< Mambo ya Walawi 8 >
1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
L'Éternel parla à Moïse, en disant:
2 “Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
Prends Aaron et ses fils avec lui, les vêtements, l'huile d'onction, le taureau du sacrifice pour le péché, les deux béliers, et la corbeille de pains sans levain;
3 Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
Et convoque toute l'assemblée à l'entrée du tabernacle d'assignation.
4 Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
Moïse fit donc comme l'Éternel lui avait commandé; et l'assemblée fut convoquée à l'entrée du tabernacle d'assignation.
5 “Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
Et Moïse dit à l'assemblée: Voici ce que l'Éternel a commandé de faire.
6 Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
Puis Moïse fit approcher Aaron et ses fils, et les lava avec de l'eau.
7 Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
Et il mit à Aaron la tunique, le ceignit de la ceinture, et le revêtit de la robe; il lui mit l'éphod, et le ceignit de la ceinture de l'éphod, dont il le revêtit.
8 Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
Il lui mit aussi le pectoral, et mit au pectoral l'Urim et le Thummim.
9 Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
Il posa la tiare sur sa tête, et sur le devant de la tiare, la lame d'or, la couronne sainte, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
10 Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
Ensuite Moïse prit l'huile d'onction; il oignit la Demeure, et toutes les choses qui y étaient, et les consacra.
11 Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
Il en fit aspersion sur l'autel par sept fois, et il oignit l'autel et tous ses ustensiles, et la cuve avec son soubassement, pour les consacrer.
12 Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
Il versa aussi de l'huile d'onction sur la tête d'Aaron, et l'oignit pour le consacrer.
13 Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
Puis Moïse fit approcher les fils d'Aaron, et les revêtit de tuniques, les ceignit de ceintures, et leur attacha des mitres, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
14 Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Il fit approcher le taureau du sacrifice pour le péché, et Aaron et ses fils appuyèrent leurs mains sur la tête du taureau du sacrifice pour le péché;
15 Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
Et Moïse l'égorgea, prit le sang, et en mit avec son doigt sur les cornes de l'autel tout autour, et purifia l'autel; puis il répandit le sang au pied de l'autel, et le consacra ainsi pour y faire l'expiation.
16 Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
Et il prit toute la graisse qui était sur les entrailles, la membrane qui recouvre le foie, et les deux rognons avec leur graisse, et Moïse les fit fumer sur l'autel.
17 Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
Mais il brûla au feu hors du camp le taureau, sa peau, sa chair et ses excréments, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
18 Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
Il fit aussi approcher le bélier de l'holocauste, et Aaron et ses fils appuyèrent leurs mains sur la tête du bélier;
19 Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
Et Moïse l'égorgea, et répandit le sang sur l'autel tout autour.
20 Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
Puis il coupa le bélier en morceaux; et Moïse fit fumer la tête, les morceaux, et la graisse.
21 Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
Et il lava dans l'eau les entrailles et les jambes, et Moïse fit fumer tout le bélier sur l'autel; ce fut l'holocauste d'agréable odeur; ce fut un sacrifice fait par le feu à l'Éternel, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
22 Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
Il fit aussi approcher le second bélier, le bélier d'installation; et Aaron et ses fils appuyèrent leurs mains sur la tête du bélier.
23 Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
Moïse l'égorgea, prit de son sang et en mit sur le bout de l'oreille droite d'Aaron, et sur le pouce de sa main droite, et sur le gros orteil de son pied droit.
24 Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
Moise fit aussi approcher les fils d'Aaron, mit du sang sur le bout de leur oreille droite, sur le pouce de leur main droite, et sur le gros orteil de leur pied droit, et Moïse répandit le sang sur l'autel tout autour.
25 Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
Ensuite il prit la graisse, la queue, toute la graisse qui était sur les entrailles, la membrane qui recouvre le foie, les deux rognons avec leur graisse, et la jambe droite;
26 Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
Il prit aussi de la corbeille des pains sans levain, qui était devant l'Éternel, un gâteau sans levain, un gâteau de pain à l'huile, et une galette; et il les mit sur les graisses et sur la jambe droite.
27 Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
Puis il plaça le tout dans les mains d'Aaron, et dans les mains de ses fils, et il les agita en offrande devant l'Éternel.
28 Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
Puis Moïse les prit de leurs mains, et les fit fumer à l'autel, sur l'holocauste; ce fut le sacrifice d'installation, d'agréable odeur, un sacrifice fait par le feu à l'Éternel.
29 Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
Moïse prit aussi la poitrine du bélier d'installation, et l'agita en offrande devant l'Éternel; ce fut la portion de Moïse, comme l'Éternel l'avait commandé à Moïse.
30 Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
Et Moïse prit de l'huile d'onction et du sang qui était sur l'autel; il en fit aspersion sur Aaron et sur ses vêtements, sur ses fils, et sur les vêtements de ses fils avec lui; et il consacra Aaron et ses vêtements, ses fils, et les vêtements de ses fils avec lui.
31 Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
Puis Moïse dit à Aaron et à ses fils: Faites cuire la chair à l'entrée du tabernacle d'assignation et vous la mangerez là, avec le pain qui est dans la corbeille d'installation, comme je l'ai commandé, en disant: Aaron et ses fils la mangeront.
32 Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
Mais vous brûlerez au feu ce qui restera de la chair et du pain.
33 Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
Et pendant sept jours, vous ne sortirez pas de l'entrée du tabernacle d'assignation, jusqu'à ce que les jours de votre installation soient accomplis; car on vous installera pendant sept jours.
34 Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
L'Éternel a commandé de faire comme on a fait aujourd'hui, pour faire expiation pour vous.
35 Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
Vous resterez donc sept jours à l'entrée du tabernacle d'assignation, jour et nuit, et vous observerez le commandement de l'Éternel, afin que vous ne mouriez pas; car il m'a été ainsi commandé.
36 Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.
Et Aaron et ses fils firent toutes les choses que l'Éternel avait commandées par Moïse.