< Luka 13 >
1 Kwa wakataihuo huo, kulikuwa na baadhi watu waliomtaarifu juu ya Wagalilaya ambao Pilato aliwaua na kuchanganya damu yao na sadaka zao.
En ce moment même, il se trouva là quelques personnes qui apprirent à Jésus la nouvelle de ces Galiléens, dont Pilate avait mêlé le sang à celui de leurs sacrifices?
2 Yesu akajibu na kuwaambia, “Je mwadhani kuwa Wagalilaya hao walikuwa na dhambi kuliko Wagalilaya wengine wote ndiyo maana wamepatwa na mabaya hayo?
Et lui, prenant la parole, leur dit: «Croyez-vous que ces Galiléens fussent de plus grands pécheurs que les autres Galiléens, parce qu'ils ont souffert de la sorte?
3 Hapana, nawaambia, lakini msipotubu, nanyi mtaangamia vivyo hivyo.
— Non, vous dis-je; mais si vous ne vous repentez, vous périrez tous semblablement.
4 Au wale watu kumi na nane katika Siloamu ambao mnara ulianguka na kuwaua, mnafikiri wao walikuwa wenye dhambi zaidi kuliko watu wengine katika Yerusalemu?
Ou bien, croyez-vous que ces dix-huit personnes sur qui la tour est tombée, à Siloé, et qu'elle a tuées, fussent plus coupables que toutes celles qui habitent Jérusalem?
5 Hapana, mimi nasema, lakini kama msipotubu, ninyi nyote pia mtaangamia.
— Non, vous dis-je; mais si vous ne vous repentez, vous périrez tous semblablement.»
6 Yesu aliwaambia mfano huu, “Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake na alikwenda kutafuta matunda juu yake lakini hakupata.
Il ajouta cette comparaison: «Un homme avait un figuier planté dans sa vigne; il alla y chercher du fruit, et n'en trouva point.
7 Akamwambia mtunza bustani, 'Tazama, kwa miaka mitatu nimekuja na kujaribu kutafuta matunda kwenye mtini huu lakini sikupata. Uukate. Kwani ulete uharibifu wa ardhi?
Il dit au vigneron: «Voici trois ans que je viens chercher du fruit à ce figuier et que je n'en trouve point: coupe-le. Pourquoi occupe-t-il la terre inutilement?»
8 Mtunza bustani akajibu na kusema, 'uache mwaka huu ili niupalilie na kuweka mbolea juu yake.
Le vigneron répondit: «Seigneur, laisse-le encore cette année. Je creuserai tout autour et j'y mettrai du fumier;
9 Kama ukizaa matunda mwaka ujao, ni vema; lakini kama hautazaa, uukate!”'
peut-être portera-t-il du fruit; sinon tu le couperas l'an prochain.»
10 Sasa Yesu alikuwa akifundisha katika mojawapo ya Masinagogi wakati wa Sabato.
Un jour de sabbat, Jésus enseignait dans une synagogue,
11 Tazama, alikuwepo mama mmoja ambaye kwa miaka kumi na minane alikuwa na rohomchafu wa udhaifu, na yeye alikuwa amepinda na hana uwezo kabisa wa kusimama.
et il vint une femme, qui, depuis dix-huit ans, était possédée d'un esprit qui la rendait faible: elle était toute voûtée, et ne pouvait absolument pas se redresser.
12 Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umewekwa huru kutoka kwenye udhaifu wako.”
Jésus la voyant, l'appela, et lui dit: «Femme, tu es délivrée de ta faiblesse; »
13 Akaweka mikono yake juu yake, na mara mwili wake akajinyoosha na akamtukuza Mungu.
et il lui imposa les mains: à l'instant elle se redressa, et glorifia Dieu.
14 Lakini mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo mtawala akajibu akawambia makutano, “Kuna siku sita ambazo ni lazima kufanya kazi. Njoni kuponywa basi, si katika siku ya Sabato. '
Mais le président de la synagogue, fâché de ce que Jésus avait fait cette guérison le jour du sabbat, prit la parole, et dit à la foule: «Il y a six jours pour travailler; venez-donc vous faire guérir en ces jours-là, et non pas le jour du sabbat.»
15 Bwana akamjibu na akasema, “wanafiki! Hakuna kila mmoja wenu kufungua punda wako au ng'ombe kutoka zizini na kuwaongoza kumpeleka kunywa siku ya Sabato?
Mais le Seigneur lui répondit: «Hypocrites, est-ce que chacun de vous, le jour du sabbat, ne délie pas de la crèche son boeuf ou son âne, pour le mener boire?
16 Hivyo pia binti wa Abrahamu, ambaye Shetani amemfunga kwa miaka kumi na minane, je haikumpasa kifungo chake kisifunguliwe siku ya sabato?”
Et cette fille d'Abraham, que Satan tient liée depuis dix-huit ans, il ne fallait donc pas la délivrer de cette chaîne le jour du sabbat!»
17 Alipokuwa akisema maneno hayo, wale wote waliompinga waliona aibu, bali makutano wote wa wengine walishangilia kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyotenda.
Cette réponse couvrit de confusion tous ses adversaires, et le peuple se réjouissait de toutes les merveilles que Jésus faisait.
