< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
He entered and started passing through Jericho.
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
A man named Zacchaeus was there—he was a chief tax collector, and he was wealthy!
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
He was trying to see who Jesus was, but could not because of the crowd, because he was short.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
And running on ahead he climbed up into a sycamore tree, in order to see Him, since He was about to pass by there.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
And when Jesus came to the place, He looked up and saw him, and said to him, “Zacchaeus, come down quickly, because today I must stay at your house.”
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
So he came down quickly, and received Him joyfully.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
But when they saw it, they all started complaining, saying, “He has entered to lodge with a sinful man!”
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
Then Zacchaeus stood and said to the Lord, “Indeed, Lord, I herewith give half of my goods to the poor, and if I have extorted anything from anyone, I restore fourfold.”
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
So Jesus said about him, “Today salvation has happened in this house, in that he also is a son of Abraham;
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
because the Son of the Man has come to seek and to save that which was lost.”
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
Now as they heard these things, He continued with a parable, because He was near Jerusalem and they were supposing that the Kingdom of God was on the verge of being revealed.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
So He said: “A certain nobleman went to a distant country to receive for himself a kingdom and return.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
He called ten of his slaves, gave them ten ‘minas’, and said to them, ‘Conduct business until I come.’
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
But his citizens hated him and sent a delegation after him, saying, ‘We do not want this man to reign over us.’
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
It happened that he did receive the kingdom, and upon returning he ordered that those slaves to whom he had given the money be called to him, to know who had gained what by trading.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
So the first one came and said, ‘Master, your mina earned ten minas!’
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
He said to him: ‘Super, you good slave! Because you were faithful in a very little, have authority over ten cities!’
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
And the second one came and said, ‘Master, your mina made five minas.’
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
Likewise he said to him, ‘You also be over five cities.’
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
Then a different one came, saying: ‘Master, here is your mina, that I kept laid away in a piece of cloth
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
—I feared you because you are a hard man, removing what you did not place, and reaping what you did not sow.’
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
So he said to him: ‘I will judge you out of your own mouth, you wicked slave! You knew that I am a hard man, removing what I did not place, and reaping what I did not sow.
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
Why then didn't you put my money on deposit, and upon coming I would have collected it with interest?’
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
And to those standing by he said, ‘Take the mina from him and give it to him who has the ten minas.’
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
(They even said to him, ‘Master, he already has ten minas!’)
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
‘Indeed I tell you, to everyone who has, more will be given; but from him who does not have, even what he has will be taken from him.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
But as for those enemies of mine who did not want me to reign over them, bring them here and slaughter them in front of me!’”
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
Having said these things, He went on ahead, going up to Jerusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
When He drew near to Bethphage and Bethany, at the mountain called ‘of Olives’, it happened like this: He sent two of His disciples,
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
saying: “Go to the village opposite you, where as you enter you will find a colt tied, on which no man ever yet sat. Untie and bring it.
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
And if anyone asks you, ‘Why are you untying it?’ just say this to him: ‘The Lord needs it.’”
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
So those who were sent went and found it just like He told them.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
As they were untying the colt, its owners said to them, “Why are you untying the colt?”
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
So they said, “The Lord needs it.”
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
Then they brought it to Jesus; and throwing their own clothes on the colt, they placed Jesus on it.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
And as He went along people were spreading their clothes on the road.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
Then, as He was approaching the descent of the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works they had seen,
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
saying: “Blessed is the King who comes in the name of the Lord! Peace in heaven and glory in the highest!”
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
Some of the Pharisees said to Him from the crowd, “Teacher, rebuke your disciples!”
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
In answer He said to them, “I tell you that if these should keep silent, the very stones would cry out!”
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
Now as He approached, observing the city He wept over it,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
saying: “If you, yes you, especially in this your day, had known the things pertaining to your peace! But now they are hidden from your eyes.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
Yes, the days will come upon you when your enemies will build an embankment around you; indeed they will surround you and hem you in on every side.
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
And they will raze you, and your children within you, to the ground—they will not leave in you one stone upon another—all because you did not recognize the time of your visitation.”
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
And upon entering the temple He began to drive out those who were selling and buying in it,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
saying to them, “It is written: ‘My house is a house of prayer,’ but you have made it a ‘den of robbers’!”
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
And He was teaching daily in the temple; but the chief priests and the scribes, as also the leaders of the people, were trying to destroy Him,
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
but could not figure out how to do it, because all the people were hanging on His words.

< Luka 19 >