< Luka 10 >
1 Baada ya mambo hayo, Bwana akachagua sabini wengine, na kuwatuma wawili wawili wamtangulie katika kila mji na eneo alilotarajia kwenda.
Now after these things, the Lord appointed seventy others, and sent them out two by two ahead of him to every town and place where he himself was about to go.
2 Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Hivyo basi muombeni Bwana wa mavuno, ili kwamba atume haraka wafanyakazi katika mavuno yake.
He said to them, “The harvest is plentiful, but the laborers are few. Therefore ask the Lord of the harvest to send out laborers into his harvest.
3 Enendeni katika miji. Angalieni, ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu.
Go on your way. See, I send you out as lambs in the midst of wolves.
4 Msibebe mfuko wa pesa, wala mikoba ya wasafiri, wala viatu, wala msimsalimie yeyote njiani.
Do not carry a money bag, or a traveler's bag, or sandals, and greet no one on the road.
5 Katika nyumba yeyote mtakayo ingia, kwanza semeni, 'Amani iwe katika nyumba hii.'
Whatever house you enter, first say, 'May peace be on this house!'
6 kama mtu wa amani yupo pale, amani yenu itabaki juu yake, lakini kama sivyo, itarudi kwenu.
If a person of peace is there, your peace will rest upon him, but if not, it will return to you.
7 Bakini katika nyumba hiyo, kuleni na mnywe watakachokitoa, kwa maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msihame kutoka nyumba hii kwenda nyingine.
Remain in that same house, eating and drinking what they provide, for the laborer is worthy of his wages. Do not move around from house to house.
8 Mji wowote muuingiao, na wakawapokea, kuleni chochote kitakachowekwa mbele yenu,
Whatever town you enter, and they receive you, eat what is set before you,
9 na ponyeni wagonjwa waliomo humo. Semeni kwao, 'Ufalme wa Mungu umekuja karibu yanu'
and heal the sick that are there. Say to them, 'The kingdom of God has come close to you.'
10 Lakini katika mji wowote mtakaoingia, na wasiwapokee, nendeni nje katika barabara na semeni,
Whenever you enter a town and they do not receive you, go out into its streets and say,
11 'Hata vumbi katika mji wenu lililonata miguu mwetu tunalikung'uta dhidi yenu! Lakini tambueni hili, Ufalme wa Mungu umekaribia.'
'Even the dust from your town that clings to our feet we wipe off against you! But know this: The kingdom of God has come near.'
12 Ninawambieni kwamba siku ya hukumu itakuwa ni usitahamilivu zaidi kwa Sodoma kuliko mji huo.
I say to you that on the judgment day it will be more tolerable for Sodom than for that town.
13 Ole kwako Korazini, Ole kwako Bethsaida! Kama kazi kuu zilizo fanyika ndani yako ingalifanyika Tiro na Sidoni, Wangelitubu zamani sana, wakikaa ndani ya nguo za gunia na majivu.
Woe to you, Chorazin! Woe to you, Bethsaida! If the mighty works which were done in you had been done in Tyre and Sidon, they would have repented long ago, sitting in sackcloth and ashes.
14 Lakini itakuwa usitahamilivu zaidi siku ya hukumu kwa Tiro na Sidoni zaidi yenu.
But it will be more tolerable for Tyre and Sidon at the judgment than for you.
15 Wewe Kapernaumu, Unafikiri utainuliwa mpaka Mbinguni? Hapana, utashushwa chini mpaka kuzimu (Hadēs )
You, Capernaum, do you think you will be exalted to heaven? No, you will be brought down to Hades. (Hadēs )
16 Atakaye wasikiliza ninyi anisikiliza mimi, na yeyote atakaye wakataa anikataa mimi, na yeyote anikataaye mimi anmtakaa aliyenituma”
The one who listens to you listens to me, and the one who rejects you rejects me, and the one who rejects me rejects the one who sent me.”
17 Wale sabini walirudi kwa furaha, wakisema, “Bwana, hata mapepo wanatutii katika jina lako.”
The seventy returned with joy, saying, “Lord, even the demons submitted to us in your name.”
18 Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama radi.
Jesus said to them, “I was watching Satan fall from heaven as lightning.
19 Tazama, nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za adui, na hapana chochote kwa njia yoyote kitakachowadhuru.
See, I have given you authority to tread on serpents and scorpions, and over all the power of the enemy, and nothing will in any way hurt you.
20 Hata hivyo msifurahi tu katika hili, kwamba roho zinawatii, lakini furahini zaidi kwamba majina yenu yameandikwa mbinguni.”
Nevertheless do not rejoice only in this, that the spirits submit to you, but rejoice even more that your names are engraved in heaven.”
21 Katika mda uleule alifurahi sana katika Roho Mtakatifu, na kusema, “Ninakusifu wewe, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umeyaficha mambo haya kutoka kwa wenye hekima na akili, na kuyafunua kwa wasio fundishwa, kama watoto wadogo. Ndio, Baba, kwa kuwa ilipendeza katika machoni pako.”
At that same time he rejoiced greatly in the Holy Spirit, and said, “I praise you, Father, Lord of heaven and earth, because you concealed these things from the wise and understanding, and revealed them to those who are untaught, like little children. Yes, Father, for so it was well pleasing in your sight.”
22 “Kila kitu kimekabidhiwa kwangu na Baba yangu, na hakuna afahamuye Mwana ni nani ila Baba, na hakuna afahamuye Baba ni nani ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana hutamani kujifunua kwake.”
