< Luka 21 >
1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
Then Jesus looked up and saw the rich putting their gifts into the treasury.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
He also saw a poor widow there putting in two small copper coins.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
So he said, “Truly I say to you, this poor widow has put in more than all the others.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For they have all put in gifts for God out of their abundance, but she, out of her poverty, has put in all that she had to live on.”
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
Then, as some were talking about how the temple was adorned with beautiful stones and gifts consecrated to God, Jesus said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
“As for these things that you see, the days will come when not one stone will be left upon another; all of them will be torn down.”
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
So they asked him, “Teacher, when will these things happen? And what will be the sign that these things are about to take place?”
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
He said, “Make sure you are not led astray. For many will come in my name, saying, ‘I am he,’ and, ‘The time has drawn near.’ Do not go after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
When you hear of wars and uprisings, do not be terrified, for these things must first take place, but the end will not immediately follow.”
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them, “Nation will rise up against nation, and kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
There will be great earthquakes in various places, along with famines and plagues. There will also be terrifying sights and great signs from heaven.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these things take place, they will arrest you and persecute you. They will deliver you up to synagogues and prisons, and you will be brought before kings and governors for my name's sake.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
This will lead to opportunities for you to bear witness.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Therefore settle it in your hearts not to prepare your defense in advance.
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For I will give you a mouth to speak and wisdom that none of your adversaries will be able to refute or resist.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
You will even be betrayed by parents, relatives, friends, and brothers, and they will have some of you put to death.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
You will be hated by all because of my name.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Yet not a hair of your head will by any means perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
You must gain your lives by your patient endurance.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
“When you see Jerusalem surrounded by armies, know that its desolation is near.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then those who are in Judea must flee to the mountains, those who are in the city must get out, and those who are in the countryside must not enter the city.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
For those will be days of vengeance, to fulfill all that is written.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Woe to those who are with child and to those who are nursing infants in those days! For there will be great distress in the land and wrath against this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
They will fall by the edge of the sword and be led captive into all the nations, and Jerusalem will be trampled by the Gentiles until the times of the Gentiles are fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
“There will be signs in the sun, moon, and stars, and on the earth there will be distress among the nations as they are perplexed by the roaring sea and the surging waves.
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
People will faint from fear and foreboding of what is coming upon the world, for the powers of the heavens will be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
Then they will see the Son of Man coming in a cloud with power and great glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
So when these things begin to take place, stand tall and lift up your heads, for your redemption is near.”
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
Then he told them a parable: “Consider the fig tree and all the other trees.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
As soon as they sprout leaves, you can see for yourselves and know that summer is near.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
So also, when you see these things taking place, know that the kingdom of God is near.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Truly I say to you, this generation will certainly not pass away until all things have taken place.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Heaven and earth will pass away, but my words will certainly not pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
“Watch yourselves, lest your hearts be weighed down with carousing, drunkenness, and the cares of this life, and that day come upon you suddenly.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For it will come like a trap upon all who dwell on the face of the whole earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Therefore stay alert at all times, praying that you may be considered worthy to escape everything that will take place, and to stand before the Son of Man.”
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Each day Jesus taught in the temple courts, but at night he would go out and stay at the mount called Olivet.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people would come to him early in the morning to listen to him in the temple courts.