< Luka 23 >

1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
Then the whole council rose and led Jesus away to Pilate.
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
And they began to accuse Him, saying, “We found this man subverting our nation, forbidding payment of taxes to Caesar, and proclaiming Himself to be Christ, a King.”
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
So Pilate asked Him, “Are You the King of the Jews?” “You have said so,” Jesus replied.
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
Then Pilate said to the chief priests and the crowds, “I find no basis for a charge against this man.”
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they kept insisting, “He stirs up the people all over Judea with His teaching. He began in Galilee and has come all the way here.”
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
When Pilate heard this, he asked if the man was a Galilean.
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
And learning that Jesus was under Herod’s jurisdiction, he sent Him to Herod, who himself was in Jerusalem at that time.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
When Herod saw Jesus, he was greatly pleased. He had wanted to see Him for a long time, because he had heard about Him and was hoping to see Him perform a miracle.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
Herod questioned Jesus at great length, but He gave no answer.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
Meanwhile, the chief priests and scribes stood there, vehemently accusing Him.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
And even Herod and his soldiers ridiculed and mocked Him. Dressing Him in a fine robe, they sent Him back to Pilate.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
That day Herod and Pilate became friends; before this time they had been enemies.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
Then Pilate called together the chief priests, the rulers, and the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
and said to them, “You brought me this man as one who was inciting the people to rebellion. I have examined Him here in your presence and found Him not guilty of your charges against Him.
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
Neither has Herod, for he sent Him back to us. As you can see, He has done nothing deserving of death.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
Therefore I will punish Him and release Him.”
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
But they all cried out in unison: “Away with this man! Release Barabbas to us!”
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
(Barabbas had been imprisoned for an insurrection in the city, and for murder.)
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Wanting to release Jesus, Pilate addressed them again,
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
but they kept shouting, “Crucify Him! Crucify Him!”
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
A third time he said to them, “What evil has this man done? I have found in Him no offense worthy of death. So after I punish Him, I will release Him.”
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they were insistent, demanding with loud voices for Jesus to be crucified. And their clamor prevailed.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
So Pilate sentenced that their demand be met.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
As they had requested, he released the one imprisoned for insurrection and murder, and handed Jesus over to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
As the soldiers led Him away, they seized Simon of Cyrene on his way in from the country, and put the cross on him to carry behind Jesus.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
A great number of people followed Him, including women who kept mourning and wailing for Him.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
But Jesus turned to them and said, “Daughters of Jerusalem, do not weep for Me, but weep for yourselves and for your children.
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
Look, the days are coming when people will say, ‘Blessed are the barren women, the wombs that never bore, and breasts that never nursed!’
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
At that time ‘they will say to the mountains, “Fall on us!” and to the hills, “Cover us!”’
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
For if men do these things while the tree is green, what will happen when it is dry?”
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
Two others, who were criminals, were also led away to be executed with Jesus.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
When they came to the place called The Skull, they crucified Him there, along with the criminals, one on His right and the other on His left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
Then Jesus said, “Father, forgive them, for they do not know what they are doing.” And they divided up His garments by casting lots.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
The people stood watching, and the rulers sneered at Him, saying, “He saved others; let Him save Himself if He is the Christ of God, the Chosen One.”
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
The soldiers also mocked Him and came up to offer Him sour wine.
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
“If You are the King of the Jews,” they said, “save Yourself!”
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
Above Him was posted an inscription: THIS IS THE KING OF THE JEWS.
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
One of the criminals who hung there heaped abuse on Him. “Are You not the Christ?” he said. “Save Yourself and us!”
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
But the other one rebuked him, saying, “Do you not even fear God, since you are under the same judgment?
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
We are punished justly, for we are receiving what our actions deserve. But this man has done nothing wrong.”
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
Then he said, “Jesus, remember me when You come into Your kingdom!”
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
And Jesus said to him, “Truly I tell you, today you will be with Me in Paradise.”
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
It was now about the sixth hour, and darkness came over all the land until the ninth hour.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
The sun was darkened, and the veil of the temple was torn down the middle.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
Then Jesus called out in a loud voice, “Father, into Your hands I commit My Spirit.” And when He had said this, He breathed His last.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
When the centurion saw what had happened, he gave glory to God, saying, “Surely this was a righteous man.”
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
And when all the people who had gathered for this spectacle saw what had happened, they returned home beating their breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
But all those who knew Jesus, including the women who had followed Him from Galilee, stood at a distance watching these things.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
Now there was a Council member named Joseph, a good and righteous man,
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
who had not consented to their decision or action. He was from the Judean town of Arimathea, and was waiting for the kingdom of God.
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
He went to Pilate to ask for the body of Jesus.
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
Then he took it down, wrapped it in a linen cloth, and placed it in a tomb cut into the rock, where no one had yet been laid.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
It was Preparation Day, and the Sabbath was beginning.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
The women who had come with Jesus from Galilee followed, and they saw the tomb and how His body was placed.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
Then they returned to prepare spices and perfumes. And they rested on the Sabbath, according to the commandment.

< Luka 23 >