< Luka 20 >

1 Ikawa siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuhubiri injili, makuhani wakuu na walimu wa Sheria walimwendea pamoja na wazee.
And it came to pass, that on one of the days, as he was teaching the people in the temple, and preaching the gospel, the chief priests and the scribes, with the ancients, met together,
2 Walizungumza, wakimwambia, 'Tuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Au ni nani huyo ambaye amekupa mamlaka haya? “
And spoke to him, saying: Tell us, by what authority dost thou these things? or, Who is he that hath given thee this authority?
3 Naye akajibu, akawaambia, 'Nami pia nitawauliza swali. Niambieni
And Jesus answering, said to them: I will also ask you one thing. Answer me:
4 ubatizo wa Yohana. Je, ulitoka mbinguni ama kwa watu? '
The baptism of John, was it from heaven, or of men?
5 Lakini wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, 'Tukisema, `litoka mbinguni, atatuuliza, ` Basi, mbona hamkumwamini?'
But they thought within themselves, saying: If we shall say, From heaven: he will say: Why then did you not believe him?
6 Na tukisema; ilitoka kwa wanadamu; watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii. '
But if we say, Of men, the whole people will stone us: for they are persuaded that John was a prophet.
7 Basi, wakamjibu ya kwamba hawakujua ilikotoka.
And they answered, that they knew not whence it was.
8 Yesu akawaambia, '“Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”
And Jesus said to them: Neither do I tell thee by what authority I do these things.
9 Aliwaambia watu mfano huu, “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima wa mizabibu, na akaenda nchi nyingine kwa muda mrefu.
And he began to speak to the people this parable: A certain man planted a vineyard, and let it out to husbandmen: and he was abroad for a long time.
10 Kwa muda uliopangwa, alimtuma mtumishi kwa wakulima mizabibu, kwamba wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakulima wa mzabibu wakampiga, wakamrudisha mikono- mitupu.
And at the season he sent a servant to the husbandmen, that they should give him of the fruit of the vineyard. Who, beating him, sent him away empty.
11 Kisha akamtuma tena mtumishi mwingine na nao wakampiga, kumtendea vibaya, na wakamrudisha mikono- mitupu.
And again he sent another servant. But they beat him also, and treating him reproachfully, sent him away empty.
12 Alimtuma tena wa tatu na nao wakamjeruhi na kumtupa nje.
And again he sent the third: and they wounded him also, and cast him out.
13 Hivyo bwana wa shamba akasema, 'Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa. Labda watamheshimu. '
Then the lord of the vineyard said: What shall I do? I will send my beloved son: it may be, when they see him, they will reverence him.
14 Lakini wakulima wa mzabibu walipomwona, walijadili wao kwa wao wakisema, `Huyu ndiye mrithi. Tumuue, ili urithi wake uwe wetu. '
Whom when the husbandmen saw, they thought within themselves, saying: This is the heir, let us kill him, that the inheritance may be ours.
15 Wakamtoa nje ya shamba la mizabibu na kumuua. Je bwana shamba atawafanya nini?
So casting him out of the vineyard, they killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima wa mzabibu, na atawapa shamba hilo wengine”. 'Nao waliposikia hayo, wakasema, 'Mungu amekataa'
He will come, and will destroy these husbandmen, and will give the vineyard to others. Which they hearing, said to him: God forbid.
17 Lakini Yesu akawatazama, akasema, “Je andiko hili lina maana gani? 'Jiwe walilolikataa wajenzi, limekuwa jiwe la pembeni'?
But he looking on them, said: What is this then that is written, The stone, which the builders rejected, the same is become the head of the corner?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo, atavunjika vipande vipande. Lakini yule ambaye litamwangukia, litamponda. '
Whosoever shall fall upon that stone, shall be bruised: and upon whomsoever it shall fall, it will grind him to powder.
19 Hivyo waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta njia ya kumkamata wakati huohuo, walijua kwamba alikuwa amesema mfano huu dhidi yao. Lakini waliwaogopa watu.
And the chief priests and the scribes sought to lay hands on him the same hour: but they feared the people, for they knew that he spoke this parable to them.
20 Walimuangalia kwa makini, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wapate kupata kosa kwa hotuba yake, ili kumpelekakwa watawala na wenye mamlaka.
And being upon the watch, they sent spies, who should feign themselves just, that they might take hold of him in his words, that they might deliver him up to the authority and power of the governor.
