< Luka 2 >
1 Sasa katika siku hizo, ikatokea kwamba Kaisari Agusto alitoa agizo akielekeza kwamba ichukuliwe sensa ya watu wote wanaoishi duniani.
Now it happened in those days, that a decree went out from Caesar Augustus that the whole empire should be enrolled.
2 Hii ilikuwa ni sensa ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio akiwa gavana wa Siria.
This was the first enrollment made when Quirinius was governor of Syria.
3 Hivyo kila mmoja akaenda mjini kwake kuandikishwa sensa.
All went to enroll themselves, everyone to his own city.
4 Naye Yusufu aliondoka pia katika mji wa Nazareti huko Galilaya na akasafiri Yudea katika mji wa Bethlehemu, ujulikanao kama mji wa Daudi, kwa sababu alitokea katika ukoo ya Daudi.
Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, into Judea, to the city of David, which is called Bethlehem, because he was of the house and family of David;
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Mariamu, ambaye alikuwa amemposa na alikuwa akitazamia mtoto.
to enroll himself with Mary, who was pledged to be married to him, being pregnant.
6 Sasa ilitokea kwamba, wakiwa kule wakati wake wa kujifungua mtoto ukawadia.
It happened, while they were there, that the day had come that she should give birth.
7 Akajifungua mtoto wa kiume, mzaliwa wake wa kwanza, akamzungushia nguo mwilini kumkinga na baridi mtoto. Ndipo akamweka kwenye kihori cha kulishia wanyama, kwa sababu haikuwepo nafasi kwenye nyumba za wageni.
And she gave birth to her firstborn son, and wrapped him with pieces of cloth, and placed him in a feeding trough, because there was no guest room available for them.
8 Katika eneo hilo, walikuwapo wachungaji walioishi mashambani wakilinda makundi ya Kondoo wao usiku.
There were shepherds in the same country staying in the field, and keeping watch by night over their flock.
9 Ghafla, malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Bwana ukang'aa kuwazunguka, na wakawa na hofu sana.
And look, an angel of the Lord stood by them, and the glory of the Lord shone around them, and they were terrified.
10 Ndipo malaika akwaambia, “Msiogope, kwasababu nawaletea habari njema ambayo italeta furaha kuu kwa watu wote.
The angel said to them, "Do not be afraid, for see, I bring you good news of great joy which will be to all the people.
11 Leo Mwokozi kazaliwa kwaajili yenu mjini mwa Daudi! Yeye ndiye Kristo Bwana!
For there is born to you, this day, in the city of David, a Savior, who is Messiah, the Lord.
12 Hii ndiyo ishara ambayo mtapewa, mtamkuta mtoto amefungwa nguo na amelala kwenye hori la kulishia wanyama.”
This is the sign to you: you will find a baby wrapped in strips of cloth, lying in a feeding trough."
13 Ghafla kukawa na jeshi kubwa la mbinguni likaungana na malaika huyo wakamsifu Mungu, wakisema,
Suddenly, there was with the angel a multitude of the heavenly army praising God, and saying,
14 “Utukufu kwa Mungu aliye juu sana, na amani iwe duniani kwa wote ambao anapendezwa nao.”
"Glory to God in the highest, and on earth peace, good will toward humankind."
15 Ikawa kwamba malaika walipokwisha kuondoka kwenda mbinguni, wachungaji wakasemezena wao kwa wao, “Twendeni sasa kule Bethlehemu, na tukaone hiki kitu ambacho kimetokea, ambacho Bwana ametufahamisha.”
And it happened that when the angels went away from them into the sky, the shepherds said one to another, "Let us go to Bethlehem, now, and see this thing that has happened, which the Lord has made known to us."
16 Wakaharakisha kule, na wakamkuta Mariamu na Yusufu, na wakamuona mtoto amelala kwenye hori la kulishia wanyama.
They came with haste, and found both Mary and Joseph, and the baby was lying in the feeding trough.
17 Na walipoona hivi, wakawajulisha watu kile walichokuwa wameambiwa kumhusu mtoto.
When they saw it, they made known the saying which was spoken to them about this child.
