< Luka 2 >

1 Sasa katika siku hizo, ikatokea kwamba Kaisari Agusto alitoa agizo akielekeza kwamba ichukuliwe sensa ya watu wote wanaoishi duniani.
In those days Augustus Caesar issued an edict for a census of the whole inhabited world.
2 Hii ilikuwa ni sensa ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio akiwa gavana wa Siria.
This was the first census, When Quirinius was governor of Syria.
3 Hivyo kila mmoja akaenda mjini kwake kuandikishwa sensa.
And every one went to be registered, each to the town to which he belonged.
4 Naye Yusufu aliondoka pia katika mji wa Nazareti huko Galilaya na akasafiri Yudea katika mji wa Bethlehemu, ujulikanao kama mji wa Daudi, kwa sababu alitokea katika ukoo ya Daudi.
And Joseph also went up from Galilee, out of the city if Nazareth, into Judea, to David’s town of Bethlehem, because he was of the house and family of David.
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Mariamu, ambaye alikuwa amemposa na alikuwa akitazamia mtoto.
He went to be registered along with Mary, who was espoused to him, and was pregnant.
6 Sasa ilitokea kwamba, wakiwa kule wakati wake wa kujifungua mtoto ukawadia.
But while they were there the days were fulfilled for her delivery.
7 Akajifungua mtoto wa kiume, mzaliwa wake wa kwanza, akamzungushia nguo mwilini kumkinga na baridi mtoto. Ndipo akamweka kwenye kihori cha kulishia wanyama, kwa sababu haikuwepo nafasi kwenye nyumba za wageni.
And she gave birth to her firstborn son; and she wrapped him in swaddling clothes, and laid him in a manger because there was no room for them in the inn.
8 Katika eneo hilo, walikuwapo wachungaji walioishi mashambani wakilinda makundi ya Kondoo wao usiku.
And there were in the same country shepherds abiding in the fields, keeping watch over their flocks by night.
9 Ghafla, malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Bwana ukang'aa kuwazunguka, na wakawa na hofu sana.
When suddenly an angel of the Lord stood by them, and the glory of the Lord shone round them; and they feared with a great fear. The angel said to them.
10 Ndipo malaika akwaambia, “Msiogope, kwasababu nawaletea habari njema ambayo italeta furaha kuu kwa watu wote.
"Have no fear, for behold, I bring you good tidings of great joy, which shall be for all the people.
11 Leo Mwokozi kazaliwa kwaajili yenu mjini mwa Daudi! Yeye ndiye Kristo Bwana!
"For unto you born this day in there is born in David’s town a Saviour, who is the Anointed Lord.
12 Hii ndiyo ishara ambayo mtapewa, mtamkuta mtoto amefungwa nguo na amelala kwenye hori la kulishia wanyama.”
"And this is a sign to you; You shall find the babe wrapped in swaddling-clothes lying in a manger."
13 Ghafla kukawa na jeshi kubwa la mbinguni likaungana na malaika huyo wakamsifu Mungu, wakisema,
And suddenly there was with the angel a multitude of the Heavenly army praising God and saying,
14 “Utukufu kwa Mungu aliye juu sana, na amani iwe duniani kwa wote ambao anapendezwa nao.”
"Glory to God in the highest, And in earth peace among men who please him"
15 Ikawa kwamba malaika walipokwisha kuondoka kwenda mbinguni, wachungaji wakasemezena wao kwa wao, “Twendeni sasa kule Bethlehemu, na tukaone hiki kitu ambacho kimetokea, ambacho Bwana ametufahamisha.”
Now when the angels had left them, and gone away to heaven, the shepherds said to one to another, "Let us go now even to Bethlehem, and see this saying which has come to pass, which the Lord has made known to us."
16 Wakaharakisha kule, na wakamkuta Mariamu na Yusufu, na wakamuona mtoto amelala kwenye hori la kulishia wanyama.
so they made haste, and came and found Mary and Joseph, and the babe lying in the manger.
17 Na walipoona hivi, wakawajulisha watu kile walichokuwa wameambiwa kumhusu mtoto.
When they had seen, they made known about the words which had been spoken to them concerning the child.
