< Luka 12 >

1 Kwa wakati huo, maelfu mengi ya watu walikusanyika pamoja, kiasi cha kuanza kukanyagana, akaanza kusema na wanafunzi wake kwanza, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo ambayo ni unafiki”
As ther gadered together an innumerable multitude of people (in so moche that they trood one another) he began to saye vnto his disciples: Fyrst of all beware of the leve of the Pharises which is ypocrisy.
2 Na hapatakuwepo na siri iliyofichika ambayo haitafunuliwa, wala jambo lililofichwa ambalo halitajulikana.
For ther is no thinge covered that shall not be vncovered: nether hyd that shall not be knowen.
3 Na lolote mlilolisema katika giza, litasikiwa katika mwanga. Na yoyote mliyoyasema kwenye sikio ndani ya vyumba vyenu vya ndani vilivyofungwa yatatangazwa juu ya paa la nyumba.
For whatsoever ye have spoken in in darknes: that same shalbe hearde in light. And that which ye have spoken in the the eare eve in secret places shalbe preached even on the toppe of the housses.
4 Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili na kisha hawana kitu kingine cha kufanya,
I saye vnto you my fredes: Be not afrayde of them that kyll the body and after that have no moare that they can do.
5 Lakini nitawaonya mtakaye mwogopa. Mwogopeni yule ambaye baada ya kuwa ameua, ana mamlaka ya kutupa jehanamu. Ndiyo, nawaambiani ninyi, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
But I will shewe you whom ye shall feare. Feare him which after he hath killed hath power to cast into hell. Ye I saye vnto you him feare. (Geenna g1067)
6 Je shomoro watano hawauzwi kwa sarafu mbili? hata hivyo hakuna hata mmoja wao atakayesahaulika mbele za Mungu.
Are not five sparowes bought for two farthinges? And yet not one of them is forgotten of God.
7 Lakini mjue kuwa, nywele za vichwa vyenu vimehesabiwa. Msiogope. Ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
Also even the very heres of youre heedes are nombred. Feare not therfore: ye are moare of value then many sparowes.
8 Ninawaambia, yeyote atakayenikiri Mimi mbele za watu, Mwana wa Adamu atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
I saye vnto you: Whosoever confesseth me before men eve him shall ye sonne of man confesse also before ye angels of God.
9 Lakini yeyeyote atakayenikana mbele za watu naye atakanwa mbele ya Malaika wa Mungu.
And he that denyeth me before men: shalbe denyed before ye angels of God.
10 Yeyote atakayesema neno baya juu ya Mwana wa Adamu, atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu, hatasamehewa.
And whosoever speaketh a worde agaynst ye sonne of ma it shalbe forgeven him. But vnto him yt blasphemeth the holy goost it shall not be forgeven.
11 Watakapowapeleka mbele za wakuu wa masinagogi, watawala, na wanye mamlaka, msiogope juu na namna ya kuongea katika kujitetea au nini mtakachosema,
When they bringe you vnto the synagoges and vnto the rulers and officers take no thought how or what thinge ye shall answer or what ye shall speake.
12 kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha namna mtakavyosema kwa wakati huo.”
For the holy goost shall teache you in the same houre what ye ought to saye.
13 Mtu mmoja katika kusanyiko akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie sehemu ya uruthi wangu.”
One of the company sayde vnto hym: Master byd my brother devide the enheritauce with me.
14 Yesu akamjibu, ni nani aliye niweka kuwa mwamuzi na mpatanishi kati yenu?
And he sayde vnto him: Man who made me a iudge or a devider over you?
15 Ndipo akawaambia, Jihadharini na kila namna ya tamaa, kwa sababu uzima wa mtu hauko katika wingi wa vitu alivyo navyo.”
Wherfore he sayde vnto them: take hede and beware of covetousnes. For no mannes lyfe stondeth in the aboundaunce of the thinges which he possesseth.
