< Mambo ya Walawi 7 >
1 Hii ndiyo sheria ya sadaka ya hatia. Kwa sababu hiyo ni sadaka takatifu sana.
Och detta är skuldoffrens lag, och det är det aldrahelgasta.
2 Ni lazima waichinje sadaka ya hatia mahali panapostali kuchinjwa, na ni lazima watainyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
På det rummet, der man slagtar bränneoffret, skall man ock slagta skuldoffret, och stänka dess blod på altaret allt omkring.
3 Mafuta yote yaliyomo ndani yake yataondolewa: mafuta ya mkiani, mafuta yaliyo sehamu za ndani,
Och allt dess feta skall man offra, stjerten och det feta, som är på inelfverna;
4 zile figo mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake, yaliyo karibu na kiuno, na yanayofunika ini—nyama hii yote lazima iondolewe pamoja na hizo figo.
Båda njurarna med det feta, som derpå är vid länderna, och nätet öfver lefrena med njurarna.
5 Kuhani ataviteketeza vipande hivi juu ya madhabahu viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia
Och Presten skall uppbränna det på altaret Herranom till ett offer; det är ett skuldoffer.
6 Kila mwanaume miongoni mwa familia ya kuhani anaweza kula sehemu ya sadaka hii. Lakini ni lazima iliwe ndani ya mahali patakatifu kwa sababu ni takatifu sana.
Det mankön är ibland Presterna, skola det äta på heligt rum; ty det är det aldrahelgasta.
7 Nayo sadaka ya dhambi ni kama ilivyo sadaka ya hatia. Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili. Zote ni mali ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.
Såsom syndoffret, så skall ock skuldoffret vara; begges deras skall en lag vara; och skall höra Prestenom till, som derigenom försonar.
8 Kuhani atoaye sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuchuku ngozi ya sadaka hiyo kwa ajili yake mwenyewe.
Den Prest något bränneoffer offrar, honom skall tillhöra huden af bränneoffret, som han offrat hafver.
9 Kila sadaka ya nafaka inayookwa mekoni, na kila sadaka kama hiyo ipikwayo kaangoni au kwenye sufuria itakuwa ya kuhani aitoaye.
Och allt spisoffer, som i ugn, eller på halster, eller uti panno bakadt varder, skall höra Prestenom till, som det offrar.
10 Kila sadaka ya nafaka, ama iwe unga mkavu au uliochanganywa na mafuta ya zeitu itakuwa ya ukoo wa Aroni kwa usawa.
Och allt spisoffer, som med oljo blandadt eller torrt är, det skall allom Aarons barnom tillhöra, så thy eno som thy andro.
11 Hii ndiyo sheria ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo watu watazitoa kwa Yahweh.
Och detta är tackoffers lag, det man Herranom offrar.
12 Iwapo mtu yeyote anaitoa ili kuonyesha shukrani kwa Yahweh, basi ataitoa pamoja na dhabih uya mikate iliyotengenezwa bila hamira, bali kwa mafuta ya zeituni yaliyochanganywa na unga lakini bila hamira, na maandazi yaliyotengenezwa bila hamira, bali yaliyopakwa mafuta juu yake, na mikate miembamba iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta.
Vilja de göra ett lofoffer, så skola de offra osyrade kakor, blandade med oljo, och osyrade tunnkakor, bestrukna med oljo, och i panno bakade semlokakor, blandade med oljo.
13 Kwa kusudi la kutoa shukrani, pia anapaswa kutoa pamoja na sadaka yake ya amani, vipande vya mikate iliyotiwa hamira.
Och sådana offer skola de göra på en kako af syradt bröd till sitt tackoffers lofoffer.
14 Ni lazima atatoa moja kila aina ya sadaka hizi kama sadaka iliyoletwa kwa Yahweh. Nayo itakuwa ya makuhani wanaonyunyizia damu ya sadaka ya amani kwenye madhabahu.
Och ett af thy allo skall offras Herranom till häfoffer, och skall höra Prestenom till, som stänker tackoffrens blod.
15 Mtu anayeleta sadaka ya amani kwa kusudi la kutoa shukrani ni lazima ataila nyama ya sadaka yake siku ya kutoa dhabihu. Hatakiwi kusaza chochote kilicho cha sadaka hiyo hata asubuhi ya pili.
Och lofoffrens kött, i sitt tackoffer, skall ätas på samma dagen, som det offradt varder, och intet låtas qvart intill morgonen.
16 Lakini iwapo dhabihu ya matoleo yake kusudi lake ni nadhiri, au kwa kusudi la sadaka ya hiari, nyama yake italiwa siku iyo hiyo aitoapo dhabihu yake, lakini chochote kinachosalia cha sadaka hiyo kinaweza kuliwa siku inayofuata.
Och ehvad det är ett löfte eller friviljogt offer, så skall det på samma dagen ätet varda, som det offradt är; om något qvart blifver till den andra dagen, skall man ändå ätat.
17 Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu inayobaki siku ya tatu ni lazima ichomwe moto.
Men hvad qvart blifver af offradt kött intill tredje dagen, det skall uppbrännas i elde.
18 Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu, hakitakubalika, wala hakitatolewa kwa aliyeitoa. Kitakuwa ni kitu cha kuchukiza, na mtu akilaye atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake.
Och om någor äter på tredje dagen af det offrade köttet af hans tackoffer, så blifver han icke tacknämlig, som det offrat hafver, det skall icke heller varda honom tillräknadt, utan det blifver en styggelse. Och hvad själ som deraf äter, hon är brottslig till en missgerning.
