< Mambo ya Walawi 6 >
1 Bwana alisema na Musa kumwabia,
And the Lord spake vnto Moses, saying,
2 “Kama mtu akifanya dhambi na kuvunja amri kinyume na Bwana, kama kujihusisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani cha kutokuwa mwaminifu, au kama akidanganya au kuiba au amemdhurumu jirani.
If any sinne and commit a trespasse against the Lord, and denie vnto his neighbour that, which was take him to keepe, or that which was put to him of trust, or doth by robberie, or by violence oppresse his neighbour,
3 Au akiokota kitu fulani ambacho jirani yake amepoteza na kusema uongo kuhusu hicho, na kuapa kwa uongo au kwa mambo kama haya ambayo watu wanaweza kutenda dhambi.
Or hath found that which was lost, and denieth it, and sweareth falsely, for any of these things that a man doeth, wherein he sinneth:
4 Ndipo itakuwa hivi, kama ametenda dhambi na hatia, kwamba lazima akirudishe kwa vyovyote alichoiba au kudanganya au amedhurumu au kitu kilichopotea naye kukiokota.
When, I say, he thus sinneth and trespasseth, he shall then restore the robbery that he robbed, or the thing taken by violence which hee tooke by force, or the thing which was deliuered him to keepe, or the lost thing which he founde,
5 Au kama amedanganya kwa jambo lolote, lazima atakirudisha kamilina kuongezea sehemu ya tano kwa kumlipa anayedai, kwa siku ile anayopatikana na hatia.
Or for whatsoeuer he hath sworne falsely, he shall both restore it in the whole summe, and shall adde the fift parte more thereto, and giue it vnto him to whome perteyneth, the same day that he offreth for trespasse.
6 Ataleta sadka ya hatia kwa Bwana: kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi lake kulingana na thamani yake, kama sadaka ya hatia kwa kuhani.
Also he shall bring for his trespasse vnto the Lord, a ramme without blemish out of the flocke in thy estimation worth two shekels for a trespasse offring vnto the Priest.
7 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele ya Bwana, atakuwa amesamehewa kulingana na chochote kilicho mfanya kuwa na hatia.”
And the Priest shall make an atonement for him before the Lord, and it shall be forgiuen him, whatsoeuer thing he hath done, and trespassed therein.
8 Ndipo Bwana alisema na Musa kumwambia,
Then the Lord spake vnto Moses, saying,
9 “Mwagize Haruni na wanawe, kusema, 'hii ni sheria ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa lazima iwe juu ya makaa ya madhabahu usiku wote hata asubuhi, na moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.
Commaund Aaron and his sonnes, saying, This is the lawe of the burnt offring, (it is the burnt offring because it burneth vpon the altar al the night vnto the morning, and the fire burneth on the altar)
10 Kuhani atavaa nguo zake za kitani na atavaa nguo za kitani ndani yake. Atatoa majivu yaliyobaki baada ya moto kutekeza sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu, na ataweka majivu pembeni mwa madhabahu.
And the Priest shall put on his linen garment, and shall put on his linen breeches vpon his flesh, and take away the ashes when the fire hath consumed the burnt offring vpon the altar, and he shall put them beside the altar.
11 Atavua mavazi haya na kuvaa mavazi mengine ili kuchukua majivu nje ya kambi na kupeleka mahali palipo safi.
After, he shall put off his garments, and put on other raiment, and cary the ashes foorth without the hoste vnto a cleane place.
12 Moto katika madhabahu utaendelea kuwaka. Usizimike, na kuhani ataongeza kuni kila asubuhi. Atapanga juu yake sadaka ya kuteketezwa kama inavyotakiwa, na atateketeza juu yake mafuta ya sadaka ya amani.
But the fire vpon the altar shall burne thereon and neuer be put out: wherefore the Priest shall burne wood on it euery morning, and lay the burnt offering in order vpon it, and he shall burne thereon the fat of the peace offrings.
13 Moto lazima utaendelea kuwaka katika madhabahu, kamwe usizimike.
The fire shall euer burne vpon the altar, and neuer go out.
14 Hii ni sheria ya sadaka ya nafaka. Wana wa Haruni watatoa mbele ya Bwana katika madhabahu.
Also this is the lawe of the meate offring, which Aarons sonnes shall offer in the presence of the Lord, before the altar.
15 Kuhani atachukua konzi ya unga laini wa sadaka ya nafaka na mafuta na ubani ambao uko juu ya sadaka ya nafaka, atateketeza juu ya madhabahu kuleta harufu nzuri ya shukrani ya kumpendeza Bwana.
