< Mambo ya Walawi 25 >

1 Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
And Yahweh spake unto Moses in Mount Sinai, saying—
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
Speak unto the sons of Israel, and thou shalt say unto them: —When ye enter into the land which, I, am giving you, then shall the land keep a sabbath unto Yahweh.
3 Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
Six years, shalt thou sow thy field, and, six years, shalt thou prune thy vineyard, —and gather the increase thereof;
4 Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
but, in the seventh year—a sabbath of sacred rest, shall there be unto the land, a sabbath unto Yahweh: thy field, shalt thou not sow, and, thy vineyard, shalt thou not prune;
5 Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
that which groweth of itself of thy harvest, shalt thou not reap; and the grapes of thine unpruned vines, shalt thou not cut off: a year of sacred rest, shall there be to the land.
6 Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
So shall the sabbath of the land be unto you for food: unto thee, and unto thy servant and unto thy handmaid, —and unto thy hireling, and unto thy settlers that are sojourning with thee;
7 Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
and unto thy tame-beasts, and unto the wild-beasts that are in thy land, shall belong all the increase thereof for food.
8 Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
And thou shalt count to thee seven weeks of years, seven years, seven times, —so shall the days of the seven weeks of years become to thee forty-nine years.
9 Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
Then shalt thou cause a signal-horn to pass through in the seventh month, on the tenth of the month: on the Day of Propitiation, shall ye cause a horn to pass throughout all your land.
10 Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
So shall ye hallow the fiftieth year, and proclaim freedom throughout the land to all the dwellers thereof, —a jubilee, shall it be unto you, and ye shall return, every man unto his possession, and every man unto his family, shall ye return.
11 Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
A jubilee, shall that fiftieth year be unto you, —ye shall not sow, neither shall ye reap the self-grown corn thereof, nor cut off the grapes of the unpruned vines thereof.
12 Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
For, a jubilee, it is, holy, shall it be unto you, —out of the field, shall ye eat her increase.
13 Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
In this same jubilee year, shall ye return every man unto his possession.
14 Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
And when ye sell anything to thy neighbour, or buy aught at thy neighbour’s hand, do not overreach one another.
15 Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
By the number of years after the jubilee, shalt thou buy of thy neighbour, —by the number of the years of increase, shall he sell unto thee;
16 Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
according to the multitude of the years, shalt thou increase the price thereof, and, according to the fewness of the years, shalt thou diminish the price thereof, —because the sum of the increase, it is that he selleth thee.
17 Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
So then ye shall not overreach one another; but thou shalt stand in awe of thy God, —for, I—Yahweh, am your God.
18 Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
Wherefore ye shall do my statutes, and my regulations, shall ye observe and do them, —so shall ye dwell upon the land with confidence;
19 Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
and the land shall yield her fruit; and ye shall eat to the full, —and shall dwell with confidence thereupon.
20 Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
And since ye may say, What shall we eat in the seventh year? Lo! we are not to sow, neither are we to gather our increase!
21 Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
Therefore will I command my blessing upon you, in the sixth year, —and it shall make the increase of three years;
22 Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
and ye shall sow, the eighth year, and eat of old store, —until the ninth year until the coming in of the increase thereof, shall ye eat old store.
23 Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
The land moreover shall not be sold beyond recovery, for, mine, is the land, —for, sojourners and settlers, ye are with me.
24 Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
And, in all the land of your possession, a right of redemption, shall ye give to the land.
25 Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
When thy brother waxeth poor, and so selleth aught of his possession, then may his kinsman that is near unto him come in, and redeem that which was sold by his brother.
26 Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
And, when, any man, hath no kinsman, —but his own hand getteth enough, so that he findeth what is needed to redeem it,
27 kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
then shall he reckon the years since he sold it, and restore the overplus to the man to whom he sold it, —and shall return to his possession.
28 Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
But, if his hand have not found enough to get it back unto him, then shall that which he sold remain in the hand of him that bought it, until the year of the jubilee, —and shall go out in the jubilee, and he shall return unto his possession.
