< Mambo ya Walawi 25 >
1 Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
Yahvé dit à Moïse sur la montagne du Sinaï:
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
Parle aux enfants d'Israël, et dis-leur: Quand vous serez entrés dans le pays que je vous donne, le pays observera un sabbat en l'honneur de Yahvé.
3 Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
Vous sèmerez votre champ pendant six ans, vous taillerez votre vigne pendant six ans et vous en recueillerez les fruits.
4 Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
Mais la septième année, il y aura pour le pays un sabbat de repos solennel, un sabbat pour Yahvé. Tu ne sèmeras pas ton champ et tu ne tailleras pas ta vigne.
5 Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
Tu ne moissonneras pas ce qui pousse tout seul dans ta moisson, et tu ne vendangeras pas les raisins de ta vigne non taillée. Ce sera une année de repos solennel pour le pays.
6 Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
Le sabbat du pays vous servira de nourriture, pour vous-même, pour votre serviteur, pour votre servante, pour votre mercenaire, et pour l'étranger qui vit chez vous.
7 Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
Tout le produit de ton bétail et des animaux qui sont dans ton pays servira de nourriture.
8 Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
"'Tu compteras sept sabbats d'années, sept fois sept ans, et il y aura pour toi des jours de sept sabbats d'années, soit quarante-neuf ans.
9 Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
Puis tu sonneras de la trompette à haute voix le dixième jour du septième mois. Le jour des expiations, tu sonneras de la trompette dans tout ton pays.
10 Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
Tu sanctifieras la cinquantième année et tu proclameras la liberté dans tout le pays pour tous ses habitants. Ce sera pour vous un jubilé; chacun de vous retournera dans sa propriété, et chacun de vous retournera dans sa famille.
11 Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
Cette cinquantième année sera pour vous un jubilé. Pendant cette période, vous ne sèmerez pas, vous ne moissonnerez pas ce qui pousse tout seul et vous ne cueillerez pas la vigne non taillée.
12 Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
Car c'est un jubilé; elle sera pour vous une chose sainte. Vous mangerez de ce qu'elle produira dans les champs.
13 Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
"'En cette année de jubilé, chacun de vous retournera dans sa propriété.
14 Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
"'Si tu vends quelque chose à ton prochain, ou si tu achètes quelque chose de ton prochain, tu ne te feras pas de tort l'un à l'autre.
15 Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
Tu achèteras de ton prochain en fonction du nombre d'années après le Jubilé. Il te vendra selon le nombre d'années des récoltes.
16 Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
Tu en augmenteras le prix selon la longueur des années, et tu en diminueras le prix selon la brièveté des années, car il te vendra le nombre des récoltes.
17 Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
Vous ne vous ferez pas de tort les uns aux autres, mais vous craindrez votre Dieu, car je suis Yahvé votre Dieu.
18 Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
"'C'est pourquoi vous observerez mes lois, vous garderez mes ordonnances et vous les mettrez en pratique, et vous habiterez le pays en sécurité.
19 Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
Le pays donnera son fruit, vous mangerez à satiété et vous y habiterez en sécurité.
20 Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
Si vous disiez: « Que mangerons-nous la septième année? Voici, nous ne sèmerons pas, et nous ne recueillerons pas nos produits »;
21 Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
mais j'ordonnerai ma bénédiction sur vous la sixième année, et elle donnera du fruit pendant trois ans.
22 Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
Vous sèmerez la huitième année, et vous mangerez des fruits de l'ancienne réserve jusqu'à la neuvième année. Jusqu'à ce qu'elle produise des fruits, tu mangeras de l'ancienne réserve.
23 Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
"'Le pays ne sera pas vendu à perpétuité, car le pays m'appartient; vous êtes des étrangers et vous vivez comme des étrangers chez moi.
24 Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
Dans tout le pays que vous posséderez, vous accorderez un rachat de la terre.
25 Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
"'Si ton frère s'appauvrit et vend une partie de ses biens, son parent le plus proche viendra racheter ce que son frère a vendu.
26 Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
Si un homme n'a personne pour le racheter, et qu'il devienne prospère et trouve des moyens suffisants pour le racheter,
27 kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
qu'il fasse le compte des années écoulées depuis sa vente, et qu'il restitue le surplus à celui à qui il l'a vendu; et il rentrera dans ses biens.
28 Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
Mais s'il ne peut le récupérer pour lui-même, ce qu'il a vendu restera entre les mains de celui qui l'a acheté jusqu'à l'année du Jubilé. Au Jubilé, il sera libéré, et il retournera dans sa propriété.
