< Luka 23 >
1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
And having risen, the whole company of them led him to Pilate.
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
And they began to accuse him, saying, We found this man perverting the nation, and forbidding to give tribute to Caesar, saying himself to be Christ, a king.
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
And Pilate questioned him, saying, Are thou the king of the Jews? And having answered him, he said, Thou say.
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
And Pilate said to the chief priests and the multitudes, I find nothing guilty in this man.
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they were emphatic, saying, He stirs up the people, teaching throughout all Judea, having begun from Galilee as far as here.
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
And when Pilate heard Galilee, he questioned if the man is a Galilean.
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
And when he perceived that he is from Herod's jurisdiction, he sent him to Herod, who was himself also in Jerusalem in these days.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
Now when Herod saw Jesus, he was exceedingly glad, for he was wanting of a considerable time to see him, because of hearing many things about him, and he hoped to see some sign happening by him.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
And he interrogated him in considerable words, but he answered him nothing.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
And the chief priests and the scholars had stood, vehemently accusing him.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
But Herod having disdained him with his soldiers, and having mocked him, having arraying him in a bright robe, he sent him back to Pilate.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
And both Pilate and Herod became friends with each other on the same day, for they were formerly being at enmity toward themselves.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
And Pilate having called together the chief priests, and the rulers, and the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
said to them, Ye brought this man to me as turning away the people. And behold, I, having examined him before you, found nothing guilty in this man of what ye accuse against him.
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
But not even Herod, for I sent you back to him, and lo, nothing having been done by him is worthy of death.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
Therefore, having scourged I will release him.
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
Now he had need to release one man to them at every feast.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
But they cried out all together, saying, Take away this man, and release to us Barabbas
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
(a man who was cast into prison because of a certain insurrection that occurred in the city, and for murder).
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Again therefore Pilate called out wanting to release Jesus,
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
but they shouted, saying, Crucify, crucify him.
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
And he said to them a third time, For what evil did this man do? I have found nothing guilty of death in him. I will therefore, having scourged, release him.
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they were relentless with loud voices demanding him to be crucified. And their voices and those of the chief priests prevailed.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
And Pilate decreed their request to happen.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
And he released the man who had been cast into prison because of insurrection and murder, whom they asked for, but he delivered Jesus to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
And when they led him away, having taken hold of a certain Simon, a Cyrenian coming from the countryside, they laid the cross on him to bring behind Jesus.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
And a great multitude of the people followed him, and also of women who bewailed and lamented him.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
But having turning to them, Jesus said, Daughters of Jerusalem, weep not for me, instead weep for yourselves and for your children.
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
Because, behold, the days are coming, during which they will say, Blessed are the barren, and the bellies that gave no birth, and the breasts that did not suckle.
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Then they will begin to say to the mountains, Fall on us, and to the hills, Cover us.
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
Because if they do these things in the green tree, what will happen in the dry?
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
And two other men, malefactors, were also led with him to be executed.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
And when they came to the place called Skull, there they crucified him, and the malefactors, one at the right hand and the other at the left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
And Jesus said, Father, forgive them, for they know not what they are doing. And dividing his garments, they cast a lot.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
And the people had stood watching. And also the rulers with them sneered, saying, He saved others. He should save himself, if this is the Christ, the chosen of God.
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
And the soldiers also mocked him, approaching, and bringing him vinegar,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
and saying, If thou are the king of the Jews, save thyself.
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
And there was also an inscription over him written in letters, in Greek and Latin and Hebrew: THIS IS THE KING OF THE JEWS.
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
And one of the malefactors who were hanged railed him, saying, If thou are the Christ, save thyself and us.
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
But the other man having answered, rebuking him, saying, Thou fear not even God, since thou are in the same condemnation?
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
And we indeed justly, for we receive worthy of what we did, but this man did nothing amiss.
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
And he said to Jesus, Remember me, Lord, when thou come into thy kingdom.
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
And Jesus said to him, Truly I say to thee, today thou will be with me in the paradise.
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
And it was about the sixth hour, and darkness occurred over the whole land until the ninth hour.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
And the sun was darkened, and the curtain of the temple was torn in the middle.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
And Jesus, having sounded out in a great voice, said, Father, into thy hands I entrust my spirit. And having said these things, he expired.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
And when the centurion saw that which happened, he glorified God, saying, Certainly this man was righteous.
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
And all the multitudes who came together to this scene, watching that which happened, turned back, beating their breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
And all his acquaintances, and the women who accompanied him from Galilee, had stood from afar, seeing these things.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
And behold a man named Joseph, a council member, being a good and righteous man
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
(this man not having consented to their purpose and deed), was from Arimathaea, a city of the Jews, who also himself awaited the kingdom of God.
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
This man having gone to Pilate, requested the body of Jesus.
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
And having taken it down, he wrapped it in linen, and laid it in a sepulcher cut in rock, of which no man was yet lain.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
And the day was Preparation; sabbath was beginning.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
And having followed closely, the women who were gathered to him out of Galilee, they saw the sepulcher, and how his body was laid.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
And having returned, they prepared spices and ointments. And they indeed rested on the sabbath according to the commandment.