He shall euen take thence his handfull of fine flowre of the meate offring and of the oyle, and all the incense which is vpon the meat offring, and shall burne it vpon the altar for a sweete sauour, as a memoriall therefore vnto the Lord:
16 Haruni na wanae watakula sadaka inayobaki, italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu. Watakula katika ua ya hema ya kukutania.
But the rest thereof shall Aaron and his sonnes eate: it shalbe eaten without leauen in the holy place: in the court of the Tabernacle of the Congregation they shall eate it.
17 Haitaokwa pamoja na chachu. Nimewapa kama sehemu ya sadaka yangu itolewayo kwa moto, ni takatifu sana, kama sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
It shall not be baken with leauen: I haue giuen it for their portion of mine offrings made by fire: for it is as the sinne offering and as the trespasse offring.
18 Kwa nyakati zote zijazo kupitia watu wa kizazi chako, mwanaume yeyote mzaliwa kutoka kwa Haruni aweza kula ni sehemu yake, ichukuliwayo katika sadaka ya Bwana kwa moto. Yeyote anayeigusa atakuwa mtakatifu.”
All the males among the children of Aaron shall eate of it: It shalbe a statute for euer in your generations concerning the offrings of the Lord, made by fire: whatsoeuer toucheth them shall be holy.
19 Bwana aliongea tena na Musa kumwambia,
Agayne the Lord spake vnto Moses, saying,
20 “Hii ni sadaka ya Haruni na wanawe ambayo watatoa kwa Bwana katika siku ambayo kila mwana atawekwa wakfu: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama kawaida sadaka ya nafaka nusu yake asubuhi na nusu yake jioni.
This is the offering of Aaron and his sonnes, which they shall offer vnto the Lord in the day when he is anointed: the tenth part of an Ephah of fine floure, for a meate offering perpetuall: halfe of it in ye morning, and halfe thereof at night.
21 Itatengenezwa na mafuta katika kikaango, utaileta ikiwa imeandaliwa imeokwa katika vipande utatoa sadaka ya nafaka ili kuleta harufu nzuri kwa Bwana.
In the frying panne it shalbe made with oyle: thou shalt bring it fryed, and shalt offer the baken pieces of the meate offering for a sweete sauour vnto the Lord.
22 Mwana wa Kuhani Mkuu atakayekuwa Kuhani Mkuu mpya kutoka miongoni mwa wanawe ataitoa. Kama amri ya milele, yote itateketezwa kwa Bwana.
And the Priest that is anointed in his steade, among his sonnes shall offer it: It is the Lordes ordinance for euer, it shall be burnt altogether.
23 Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itatekezwa yote. Haitaliwa kamwe.”
For euery meate offring of the Priest shall be burnt altogether, it shall not be eaten.
24 Bwana alisema tena Musa, kumwambia,
Furthermore, the Lord spake vnto Moses, saying,
25 “Sema na Haruni na watoto wake kwamba, 'Hii ni sheria ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi lazima kuchinjwa mahali pa sadaka ya kuteketezwa itachinjwa mbeleya Bwana. Ni takatifu sana.
Speake vnto Aaron, and vnto his sonnes, and say, This is the Lawe of the sinne offering, In the place where the burnt offring is killed, shall the sinne offring be killed before the Lord, for it is most holy.
26 Kuhani atakayeitoa kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila. Italiwa mahali patakatifu katika ua wa hema ya kukutania.
The Priest that offreth this sinne offring, shall eate it: in the holy place shall it be eaten, in the court of ye Tabernacle of the Congregation.
27 Yeyote atakayeigusa nyama yake atakuwa ni mtakatifu na kama damu itadondokea mavazi yatafuliwa mahali palipodondokewa, mahali patakatifu.
Whatsoeuer shall touch the flesh thereof shalbe holy: and when there droppeth of the blood thereof vpon a garment, thou shalt wash that whereon it droppeth in the holy place.
28 Lakini chungu kikipikiwa kitavunjwa, kama imepikiwa katika chombo cha shaba, lazima kitasuguliwa na kusafishwa kwa maji.
Also the earthen pot that it is sodden in, shalbe broken, but if it be sodden in a brasen pot, it shall both be scoured and washed with water.
29 Mwanaume yeyote miongoni mwa makuhani anaweza kula nyama hiyo kwa sababu ni takatifu sana.
All the males among the Priestes shall eate thereof, for it is most holy.
30 Na hakuna sadaka ya dhambi italiwa ambayo damu yake imeletwa katika hema ya kukutania kufanya upatanisho katika mahali patakatifu. Ni lazima iteketezwe.
But no sinne offering, whose blood is brought into the Tabernacle of the Congregation to make reconciliation in the holy place, shalbe eaten, but shalbe burnt in the fire.