< Luka 20 >
1 Ikawa siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuhubiri injili, makuhani wakuu na walimu wa Sheria walimwendea pamoja na wazee.
And it came to pass, on one of those days, as He is teaching the people in the temple, and proclaiming good news, the chief priests and the scribes, with the elders, came on [Him],
2 Walizungumza, wakimwambia, 'Tuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Au ni nani huyo ambaye amekupa mamlaka haya? “
and spoke to Him, saying, “Tell us by what authority You do these things? Or who is he that gave to You this authority?”
3 Naye akajibu, akawaambia, 'Nami pia nitawauliza swali. Niambieni
And He answering said to them, “I will question you—I also—one thing, and tell Me:
4 ubatizo wa Yohana. Je, ulitoka mbinguni ama kwa watu? '
the immersion of John, was it from Heaven, or from men?”
5 Lakini wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, 'Tukisema, `litoka mbinguni, atatuuliza, ` Basi, mbona hamkumwamini?'
And they reasoned with themselves, saying, “If we may say, From Heaven, He will say, Why, then, did you not believe him?
6 Na tukisema; ilitoka kwa wanadamu; watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii. '
And if we may say, From men, all the people will stone us, for they are having been persuaded John to be a prophet.”
7 Basi, wakamjibu ya kwamba hawakujua ilikotoka.
And they answered that they did not know from where [it was],
8 Yesu akawaambia, '“Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”
and Jesus said to them, “Neither do I say to you by what authority I do these things.”
9 Aliwaambia watu mfano huu, “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima wa mizabibu, na akaenda nchi nyingine kwa muda mrefu.
And He began to speak to the people this allegory: “A certain man planted a vineyard, and gave it out to farmers, and went abroad for a long time,
10 Kwa muda uliopangwa, alimtuma mtumishi kwa wakulima mizabibu, kwamba wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakulima wa mzabibu wakampiga, wakamrudisha mikono- mitupu.
and at the season he sent a servant to the farmers, that they may give to him from the fruit of the vineyard, but the farmers having beat him, sent [him] away empty.
11 Kisha akamtuma tena mtumishi mwingine na nao wakampiga, kumtendea vibaya, na wakamrudisha mikono- mitupu.
And he added to send another servant, and they also having beaten and dishonored that one, sent [him] away empty;
12 Alimtuma tena wa tatu na nao wakamjeruhi na kumtupa nje.
and he added to send a third, and this one also, having wounded, they cast out.
13 Hivyo bwana wa shamba akasema, 'Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa. Labda watamheshimu. '
And the owner of the vineyard said, What will I do? I will send my son, the beloved, perhaps having seen this one, they will respect [him];
14 Lakini wakulima wa mzabibu walipomwona, walijadili wao kwa wao wakisema, `Huyu ndiye mrithi. Tumuue, ili urithi wake uwe wetu. '
and having seen him, the farmers reasoned among themselves, saying, This is the heir; come, we may kill him, that the inheritance may become ours;
15 Wakamtoa nje ya shamba la mizabibu na kumuua. Je bwana shamba atawafanya nini?
and having cast him outside of the vineyard, they killed [him]; what, then, will the owner of the vineyard do to them?
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima wa mzabibu, na atawapa shamba hilo wengine”. 'Nao waliposikia hayo, wakasema, 'Mungu amekataa'
He will come, and destroy these farmers, and will give the vineyard to others.” And having heard, they said, “Let it not be!”
17 Lakini Yesu akawatazama, akasema, “Je andiko hili lina maana gani? 'Jiwe walilolikataa wajenzi, limekuwa jiwe la pembeni'?
And He, having looked on them, said, “What, then, is this that has been written: A stone that the builders rejected—this became head of a corner?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo, atavunjika vipande vipande. Lakini yule ambaye litamwangukia, litamponda. '
Everyone who has fallen on that stone will be broken, and on whom it may fall, it will crush him to pieces.”
19 Hivyo waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta njia ya kumkamata wakati huohuo, walijua kwamba alikuwa amesema mfano huu dhidi yao. Lakini waliwaogopa watu.
And the chief priests and the scribes sought to lay hands on Him in that hour, and they feared the people, for they knew that He spoke this allegory against them.
20 Walimuangalia kwa makini, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wapate kupata kosa kwa hotuba yake, ili kumpelekakwa watawala na wenye mamlaka.
