< Mambo ya Walawi 8 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
Take Aaron and his sons with him, and the garments, and the anointing oil, and the bullock of the sin offering, and the two rams, and the basket of unleavened bread,
3 Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
and assemble thou all the congregation at the door of the tent of meeting.
4 Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
And Moses did as Jehovah commanded him, and the congregation was assembled at the door of the tent of meeting.
5 “Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
And Moses said to the congregation, This is the thing which Jehovah has commanded to be done.
6 Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
And Moses brought Aaron and his sons, and washed them with water.
7 Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
And he put upon him the tunic, and girded him with the sash, and clothed him with the robe, and put the ephod upon him, and he girded him with the skillfully woven band of the ephod, and bound it to him therewith.
8 Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
And he placed the breastplate upon him, and he put the Urim and the Thummim in the breastplate.
9 Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
And he set the miter upon his head. And upon the miter, in front, he set the golden plate, the holy crown, as Jehovah commanded Moses.
10 Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
And Moses took the anointing oil, and anointed the tabernacle and all that was in it, and sanctified them.
11 Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
And he sprinkled of it upon the altar seven times, and anointed the altar and all its vessels, and the laver and its base, to sanctify them.
12 Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
And he poured of the anointing oil upon Aaron's head, and anointed him, to sanctify him.
13 Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
And Moses brought Aaron's sons, and clothed them with tunics, and girded them with sashes, and bound head-coverings upon them, as Jehovah commanded Moses.
14 Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
And he brought the bullock of the sin offering. And Aaron and his sons laid their hands upon the head of the bullock of the sin offering,
15 Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
and he killed it. And Moses took the blood, and put it upon the horns of the altar round about with his finger, and purified the altar, and poured out the blood at the base of the altar, and sanctified it, to make atonement for it.
16 Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
And he took all the fat that was upon the innards, and the caul of the liver, and the two kidneys, and their fat, and Moses burned it upon the altar.
17 Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
But the bullock, and its skin, and its flesh, and its dung, he burnt with fire outside the camp, as Jehovah commanded Moses.
18 Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
And he presented the ram of the burnt offering. And Aaron and his sons laid their hands upon the head of the ram,
19 Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
and he killed it. And Moses sprinkled the blood upon the altar round about.
20 Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
And he cut the ram into its pieces, and Moses burnt the head, and the pieces, and the fat.
21 Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
And he washed the innards and the legs with water. And Moses burnt the whole ram upon the altar. It was a burnt offering for a sweet savor. It was an offering made by fire to Jehovah, as Jehovah commanded Moses.
22 Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
And he presented the other ram, the ram of consecration. And Aaron and his sons laid their hands upon the head of the ram,
23 Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
and he killed it. And Moses took of the blood of it, and put it upon the tip of Aaron's right ear, and upon the thumb of his right hand, and upon the great toe of his right foot.
24 Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
And he brought Aaron's sons, and Moses put of the blood upon the tip of their right ear, and upon the thumb of their right hand, and upon the great toe of their right foot. And Moses sprinkled the blood upon the altar round about.
25 Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
And he took the fat, and the fat tail, and all the fat that was upon the innards, and the caul of the liver, and the two kidneys, and their fat, and the right thigh,
26 Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
and out of the basket of unleavened bread, that was before Jehovah, he took one unleavened cake, and one cake of oiled bread, and one wafer, and placed them on the fat, and upon the right thigh.
27 Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
And he put the whole upon the hands of Aaron, and upon the hands of his sons, and waved them for a wave offering before Jehovah.
28 Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
And Moses took them from off their hands, and burnt them on the altar upon the burnt offering. They were a consecration for a sweet savor. It was an offering made by fire to Jehovah.
29 Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
And Moses took the breast, and waved it for a wave offering before Jehovah. It was Moses' portion of the ram of consecration, as Jehovah commanded Moses.
30 Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
And Moses took of the anointing oil, and of the blood which was upon the altar, and sprinkled it upon Aaron, upon his garments, and upon his sons, and upon his sons' garments with him, and sanctified Aaron, his garments, and his sons, and his sons' garments with him.
31 Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
And Moses said to Aaron and to his sons, Boil the flesh at the door of the tent of meeting, and there eat it and the bread that is in the basket of consecration, as I commanded, saying, Aaron and his sons shall eat it.
32 Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
And that which remains of the flesh and of the bread ye shall burn with fire.
33 Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
And ye shall not go out from the door of the tent of meeting seven days, until the days of your consecration be fulfilled, for he shall consecrate you seven days.
34 Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
As has been done this day, so Jehovah has commanded to do, to make atonement for you.
35 Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
And ye shall remain at the door of the tent of meeting day and night seven days, and keep the charge of Jehovah, that ye not die, for so I am commanded.
36 Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.
And Aaron and his sons did all the things which Jehovah commanded by Moses.

< Mambo ya Walawi 8 >