19 Nyama yoyote inayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa. Ni lazima ichomwe moto. Na kwa ajili ya nyama inayobaki, yeyote aliye safi anaweza kuila.
Och det kött, som kommer vid något orent, det skall icke varda ätet, utan uppbrändt i elde. Den der ren är till lekamen, han skall äta det köttet.
20 Hata hivyo, mtu najisi anayekula nyama kutoka kwenye dhabihu ya matoleo ya amani ambayo ni ya Yahweh yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
Och den själ, som äter af tackoffrens kött, det Herranom tillhörer, hennes orenhet vare öfver henne, och hon skall varda utrotad utu sitt folk.
21 Iwapo mtu yeyote anagusa kitu chochote kilichonajisi—iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi, au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza, na kisha akala baadhi ya nyama ya dhabihu ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Yahweh, lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
Och om en själ kommer vid något det orent är, vare sig oren menniska, boskap, eller hvad eljest styggeligit är, eller ock äter af tackoffrens kött, det Herranom tillhörer, den skall utrotad varda utu sitt folk.
22 Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
Och Herren talade med Mose, och sade:
23 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta ya fahali au kondoo au mbuzi.
Tala med Israels barn, och säg: I skolen intet fett äta af fä, lambom och getom.
24 Mafuta ya mnyama yoyote afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu, au mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori, yanaweza kutumika kwa makusudi mengine, lakini hakika hamtayala.
Men det feta af ett as, och hvad af vilddjur rifvet är, bruker eder till allahanda nytto; men icke skolen I ätat.
25 Yeyote atakayekula mafuta ya mnyama ambayo watu wanaweza kuyatoa kuwa dhabihu ya iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
Ty den som äter det feta af den boskap, som Herranom till offer gifven är, den samma själen skall utrotad varda utu sitt folk.
26 Hamtakula damu yoyote katika mojawapo ya nyumba zenu, ama iwe kutoka kwa ndege au mnyama.
I skolen ock intet blod äta, antingen af boskap, eller af foglar, der I bon.
27 Yeyote alaye damu yoyote, mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'”
Hvilken själ, som äter något blod, hon skall utrotad varda utu sitt folk.
28 Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema,
Och Herren talade med Mose, och sade:
29 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye dhabidhu ya sadaka ya amani kwa Yahweh lazima alete sehemu ya dhabihu yake kwa Yahweh.
Tala med Israels barn, och säg: Den som Herranom sitt tackoffer göra vill, han skall ock bära med hvad som Herranom till ett tackoffer tillhörer.
30 Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto. Naye atayaleta hayo mafuta pamoja na kidari, ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
Han skall med sine hand bärat fram till Herrans offer, nämliga det feta på bröstena skall han frambära, samt med bröstet, att de skola varda ett veftoffer för Herranom.
31 Kuhani atayachoma mafuta hayo juu ya madhabahu, lakini kile kidari kitakuwa mali ya Aroni na uzao wake.
Och Presten skall uppbränna det feta på altaret. Och bröstet skall höra Aaron till, och hans söner.
32 Ni lazima utatoa paja la kulia kwa kuhani kama sadaka iliyotokana na dhabihu ya sadaka yako ya amani.
Och den högra bogen skola de gifva Prestenom till häfoffer af deras tackoffer.
33 Yule kuhani, mmoja wa wazao wa Aroni, atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani—ni lazima atapata paja la kulia kama mgao wake wa sadaka.
Och hvilken ibland Aarons söner offrar blodet af tackoffret, och det feta, han skall ock hafva den högra bogen på sin del.
34 Kwa kuwa nimetwaa kidari, na paja la sadaka ya kutikiswa kutoka kwa watu wa Israeli uwe mchango wao, na amepewa Aroni kuhani na wanawe kuwa mgao wao wa kawaida.
Ty veftebröstet och häfvebogen hafver jag tagit af Israels barn, af deras tackoffer, och hafver gifvit det Prestenom Aaron och hans söner, till en evig rätt.
35 Huu ndiyo mgao wa Aroni na uzao wake utokanao na matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, siku ile Musa alipowaweka wakfu ili kumtumikia Yahweh katika kazi ya kuhani.
Detta är Aarons och hans söners vigelse af Herrans offer, på den dagen då de öfverantvardade vordo till att vara Herranom Prester;
36 Huu ndio mgao ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israeli, katika siku hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani. Nao utakuwa mgao wao wa kila siku katika vizazi vyote.
Då Herren böd, på den dagen, då han dem vigde, hvad dem af Israels barnom gifvas skulle, till en evig rätt, allom deras efterkommandom.
37 Hii ndiyo sheria ya sadaka ya kuteketezwa, ya sadaka ya nafaka, ya sadaka ya dhambi, ya sadaka ya hatia, ya sadaka ya kuweka wakfu, na ya dhabihu, ya sadaka za amani,
Och detta är bränneoffrens lag, spisoffrens, syndoffrens, skuldoffrens, fyllooffrens och tackoffrens;
38 ni sheria ambazo Yahweh alizitoa kwa Musa kwenye Mlima Sinai siku aliyowaamru watu wa Israeli kutoa dhabihu zao kwa Yahweh katika jangwa la Sinai.'”
Det Herren på Sinai berg Mose böd, den dagen då han böd honom till Israels barn, att de skulle offra deras offer Herranom uti den öknene Sinai.