< Mambo ya Walawi 25 >

1 Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
And he spoke Yahweh to Moses on [the] mountain of Sinai saying.
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
Speak to [the] people of Israel and you will say to them if you will go into the land which I [am] about to give to you and it will cease the land a sabbath to Yahweh.
3 Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
Six years you will sow field your and six years you will prune vineyard your and you will gather produce its.
4 Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
And in the year seventh a sabbath of sabbath observance it will belong to the land a sabbath to Yahweh field your not you will sow and vineyard your not you will prune.
5 Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
[the] self-sown grain of Harvest your not you will harvest and [the] grapes untrimmed vines your not you will gather grapes a year of sabbath observance it will belong to the land.
6 Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
And it will belong [the] sabbath of the land to you to food to you and to [male] slave your and to female slave your and to hired laborer your and to resident alien your who are sojourning with you.
7 Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
And to livestock your and to the animal[s] which [is] in land your it will be all produce its to eat.
8 Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
And you will count for yourself seven sabbaths of years seven years seven times and they will be to you [the] days of seven [the] sabbaths of years nine and forty year[s].
9 Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
And you will cause to pass through a ram's horn of [the] sound of a loud blast in the month seventh on the ten of the month on [the] day of atonement you will cause to pass a ram's horn in all land your.
10 Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
And you will set apart as holy [the] year of the fifty year and you will proclaim liberty in the land for all inhabitants its a jubilee it it will be to you and you will return each one to possession his and each one to clan his you will return.
11 Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
A jubilee it [the] year of the fifty year it will be to you not you will sow and not you will harvest self-sown grain its and not you will gather grapes untrimmed vines its.
12 Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
For [is] a jubilee it a holy thing it will be to you from the field you will eat produce its.
13 Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
In [the] year of the jubilee this you will return each one to possession his.
14 Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
And if you will sell a thing sold to fellow citizen your or you will buy from [the] hand of fellow citizen your may not you maltreat each brother his.
15 Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
By [the] number of years after the jubilee you will buy from with fellow citizen your by [the] number of [the] years of produce he will sell [it] to you.
16 Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
To [the] mouth of - [the] abundance of the years you will increase purchase price its and to [the] mouth of [the] being small of the years you will make small purchase price its for [the] number of produce he [is] selling to you.
17 Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
And not you will maltreat anyone fellow citizen his and you will fear from God your for I [am] Yahweh God your.
18 Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
And you will do statutes my and judgments my you will keep and you will do them and you will dwell on the land to security.
19 Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
And it will give the land fruit its and you will eat to abundance and you will dwell to security on it.
20 Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
And if you will say what? will we eat in the year seventh here! not we will sow and not we will gather produce our.
21 Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
And I will command blessing my for you in the year sixth and it will make the produce for [the] three the years.
22 Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
And you will sow the year eighth and you will eat from the produce old harvest until - the year ninth until comes produce its you will eat old harvest.
23 Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
And the land not it will be sold to perpetuity for [belongs] to me the land for [are] sojourners and resident aliens you with me.
24 Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
And in all [the] land of possession your [the] right of redemption you will give of the land.
25 Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
If he will become impoverished brother your and he will sell some of possession his and he will come kinsman-redeemer his near to him and he will redeem [the] thing sold of brother his.
26 Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
And anyone if not he will belong to him a kinsman-redeemer and it will reach hand his and he will find according to [the] sufficiency of redemption its.
27 kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
And he will calculate [the] years of sale its and he will repay the surplus to the person whom he sold [it] to him and he will return to possession his.
28 Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
And if not it has found hand his sufficiency to repay to him and it will be thing sold his in [the] hand of the [one who] bought it until [the] year of the jubilee and it will go out in the jubilee and he will return to possession his.
29 Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
And anyone if he will sell a house of dwelling of a city of a wall and it will be right of redemption its until is finished [the] year of sale its days it will be right of redemption its.
30 Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
And if not it will be redeemed until is completed to it a year complete and it will stand the house which [is] in the city which ([belongs] to it *Q(K)*) a wall to perpetuity to the [one who] bought it to generations his not it will go out in the jubilee.
31 Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
And [the] houses of the villages which not [belongs] to them a wall round about to [the] field of the land it will be reckoned a right of redemption it will belong to it and in the jubilee it will go out.
32 Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
And [the] cities of the Levites [the] houses of [the] cities of possession their a right of redemption of perpetuity it will belong to the Levites.
33 Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
And that he will redeem one of the Levites and it will go out [the] sale of [the] house and [the] city of possession his in the jubilee for [the] houses of [the] cities of the Levites it [is] possession their in among [the] people of Israel.
34 Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
And [the] field of [the] pasture land of cities their not it will be sold for [is] a possession of perpetuity it to them.
35 Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
And if he will become impoverished brother your and it will slip hand his with you and you will strengthen him a sojourner and a resident alien and he will live with you.
36 Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
May not you take from with him interest and profit and you will fear from God your and he will live brother your with you.
37 Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
Silver your not you will give to him for interest and for profit not you will give food your.
38 Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
I [am] Yahweh God your who I brought out you from [the] land of Egypt to give to you [the] land of Canaan to become for you God.
39 Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
And if he will become impoverished brother your with you and he will sell himself to you not you will labor by him [the] labor of a slave.
40 Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
Like a hired laborer like a resident alien he will be with you until [the] year of the jubilee he will serve with you.
41 Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
And he will go out from with you he and sons his with him and he will return to clan his and to [the] possession of ancestors his he will return.
42 Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
For [are] servants my they whom I brought out them from [the] land of Egypt not they will be sold a sale of a slave.
43 Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
Not you will rule over him with harshness and you will fear from God your.
44 Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
And [male] slave your and female slave your who they will belong to you from with the nations which [are] around you from them you will buy a [male] slave and a female slave.
45 Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
And also some of [the] children of the resident aliens who sojourn with you from them you will buy and from clan their which [is] with you which they have fathered in land your and they will belong to you to a possession.
46 Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
And you will give as an inheritance them to sons your after you to take possession of a possession for ever by them you will labor and over brothers your [the] people of Israel each over brother his not you will rule over him with harshness.
47 Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
And if it will reach [the] hand of a sojourner and a resident alien with you and he will become impoverished brother your with him and he will sell himself to a sojourner a resident alien with you or to a member of [the] clan of a sojourner.
48 baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
After he has sold himself a right of redemption it will belong to him one of brothers his he will redeem him.
49 Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
Or uncle his or [the] son of uncle his he will redeem him or any of [the] relative[s] of flesh his from clan his he will redeem him or it has reached hand his and he will redeem himself.
50 Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
And he will calculate with [the] [one who] bought him from [the] year he sold himself to him until [the] year of the jubilee and it will be [the] silver of sale his by [the] number of years according to [the] days of a hired laborer he will be with him.
51 Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
If still many in the years to mouth their he will repay redemption his some of [the] silver of purchase his.
52 Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
And if few it remains in the years until [the] year of the jubilee and he will calculate for himself according to [the] mouth of years his he will repay redemption his.
53 Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
Like a hired laborer of a year in a year he will be with him not he will rule over him with harshness to eyes your.
54 Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
And if not he will be redeemed in these [ways] and he will go out in [the] year of the jubilee he and sons his with him.
55 Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
For of me [the] people of Israel [are] servants [are] servants my they whom I brought out them from [the] land of Egypt I [am] Yahweh God your.

< Mambo ya Walawi 25 >