18 Wote waliosikia habari hii wakashangazwa na kile kilichosemwa na wachungaji.
And all who heard it were astonished at the things which were told to them by the shepherds.
19 Lakini Mariamu akaendelea kufikiri kuhusu yote aliyokwisha kuyasikia, akiyatunza moyoni mwake.
But Mary treasured up all those words, Often pondering on on them in her heart.
20 Wachungaji wakarudi wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa ajili ya kila kitu walichokwisha sikia na kuona, kama tu ilivyokuwa imenenwa kwao.
And the shepherds returned, glorifying God and praising him for all those things that they had seen and heard, even as it was told to them.
21 Ilipofika siku ya nane na ilikuwa ni wakati wa kumtahiri mtoto, wakamwita jina Yesu, jina alilokwishapewa na yule malaika kabla mimba haijatungwa tumboni.
When eight days had passed, and the time had come to circumcise him, he was called Jesus, the name given him by the angel before his conception in the womb.
22 zao zilizotakiwa za utakaso zilipopita, kulingana na sheria ya Musa, Yusufu na Mariamu wakampeleka hekaluni kule Yerusalemu kumweka mbele za Bwana.
And when the days for purification according to the law of Moses had passed, they took him up to Jerusalem, to present him to the Lord,
23 Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, “Kila mwanaume anayefungua tumbo ataitwa aliyetolewa wakfu kwa Bwana.”
as it is written in the law of Moses, Every firstborn male shall be called holy to the Lord.
24 Wao vilevile walikuja kutoa sadaka kulingana na kile kinachosemwa katika sheria ya Bwana, “Jozi ya njiwa au makinda mawili ya njiwa.”
And they also offered a sacrifice as commanded in the Law of the Lord A pair of turtle-doves or two young pigeons.
25 Tazama, palikuwa na mtu katika Yerusalemu ambaye jina lake alikuwa akiitwa Simeoni. mtu huyu alikuwa mwenye haki na mcha Mungu. Yeye alikuwa akisubiri kwa ajili ya mfariji wa Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
Now there was in Jerusalem a man whose name was Simeon. He was righteous and devout, and was waiting for the consolation of Israel. The Holy Spirit was upon him.
26 Ilikuwa imekwisha funuliwa kwake kupitia Roho Mtakatifu kwamba yeye hangelikufa kabla ya kuwomwona Kristo wa Bwana.
Now it has been revealed to him by the Holy Spirit that he should not see death, before he had seen the Lord’s Christ.
27 Siku moja alikuja ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho Mtakatifu. Ambapo wazazi walimleta mtoto, Yesu, kumfanyia yale yaliyopasa kawaida ya sheria,
And he came into the Temple, led by the Spirit. and when his parents brought in the child Jesus, to do for him according to the custom of the law,
28 ndipo Simeoni alimpokea mikononi mwake, na akamsifu Mungu na kusema,
he took him up in his arms and blessed God and said,
29 “Sasa ruhusu mtumishi wako aende kwa amani Bwana, kulingana na Neno lako.
"Now lettest thou thy slave depart, O Master; according to thy word in peace,
30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wakovu wako,
"Because my eyes had seen the salvation,
31 ambao umeonekana kwa macho ya watu wote.
"Which thou hast prepared before the face of all peoples;
32 Yeye ni nuru kwa ajili ya ufunuo kwa Wamataifa na utukufu wa watu Israeli.”
"A light for the unveiling of the Gentiles And the glory of thy people Israel."
33 Baba na Mama wa mtoto walishangazwa kwa mambo ambayo yalizungumzwa juu yake.
And while his father and mother were marveling at the words that were spoken concerning him, Simeon blessed them and said to Mary, his mother.
34 Ndipo Simeoni akawabariki na akasema kwa Mariamu mama yake, “Sikiliza kwa makini! Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli na ni ishara ambayo watu wengi wataipinga.
"Behold this child is set for the falling and rising up of many in Israel, and for a sign which is spoken against.
35 Pia ni upanga utakaochoma nafsi yako mwenyewe, ili kwamba mawazo ya mioyo ya wengi yadhihirike”.
Yea, and a sword shall pierce through your own soul also, that the thoughts out of many hearts may be revealed."
