< Mambo ya Walawi 25 >

1 Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
Rzekł nad to Pan do Mojżesza na górze Synaj, mówiąc:
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
Powiedz synom Izraelskim, a mów do nich: Gdy wnijdziecie do ziemi, którą Ja wam daję, tedy święcić będzie ziemia sabat Panu.
3 Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
Przez sześć lat osiewać będziesz pole twoje, i przez sześć lat winnice twoje obrzynać będziesz, zbierając urodzaje z niej;
4 Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
Ale roku siódmego sabat odpocznienia mieć będzie ziemia, sabat Pański; pola twego nie będziesz osiewał, ani winnicy twojej obrzynał.
5 Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
Co się samo przez się zrodzi zboża twego, nie będziesz żął, i jagód zaniechanej winnicy twojej nie będziesz zbierał; rok odpocznienia będzie miała ziemia.
6 Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
I będzie, co się urodzi w onem odpocznieniu ziemi, tobie na pokarm, i słudze twemu, i służebnicy twej, i najemnikowi twemu i przychodniowi twemu, który mieszka z tobą.
7 Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
Także bydłu twemu, i zwierzowi, który jest w ziemi twojej, będzie wszystek urodzaj jej na pokarm.
8 Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
Naliczysz też sobie siedem tygodni lat, to jest siedem kroć siedem lat; i uczyniąć dni siedmiu tygodni lat czterdzieści i dziewięć lat.
9 Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
Tedy każesz zatrąbić w trąbę huczną miesiąca siódmego, dnia dziesiątego tegoż miesiąca; w dzień oczyszczenia każecie zatrąbić po wszystkiej ziemi waszej.
10 Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
I święcić będziecie rok pięćdziesiąty, a obwołacie wolność w ziemi wszystkim obywatelom jej. Lato miłościwe mieć będziecie; i wróci się każdy do osiadłości swojej, i każdy do rodziny swojej wróci się.
11 Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
To miłościwe lato pięćdziesiątego roku miewać będziecie; nie będziecie siać, i nie będziecie żąć tego, co się samo przez się zrodzi, ani zbierać będziecie gron z winnic zaniechanych.
12 Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
Bo miłościwy rok jest, święty wam będzie; co się na polu przedtem zrodziło, to jeść będziecie.
13 Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
W ten miłościwy rok wróci się każdy do osiadłości swojej.
14 Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
Jeźli co sprzedasz bliźniemu twemu, albo co kupisz od bliźniego twego, niech nie oszukiwa jeden drugiego.
15 Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
Według liczby lat po miłościwym roku kupisz od bliźniego twego; i według liczby lat dochody sprzeda tobie.
16 Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
Jeźli więcej będzie lat, tem drożej oszacujesz kupno ono; a jeźli mniej będzie lat, tedy też taniej oszacujesz kupno ono, ponieważ tylko liczba dochodów sprzedawa się tobie.
17 Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
A tak nie oszukiwajcie żaden bliźniego swego, ale się bój każdy Boga swego; bom Ja Pan, Bóg wasz.
18 Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
Przestrzegajcie ustaw moich, i sądy moje zachowywajcie, i czyńcie je, abyście mieszkać mogli w ziemi onej bezpiecznie.
19 Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
Tedy wyda ziemia owoc swój, a będziecie jeść aż do sytości, i będziecie mieszkać bezpiecznie w niej.
20 Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
A jeźlibyście rzekli: Cóż będziemy jeść roku siódmego, jeźli nie będziem siać ani zbierać urodzajów naszych?
21 Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
Tedy rozkażę błogosławieństwu memu przyjść na was roku szóstego, i przyniesie urodzaj na trzy lata.
22 Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
I będziecie siać roku ósmego, a będziecie jeść urodzaj stary aż do roku dziewiątego; póki nie nadejdą pożytki jego, stare jeść będziecie.
23 Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
Ziemia tedy nie będzie sprzedawana na wieczność; bo moja jest ziemia, a wyście gośćmi i przychodniami u mnie.
24 Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
A po wszystkiej ziemi osiadłości waszej pozwolicie wykupywać ziemię.
25 Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
Gdyby zubożał brat twój, a sprzedałby nieco z majętności swojej, i przyszedłby mający prawo odkupienia, powinny jego niech wykupi, co sprzedał brat jego.
26 Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
A jeźliby kto nie miał tego coby odkupić mógł, a sam by przemógł, i znalazł dostatek na to wykupno:
27 kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
Tedy obrachowawszy lata od sprzedania swego, wróci co zbywa temu, któremu sprzedał: a wróci się do majętności swojej.
28 Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
A jeźliby nie miał dostatku, aby wrócił, tedy zostanie majętność sprzedana w ręku tego, który ją kupił, aż do roku miłościwego, i ustąpi mu jej w rok miłościwy, a on wróci się do majętności swojej.
