< Mambo ya Walawi 5 >

1 Kama mtu atatenda dhambi kwa sababu hakusema ukweli wakati alipotakiwa kutoa ushahidi fulani kuhusu kile alichotakiwa, ameona au kufahamu habari zake, yeye anastahili adhabu.
And anyone if it will sin and it will hear [the] sound of an oath and he [was] a witness or he saw or he knew if not he will tell and he will bear iniquity his.
2 Au mtu akigusa kitu chochote ambacho Mungu amekitaja kuwa ni najisi hata kama ni mzoga wa wanyama wa porini au ni mzoga wa wanyama wa kufugwa au wataambaao hata kama mtu huyo hakukusudia kumgusa, yeye ni najisi na mwenye hatia.
Or anyone who it will touch every thing unclean or a carcass of an animal unclean or a carcass of livestock unclean or a carcass of a swarming thing unclean and it will be hidden from him and he [is] unclean and he will be guilty.
3 Au amegusa kitu chochote kilicho kichafu, kwa vyovyote kama hakujua, ndipo atakuwa na hatia akijua vile.
Or if he will touch [the] uncleanness of a human to all uncleanness his which he will be unclean by it and it will be hidden from him and he he knew and he will be guilty.
4 Au kama yeyote akiapa bila kufikiri kwa midomo yake kufanya ubaya, au kufanya vyema kwa vyovyote vile mtu ameapa kwa haraka atakapotambua atakuwa na hatia kwa vitu hivyo.
Or anyone if it will swear an oath by speaking rashly with lips to do evil - or to do good to all that he will speak rashly humankind in an oath and it will be hidden from him and he he knew and he will be guilty to one of these [things].
5 Mtu yeyote akiwa na hatia kwa vitu hivi, lazima akiri kwa yoyote dhambi aliyotenda.
And it will be that he will be guilty to one of these [things] and he will confess that he had sinned on it.
6 Ndipo atakapoleta sadaka yake ya hatia mbele za Bwana kwa dhambi aliyokwisha tenda. Ataleta kondoo jike au mbuzi kutoka katika kundi lake kuwa matoleo ya dhambi, kuhani atafanya upatanisho kuhusu dhambi yake.
And he will bring guilt offering his to Yahweh on sin his which he has sinned a female from the flock a ewe lamb or a female goat of goats to a sin offering and he will make atonement on him the priest from sin his.
7 Kama hataweza kununua mwana kondoo ataleta kama sadaka ya hatia, hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana, mmoja kwa sadaka ya dhambi na mwingine ni sadaka ya kutekeketezwa.
And if not it will reach hand his sufficiency of a sheep and he will bring guilt offering his which he has sinned two turtle-doves or two young ones of a dove to Yahweh one to a sin offering and one to a burnt offering.
8 Atawaleta kwa kuhani, wa kwanza atatoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo yake lakini ataacha kichwa chake kinaning'inia wala hataiondoa kabisa shingo yake katika mwili.
And he will bring them to the priest and he will present [the one] which [is] for the sin offering first and he will nip off head its from in front of neck its and not he will separate [it].
9 Ndipo atanyunyizia damu yake katika sehemu za madhabahu, na damu inayobaki ataimwaga chini ya madhabahu. Hii ni dhabihu ya dhambi.
And he will spatter some of [the] blood of the sin offering on [the] side of the altar and the remainder in the blood it will be drained out to [the] base of the altar [is] a sin offering it.
10 Ndipo ataoa ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kama ilivyoelekezwa, na kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi alizokwisha kufanya, na huyo mtu atakuwa amesamehewa.
And the second [bird] he will offer a burnt offering according to the ordinance and he will make atonement on him the priest from sin his which he has sinned and it will be forgiven to him.
11 Lakini kama hataweza kununua hua wawili au makinda ya njiwa mawili, ndipo ataleta kama dhabihu ya dhambi zake sehemu ya kumi ya unga laini kama sadaka ya dhambi. Asiweke mafuta wala ubani juu yake, kwa kuwa ni sadaka ya dhambi.
And if not it will reach hand his to two turtle-doves or to two young ones of a dove and he will bring present his which he has sinned tenth of ephah fine flour to a sin offering not he will place on it oil and not he will put on it frankincense for [is] a sin offering it.
12 Atauleta kwa kuhani, na kuhani atachukua konzi moja ya unga kama ukumbusho wa wema wa Bwana na atauweka juu ya madhabahu na kuteketeza juu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
And he will bring it to the priest and he will take a handful the priest - from it [the] fullness of handful his memorial offering its and he will make [it] smoke the altar towards on [the] fire offerings of Yahweh [is] a sin offering it.
13 Kuhani atafanya upatanisho kwa dhambi yoyote aliyofanya mtu yeyote, mtu huyo atasamehewa. Na sadaka inayobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyo sadaka ya nafaka.'”
And he will make atonement on him the priest on sin his which he has sinned any one of these [things] and it will be forgiven to him and it will belong to the priest like the grain offering.
14 Bwana akamwambia Musa, akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
15 “Kama mtu akikiuka amri na kufanya dhambi kinyume na mambo matakatifu ya Bwana, lakini akifanya bila kukusudia ataleta sadaka ya hatia kwa Bwana. Sadaka hii itakuwa ni kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi; thamani yake halisi kifedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kama sadaka ya hatia.
Anyone if it will act unfaithfully unfaithfulness and it will sin by inadvertence from [the] holy things of Yahweh and he will bring guilt offering his to Yahweh a ram unblemished from the flock by valuation your silver of shekels by [the] shekel of the holy place to a guilt offering.
16 Lazima atalipa kwa Bwana kwa kile alichokosa kulingana na kitakatifu, na ataongezea moja ya tano na kumpa kuhani. Ndipo kuhani ataweka upatanisho kwa ajili yake pamoja na kondoo wa sadaka ya hatia, na mtu atakuwa amesamehewa.
And [that] which he sinned from the holy thing he will repay and fifth its let him add to it and he will give it to the priest and the priest he will make atonement on him by [the] ram of the guilt offering and it will be forgiven to him.
17 Kama mtu akitenda dhambi kwa kufanya kile ambacho Bwana aliagiza kisifanyike, hata kama hakujuwa, atakuwa na hatia na ataibeba hatia yake.
And if anyone that it will sin and it will do one of all [the] commandments of Yahweh which not they will be done and not he knew and he will be guilty and he will bear iniquity his.
18 Lazima ataleta kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi, anayestahili thamani ya fedha, kama sadaka ya hatia kwa kuhani. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kulingana na dhambi aliyotenda, ambayo hakujua atakuwa amesamehewa.
And he will bring a ram unblemished from the flock by valuation your to a guilt offering to the priest and he will make atonement on him the priest on inadvertence his which he has gone astray and he not he knew and it will be forgiven to him.
19 Ni sadaka ya hatia, na amekuwa na hatia mbele za Bwana.”
[is] a guilt offering It certainly he was guilty to Yahweh.

< Mambo ya Walawi 5 >