“All things have been entrusted to me from my Father, and no one knows who the Son is except the Father, and no one knows who the Father is except the Son and those to whom the Son chooses to reveal him.”
23 Akawageukia wanafunzi, akasema faraghani, “Wamebarikiwa wayaonayo haya ambayo ninyi mnayaona.
Then he turned around to the disciples and said privately, “Blessed are those who see the things that you see.
24 Ninawambia ninyi, kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuona mambo myaonayo, na hawakuyaona, na kusikia kusikia mnayoyaikia, na hawakuyasikia.”
I say to you, many prophets and kings desired to see the things you see, and they did not see them, and to hear the things that you hear, and they did not hear them.”
25 Tazama, mwalimu fulani wa sheria ya Kiyahudi alisimama na kumjaribu, akisema, “Mwalimu, nifanye nini niurithi izima wa milele?” (aiōnios )
Behold, a certain teacher of the Jewish laws stood up so that he might test him, saying, “Teacher, what must I do to inherit eternal life?” (aiōnios )
26 Yesu akamwambia, “Kimeandikwa nini katika sheria? Unaisoma je?”
Jesus said to him, “What is written in the law? How do you read it?”
27 Akajibu akasema, “Utampenda Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote, na jirani yako kama nafsi yako mwenyewe.”
He gave an answer and he said, “You will love the Lord your God with all your heart, with all your soul, with all your strength, and with all your mind, and your neighbor as yourself.”
28 Yesu akasema, “Umejibu kwa usahihi. Fanya hivi na utaishi.”
Jesus said to him, “You have answered correctly. Do this, and you will live.”
29 Lakini mwalimu, akitamani kujihesabia haki mwenyewe, Akamwambia Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
But the teacher, desiring to justify himself, said to Jesus, “Who is my neighbor?”
30 Yesu akijibu akasema, “Mtu fulani alikuwa akitelemka kutoka Yerusalem kwenda Yeriko. Akaangukia kati ya wanyang'anyi, waliomnyang'anya mali yake, na kumpiga na kumuacha karibu akiwa nusu mfu.
Jesus answered him and said, “A certain man was going down from Jerusalem to Jericho. He fell among robbers, who stripped him of his belongings, and beat him, and left him half dead.
31 Kwa bahati kuhani fulani alikuwa akishuka katika njia hiyo, alipo muona alipita upande mwingine.
By chance a certain priest was going down that way, and when he saw him, he passed by on the other side.
32 Vivyo hivyo Mlawi pia, alipofika mahali pale na kumuona, akapita upande mwingine.
Similarly a Levite also, when he came to the place and saw him, passed by on the other side.
33 Lakini Msamaria mmoja, alipokuwa akisafiri, alipita pale alipokuwa mtu huyo. alipomuona, alisukumwa kwa huruma.
But a certain Samaritan, as he journeyed, came to where he was. When he saw him, he was moved with compassion.
34 Alimkaribia na kumfunga vidonda vyake, akimwiga mafuta na divai juu yake. Alimpandisha juu ya mnyama wake, na kumpeleka katika nyumba ya wageni na kumhudumia.
He approached him and bound up his wounds, pouring oil and wine on them. He set him on his own animal, and brought him to an inn, and took care of him.
35 Siku ilyofuata alichukua dinari mbili, na akampatia mmiliki wa nyumba ya wageni na kumwambia, 'Muhudumie na chochote cha ziada utakacho tumia, nitakulipa nitakaporudi.'
The next day he took out two denarii, and gave them to the host, and said, 'Take care of him and whatever extra you spend, when I return, I will repay you.'
36 Ni yupi kati ya hawa watatu, unafikiri, alikuwa ni jirani kwake yeye aliyeangukia kati ya wanyang'anyi?”
Which of these three do you think was a neighbor to him who fell among the robbers?”
37 Mwalimu alisema, “Ni yule aliyeonesha huruma kwake.” Yesu akamwambia, “Nenda na ukafanye vivyo hivyo”
The teacher said, “The one who showed mercy to him.” Jesus said to him, “Go and do the same.”
38 Sasa walipokuwa wakisafiri, waliingia katika kijiji fulani, na mwanamke mmoja jina lake Martha alimkaribisha nyumbani kwake.
Now as they were traveling along, he entered into a certain village, and a certain woman named Martha welcomed him into her house.
39 Alikuwa na dada aliyeitwa Mariamu, aliekaa miguuni pa Bwana na kusikiliza neno lake.
She had a sister named Mary, who sat at the Lord's feet and heard his word.
40 Lakini Martha alijipa shughuli nyingi za kuandaa mlo. Alikwenda kwa Yesu, na kusema, “Bwana, haujali kwamba dada yangu ameniacha nihudumu peke yangu? Hivyo basi mwambie anisaidie.”
But Martha was overly busy with preparing to serve a meal. She came up to Jesus, and said, “Lord, do you not care that my sister left me to serve alone? Therefore tell her to help me.”
41 Lakini Bwana alimjibu na kumwambia, “Martha, Martha, una sumbuka juu ya mambo mengi,
But the Lord answered and said to her, “Martha, Martha, you are anxious about many things,
42 lakini ni kitu kimoja tu cha muhimu. Mariamu amechagua kilicho chema, ambacho hakitaondolewa kutoka kwake.”
but only one thing is necessary. Mary has chosen what is best, which will not be taken away from her.”