29 Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
Jeźliby też sprzedał dom mieszkania w mieście murowanem, będzie miał wolność wykupić go, póki nie wynijdzie rok sprzedania jego, cały rok będzie miał prawo do wykupienia jego.
30 Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
A jeźli go nie wykupi, póki nie wynijdzie rok cały, tedy zostanie on dom w mieście murowanem temu, który go kupił, dziedzicznie, i potomkom jego
31 Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
I nie ustąpi w miłościwe lato. Ale domy we wsiach, które nie są murem obtoczone, te prawem jako pole ziemi szacowane będą; będą mogły być odkupowane, i w miłościwe lato z rąk obcych wynijdą.
32 Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
Ale miasta Lewitów, i domy w dziedzicznych mieściech ich każdego czasu wykupowane być mogą przez Lewity.
33 Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
Lecz temu co kupuje od Lewitów, wynijdzie kupno domu, i miejskiej osiadłości jego, w rok miłościwy gdyż domy miast Lewickich są dziedziczne ich, w pośrodku synów Izraelskich.
34 Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
Ale pole na przedmieściu ich nie będzie sprzedawane; bo dziedzictwem ich jest wiecznem.
35 Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
Gdyby też zubożał brat twój, a osłabiałaby ręka jego przy tobie, podeprzesz go; a jako i przychodzień niech się żywi przy tobie.
36 Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
Nie bierz od niego lichwy, ani płatu, ale się bój Boga swego, aby się żywił brat twój przy tobie.
37 Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
Pieniędzy twoich nie dawaj mu na lichwę, ani mu z zysku pożyczaj żywności twojej.
38 Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
Jam Pan, Bóg wasz, którym was wywiódł z ziemi Egipskiej, abym wam dał ziemię Chananejską, a był wam za Boga.
39 Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
Jeźliby też zubożał brat twój przy tobie, tak żeby się tobie zaprzedał, nie będziesz go dręczył służbą niewolniczą;
40 Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
Jako najemnik, jako przychodzień będzie u ciebie, aż do roku miłościwego służyć ci będzie.
41 Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
Potem wynijdzie od ciebie on, i dzieci jego z nim, a wróci się do rodziny swojej, i do dziedzictwa przodków swych wróci się.
42 Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
Słudzy bowiem moi są, którem Ja wywiódł z ziemi Egipskiej, niechże nie będą sprzedawani jako niewolnicy.
43 Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
Nie będziesz panował nad nimi surowie, ale się będziesz bał Pana Boga twego.
44 Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
Niewolnik też twój, i niewolnica twoja, które mieć będziesz, będą z narodów tych, które są około was, z nich kupować będziecie niewolnika i niewolnicę.
45 Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
Także też syny przychodniów mieszkających między wami kupować będziecie, i z potomstwa tych, którzy są z wami, które spłodzili w ziemi waszej, a ci będą wam za dziedzictwo.
46 Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
Prawem dziedzicznem trzymać je będziecie, i synowie wasi po was, abyście je dziedzicznie odzierżeli, na wieki służby ich używać będziecie; lecz nad bracią swą, syny Izraelskimi, żaden nad bratem swoim nie będzie panował surowie.
47 Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
Jeźliby się też gość albo przychodzień zbogacił, który mieszka z tobą, a zubożałby brat twój przy nim, tak żeby się zaprzedał gościowi, albo przychodniowi, który jest z tobą, albo potomstwu z domu cudzoziemców,
48 baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
Gdyby się zaprzedał, może być wykupiony; ktokolwiek z braci jego odkupi go;
49 Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
Albo stryj jego, albo syn stryja jego odkupi go, albo z bliskich pokrewnych jego z rodziny jego, odkupi go, albo jeźliby przemógł, wykupi się sam.
50 Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
I porachuje się z onym, co go kupił, od roku, którego mu się sprzedał, aż do miłościwego lata, aby pieniądze, za które się sprzedał, odłożone były według liczby lat, jako z najemnikiem, z nim sobie postąpi.
51 Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
Jeźliby jeszcze nie mało lat zostawało, wedle nich wróci okup swój z pieniędzy, za które kupiony jest.
52 Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
A jeźliby nie wiele lat zostawało do miłościwego lata, tedy porachuje się z nim, a według onych lat wróci okup swój.
53 Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
Jako najemnik doroczny niech będzie u niego; nie będzie nad nim surowie panował przed oczyma twemi.
54 Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
A jeźliby się tym obyczajem nie wykupił, tedy wynijdzie w miłościwe lato, on i dzieci jego z nim;
55 Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Albowiem synowie Izraelscy są sługami moimi; sługami moimi są, którem wywiódł z ziemi Egipskiej, Ja Pan, Bóg wasz.

< Mambo ya Walawi 25 >