18 Wote waliosikia habari hii wakashangazwa na kile kilichosemwa na wachungaji.
All who heard it wondered at the things which were spoken to them by the shepherds.
19 Lakini Mariamu akaendelea kufikiri kuhusu yote aliyokwisha kuyasikia, akiyatunza moyoni mwake.
But Mary kept all these sayings, pondering them in her heart.
20 Wachungaji wakarudi wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa ajili ya kila kitu walichokwisha sikia na kuona, kama tu ilivyokuwa imenenwa kwao.
The shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, just as it was told them.
21 Ilipofika siku ya nane na ilikuwa ni wakati wa kumtahiri mtoto, wakamwita jina Yesu, jina alilokwishapewa na yule malaika kabla mimba haijatungwa tumboni.
When eight days were fulfilled to circumcise him, his name was called Jesus, which was given by the angel before he was conceived in the womb.
22 zao zilizotakiwa za utakaso zilipopita, kulingana na sheria ya Musa, Yusufu na Mariamu wakampeleka hekaluni kule Yerusalemu kumweka mbele za Bwana.
When the days of their purification according to the Law of Moses were fulfilled, they brought him up to Jerusalem, to present him to the Lord
23 Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, “Kila mwanaume anayefungua tumbo ataitwa aliyetolewa wakfu kwa Bwana.”
(as it is written in the Law of the Lord, "Every male who opens the womb will be called holy to the Lord"),
24 Wao vilevile walikuja kutoa sadaka kulingana na kile kinachosemwa katika sheria ya Bwana, “Jozi ya njiwa au makinda mawili ya njiwa.”
and to offer a sacrifice according to that which is said in the Law of the Lord, "A pair of turtledoves, or two young pigeons."
25 Tazama, palikuwa na mtu katika Yerusalemu ambaye jina lake alikuwa akiitwa Simeoni. mtu huyu alikuwa mwenye haki na mcha Mungu. Yeye alikuwa akisubiri kwa ajili ya mfariji wa Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
And look, there was a man in Jerusalem whose name was Simeon. This man was righteous and devout, looking for the consolation of Israel, and the Holy Spirit was on him.
26 Ilikuwa imekwisha funuliwa kwake kupitia Roho Mtakatifu kwamba yeye hangelikufa kabla ya kuwomwona Kristo wa Bwana.
It had been revealed to him by the Holy Spirit that he should not see death before he had seen the Lord's Messiah.
27 Siku moja alikuja ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho Mtakatifu. Ambapo wazazi walimleta mtoto, Yesu, kumfanyia yale yaliyopasa kawaida ya sheria,
He came in the Spirit into the temple. When the parents brought in the child, Jesus, that they might do concerning him according to the requirement of the Law,
28 ndipo Simeoni alimpokea mikononi mwake, na akamsifu Mungu na kusema,
then he received him into his arms, and blessed God, and said,
29 “Sasa ruhusu mtumishi wako aende kwa amani Bwana, kulingana na Neno lako.
"Now you are releasing your servant, Lord, according to your word, in peace;
30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wakovu wako,
for my eyes have seen your salvation,
31 ambao umeonekana kwa macho ya watu wote.
which you have prepared before the face of all peoples;
32 Yeye ni nuru kwa ajili ya ufunuo kwa Wamataifa na utukufu wa watu Israeli.”
a light for revelation to the nations, and the glory of your people Israel."
33 Baba na Mama wa mtoto walishangazwa kwa mambo ambayo yalizungumzwa juu yake.
And his father and his mother were marveling at the things which were spoken concerning him,
34 Ndipo Simeoni akawabariki na akasema kwa Mariamu mama yake, “Sikiliza kwa makini! Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli na ni ishara ambayo watu wengi wataipinga.
and Simeon blessed them, and said to Mary, his mother, "Look, this child is set for the falling and the rising of many in Israel, and for a sign which is spoken against.
35 Pia ni upanga utakaochoma nafsi yako mwenyewe, ili kwamba mawazo ya mioyo ya wengi yadhihirike”.
Yes, a sword will pierce through your own soul, that the thoughts of many hearts may be revealed."