29 Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
And, when, any man, selleth a dwelling-house in a walled city, then shall his right of redemption remain until the completion of a year after he sold it, —for, [a year of] days, shall his right of redemption remain.
30 Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
But, if it be not redeemed before the end of a full year, then shall the house that is in the city that hath walls be confirmed, beyond recovery, to him who bought it, unto his generations, —it shall not go out in the jubilee.
31 Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
But as for the houses of villages which have no wall round about them, with the fields of land, shall it be reckoned, —a right of redemption, shall belong to it, and, in the jubilee, shall it go out.
32 Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
And as for the cities of the Levites, the houses of the cities of their possession, an age-abiding right of redemption, shall pertain unto the Levites.
33 Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
And, if one of the Levites should not redeem, then shall the sale of the house and the city of his possession go out in the jubilee; for, the houses of the cities of the Levites are their possession, in the midst of the sons of Israel.
34 Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
But the field of the pasture-land of their cities, shall not be sold, —for an age-abiding possession, it is unto them.
35 Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
And, when thy brother waxeth poor, and his hand becometh feeble with thee, then shalt thou strengthen him, as a sojourner and a settler, so shall he live with thee.
36 Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
Do not accept from him interest or profit, but stand thou in awe of thy God, —so shall thy brother live with thee.
37 Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
Thy silver, shalt thou not give him on interest, —neither, for profit, shalt thou give him thy food.
38 Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
I—Yahweh, am your God, who brought you forth out of the land of Egypt, —to give unto you the land of Canaan, to become your God,
39 Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
And when thy brother waxeth poor with thee, and so selleth himself unto thee, thou shalt not bind him with the bondage of a bondman:
40 Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
as a hired servant, as a settler, shall he remain with thee, —until the year of the jubilee, shall he serve with thee:
41 Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
then shall he go forth from thee, he and his sons with him, —and shall return unto his family, and unto the possession of his fathers, shall he return.
42 Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
For, my bondmen, they are, whom I brought forth out of the land of Egypt, —they shall not sell themselves with the sale of a bondman.
43 Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
Thou shalt not rule over him with rigour, —so shalt thou stand in awe of thy God.
44 Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
And as for thy bondman and thy bond-maid which thou shalt have, of the nations that are round about you—from them, may ye buy bondman and bond-maid.
45 Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
Moreover also, of the sons of the settlers who are sojourning with you—of them, may ye buy, and of their families that are with you, which they have begotten in your land, —so shall they become yours, as a possession;
46 Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
and ye may take them as an inheritance for your sons after you to inherit as a possession, unto times age-abiding, of them, may ye take to be bondmen, —but, over your brethren the sons of Israel—a man over his brother, ye shall not rule, over him with rigour.
47 Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
And, when the hand of the sojourner and settler with thee getteth possessions, and thy brother with him, waxeth poor, —and so he selleth himself to the sojourner [who is] a settler with thee, or to one who hath taken root, of the family of the sojourner,
48 baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
after that he hath sold himself, a right of redemption, pertaineth to him, —one of his brethren, may redeem him;
49 Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
or, his uncle or his uncle’s son, may redeem him, or, a near flesh-relation of his, of his family, may redeem him, or, his own hand may have gotten enough, and, so he may redeem himself.
50 Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
Then shall he reckon with him that bought him, from the year that he was sold to him, unto the year of the jubilee, —and the silver for which he was sold shall be by the number of years, according to the days of a hired servant, shall he be with him.
51 Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
If there is yet a multitude of years, according to them, shall he return, as his redemption price, of the silver of him that bought him.
52 Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
Or, if [there is] but a small remainder of years, until the year of the jubilee, then shall he reckon to himself, according to the years thereof, shall he return his price of redemption.
53 Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
As a servant hired year by year, shall he be with him, he shall not rule over him with rigour, before thine eyes.
54 Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
But if he be not redeemed in any of these ways, then shall he go out in the jubilee year, he, and his sons with him.
55 Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
For, unto me, are the sons of Israel, bondmen, my bondmen, they are, whom I brought forth out of the land of Egypt. I, Yahweh, am your God.

< Mambo ya Walawi 25 >