16 Yesu akawaambia mfano, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana,
And he put forth a similitude vnto them sayinge: The groude of a certayne riche ma brought forth frutes plenteously
17 na akajiuliza ndani yake, akisema, nitafanyaje kwani sina mahali pa kuhifadhi mazao yangu?
and he thought in himsilfe sayinge: what shall I do? because I have noo roume where to bestowe my frutes?
18 Akasema, nitafanya hivi. Nitavunja ghala zangu ndogo na kujenga iliyo kubwa, na kuyahifadhi mazao yangu yote na vitu vingine.
And he sayde: This will I do. I will destroye my barnes and bilde greater and therin will I gadder all my frutes and my goodes:
19 Nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, umejiwekea akiba ya vitu vingi kwa miaka mingi. Pumzika, ule, unywe na kustarehe.”
and I will saye to my soule: Soule thou hast moch goodes layde vp in stoore for many yeares take thyne ease: eate drinke and be mery.
20 Lakini Mungu akamwambia, ewe mtu mpumbavu, usiku wa leo wanahitaji roho kutoka kwako, na vitu vyote ulivyoviandaa vitakuwa vya nini?
But God sayde vnto him: Thou fole this night will they fetche awaye thy soule agayne from the. Then whose shall thoose thinges be which thou hast provyded?
21 Ndivyo itakavyokuwa kwa kila mtu anayejiwekea mali na si kujitajirisha kwa ajili ya Bwana.
So is it with him that gadereth ryches and is not ryche in God.
22 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Kwa hiyo nawaambia msihofu juu ya maisha yenu ya kuwa mtakula nini au juu ya miili yenu ya kuwa mtavaa nini
And he spake vnto his disciples: Therfore I saye vnto you: take no thought for youre lyfe what ye shall eate nether for youre body what ye shall put on.
23 Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
The lyfe is moare then meate and the bodye is moare then rayment.
24 Angalieni ndege wa angani, hawalimi wala hawavuni. Hawana chumba wala ghala ya kuhifadhia, lakini Baba yenu huwalisha. Ninyi si bora zaidi kuliko ndege!
Considre the ravens for they nether sowe nor repe which nether have stoorehousse ner barne and yet God fedeth them. How moche are ye better then the foules.
25 Ni yupi kati yenu ambaye akijisumbua ataweza kuongeza dhiraa moja katika maisha yake?
Which of you with takynge thought can adde to his stature one cubit?
26 Ikiwa basi hamuwezi kufanya hicho kitu kidogo kilicho rahisi kwa nini basi kusumbukia hayo mengine?
Yf ye then be not able to do that thinge which is least: why take ye thought for the remmaunt?
27 Angalieni maua -yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayasokoti. Lakini nawaambia, hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kama mojawapo ya haya,
Considre the lylies how they growe: They laboure not: they spyn not: and yet I saye vnto you that Salomon in all this royalte was not clothed lyke to one of these.
28 Kama Mungu huyavika vizuri majani ya kondeni, ambayo leo yapo, na kesho hutupwa kwenye moto. Je si zaidi atawavika ninyi? enyi wa imani haba!
Yf the grasse which is todaye in the felde and tomorowe shalbe cast into the fornace God so clothe: how moche moore will he clothe you o ye endued wt litell faith?
29 Msisumbukie juu ya kuwa mtakula nini au mtakunywa nini, wala msiwe na hofu.
And axe not what ye shall eate or what ye shall drinke nether clyme ye vp an hye
30 Kwa kuwa Mataifa yote ya dunia husumbukia mambao yao. Na Baba yenu anajua ya kuwa mnahitaji hayo.
for all suche thinges the hethen people of the worlde seke for. Youre father knoweth that ye have nede of suche thinges.
31 Lakini tafuteni ufalme wake kwanza, na hayo mengine mtazidishiwa,
Wherfore seke ye after the kyngedome of God and all these thinges shalbe ministred vnto you.
32 msiogope, enyi kundi dogo, kwa sababu Baba yenu anafurahia kuwapa ninyi huo ufalme.
Feare not litell floocke for it is youre fathers pleasure to geve you a kingdome.
