< Luka 20 >

1 Ikawa siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuhubiri injili, makuhani wakuu na walimu wa Sheria walimwendea pamoja na wazee.
And it came to pass, on one of those days, as he was teaching the people in the temple, and publishing the good tidings, that the priests and the scribes with the elders came upon him,
2 Walizungumza, wakimwambia, 'Tuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Au ni nani huyo ambaye amekupa mamlaka haya? “
and spoke to him, saying, Tell us, by what authority doest thou these things? Or who is he that gave thee this authority?
3 Naye akajibu, akawaambia, 'Nami pia nitawauliza swali. Niambieni
And he answering said to them, I also will ask you a question; and tell me:
4 ubatizo wa Yohana. Je, ulitoka mbinguni ama kwa watu? '
The baptism of John, was it from heaven, or from men?
5 Lakini wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, 'Tukisema, `litoka mbinguni, atatuuliza, ` Basi, mbona hamkumwamini?'
And they reasoned among themselves, saying, If we say, From heaven, he will say, Why did ye not believe him?
6 Na tukisema; ilitoka kwa wanadamu; watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii. '
But if we say, From men, all the people will stone us; for they are persuaded that John was a prophet.
7 Basi, wakamjibu ya kwamba hawakujua ilikotoka.
And they answered, that they did not know whence it was.
8 Yesu akawaambia, '“Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”
And Jesus said to them, Neither do I tell you by what authority I do these things.
9 Aliwaambia watu mfano huu, “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima wa mizabibu, na akaenda nchi nyingine kwa muda mrefu.
And he began to speak to the people this parable: A man planted a vineyard, and let it out to husbandmen, and went abroad for a long time.
10 Kwa muda uliopangwa, alimtuma mtumishi kwa wakulima mizabibu, kwamba wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakulima wa mzabibu wakampiga, wakamrudisha mikono- mitupu.
And at the season he sent a servant to the husbandmen, that they should give him of the fruit of the vineyard; but the husbandmen beat him, and sent him away empty-handed.
11 Kisha akamtuma tena mtumishi mwingine na nao wakampiga, kumtendea vibaya, na wakamrudisha mikono- mitupu.
And he sent still another servant; and they beat him also, and treated him shamefully, and sent him away empty-handed.
12 Alimtuma tena wa tatu na nao wakamjeruhi na kumtupa nje.
And he went on to send a third; and they wounded him also, and cast him out.
13 Hivyo bwana wa shamba akasema, 'Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa. Labda watamheshimu. '
And the lord of the vineyard said, What shall I do? I will send my beloved son; perhaps they will respect him.
14 Lakini wakulima wa mzabibu walipomwona, walijadili wao kwa wao wakisema, `Huyu ndiye mrithi. Tumuue, ili urithi wake uwe wetu. '
But when the husbandmen saw him, they reasoned among themselves, saying, This is the heir; let us kill him, that the inheritance may become ours.
15 Wakamtoa nje ya shamba la mizabibu na kumuua. Je bwana shamba atawafanya nini?
So they cast him out of the vineyard, and killed him. What then will the lord of the vineyard do to them?
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima wa mzabibu, na atawapa shamba hilo wengine”. 'Nao waliposikia hayo, wakasema, 'Mungu amekataa'
He will come and destroy these husbandmen, and will give the vineyard to others. And when they heard this, they said, God forbid!
17 Lakini Yesu akawatazama, akasema, “Je andiko hili lina maana gani? 'Jiwe walilolikataa wajenzi, limekuwa jiwe la pembeni'?
But he, looking upon them, said, What then is this which is written, “The stone which the builders rejected, the same hath become the corner-stone”?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo, atavunjika vipande vipande. Lakini yule ambaye litamwangukia, litamponda. '
Every one who falleth upon that stone will be broken; but on whomever it falleth, it will grind him to powder.
19 Hivyo waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta njia ya kumkamata wakati huohuo, walijua kwamba alikuwa amesema mfano huu dhidi yao. Lakini waliwaogopa watu.
And the scribes and the chief priests sought to lay hands on him in that hour, but they feared the people; for they knew that he spoke this parable against them.
20 Walimuangalia kwa makini, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wapate kupata kosa kwa hotuba yake, ili kumpelekakwa watawala na wenye mamlaka.
And they kept watch on him, and sent forth spies feigning themselves to be righteous men, that they might take hold of his words, in order to deliver him up to the civil power and to the authority of the governor.