29 Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
"'Si un homme vend une maison d'habitation dans une ville fortifiée, il peut la racheter dans l'année qui suit sa vente. Pendant une année entière, il aura le droit de rachat.
30 Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
Si elle n'est pas rachetée dans l'espace d'une année entière, la maison qui se trouve dans la ville fortifiée sera garantie à perpétuité à celui qui l'a achetée, de génération en génération. Elle ne sera pas libérée au Jubilé.
31 Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
Mais les maisons des villages qui ne sont pas entourés de murs seront comptabilisées avec les champs de la campagne: elles pourront être rachetées, et elles seront libérées au Jubilé.
32 Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
"'Néanmoins, dans les villes des Lévites, les Lévites peuvent racheter les maisons des villes de leur possession à tout moment.
33 Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
Les Lévites peuvent racheter la maison qui a été vendue, ainsi que la ville de sa possession, et elle sera libérée au Jubilé; car les maisons des villes des Lévites sont leur possession parmi les enfants d'Israël.
34 Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
Mais le champ des pâturages de leurs villes ne pourra pas être vendu, car c'est leur possession perpétuelle.
35 Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
"'Si ton frère est devenu pauvre, et que sa main ne puisse pas subvenir à ses besoins parmi vous, tu le soutiendras. Il vivra avec toi comme un étranger et un résident temporaire.
36 Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
Tu ne prendras de lui aucun intérêt ni aucun profit, mais tu craindras ton Dieu, afin que ton frère puisse vivre parmi toi.
37 Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
Tu ne lui prêteras pas ton argent à intérêt, et tu ne lui donneras pas ta nourriture à profit.
38 Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
Je suis Yahvé, ton Dieu, qui t'ai fait sortir du pays d'Égypte, pour te donner le pays de Canaan, et pour être ton Dieu.
39 Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
"'Si ton frère est devenu pauvre au milieu de toi et qu'il se vend à toi, tu ne le feras pas servir comme esclave.
40 Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
Il sera chez toi comme mercenaire et comme résident temporaire; il servira chez toi jusqu'à l'année du jubilé.
41 Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
Puis il sortira de chez toi, lui et ses enfants avec lui, et il retournera dans sa famille et dans la propriété de ses pères.
42 Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
Car ce sont mes serviteurs, que j'ai fait sortir du pays d'Égypte. Ils ne seront pas vendus comme esclaves.
43 Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
Tu ne domineras pas sur lui avec dureté, mais tu craindras ton Dieu.
44 Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
"'Quant à tes esclaves mâles et femelles, que tu peux avoir des nations qui t'entourent, tu pourras acheter d'elles des esclaves mâles et femelles.
45 Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
De plus, tu pourras acheter des enfants des étrangers qui vivent parmi toi, et de leurs familles qui sont avec toi, ceux qu'ils auront conçus dans ton pays; et ils seront ta propriété.
46 Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
Tu pourras en faire un héritage pour tes enfants après toi, pour qu'ils en prennent possession. Tu pourras prendre d'eux tes esclaves pour toujours, mais tu ne domineras pas avec dureté sur tes frères, les enfants d'Israël, les uns sur les autres.
47 Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
"'Si un étranger ou un résident temporaire chez toi devient riche, et que ton frère à côté de lui soit devenu pauvre, et qu'il se vende à l'étranger ou à l'étranger qui vit parmi vous, ou à un membre de la famille de l'étranger,
48 baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
après avoir été vendu, il pourra être racheté. L'un de ses frères pourra le racheter;
49 Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
ou son oncle, ou le fils de son oncle, pourra le racheter, ou tout proche parent de sa famille pourra le racheter; ou s'il est devenu riche, il pourra se racheter lui-même.
50 Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
Il comptera avec celui qui l'a acheté depuis l'année où il s'est vendu à lui jusqu'à l'année du Jubilé. Le prix de sa vente sera fonction du nombre d'années; il sera avec lui selon le temps d'un mercenaire.
51 Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
S'il reste encore beaucoup d'années, il restituera le prix de son rachat sur l'argent pour lequel il a été acheté.
52 Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
S'il ne reste que quelques années jusqu'à l'année du jubilé, on fera le compte avec lui; il rendra le prix de son rachat selon ses années de service.
53 Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
Il sera avec lui comme un serviteur loué d'année en année. Il ne régnera pas sur lui avec dureté à tes yeux.
54 Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
S'il n'est pas racheté par ces moyens, il sera libéré l'année du Jubilé, lui et ses enfants avec lui.
55 Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Car pour moi, les enfants d'Israël sont des serviteurs, ce sont mes serviteurs que j'ai fait sortir du pays d'Égypte. Je suis Yahvé votre Dieu.