< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
So He entered Jericho and was passing through the town.
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
There was a man there called Zacchaeus, who was the local surveyor of taxes, and was wealthy.
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
He was anxious to see what sort of man Jesus was; but he could not because of the crowd, for he was short in stature.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
So he ran on in front and climbed up a mulberry tree to see Him; for He was about to pass that way.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
As soon as Jesus came to the place, He looked up and said to him, "Zacchaeus, come down quickly, for I must stay at your house to-day."
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
So he came down in haste, and welcomed Him joyfully.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
When they all saw this, they began to complain with indignation. "He has gone in to be the guest of a notorious sinner!" they said.
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
Zacchaeus however stood up, and addressing the Lord said, "Here and now, Master, I give half my property to the poor, and if I have unjustly exacted money from any man, I pledge myself to repay to him four times the amount."
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
Turning towards him, Jesus replied, "To-day salvation has come to this house, seeing that he too is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
For the Son of Man has come to seek and to save that which was lost."
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
As they were listening to His words, He went on to teach them by a parable, because He was near to Jerusalem and they supposed that the Kingdom of God was going to appear immediately.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
So He said to them, "A man of noble family travelled to a distant country to obtain the rank of king, and to return.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
And he called ten of his servants and gave each of them a pound, instructing them to trade with the money during his absence.
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
"Now his countrymen hated him, and sent a deputation after him to say, 'We are not willing that he should become our king.'
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
And upon his return, after he had obtained the sovereignty, he ordered those servants to whom he had given the money to be summoned before him, that he might learn their success in trading.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
"So the first came and said, "'Sir, your pound has produced ten pounds more.'
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
"'Well done, good servant,' he replied; 'because you have been faithful in a very small matter, be in authority over ten towns.'
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
"The second came, and said, "'Your pound, Sir, has produced five pounds.'
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
"So he said to this one also, "'And you, be the governor of five towns.'
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
"The next came. "'Sir,' he said, 'here is your pound, which I have kept wrapt up in a cloth.
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
For I was afraid of you, because you are a severe man: you take up what you did not lay down, and you reap what you did not sow.'
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
"'By your own words,' he replied, 'I will judge you, you bad servant. You knew me to be a severe man, taking up what I did not lay down, and reaping what I did not sow:
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
why then did you not put my money into a bank, that when I came I might have received it back with interest?
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
"And he said to those who stood by, "'Take the pound from him and give it to him who has the ten pounds.'
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
("They said to him, "'Sir, he already has ten pounds.')
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
"'I tell you that to every one who has anything, more shall be given; and from him who has not anything, even what he has shall be taken away.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
But as for those enemies of mine who were unwilling that I should become their king, bring them here, and cut them to pieces in my presence.'"
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
After thus speaking, He journeyed onward, proceeding up to Jerusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
And when he was come near Bethphage and Bethany, at the Mount called the Oliveyard, He sent two of the disciples on in front,
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
saying to them, "Go into the village facing you. On entering it you will find an ass's foal tied up which no one has ever yet ridden: untie it, and bring it here.
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
And if any one asks you, 'Why are you untying the colt?' simply say, 'The Master needs it.'"
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
So those who were sent went and found things as He had told them.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
And while they were untying the colt the owners called out, "Why are you untying the colt?"
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
and they replied, "The Master needs it."
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
Then they brought it to Jesus, and after throwing their outer garments on the colt they placed Jesus on it.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
So He rode on, while they carpeted the road with their garments.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
And when He was now getting near Jerusalem, and descending the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began in their joy to praise God in loud voices for all the mighty deeds they had witnessed.
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
"Blessed is the King," they cried, "who comes in the name of the Lord: in Heaven peace, and glory in the highest realms."
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
Thereupon some of the Pharisees in the crowd appealed to Him, saying, "Rabbi, reprove your disciples."
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
"I tell you," He replied, "that if they became silent, the very stones would cry out."
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
When He came into full view of the city, He wept aloud over it, and exclaimed,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
"O that at this time thou hadst known--yes even thou--what makes peace possible! But now it is hid from thine eyes.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
For the time is coming upon thee when thy foes will throw up around thee earthworks and a wall, investing thee and hemming thee in on every side.
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
And they will dash thee to the ground and thy children within thee, and will not leave one stone upon another within thee; because thou hast not recognized the time of thy visitation."
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
Then Jesus entered the Temple and proceeded to drive out the dealers.
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
"It is written," He said, "'And My house shall be the House of Prayer,' but you have made it a robbers' cave."
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
And day after day He taught in the Temple, while the High Priests and the Scribes were devising some means of destroying Him, as were also the leading men of the people.
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
But they could not find any way of doing it, for the people all hung upon His lips.

< Luka 19 >