21 Nao wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli na si kushawishiwa na mtu yeyote, lakini wewe hufundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu.
And they asked him, saying, Teacher, we know that thou sayest and teachest rightly, and hast no regard to the person of men, but teachest the way of God truly.
22 Je, ni halali kwetu kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it lawful for us to give tribute to Caesar, or not?
23 Lakini Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
But perceiving their craftiness, he said to them,
24 “Nionyesheni dinari. Sura na chapa ya nani ipo juu yake?” Walisema, '“Ya Kaisari.”
Show me a denary. Whose image and inscription hath it? And they answered and said, Caesar's.
25 Naye akawaambia, 'Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu.'
And he said to them, Render then to Caesar the things that are Caesar's, and to God the things that are God's.
26 Waandishi na wakuu wa makuhani hawakuwa na uwezo wa kukosoa kile alichosema mbele ya watu. Wakastaajabia majibu yake na hawakusema chochote.
And they could not take hold of his words before the people; and marveling at his answer, they held their peace.
27 Baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale ambao wanasema kwamba hakuna ufufuo,
Then some of the Sadducees, who deny that there is a resurrection, came to him, and asked him,
28 wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba kama mtu akifiwa na ndugu mwenye mke ambaye hana mtoto basi anapaswa kumchukuna mke wa ndugu yake na kuzaa nae kwa ajili ya kaka yake.
saying, Teacher, Moses wrote to us, “If a man's brother die, having a wife, and the same die without children, his brother shall take his wife, and raise up seed to his brother.”
29 Kulikuwa na ndugu saba Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto,
Now there were seven brothers; and the first took a wife and died childless.
30 na wa pili pia.
And the second
31 Wa tatu akamchukua vilevile, vivyo hivyo wa saba hakuacha watoto na akafa.
and the third took her; and in like manner also the seven left no children, and died.
32 Baadaye yule mwanamke pia akafa.
At last the woman also died.
33 Katika ufufuo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa. '
In the resurrection then, of which of them is the woman the wife? for the seven had her for a wife.
34 Yesu akawaambia, “Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
And Jesus said to them, The sons of this world marry, and are given in marriage; (aiōn g165)
35 Lakini wale wanastaohili kupokea ufufuo wa wafu na kuingia uzima wa milele hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
but they who have been accounted worthy to obtain that world, and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage; (aiōn g165)
36 Wala hawawezi kufa tena, kwa sababu huwa sawasawa na malaika na ni watoto wa Mungu, wana wa ufufuo.
for they cannot die any more; for they are like the angels, and are sons of God, being sons of the resurrection.
37 Lakini hiyo wafu wanafufuliwa, hata Musa alionyesha mahali katika habari za kichaka, pale alimwita Bwana kama Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
But that the dead are raised, even Moses hath shown at the Bush, when he calleth the Lord the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob.
38 Sasa, yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa sababu wote huishi kwake. “
Now he is not a God of the dead, but of the living; for all live to him.
39 Baadhi ya walimu wa Sheria wakamjibu, 'Mwalimu, umejibu vema. '
Then some of the scribes answering, said, Teacher, thou hast well said.
40 Hawakuthubutu kumwuliza maswali mengine zaidi.
For they dared no longer to ask him any question.
41 Yesu akawaambia, “Ki vipi watu wanasema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
And he said to them, How is it that men say that the Christ is David's son?
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti mkono wa kulia,
For David himself saith in the book of Psalms, “The Lord said to my lord, Sit thou on my right hand,
43 mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako. '
till I make thine enemies thy footstool.”
44 Daudi anamwita Kristo 'Bwana', basi atakuwaje mwana wa Daudi?”
David then calleth him lord; and how is he his son?
45 Watu wote walipokuwa wakimsikiliza akawaambia wanafunzi wake,
And in the hearing of all the people he said to his disciples,
46 'Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na wapenda salamu maalum sokoni na viti vya heshima katika masinagogi, na maeneo ya heshima karamuni.
Beware of the scribes, who like to walk about in long robes, and love salutations in the markets, and the chief seats in the synagogues, and the first places at feasts;
47 Wao pia hula nyumba za wajane, na wanajifanya wanasali sala ndefu. Hawa watapokea hukumu kubwa zaidi. '
who devour widows' houses, and for a pretence make long prayers. These will receive a far greater condemnation.

< Luka 20 >