36 Nabii mwanamke aliyeitwa Ana pia alikuwako hekaluni. Yeye alikuwa binti wa Fanueli kutoka kabila la Asheri. Alikuwa na miaka mingi sana. Naye aliishi na mume wake kwa miaka saba baada ya kuoana,
There was one Anna, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Asher. She was advanced in age, having lived with her husband seven years, after her girlhood,
37 na ndipo akawa mjane kwa miaka themanini na minne. Naye hakuwahi kuondoka hekaluni na alikuwa akiendelea kumwabudu Mungu pamoja na kufunga na kuomba, usiku na mchana.
and then being a widow even for fourscore and four years. She departed not from the temple, but worshiped with the fasting and prayer, night and day.
38 Na kwa wakati huo, alikuja pale walipo akaanza kumshukuru Mungu. Aliongea kumhusu mtoto kwa kila mtu ambaye alikuwa akisubiri ukombozi wa Yerusalemu.
She came up at that very hour, and gave thanks to God, and spoke of the child to all who were looking for the redemption of Jerusalem.
39 Walipomaliza kila kitu walichotakiwa kufanya kuligana na na sheria ya Bwana, walirudi Galilaya, mjini kwao, Nazareti.
As soon as all that the law required had been done, they returned to Galilee to their own town, Nazareth.
40 Mtoto alikua, na akawa na nguvu, akiongezeka katika hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
And the child grew and became strong, becoming full of wisdom, and the grace of God was upon him.
41 Wazazi wake kila mwaka walikwenda Yerusalemu kwaajili ya sikukuu ya Pasaka.
Now his parents were accustomed to go up to Jerusalem every year at the feast of the Passover.
42 Alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walikwenda tena wakati mwafaka kidesturi kwa ajili ya sikukuu.
And when he was twelve years old they went up, as was customary, at the time of the feast
43 Baada ya kubaki siku zote kwa ajili ya sikukuu, walianza kurudi nyumbani. Lakini mvulana Yesu alibaki nyuma mle Yerusalemu na wazazi wake hawakujua hili.
After spending the full number of days they started home, but the boy Jesus remained behind in Jerusalem. Joseph and his mother did not know this,
44 Walidhani kwamba yumo kwenye kundi walilokuwa wakisafiri nalo, hivyo walisafiri safari ya siku. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni wa ndugu na marafiki zao.
but supposed that he was in the company, and went a days journey. Then they hunted for him among his kinsfolk and acquaintance;
45 Waliposhindwa kumpata, walirudi Yerusalemu na wakaanza kumtafuta humo.
and when they did not find him they returned to Jerusalem, making anxious inquiry for him.
46 Ikatokea kwamba baada ya siku tatu, wakampata hekaluni, akiwa ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
On the third day they found him sitting in the Temple, among the Rabbis, both listening to them and asking questions.
47 Wote waliomsikia walishangazwa na ufahamu wake na majibu yake.
All that heard him were amazed at his understanding and his answers.
48 Walipomwona, walistaajabu. Mama yake akamwambia, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivi? Sikiliza, baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa.”
When they saw him they were astonished, and his mother said to him "Child, why have you treated us so? Behold your father and I have been looking for you in anguish."
49 Akawaambia, “Kwa nini mmekuwa mkinitafuta? Hamkujua kwamba lazima niwe kwenye nyumba ya Baba yangu?
He answered, "Why is it that you have been looking for me, did you not realize that I had to be in my Father’s house?"
50 Lakini hawakuelewa nini alichomaanisha kwa maneno hayo.
But they did not understand the words that he spoke to them.
51 Ndipo akaenda pamoja nao mpaka nyumbani Nazareti na alikuwa mtii kwao. Mama yake alihifadhi mambo yote moyoni mwake.
Then he went down with them, and came to Nazareth, and he was always obedient to them. But his mother kept treasuring up all these incidents in her hearts.
52 Lakini Yesu aliendelea kukua katika hekima na kimo, na akazidi kupendwa na Mungu na watu.
And Jesus was ever advancing in wisdom and in status and in favor with God and man.

< Luka 2 >