< Luka 14 >

1 Iltokea siku ya Sabato, alipokua akienda nyumbani kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo kula mkate, nao walikuwa wakimchunguza kwa karibu.
And it chaunsed that he went into the housse of one of ye chefe pharises to eate breed on a saboth daye: and they watched him.
2 Tazama, pale mbele yake alikuwa mtu ambaye anasumbuliwa na uvimbe.
And beholde ther was a man before him which had the dropsye.
3 Yesu aliuliza wataalam katika sheria ya Wayahudi na Mafarisayo, “Je, ni halali kumponya siku ya Sabato, au sivyo?”
And Iesus answered and spake vnto the lawears and pharises sayinge: is it laufull to heale on the saboth daye?
4 Lakini wao walikuwa kimya, kwahiyo Yesu akamshika, akamponya na kumruhusu aende zake.
And they helde their peace. And he toke him and healed him and let him goo:
5 Naye akawaambia, “Ni nani kati yenu ambaye ana mtoto au ng'ombe anatumbukia kisimani siku ya Sabato hata mvuta nje mara moja?”
and answered the sayinge whiche of you shall have an asse or an oxe fallen into a pitt and will not strayght waye pull him out on the Saboth daye?
6 Wao hawakuwa na uwezo wa kutoa jibu kwa mambo haya.
And they coulde not answer him agayne to that.
7 Wakati Yesu alipogundua jinsi wale walioalikwa kwamba wamechagua viti vya heshima, akawaambia mfano, akiwaambia,
He put forthe a similitude to ye gestes whe he marked how they preased to the hyest roumes and sayd vnto the:
8 “Wakati mnapoalikwa na mtu harusini, usiketi katika nafasi za heshima, kwa sababu inawezekana amealikwa mtu ambaye ni wakuheshimiwa zaidi kuliko wewe.
When thou arte bidde to a weddynge of eny man syt not doune in ye hyest roume lest a more honorable man then thou be bidden of him
9 Wakati mtu aliyewaalika ninyi wawili akifika, atakuambia wewe, “mpishe mtu huyu nafasi yako,” na kisha kwa aibu utaanza kuchukua nafasi ya mwisho.
and he that bade bothe him and the come and saye to the: geve this man roume and thou then beginne with shame to take the lowest roume.
10 Lakini wewe ukialikwa, nenda ukakae mahali pa mwisho, ili wakati yule aliyekualika akija, aweze kukuambia wewe, `Rafiki, nenda mbele zaidi.” ndipo utakuwa umeheshimika mbele ya wote walioketi pamoja nawe mezani.
But rather when thou arte bidden goo and syt in the lowest roume that when he that bade the cometh he maye saye vnto the: frende syt vp hyer. Then shalt thou have worshippe in the presence of them that syt at meate with the.
11 Kwa maana kila ajikwezaye atashushwa, na yeye ajishushae atakwezwa. '
For whosoever exalteth him sylfe shalbe brought lowe. And he yt hubleth him sylfe shalbe exalted
12 Yesu pia alimwambia mtu aliyemwalika, 'Unapotoa chakula cha mchana au cha jioni, usiwaalike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako matajiri, ili kwamba wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo.
Then sayde he also to him that had desyred him to diner: When thou makest a diner or a supper: call not thy frendes nor thy brethre nether thy kinsmen nor yet ryche neghbours: lest they bidde the agayne and a recompence be made the.
13 Badala yake, unapofanya sherehe, waalike maskini, vilema, viwete na vipofu,
But when thou makest afeast call the poore the maymed the lame and the blynde
14 na wewe utabarikiwa, kwa sababu hawawezi kukulipa. Kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.”
and thou shalt be happy for they cannot recompence the. But thou shalt be recompensed at the resurreccion of the iuste men.
15 Wakati mmoja wa wale walioketi mezani pamoja na Yesu aliposikia hayo, naye akamwambia, “Amebarikiwe yule atakayekula mkate katika Ufalme wa Mungu!”
When one of them that sate at meate also hearde that he sayde vnto him: happy is he that eateth breed in the kyngdome of God.
16 Lakini Yesu akamwambia, “Mtu mmoja aliandaa sherehe kubwa, akaalika watu wengi.
Then sayd he to him. A certayne man ordened a greate supper and bade many
17 Wakati sherehe ilipokuwa tayari, alimtuma mtumishi wake kuwaambia wale walioalikwa, `'Njooni, kwa sababu vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.'
and sent his servaunt at supper tyme to saye to them that wer bidden come: for all thinges are now redy.