33 Uzeni mali zenu na mkawape maskini, mjifanyie mifuko isiyoishiwa hazina ya mbinguni isiyokoma, sehemu ambapo wezi hawatakaribia wala nondo haitaweza kuharibu.
Sell that ye have and geve almes. And make you bagges which wexe not olde and treasure that fayleth not in heaven where noo these commeth nether moth corrupteth.
34 Kwa kuwa palipo na hazina yako, ndipo na roho yako itakapokuwepo.
For where youre treasure is there will youre hertes be also.
35 Nguo zenu ndefu ziwe zimefungwa kwa mkanda, na taa zenu zihakikishwe kuwa zinaendelee kuwaka,
Let youre loynes be gerdde about and youre lightes brennynge
36 na muwe kama watu wanaomtazamia Bwana wao kutoka kwenye sherehe ya harusi, ili kwamba akija na kupiga hodi, wataweze kumfungulia mlango kwa haraka.
and ye youre selves lyke vnto men that wayte for their master when he will returne fro a weddinge: that assone as he cometh and knocketh they maye ope vnto him.
37 Wamebarikiwa wale watumishi, ambao Bwana atawakuta wako macho. Hakika atafunga nguo yake ndefu kwa mkanda, kisha atawaketisha chini kwa chakula, na kisha kuwahudumia.
Happy are those servauntes which the Lorde when he cometh shall fynde wakynge. Verely I saye vnto you he will gerdde him selfe about and make them sit doune to meate and walke by and minister vnto them.
38 Kama Bwana atakuja kwa zamu ya pili ya ulinzi ya usiku, au hata zamu ya tatu ya ulinzi, na kuwakuta wakiwa tayari, itakuwa ni heri kwa hao watumishi.
And yf he come in the seconde watche ye if he come in the thyrde watche and shall fynde them soo happy are those servauntes.
39 Zaidi ya hayo, mjue hili, kama bwana mwenye nyumba angelijua saa ambayo mwivi anakuja, asingeliruhusu nyumba yake ifunjwe.
This vnderstonde that yf the good man of the housse knewe what houre ye these wolde come he wolde suerly watche: and not suffer his housse to be broken vp.
40 Iweni tayari pia kwani hamjui ni wakati gani mwana wa Adamu atarudi.
Be ye prepared therfore: for the sonne of man will come at an houre when ye thinke not.
41 Petro akasema, “Bwana, watuambia sisi wenyewe hii mifano, au unamwambia kila mtu?
Then Peter sayde vnto him: Master tellest thou this similitude vnto vs or to all men?
42 Bwana akawaambia, “Ni nani mtumwa mwaminifu au mwenye hekima ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wengine, ili awagawie chakula chao kwa wakati mwafaka?
And the Lorde sayde: If there be any faith full servaut and wise whom his Lorde shall make ruler over his housholde to geve them their duetie of meate at due season:
43 Amebarikiwa mtumishi yule, ambaye bwana wake akija atamkuta akifanya yale aliyoagizwa.
happy is that servaunt whom his master when he cometh shall finde soo doinge.
44 Hakika nawaambia ninyi ya kuwa atamweka juu ya mali yake yote.
Of a trueth I saye vnto you: that he will make him ruler over all that he hath.
45 Lakini Mtumishi yule akisema moyoni mwake, “bwana wangu anachelewa kurudi; hivyo akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, kisha akaanza kula, kunywa na kulewa,
But and yf the evyll servaunt shall saye in his hert: My master wyll differre his cominge and shall beginne to smyte the servauntes and maydens and to eate and drinke and to be dronken:
46 bwana wake yule mtumwa atakuja katika siku asiyotegemea na saa asiyoijua, naye atamkata vipande vipande na kumuweka katika sehemu pamoja na wasiokuwawaaminifu'
the Lorde of that servaunt will come in a daye when he thinketh not and at an houre when he is not ware and will devyde him and will geve him his rewarde with the vnbelevers.
