< Mambo ya Walawi 5 >

1 Kama mtu atatenda dhambi kwa sababu hakusema ukweli wakati alipotakiwa kutoa ushahidi fulani kuhusu kile alichotakiwa, ameona au kufahamu habari zake, yeye anastahili adhabu.
“And when a person sins, and has heard the voice of an oath, and he [is] witness, or has seen, or has known—if he does not declare [it], then he has borne his iniquity.
2 Au mtu akigusa kitu chochote ambacho Mungu amekitaja kuwa ni najisi hata kama ni mzoga wa wanyama wa porini au ni mzoga wa wanyama wa kufugwa au wataambaao hata kama mtu huyo hakukusudia kumgusa, yeye ni najisi na mwenye hatia.
Or when a person comes against anything unclean, or against a carcass of an unclean beast, or against a carcass of unclean livestock, or against a carcass of an unclean teeming creature, and it has been hidden from him, then he [is] unclean and guilty;
3 Au amegusa kitu chochote kilicho kichafu, kwa vyovyote kama hakujua, ndipo atakuwa na hatia akijua vile.
or when he comes against [the] uncleanness of man, even any of his uncleanness whereby he is unclean, and it has been hidden from him, and he has known, then he has been guilty.
4 Au kama yeyote akiapa bila kufikiri kwa midomo yake kufanya ubaya, au kufanya vyema kwa vyovyote vile mtu ameapa kwa haraka atakapotambua atakuwa na hatia kwa vitu hivyo.
Or when a person swears, speaking wrongfully with the lips to do evil, or to do good, even anything which man speaks wrongfully with an oath, and it has been hid from him—when he has known then he has been guilty of one of these;
5 Mtu yeyote akiwa na hatia kwa vitu hivi, lazima akiri kwa yoyote dhambi aliyotenda.
and it has been when he is guilty of one of these, that he has confessed concerning that which he has sinned,
6 Ndipo atakapoleta sadaka yake ya hatia mbele za Bwana kwa dhambi aliyokwisha tenda. Ataleta kondoo jike au mbuzi kutoka katika kundi lake kuwa matoleo ya dhambi, kuhani atafanya upatanisho kuhusu dhambi yake.
and has brought in his guilt-offering to YHWH for his sin which he has sinned, a female out of the flock, a lamb, or a kid of the goats, for a sin-offering, and the priest has made atonement for him because of his sin.
7 Kama hataweza kununua mwana kondoo ataleta kama sadaka ya hatia, hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana, mmoja kwa sadaka ya dhambi na mwingine ni sadaka ya kutekeketezwa.
And if his hand does not reach to the sufficiency of a lamb, then he has brought in his guilt-offering—he who has sinned—two turtle-doves or two young pigeons to YHWH, one for a sin-offering and one for a burnt-offering;
8 Atawaleta kwa kuhani, wa kwanza atatoa kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo yake lakini ataacha kichwa chake kinaning'inia wala hataiondoa kabisa shingo yake katika mwili.
and he has brought them to the priest, and has brought near that which [is] for a sin-offering first, and has wrung off its head from its neck, and does not separate [it],
9 Ndipo atanyunyizia damu yake katika sehemu za madhabahu, na damu inayobaki ataimwaga chini ya madhabahu. Hii ni dhabihu ya dhambi.
and he has sprinkled of the blood of the sin-offering on the side of the altar, and that which is left of the blood is wrung out at the foundation of the altar; it [is] a sin-offering.
10 Ndipo ataoa ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kama ilivyoelekezwa, na kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi alizokwisha kufanya, na huyo mtu atakuwa amesamehewa.
And he makes the second a burnt-offering, according to the ordinance, and the priest has made atonement for him because of his sin which he has sinned, and it has been forgiven him.
11 Lakini kama hataweza kununua hua wawili au makinda ya njiwa mawili, ndipo ataleta kama dhabihu ya dhambi zake sehemu ya kumi ya unga laini kama sadaka ya dhambi. Asiweke mafuta wala ubani juu yake, kwa kuwa ni sadaka ya dhambi.
And if his hand does not reach to two turtle-doves, or to two young pigeons, then he has brought in his offering—he who has sinned—a tenth of an ephah of flour for a sin-offering; he puts no oil on it, nor does he put frankincense on it, for it [is] a sin-offering,
12 Atauleta kwa kuhani, na kuhani atachukua konzi moja ya unga kama ukumbusho wa wema wa Bwana na atauweka juu ya madhabahu na kuteketeza juu ya sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
and he has brought it to the priest, and the priest has taken a handful from it of the fullness of his hand—its memorial—and has made incense on the altar, according to the fire-offerings of YHWH; it [is] a sin-offering.
13 Kuhani atafanya upatanisho kwa dhambi yoyote aliyofanya mtu yeyote, mtu huyo atasamehewa. Na sadaka inayobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyo sadaka ya nafaka.'”
And the priest has made atonement for him, for his sin which he has sinned against one of these, and it has been forgiven him, and [the remnant] has been for the priest, like the present.”
14 Bwana akamwambia Musa, akasema,
And YHWH speaks to Moses, saying,
15 “Kama mtu akikiuka amri na kufanya dhambi kinyume na mambo matakatifu ya Bwana, lakini akifanya bila kukusudia ataleta sadaka ya hatia kwa Bwana. Sadaka hii itakuwa ni kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi; thamani yake halisi kifedha kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, kama sadaka ya hatia.
“When a person commits a trespass, and has sinned through ignorance against the holy things of YHWH, then he has brought in his guilt-offering to YHWH, a ram, a perfect one, out of the flock, at your valuation [in] silver—shekels by the shekel of the holy place—for a guilt-offering.
16 Lazima atalipa kwa Bwana kwa kile alichokosa kulingana na kitakatifu, na ataongezea moja ya tano na kumpa kuhani. Ndipo kuhani ataweka upatanisho kwa ajili yake pamoja na kondoo wa sadaka ya hatia, na mtu atakuwa amesamehewa.
And that which he has sinned against the holy thing he repays, and is adding to it its fifth, and has given it to the priest, and the priest makes atonement for him with the ram of the guilt-offering, and it has been forgiven him.
17 Kama mtu akitenda dhambi kwa kufanya kile ambacho Bwana aliagiza kisifanyike, hata kama hakujuwa, atakuwa na hatia na ataibeba hatia yake.
And when any person sins, and has done [something against] one of all the commands of YHWH [regarding things] which are not to be done, and has not known, then he has been guilty, and has borne his iniquity.
18 Lazima ataleta kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi, anayestahili thamani ya fedha, kama sadaka ya hatia kwa kuhani. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kulingana na dhambi aliyotenda, ambayo hakujua atakuwa amesamehewa.
Then he has brought in a ram, a perfect one, out of the flock, at your valuation, for a guilt-offering, to the priest; and the priest has made atonement for him, for his ignorance in which he has erred and he has not known, and it has been forgiven him;
19 Ni sadaka ya hatia, na amekuwa na hatia mbele za Bwana.”
it [is] a guilt-offering; he has certainly been guilty before YHWH.”

< Mambo ya Walawi 5 >