18 Wote, wakaanza kuomba radhi. Wa kwanza akamwambia mtumishi, 'Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali unisamehe.'
And they all atonce begane to make excuse. The fyrst sayd vnto him: I have bought a ferme and I must nedes goo and se it I praye the have me excused.
19 Na mwingine akasema, `'Nimenunua jozi tano za ng'ombe, na mimi naenda kuwajaribu. Tafadhali uniwie radhi.'
And another sayd: I hove bought fyve yooke of oxen and I goo to prove them I praye the have me excused.
20 Na mtu mwingine akasema, 'Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.'
The thyrde sayd: I have maried a wyfe and therfore I cannot come.
21 Mtumishi akarudi na kumwambia bwana wake mambo hayo. Yule mwenye nyumba alikasirika akamwambia mtumishi wake, `'Nenda upesi mitaani na katika vichochoro vya mji ukawalete hapa maskini, vilema, vipofu na walemavu.”
And the servaunt went and brought his master worde therof. Then was the good man of the housse displeased and sayd to his servaut: Goo out quickly into ye stretes and quarters of the cite and bringe in hidder the poore and the maymed and the halt and the blynde.
22 Mtumimishi akasema, `Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa bado kuna nafasi.'
And the servaut sayd: lorde it is done as thou comaundedst and yet ther is roume.
23 Bwana akamwambia mtumishi, 'Nenda katika njia kuu na vichochoro na uwashurutishe watu waingie, ili nyumba yangu ijae.
And the lorde sayd to the servaunt: Go out into ye hye wayes and hedges and compell the to come in that my housse maye be filled.
24 Kwamaana nawaambia, katika wale walioalikwa wa kwanza hapana atakayeonja sherehe yangu. '
For I saye vnto you that none of those men which were bidde shall tast of my supper.
25 Sasa umati mkubwa walikuwa wanakwenda pamoja naye, naye akageuka na akawaambia,
Ther went agreate copany with him and he turned and sayde vnto them:
26 'Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, mama yake, mke wake, watoto wake, ndugu zake waume na wanawake- ndio, na hata maisha yake pia -hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
If a man come to me and hate not his father and mother and wyfe and chyldren and brethren and sisters more over and his awne lyfe he cannot be my disciple.
27 Mtu asipochukua msalaba wake na kuja nyuma yangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
And whosoever beare not his crosse and come after me cannot be my disciple.
28 Maana ni nani kati yenu, ambaye anatamani kujenga mnara hataketi kwanza akadirie gharama kwa mahesabu kama ana kile anachohitaji ili kukamilisha hilo?
Which of you disposed to bilde a toure sytteth not doune before and counteth ye cost whether he have sufficient to performe it?
29 Vinginevyo, baada ya kuweka msingi na kushindwa kumaliza, wote walioona wataanza kumdhihaki,
lest after he hath layde ye foundacion and is not able to performe it all yt beholde it beginne to mocke him
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.'
sayinge: this man beganne to bilde and was not able to make an ende.
31 Au mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine katika vita, ambae hatakaa chini kwanza na kuchukua ushauri kuhusu kama ataweza, pamoja na watu elfu kumi kupigana na mfalme mwingine anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?
Or what kynge goeth to make batayle agaynst another kinge and sitteth not doune fyrst and casteth in his mynde whether he be able wt ten thousande to mete him that cometh agaynst him wt. xx thousand.
32 Na kama sivyo, wakati jeshi la wengine bado liko mbali, hutuma balozi kutaka masharti ya amani.
Or els whyll ye other is yet a greate waye of he will sende embasseatours and desyre peace.
33 Kwa hiyo basi, yeyote kati yenu ambaye hataacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
So lykewyse none of you yt forsaketh not all yt he hath can be my disciple.
34 Chumvi ni nzuri, lakini ikiwa Chumvi imepoteza ladha yake, jinsi gani inaweza kuwa chumvi tena?
Salt is good but yf salt have loste hyr saltnes what shall be seasoned ther with?
35 Haina matumizi kwa udongo au hata kwa mbolea. hutupwa mbali. Yeye aliye na masikio ya kusikia, na asikie.”
It is nether good for ye londe nor yet for ye donge hill but men cast it out at ye dores. He yt hath eares to heare let him heare.

< Luka 14 >