< Luka 14 >
1 Iltokea siku ya Sabato, alipokua akienda nyumbani kwa mmoja wa viongozi wa Mafarisayo kula mkate, nao walikuwa wakimchunguza kwa karibu.
It happened on the Sabbath Day when he went into the house of a certain ruler among Pharisees to take a meal, that they were watching him.
2 Tazama, pale mbele yake alikuwa mtu ambaye anasumbuliwa na uvimbe.
And lo! there was in front of him a man who had dropsy.
3 Yesu aliuliza wataalam katika sheria ya Wayahudi na Mafarisayo, “Je, ni halali kumponya siku ya Sabato, au sivyo?”
So Jesus questioned the lawyers and the Pharisees, "Is it lawful to heal on the Sabbath Day or not?"
4 Lakini wao walikuwa kimya, kwahiyo Yesu akamshika, akamponya na kumruhusu aende zake.
They kept silent. Then Jesus took him and healed him and let him go.
5 Naye akawaambia, “Ni nani kati yenu ambaye ana mtoto au ng'ombe anatumbukia kisimani siku ya Sabato hata mvuta nje mara moja?”
And to them he said, "Which of you when an ox or ass has fallen into a well, will at once pull him out on the Sabbath Day?"
6 Wao hawakuwa na uwezo wa kutoa jibu kwa mambo haya.
They could not answer this.
7 Wakati Yesu alipogundua jinsi wale walioalikwa kwamba wamechagua viti vya heshima, akawaambia mfano, akiwaambia,
He told a parable to the guests when he noticed how they began choosing the best seats. He said to them.
8 “Wakati mnapoalikwa na mtu harusini, usiketi katika nafasi za heshima, kwa sababu inawezekana amealikwa mtu ambaye ni wakuheshimiwa zaidi kuliko wewe.
"When you are invited by any one to a marriage-feast, do not sit down in the best seat, lest a guest more distinguished than yourself has been invited, and your host come to you and say,
9 Wakati mtu aliyewaalika ninyi wawili akifika, atakuambia wewe, “mpishe mtu huyu nafasi yako,” na kisha kwa aibu utaanza kuchukua nafasi ya mwisho.
"‘Give place to this man,’ and then with mortification you proceed to take the lowest place.
10 Lakini wewe ukialikwa, nenda ukakae mahali pa mwisho, ili wakati yule aliyekualika akija, aweze kukuambia wewe, `Rafiki, nenda mbele zaidi.” ndipo utakuwa umeheshimika mbele ya wote walioketi pamoja nawe mezani.
"But when you are invited, go and sit down in the lowest place, so that when your host arrives he may say to you, ‘My friend, come up higher.’ Then you will be honored before the other guest.
11 Kwa maana kila ajikwezaye atashushwa, na yeye ajishushae atakwezwa. '
"For every one who exalts himself shall be humbled, and he who humbles himself shall be exalted."
12 Yesu pia alimwambia mtu aliyemwalika, 'Unapotoa chakula cha mchana au cha jioni, usiwaalike rafiki zako au ndugu zako au jamaa zako au majirani zako matajiri, ili kwamba wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo.
Also to his host who had invited him, he continued, saying. "When you are making a dinner-party or a supper, do not invite your friends, or your brothers, or your relatives, or your rich neighbors, lest it chance that they invite you in return, and a recompense be made by you.
13 Badala yake, unapofanya sherehe, waalike maskini, vilema, viwete na vipofu,
"But when you make a reception, invite the poor, the maimed, the lame, the blind.
14 na wewe utabarikiwa, kwa sababu hawawezi kukulipa. Kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.”
"Then you will be blessed, because they have no means to repay you, but you shall be paid in the Resurrection of the Just."
15 Wakati mmoja wa wale walioketi mezani pamoja na Yesu aliposikia hayo, naye akamwambia, “Amebarikiwe yule atakayekula mkate katika Ufalme wa Mungu!”
One of his fellow guest who was listening to him, said to him, "Blessed are those who eat bread in the kingdom of God."
16 Lakini Yesu akamwambia, “Mtu mmoja aliandaa sherehe kubwa, akaalika watu wengi.
Jesus answered. "A certain man was making a great feast to which he invited many guests.
17 Wakati sherehe ilipokuwa tayari, alimtuma mtumishi wake kuwaambia wale walioalikwa, `'Njooni, kwa sababu vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.'