18 Yesu akasema, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini, na naweza kuulinganisha na nini?
Il ajouta donc: «A quoi ressemble le royaume de Dieu, et à quoi le comparerai-je?
19 Ni kama mbegu ya haradari aliyoitwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake, na ikamea ikawa mti mkubwa, na ndege wa mbinguni wakajenga viota vyao katika matawi yake.
Il est semblable à un grain de moutarde qu'un homme a pris et a jeté dans son jardin: le grain a poussé, il est devenu un arbre, et les oiseaux du ciel se sont abrités dans ses branches.»
20 Tena akasema, “Niufananishe na nini ufalme wa Mungu?
Il dit encore: «A quoi comparerai-je le royaume de Dieu?
21 Ni kama chachu ambayo mwanamke aliichukua na kuchanganyakwenye vipimo vitatu vya unga hata ukaumuka.”
Il est semblable à du levain qu'une femme a pris et mis dans trois mesures de farine, jusqu’à ce que tout ait levé.»
22 Yesu alitembelea kila mji na kijiji njiani akielekea Yerusalemu na kuwafundisha.
Et Jésus traversait les villes et les villages, enseignant, et faisant route vers Jérusalem.
23 Mtu mmoja akauliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?” Hivyo akawaambia,
Quelqu'un lui dit: «N'y a-t-il que peu de personnes de sauvées?» Il répondit:
24 “Jitahidi kuingia kwa kupitia mlango mwembamba, kwa sababu wengi watajaribu na hawataweza kuingia.
«Efforcez- vous d'entrer par la porte étroite; car beaucoup, je vous le dis, chercheront à entrer, et ne le pourront pas.
25 Mara baada ya mmiliki wa nyumba kusimama na kufunga mlango, basi mtasimama nje na kupiga hodi mlangoni na kusema, Bwana, Bwana, tufungulie yeye atajibu na kuwaambia, siwajui ninyi wala mtokako.'
Une fois que le maître de la maison se sera levé, et aura fermé la porte, si vous êtes dehors, et que vous commenciez à heurter, en disant: «Seigneur, Seigneur, ouvre-nous; » il vous dira: «Je ne sais d'où vous êtes.»
26 Ndipo mtasema, Tulikula na kunywa mbele yako na wewe ulifundisha katika mitaa yetu.”
Alors vous vous mettrez à dire: «Nous avons mangé et bu avec toi; c'est dans nos places publiques que tu as enseigné; »
27 Lakini yeye atawajibu, `nawaambia, siwajui mtokako, ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!'
et il répondra: «Je vous le dis, je ne sais d'où vous êtes; éloignez-vous de moi, vous tous, ouvriers d'iniquité.»
28 Kutakuwa na kilio na kusaga meno wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mumetupwa nje.
C'est alors qu'il y aura des pleurs et des grincements de dents, quand vous verrez Abraham, Isaac et Jacob, et tous les prophètes, dans le royaume de Dieu, et que vous serez jetés dehors.
29 Watafika kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini, na kupumzika katika meza ya chakula cha jioni katika ufalme wa Mungu.
Il viendra de l'orient et de l'occident, du nord et du midi, des gens qui seront à table dans le royaume de Dieu.
30 Na tambua hili, wa mwisho ni wa kwanza na wa kwanza atakuwa wa mwisho.”
Et voici, il y en a des derniers qui seront les premiers, et des premiers qui seront les derniers.»
31 Muda mfupi baadaye, baadhi ya Mafarisayo walikuja na kumwambia, “Nenda na ondoka hapa kwa sababu Herode anataka kukuua.”
Ce même jour, quelques pharisiens vinrent dire à Jésus: «Pars, éloigne-toi d'ici, parce qu'Hérode veut te faire mourir.»
32 Yesu akasema, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, `Tazama, ninawafukuza pepo na kufanya uponyaji leo na kesho, na siku ya tatu nitatimiza lengo langu.
Il leur dit: «Allez dire à ce renard: Voici, je chasse les démons et je fais des guérisons aujourd'hui et demain; et après-demain j'ai fini;
33 Katika hali yoyote, ni muhimu kwa ajili yangu kuendelea leo, kesho, na siku iliyofuata, kwa vile haikubaliki kumuua nabii mbali na Yerusalemu.
seulement il faut qu'aujourd'hui et demain, et après-demain, je poursuive ma route, car il ne convient pas qu'un prophète périsse hors de Jérusalem.
34 Yerusalemu, Yerusalemu, nani anawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu. Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wenu kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini humkulitaka hili.
Jérusalem, Jérusalem, toi qui tues les prophètes et qui lapides ceux qui te sont envoyés, combien de fois j'ai voulu rassembler tes enfants comme une poule rassemble sa couvée sous ses ailes, et vous ne l'avez pas voulu!
35 Tazama, nyumba yako imetelekezwa. Nami nawaambia, hamuwezi kuniona hata mtakaposema 'Amebarikiwa huyo ajaye kwa jina la Bwana.'”
Voici, votre maison va vous être laissée, et je vous dis que vous ne me verrez plus, jusqu’à ce que le temps vienne, où vous direz: «Béni soit celui qui vient au nom du Seigneur!»