47 Mtumishi, anayejua mapenzi ya bwana wake, naye hakujiandaaa wala hakufanya sawa sawa na mapenzi yake, atapigwa viboko vingi.
The servaut that knewe his masters will and prepared not him selfe nether dyd accordinge to his will shalbe bete with many strypes.
48 Lakini mtumishi asiyejua mapenzi ya bwana wake, lakini akafanya yanayostahili adhabu, atapigwa viboko vichache. Kwa kuwa yeye aliyepewa vingi, vingi hudaiwa kutoka kwake, na yeye aliyeaminiwa kwa vingi, kwake vitadaiwa vingi zaidi.
But he that knewe not and yet dyd committe thinges worthy of strypes shalbe beaten with feawe strypes. For vnto whom moche is geven of him shalbe moche requyred. And to whom men moche commyt the moare of him will they axe.
49 Nimekuja kuwasha moto duniani, na natamani iwe umekwishawaka,
I am come to sende fyre on erth: and what is my dysyre but that it were all redy kyndled?
50 Lakini nina ubatizo ambao nitabatizwa, na nina huzuni mpaka utkapokamilika!
Not with stondinge I must de baptised with a baptyme: and how am I payned till it be ended?
51 Je mnafikiri kuwa nimekuja kuleta amani duniani? Hapana, Nawaambieni, badala yake nimeleta mgawanyiko.
Suppose ye that I am come to sende peace on erth? I tell you naye: but rather debate.
52 Tangu sasa na kuendelea kutakuwa na watu watano katika nyumba moja wamegawanyika, na watatu watakuwa kinyume na wawili, na wawili watakuwa kinyume na watatu.
For fro hence forthe ther shalbe five in one housse devided thre agaynst two and two agaynst thre.
53 Watagawanyika, baba atakuwa kinyume na mwanae, na mwanae atakuwa kinyume na babaye, mama atakuwa kinyume na binti yake, na binti atakuwa kinyume na mama yake, Mama mkwe atakuwa kinyume na mkwe wake naye mkwe atakuwa kinyume na mama mkwe wake.
The father shalbe devided agaynst the sonne and the sonne agaynst the father. The mother agaynst the doughter and the doughter agaynst the mother. The motereleawe agaynst hir doughterelawe and the doughterelawe agaynst hir motherelawe.
54 Yesu akawa anawaambia makutano pia, “Mara muonapo mawingu yakitokea magharibi, mnasema nyakati za mvua zimewadia; na ndivyo inavyo kuwa,
Then sayde he to the people: when ye se a cloude ryse out of the west strayght waye ye saye: we shall have a shower and soo it is.
55 Na upepo wa kusini ukivuma, mnasema, Patakuwepo na joto kali, na ndivyo inavyokuwa.
And when ye se the south wynde blow ye saye: we shall have heet and it cometh to passe.
56 Enyi wanafiki, mnaweza kutafsiri mwonekano wa nchi na anga, lakini inakuwaje hamuwezi kuutafsiri wakati uliopo?
Ypocrites ye can skyll of the fassion of the erth and of the skye: but what is ye cause that ye canot skyll of this time?
57 Ni kwa nini kila mmoja wenu asipambanue lililo sahihi kwake kulifanya wakati ambapo angali na nafasi ya kufanya hivyo?
Ye and why iudge ye not of youre selves what is righte?
58 Maana mkienda na mshitaki wako mbele ya hakimu, jitahidi kupatana na mshitaki wako mungali bado mko njiani asije akakupeleka kwa hakimu, na hakimu akupeleka kwa ofisa, na ofisa akakutupa gerezani.
Whill thou goest with thyne adversary to the ruler: as thou arte in the waye geve diligence that thou mayst be delivered fro him least he bringe the to the iudge and the iudge delyver the to the iaylar and the iaylar cast the in to preson.
59 Nakuambia, hutatoka huko hadi umelipa mpaka senti ya mwisho.
I tell ye thou departest not thence tyll thou have made good ye vtmost myte.

< Luka 12 >