into your kingdom.”
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
And Jesus said to him, “Amen I say to you, this day you shall be with me in Paradise.”
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
Now it was nearly the sixth hour, and a darkness occurred over the entire earth, until the ninth hour.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
And the sun was obscured. And the veil of the temple was torn down the middle.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
And Jesus, crying out with a loud voice, said: “Father, into your hands I commend my spirit.” And upon saying this, he expired.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
Now, the centurion, seeing what had happened, glorified God, saying, “Truly, this man was the Just One.”
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
And the entire crowd of those who came together to see this spectacle also saw what had happened, and they returned, striking their breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
Now all those who knew him, and the women who had followed him from Galilee, were standing at a distance, watching these things.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
And behold, there was a man named Joseph, who was a councilman, a good and just man,
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
(for he had not consented to their decision or their actions). He was from Arimathea, a city of Judea. And he was himself also anticipating the kingdom of God.
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
This man approached Pilate and petitioned for the body of Jesus.
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
And taking him down, he wrapped him in a fine linen cloth, and he placed him in a tomb hewn from rock, in which no one had ever been placed.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
And it was the day of Preparation, and the Sabbath was drawing near.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
Now the women who had come with him from Galilee, by following, saw the tomb and the manner in which his body was placed.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
And upon returning, they prepared aromatic spices and ointments. But on the Sabbath, indeed, they rested, according to the commandment.