< Luka 1 >
1 Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
Plusieurs ayant entrepris d'écrire l'histoire des faits accomplis parmi nous,
2 kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
— tels que nous les ont transmis ceux qui en ont été, dès le commencement, les témoins oculaires, et qui sont devenus ministres de la Parole,
3 Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
— j'ai cru bon, moi aussi, très excellent Théophile, de te les exposer par écrit et dans leur ordre, après m'être exactement informé de tout, depuis l'origine,
4 Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
afin que tu reconnaisses la solidité des enseignements que tu as reçus.
5 Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
Au temps d'Hérode, roi de Judée, il y avait un sacrificateur nommé Zacharie, de la classe d'Abia; sa femme était de la race d'Aaron et s'appelait Élisabeth.
6 Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
Ils étaient tous deux justes devant Dieu, et ils suivaient tous les commandements et toutes les prescriptions du Seigneur d'une manière irréprochable.
7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
Ils n'avaient point d'enfants, parce qu'Elisabeth était stérile; et ils étaient tous deux avancés en âge.
8 Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
Or, il arriva, comme Zacharie remplissait devant Dieu les fonctions du sacerdoce, suivant le rang de sa classe,
9 Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
qu'il fut appelé par le sort, d'après la coutume établie parmi les sacrificateurs, à entrer dans le sanctuaire du Seigneur pour y offrir le parfum.
10 Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
Toute la multitude du peuple était dehors en prière, à l'heure où le parfum était offert.
11 Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
Alors un ange du Seigneur lui apparut, debout à droite de l'autel des parfums.
12 Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
Zacharie, en le voyant, fut troublé, et la frayeur le saisit.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
Mais l'ange lui dit: Ne crains point, Zacharie; car ta prière a été exaucée. Elisabeth, ta femme, t'enfantera un fils, et tu lui donneras le nom de Jean.
14 Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
Il sera pour toi un sujet de joie et d'allégresse, et plusieurs se réjouiront de sa naissance.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
En effet, il sera grand devant le Seigneur; il ne boira ni vin ni cervoise, et il sera rempli du Saint-Esprit dès le sein de sa mère.
16 Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
Il convertira plusieurs des fils d'Israël au Seigneur, leur Dieu;
17 Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
et lui-même marchera devant le Seigneur, dans l'esprit et avec la puissance d'Élie, pour ramener les coeurs des pères vers les enfants, et les rebelles à la sagesse des justes, afin de préparer au Seigneur un peuple bien disposé.
18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
Zacharie dit à l'ange: A quoi reconnaîtrai-je cela? Car je suis vieux, et ma femme est avancée en âge.
19 Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
L'ange lui répondit: Je suis Gabriel, qui me tiens devant Dieu; j'ai été envoyé pour te parler et t'annoncer cette bonne nouvelle.
20 Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
Voici que tu vas devenir muet, et tu ne pourras parler jusqu'au jour où ces choses arriveront, parce que tu n'as pas cru à mes paroles, qui s'accompliront en leur temps.
21 Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
Cependant, le peuple attendait Zacharie, et s'étonnait de ce qu'il s'attardait dans le sanctuaire.
22 Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
Quand il sortit, Zacharie ne pouvait leur parler; et ils comprirent qu'il avait eu quelque vision dans le sanctuaire; il leur faisait des signes, et il demeura muet.
23 Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
Lorsque les jours de son ministère furent achevés, il retourna dans sa maison.
24 Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
Quelque temps après, Elisabeth sa femme, devint enceinte; elle se tint cachée durant cinq mois, et elle disait:
25 “Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
Voilà ce que le Seigneur m'a fait, quand il a jeté les yeux sur moi, pour ôter l'opprobre qui pesait sur moi parmi les hommes.
26 Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
Au sixième mois. Dieu envoya l'ange Gabriel dans une ville de Galilée, appelée Nazareth,
27 kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
auprès d'une vierge fiancée à un homme nommé Joseph, de la maison de David; cette vierge s'appelait Marie.
28 Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
L'ange, étant entré dans le lieu où elle était, lui dit: Je te salue, toi qui as été comblée de grâces; le Seigneur est avec toi.
29 Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
Elle fut troublée de ces paroles, et elle se demandait ce que signifiait cette salutation.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
Alors l'ange lui dit: Ne crains point, Marie; car tu as trouvé grâce devant Dieu.
31 Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
Voici que tu enfanteras et mettras au monde un fils, à qui tu donneras le nom de Jésus.
32 Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
Il sera grand, et il sera appelé le Fils du Très-Haut; et le Seigneur, Dieu, lui donnera le trône de David, son père.
33 Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn )
Il régnera éternellement sur la maison de Jacob, et son règne n'aura pas de fin. (aiōn )
34 Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
Alors Marie dit à l'ange: Comment cela arrivera-t-il, puisque je ne connais point d'homme?
35 Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
L'ange lui répondit: L'Esprit saint viendra sur toi, et la puissance du Très-Haut te couvrira de son ombre; c'est pourquoi aussi, le saint enfant qui naîtra sera appelé le Fils de Dieu.
36 Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
Et voici qu'Elisabeth, ta parente, a aussi conçu un fils en sa vieillesse; c'est ici le sixième mois de celle qui était appelée stérile.
