< Luka 23 >

1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
,他們全體起來,把耶穌押送到比拉多面前,
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
開始控告祂說:「我們查得這個人煽惑我們的民族,阻止給凱撒納稅,且自稱為默西亞君王。」
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
比拉多遂問耶穌說:「你是猶太人的君王嗎﹖」耶穌回答說:「你說的是。」
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
比拉多對司祭長及群眾說:「我在這人身上查不出什麼罪狀來。」
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
他們越發堅持說:「他在猶太全境,從加利肋亞起,直到這裏施教,煽惑民眾。」
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
比拉多聽了,就問耶穌是不是加利肋亞人。
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
既知道他屬於黑落德統治,就把他轉送到黑落德那裏。這幾天,黑落德也在耶路撒冷。
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
黑落德見二耶穌,不勝欣喜,原來他早就願意看看耶穌,因為他曾聽說過關於耶穌的事,也指望他顯個奇蹟。
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
於是問了耶穌許多事,但耶穌什麼都不回答。
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
司祭長及經師站在那裡,極力控告祂。
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
黑落德及自己的待衛鄙視祂,戲笑祂,並給祂穿上華麗的長袍,把祂解回比拉多那裏。
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
黑落德與比拉多就在那一天彼此成了朋友,因為他們原先彼此有仇。
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
比拉多召集司祭長、官吏及人民來,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
對他們說:「你們給我送這個人來,好像是一個煽動民眾的人。看,我在你們面前審問了他,而你們告他的罪狀,我在這人身上並查不出一條來,
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
而且黑落德也沒有查出,因而又把他解回到我們這裏來,足見他沒有做過應死的事。
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
所以,我懲治他以後,便釋放他。」
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
每逢節日,他必須照例給他們釋放一個囚犯。
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
他們卻齊聲喊叫說:「除掉這個人,給我們釋放巴拉巴。」
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
巴拉巴卻是為了在城中作亂而下獄的。
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
比拉多又向他們聲明,願意釋放耶穌。
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
他們卻不斷地喊叫說:「釘在十字架上,釘在十字架上! 」
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
比拉多第三次對他們說:「這人到底作了什麼惡事﹖我在他身上查不出廳死的罪狀來。所以我懲治他以後,便釋放他。」
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
但是他們仍厲聲逼迫,要求釘祂在十字架上。他們的喊聲,越來越厲害。
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
比拉多遂宣判:照他們所請求的執行,
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
便釋放了他們所要求的那個因作亂殺人而下獄的犯人;至於耶穌,卻交出來,讓他們隨意處理。
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
他們把耶穌帶走的時候,抓住一個從田間來的基勒乃人西滿,把十字架放在他身上,叫他在耶穌後面背著。
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
有許多人民及婦女跟隨著耶穌,婦女搥胸痛哭祂。
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
耶穌轉身向她們說:「耶路撒冷女子! 們不要哭我,但應哭妳們自己及妳們的子女,
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
因為日子將到,那時,人要說:那荒胎的,那沒有生產過的胎,和沒有哺養過的乳,是有福的。
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
那時,人要開始對高山說:倒在我們身上吧! 對丘陵說:蓋起我們來吧!
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
如果對於青綠的樹木,他們還這做,對於枯槁的樹木,又將怎樣呢﹖
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
另有二倨兇犯,也被帶去,同尸一同受死。
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
他們既到了那名叫髑髏的地方,就在那裏把耶穌釘在十字架上;也釘了那兩個兇犯:一個在右邊,一個在左邊。
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
耶穌說:「父啊,寬赦他們吧! 因為他們不知道他們做的是什麼。」他們拈鬮分了祂的衣服。
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
民眾站著觀望。首領們嗤笑說:「別人,他救了;如果這人是天主的受傅者,被選者,就救他自己吧! 」
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
兵士也戲弄祂,前來把醋給祂遞上去,說:
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
「如果你是猶太人的君王,就救救你自己吧! 」
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
在祂上頭還有一塊用希臘文、拉丁及希伯來文字寫的罪狀牌:「這是猶太人的君王。」
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
懸掛中的凶犯中,有一個侮辱耶穌說:「你百是默西亞嗎﹖救救你自己和我們吧! 」
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
另一個凶犯應聲責斥他說:「你既然受同樣的刑罰,連天主你都不怕嗎﹖
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
這對我們是理所當然的,因為我們所受的,正配我們所行的;但是,這個人從未做過什麼不正當的事。」
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
髓後說:「耶穌,當你來為王時,請你記念我! 」
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
耶穌給他說:「我實在告訴你:今天你就要與我一同在樂園裏。」
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
這時,大約已是第六時辰,遍地都昏暗了,直到第九時辰。
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
太陽失去了光,聖所的帳幕從中日間裂開,
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
耶穌中大聲呼喊說:「父啊! 我把我的靈魂交托在你手中。」說完這話,便了氣。
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
百夫長看見所發生的事,遂光榮天主說:「這人實在是一個義人。」
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
所有同來看這景像的群眾,見了這些情形,都搥著胸膛,回去了。
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
所有與耶穌相識的人,和那些由加利肋亞隨侍祂的婦女們,遠遠地站著,觀看這些事。
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
有一個人名叫若瑟,是一個議員,又是一個善良公正的人。
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
他原是猶太阿黎瑪特雅城人,一向期待天主的國;他沒有贊同其他人的計謀和作為。
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
他去見比拉多,要求耶穌的遺體。
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
他把遺體卸下,用殮布裹好,安葬在由巖石鑿成,而尚未過人的墓穴裏。
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
那天是預備日,安息日快到了。
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
從加利肋亞同耶穌來的那些婦女,在後邊跟著,觀看那墓穴,並觀看耶穌的遺體,是怎麼安葬的。
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
她們回去,就預備下香料和香膏。安息日,她們依照誡命安息。

< Luka 23 >