And having watched [Him], they sent forth ones lying in wait, feigning themselves to be righteous, that they might take hold of His word, to deliver Him up to the rule and to the authority of the governor,
21 Nao wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli na si kushawishiwa na mtu yeyote, lakini wewe hufundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu.
and they questioned Him, saying, “Teacher, we have known that You say and teach correctly, and do not receive a person, but in truth teach the way of God.
22 Je, ni halali kwetu kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it lawful to us to give tribute to Caesar or not?”
23 Lakini Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
And He, having perceived their craftiness, said to them, “Why do you tempt Me?
24 “Nionyesheni dinari. Sura na chapa ya nani ipo juu yake?” Walisema, '“Ya Kaisari.”
Show Me a denarius; of whom does it have an image and inscription?” And they answering said, “Of Caesar”:
25 Naye akawaambia, 'Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu.'
and He said to them, “Give back, therefore, the things of Caesar to Caesar, and the things of God to God”;
26 Waandishi na wakuu wa makuhani hawakuwa na uwezo wa kukosoa kile alichosema mbele ya watu. Wakastaajabia majibu yake na hawakusema chochote.
and they were not able to take hold on His saying before the people, and having wondered at His answer, they were silent.
27 Baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale ambao wanasema kwamba hakuna ufufuo,
And certain of the Sadducees, who are denying that there is a resurrection, having come near, questioned Him,
28 wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba kama mtu akifiwa na ndugu mwenye mke ambaye hana mtoto basi anapaswa kumchukuna mke wa ndugu yake na kuzaa nae kwa ajili ya kaka yake.
saying, “Teacher, Moses wrote to us if anyone’s brother may die, having a wife, and he may die childless—that his brother may take the wife, and may raise up seed to his brother.
29 Kulikuwa na ndugu saba Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto,
There were, then, seven brothers, and the first having taken a wife, died childless,
and the second took the wife, and he died childless,
31 Wa tatu akamchukua vilevile, vivyo hivyo wa saba hakuacha watoto na akafa.
and the third took her, and in like manner also the seven—they left no children, and they died;
32 Baadaye yule mwanamke pia akafa.
and last of all the woman also died:
33 Katika ufufuo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa. '
in the resurrection, then, of which of them does she become wife? For the seven had her as wife.”
34 Yesu akawaambia, “Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa. (aiōn )
And Jesus answering said to them, “The sons of this age marry and are given in marriage, (aiōn )
35 Lakini wale wanastaohili kupokea ufufuo wa wafu na kuingia uzima wa milele hawaoi wala hawaolewi. (aiōn )
but those accounted worthy to obtain that age, and the resurrection that is out of the dead, neither marry, nor are they given in marriage; (aiōn )
36 Wala hawawezi kufa tena, kwa sababu huwa sawasawa na malaika na ni watoto wa Mungu, wana wa ufufuo.
for neither are they able to die anymore—for they are like messengers—and they are sons of God, being sons of the resurrection.
37 Lakini hiyo wafu wanafufuliwa, hata Musa alionyesha mahali katika habari za kichaka, pale alimwita Bwana kama Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
And that the dead are raised, even Moses showed at the Bush, since he calls the LORD the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob;
38 Sasa, yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa sababu wote huishi kwake. “
and He is not a God of dead men, but of living, for all live to Him.”
39 Baadhi ya walimu wa Sheria wakamjibu, 'Mwalimu, umejibu vema. '
And certain of the scribes answering said, “Teacher, You said well”;
40 Hawakuthubutu kumwuliza maswali mengine zaidi.
and they no longer dared question Him anything.
41 Yesu akawaambia, “Ki vipi watu wanasema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
And He said to them, “How do they say the Christ is [the] son of David,
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti mkono wa kulia,
and David himself says in [the] Scroll of Psalms, The LORD said to my Lord, Sit on My right hand,
43 mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako. '
Until I will make Your enemies Your footstool;
44 Daudi anamwita Kristo 'Bwana', basi atakuwaje mwana wa Daudi?”
David, then, calls Him Lord, and how is He his son?”
45 Watu wote walipokuwa wakimsikiliza akawaambia wanafunzi wake,
And all the people hearing, He said to His disciples,
46 'Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na wapenda salamu maalum sokoni na viti vya heshima katika masinagogi, na maeneo ya heshima karamuni.
“Take heed of the scribes, who are wishing to walk in long robes, and are cherishing salutations in the markets, and first seats in the synagogues, and first couches at the banquets,
47 Wao pia hula nyumba za wajane, na wanajifanya wanasali sala ndefu. Hawa watapokea hukumu kubwa zaidi. '
who devour the houses of the widows, and make long prayers for a pretense, these will receive more abundant judgment.”