"At dinnertime he sent his slave to say to those who had been invited, ‘Come, for all things are now ready.’
18 Wote, wakaanza kuomba radhi. Wa kwanza akamwambia mtumishi, 'Nimenunua shamba, lazima niende kuliona. Tafadhali unisamehe.'
"And they all, without exception, proceeded to excuse themselves. The first told him. ‘I have bought a field, and must needs go and see it. Pray have me excused.’
19 Na mwingine akasema, `'Nimenunua jozi tano za ng'ombe, na mimi naenda kuwajaribu. Tafadhali uniwie radhi.'
"The second said. ‘I have bought five yolk of oxen and am on my way to try them. I pray that you will have me excused.’
20 Na mtu mwingine akasema, 'Nimeoa mke, kwa hiyo siwezi kuja.'
"‘I have taken a wife,’ said the another, ‘and for that reason I am unable to come.’
21 Mtumishi akarudi na kumwambia bwana wake mambo hayo. Yule mwenye nyumba alikasirika akamwambia mtumishi wake, `'Nenda upesi mitaani na katika vichochoro vya mji ukawalete hapa maskini, vilema, vipofu na walemavu.”
"So the slave came and presented all these answers to his master. Then the master of the house was indignant, and said to his slave. ‘Go out, quickly, into the streets and alleys of the city, and bring in hither the poor, the maimed, the blind, the lame.’
22 Mtumimishi akasema, `Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa bado kuna nafasi.'
"And the slave said, ‘My master, your orders have been carried out, but yet there is room.’
23 Bwana akamwambia mtumishi, 'Nenda katika njia kuu na vichochoro na uwashurutishe watu waingie, ili nyumba yangu ijae.
"Said the master to his slave. ‘Go out into the roads and the hedges, and make them come in, so that my house may be filled.
24 Kwamaana nawaambia, katika wale walioalikwa wa kwanza hapana atakayeonja sherehe yangu. '
"‘For I tell you that not one of those invited guests shall taste my supper.’"
25 Sasa umati mkubwa walikuwa wanakwenda pamoja naye, naye akageuka na akawaambia,
Great crowds were along with him, and he turned to them and said.
26 'Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, mama yake, mke wake, watoto wake, ndugu zake waume na wanawake- ndio, na hata maisha yake pia -hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
"If any one comes to me and does not hate father and his mother, his wife and children, his brothers and sisters, yes, and his own very life also, he cannot be a disciple of mine.
27 Mtu asipochukua msalaba wake na kuja nyuma yangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
"Whoever does not carry his own cross and come after me, cannot be a disciple of mine.
28 Maana ni nani kati yenu, ambaye anatamani kujenga mnara hataketi kwanza akadirie gharama kwa mahesabu kama ana kile anachohitaji ili kukamilisha hilo?
"Which of you who is desirous of building a tower, does not sit down first and count the cost, to see if he has the means to complete it?
29 Vinginevyo, baada ya kuweka msingi na kushindwa kumaliza, wote walioona wataanza kumdhihaki,
"Lest it happen that after he has laid the foundations and is unable to complete it, all who see it shall begin to jeer at him saying,
30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.'
"‘This fellow began to build and could not finish.’
31 Au mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine katika vita, ambae hatakaa chini kwanza na kuchukua ushauri kuhusu kama ataweza, pamoja na watu elfu kumi kupigana na mfalme mwingine anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?
"Or what king as he goes forth to join battle with another king in war does not sit down first and deliberate whether he can meet with ten thousand men the one who is advancing against him with twenty thousand?
32 Na kama sivyo, wakati jeshi la wengine bado liko mbali, hutuma balozi kutaka masharti ya amani.
"If he cannot, while the other king is yet a great way off, he sends an embassy to ask conditions of peace.
33 Kwa hiyo basi, yeyote kati yenu ambaye hataacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
"Just so any one of you who does not renounce all that he has cannot be my disciple.
34 Chumvi ni nzuri, lakini ikiwa Chumvi imepoteza ladha yake, jinsi gani inaweza kuwa chumvi tena?
"Salt is good, but if even the salt have lost its flavor, with what shall it be seasoned?
35 Haina matumizi kwa udongo au hata kwa mbolea. hutupwa mbali. Yeye aliye na masikio ya kusikia, na asikie.”
"It is fit neither for the land nor the dung-hill; men cast it out. He who has ears to hear let him listen to this!"