37 Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
Car rien n'est impossible à Dieu!
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
Marie répondit: Me voici: je suis la servante du Seigneur. Qu'il me soit fait selon ta parole! Puis l'ange la quitta.
39 Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
En ces jours-là, Marie, s'étant levée, s'empressa d'aller dans le pays des montagnes, dans, une ville de Juda.
40 Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
Elle entra dans la maison de Zacharie, et salua Elisabeth.
41 Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
Or il arriva, quand Elisabeth eut entendu la salutation de Marie, que le petit enfant tressaillit dans son sein; et Elisabeth fut remplie du Saint-Esprit.
42 Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
Alors élevant la voix, elle s'écria: Tu es bénie entre les femmes, et le fruit de tes entrailles est béni.
43 Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
Et d'où me vient cet honneur, que la mère de mon Seigneur vienne me visiter?
44 Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
Car ta voix, quand tu m'as saluée, n'a pas plus tôt frappé mes oreilles, que le petit enfant a tressailli de joie dans mon sein.
45 Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
Bienheureuse est celle qui a cru; car ce qui lui a été dit de la part du Seigneur aura son accomplissement!
46 Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
Alors Marie dit: Mon âme magnifie le Seigneur,
47 na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
et mon esprit se réjouit en Dieu, qui est mon Sauveur,
48 Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
parce qu'il a jeté les yeux sur la bassesse de sa servante. Et voici que désormais tous les âges m'appelleront bienheureuse;
49 Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
car le Tout-Puissant a fait pour moi de grandes choses. Son nom est saint,
50 Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
et sa miséricorde s'étend d'âge en âge sur ceux qui le craignent.
51 Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
Il a manifesté la vigueur de son bras. Il a dissipé les desseins que les orgueilleux formaient dans leur coeur.
52 Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
Il a renversé de leurs trônes les puissants, et il a élevé les humbles.
53 Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
Il a comblé de biens les affamés, et il a renvoyé les riches les mains vides.
54 Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
Il est venu au secours d'Israël, son serviteur, et il s'est souvenu de sa miséricorde
55 (kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn )
— ainsi qu'il en avait parlé à nos pères — à l'égard d'Abraham et de sa postérité, pour toujours. (aiōn )
56 Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
Marie demeura avec Elisabeth environ trois mois; puis elle s'en retourna dans sa maison.
57 Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
Cependant, le terme d'Elisabeth étant venu, elle enfanta un fils.
58 Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
Ses voisins et ses parents, ayant appris que le Seigneur avait fait éclater en elle la grandeur de sa miséricorde, s'en réjouissaient avec elle.
59 Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
Le huitième jour, ils vinrent pour circoncire l'enfant; ils l'appelaient Zacharie, du nom de son père.
60 Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
Mais sa mère dit: Non! Il sera nommé Jean.
61 Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
Ils lui dirent: Il n'y a personne dans ta famille qui soit appelé de ce nom.
62 Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
Alors ils demandèrent au père, par signes, comment il voulait que l'enfant fût nommé.
63 Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
Zacharie ayant demandé des tablettes, écrivit: Jean est son nom. Et ils furent tous surpris.
64 Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
A l'instant sa bouche s'ouvrit, sa langue se délia, et il parlait, bénissant Dieu.
65 Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
Tous leurs voisins furent remplis de crainte, et l'on s'entretenait de toutes ces choses dans tout le pays des montagnes de la Judée.
66 Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
Tous ceux qui les entendirent les conservèrent dans leur coeur et ils disaient: Que deviendra donc ce petit enfant? Car la main du Seigneur était avec lui.
67 Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
Alors Zacharie, son père, fut rempli de l'Esprit saint. Il prophétisa et il dit:
68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
Béni soit le Seigneur, le Dieu d'Israël, de ce qu'il a visité et racheté son peuple,
69 Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
et nous a suscité un puissant Sauveur dans la maison de David, son serviteur,
70 kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn )
comme il l'avait proclamé par la bouche de ses saints prophètes, dès les anciens temps. (aiōn )
71 Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
Il nous délivre de nos ennemis et de la main de tous ceux qui nous haïssent.
72 Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
Il exerce sa miséricorde envers nos pères et se souvient de sa sainte alliance;
73 kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
car il a fait à Abraham, notre père, le serment de nous accorder cette grâce,
74 Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
qu'après avoir été délivrés de la main de nos ennemis, nous pourrions le servir sans crainte,
75 katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
en sa présence, dans la sainteté et la justice, tous les jours de notre vie.
76 Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
Et toi, petit enfant, tu seras appelé le prophète du Très-Haut; car tu marcheras devant la face du Seigneur, pour préparer ses voies,
77 kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
pour donner à son peuple la connaissance du salut par la rémission de ses péchés.
78 Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
Les entrailles de la miséricorde de notre Dieu se sont émues, et le soleil levant nous a visités d'en haut,
79 kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
pour éclairer ceux qui sont assis dans les ténèbres et l'ombre de la mort, et pour conduire nos pas dans le chemin de la paix.
80 Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.
Or, le petit enfant grandissait et se fortifiait en esprit; et il demeura dans les déserts jusqu'au jour de sa manifestation à Israël.