21 Nao wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli na si kushawishiwa na mtu yeyote, lakini wewe hufundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu.
And they asked him, saying: Master, we know that thou speakest and teachest rightly: and thou dost not respect any person, but teachest the way of God in truth.
22 Je, ni halali kwetu kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it lawful for us to give tribute to Caesar, or no?
23 Lakini Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
But he considering their guile, said to them: Why tempt you me?
24 “Nionyesheni dinari. Sura na chapa ya nani ipo juu yake?” Walisema, '“Ya Kaisari.”
Shew me a penny. Whose image and inscription hath it? They answering, said to him, Caesar’s.
25 Naye akawaambia, 'Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu.'
And he said to them: Render therefore to Caesar the things that are Caesar’s: and to God the things that are God’s.
26 Waandishi na wakuu wa makuhani hawakuwa na uwezo wa kukosoa kile alichosema mbele ya watu. Wakastaajabia majibu yake na hawakusema chochote.
And they could not reprehend his word before the people: and wondering at his answer, they held their peace.
27 Baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale ambao wanasema kwamba hakuna ufufuo,
And there came to him some of the Sadducees, who deny that there is any resurrection, and they asked him,
28 wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba kama mtu akifiwa na ndugu mwenye mke ambaye hana mtoto basi anapaswa kumchukuna mke wa ndugu yake na kuzaa nae kwa ajili ya kaka yake.
Saying: Master, Moses wrote unto us, If any man’s brother die, having a wife, and he leave no children, that his brother should take her to wife, and raise up seed unto his brother.
29 Kulikuwa na ndugu saba Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto,
There were therefore seven brethren: and the first took a wife, and died without children.
30 na wa pili pia.
And the next took her to wife, and he also died childless.
31 Wa tatu akamchukua vilevile, vivyo hivyo wa saba hakuacha watoto na akafa.
And the third took her. And in like manner all the seven, and they left no children, and died.
32 Baadaye yule mwanamke pia akafa.
Last of all the woman died also.
33 Katika ufufuo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa. '
In the resurrection therefore, whose wife of them shall she be? For all the seven had her to wife.
34 Yesu akawaambia, “Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
And Jesus said to them: The children of this world marry, and are given in marriage: (aiōn g165)
35 Lakini wale wanastaohili kupokea ufufuo wa wafu na kuingia uzima wa milele hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
But they that shall be accounted worthy of that world, and of the resurrection from the dead, shall neither be married, nor take wives. (aiōn g165)
36 Wala hawawezi kufa tena, kwa sababu huwa sawasawa na malaika na ni watoto wa Mungu, wana wa ufufuo.
Neither can they die any more: for they are equal to the angels, and are the children of God, being the children of the resurrection.
37 Lakini hiyo wafu wanafufuliwa, hata Musa alionyesha mahali katika habari za kichaka, pale alimwita Bwana kama Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
Now that the dead rise again, Moses also shewed, at the bush, when he called the Lord, The God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob;
38 Sasa, yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa sababu wote huishi kwake. “
For he is not the God of the dead, but of the living: for all live to him.
39 Baadhi ya walimu wa Sheria wakamjibu, 'Mwalimu, umejibu vema. '
And some of the scribes answering, said to him: Master, thou hast said well.
40 Hawakuthubutu kumwuliza maswali mengine zaidi.
And after that they durst not ask him any more questions.
41 Yesu akawaambia, “Ki vipi watu wanasema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
But he said to them: How say they that Christ is the son of David?
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti mkono wa kulia,
And David himself saith in the book of Psalms: The Lord said to my Lord, sit thou on my right hand,
43 mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako. '
Till I make thy enemies thy footstool.
44 Daudi anamwita Kristo 'Bwana', basi atakuwaje mwana wa Daudi?”
David then calleth him Lord: and how is he his son?
45 Watu wote walipokuwa wakimsikiliza akawaambia wanafunzi wake,
And in the hearing of all the people, he said to his disciples:
46 'Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na wapenda salamu maalum sokoni na viti vya heshima katika masinagogi, na maeneo ya heshima karamuni.
Beware of the scribes, who desire to walk in long robes, and love salutations in the marketplace, and the first chairs in the synagogues, and the chief rooms at feasts:
47 Wao pia hula nyumba za wajane, na wanajifanya wanasali sala ndefu. Hawa watapokea hukumu kubwa zaidi. '
Who devour the houses of widows, feigning long prayer. These shall receive greater damnation.

< Luka 20 >