36 Nabii mwanamke aliyeitwa Ana pia alikuwako hekaluni. Yeye alikuwa binti wa Fanueli kutoka kabila la Asheri. Alikuwa na miaka mingi sana. Naye aliishi na mume wake kwa miaka saba baada ya kuoana,
There was one Anna, a prophetess, the daughter of Penuel, of the tribe of Asher (she was of a great age, having lived with a husband seven years from her virginity,
37 na ndipo akawa mjane kwa miaka themanini na minne. Naye hakuwahi kuondoka hekaluni na alikuwa akiendelea kumwabudu Mungu pamoja na kufunga na kuomba, usiku na mchana.
and she had been a widow for about eighty-four years), who did not depart from the temple, worshipping with fastings and petitions night and day.
38 Na kwa wakati huo, alikuja pale walipo akaanza kumshukuru Mungu. Aliongea kumhusu mtoto kwa kila mtu ambaye alikuwa akisubiri ukombozi wa Yerusalemu.
Coming up at that very hour, she gave thanks to God, and spoke of him to all those who were looking for the redemption of Jerusalem.
39 Walipomaliza kila kitu walichotakiwa kufanya kuligana na na sheria ya Bwana, walirudi Galilaya, mjini kwao, Nazareti.
When they had accomplished all things that were according to the Law of the Lord, they returned into Galilee, to their own city, Nazareth.
40 Mtoto alikua, na akawa na nguvu, akiongezeka katika hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
The child was growing, and was becoming strong, being filled with wisdom, and the favor of God was upon him.
41 Wazazi wake kila mwaka walikwenda Yerusalemu kwaajili ya sikukuu ya Pasaka.
His parents went every year to Jerusalem at the feast of the Passover.
42 Alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walikwenda tena wakati mwafaka kidesturi kwa ajili ya sikukuu.
When he was twelve years old, they went up according to the custom of the feast,
43 Baada ya kubaki siku zote kwa ajili ya sikukuu, walianza kurudi nyumbani. Lakini mvulana Yesu alibaki nyuma mle Yerusalemu na wazazi wake hawakujua hili.
and when they had fulfilled the days, as they were returning, the boy Jesus stayed behind in Jerusalem. His parents did not know it,
44 Walidhani kwamba yumo kwenye kundi walilokuwa wakisafiri nalo, hivyo walisafiri safari ya siku. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni wa ndugu na marafiki zao.
but supposing him to be in the company, they went a day's journey, and they looked for him among their relatives and acquaintances.
45 Waliposhindwa kumpata, walirudi Yerusalemu na wakaanza kumtafuta humo.
When they did not find him, they returned to Jerusalem, looking for him.
46 Ikatokea kwamba baada ya siku tatu, wakampata hekaluni, akiwa ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
It happened after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both listening to them, and asking them questions.
47 Wote waliomsikia walishangazwa na ufahamu wake na majibu yake.
All who heard him were amazed at his understanding and his answers.
48 Walipomwona, walistaajabu. Mama yake akamwambia, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivi? Sikiliza, baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa.”
When they saw him, they were astonished, and his mother said to him, "Son, why have you treated us this way? Look, your father and I were anxiously looking for you."
49 Akawaambia, “Kwa nini mmekuwa mkinitafuta? Hamkujua kwamba lazima niwe kwenye nyumba ya Baba yangu?
He said to them, "Why were you looking for me? Did you not know that I must be doing the works of my Father?"
50 Lakini hawakuelewa nini alichomaanisha kwa maneno hayo.
They did not understand the saying which he spoke to them.
51 Ndipo akaenda pamoja nao mpaka nyumbani Nazareti na alikuwa mtii kwao. Mama yake alihifadhi mambo yote moyoni mwake.
And he went down with them, and came to Nazareth. He was subject to them, and his mother kept all these sayings in her heart.
52 Lakini Yesu aliendelea kukua katika hekima na kimo, na akazidi kupendwa na Mungu na watu.
And Jesus increased in wisdom and stature, and in favor with God and people.