< Mambo ya Walawi 25 >
1 Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
And YHWH speaks to Moses, in Mount Sinai, saying,
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
“Speak to the sons of Israel, and you have said to them: When you come into the land which I am giving to you, then the land has kept a Sabbath to YHWH.
3 Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
[For] six years you sow your field, and [for] six years you prune your vineyard, and have gathered its increase,
4 Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
and in the seventh year is a Sabbath of rest for the land, a Sabbath to YHWH; you do not sow your field, and you do not prune your vineyard;
5 Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
you do not reap the spontaneous growth of your harvest, and you do not gather the grapes of your separated thing; it is a year of rest for the land.
6 Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
And the Sabbath [increase] of the land has been for you for food, to you, and to your manservant, and to your handmaid, and to your hired worker, and to your settler, who are sojourning with you;
7 Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
and for your livestock, and for the beast which [is] in your land, is all its increase for [them] to eat.
8 Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
And you have numbered seven Sabbaths of years for yourself, seven times seven years, and the days of the seven Sabbaths of years have been forty-nine years for you,
9 Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
and you have caused a horn of shouting to pass over in the seventh month, on the tenth of the month; in the Day of Atonements you cause a horn to pass over through all your land;
10 Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
and you have hallowed the year, the fiftieth year; and you have proclaimed liberty in the land to all its inhabitants; it is a Jubilee for you; and you have turned back each to his possession; indeed, you return each to his family.
11 Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
It [is] a Jubilee, the fiftieth year, it is a year for you; you do not sow, nor reap its spontaneous growth, nor gather its separated things;
12 Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
for it [is] a Jubilee—it is holy to you; you eat its increase from the field;
13 Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
you return each to his possession in this Year of the Jubilee.
14 Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
And when you sell anything to your fellow, or buy from the hand of your fellow, you do not oppress one another;
15 Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
you buy from your fellow by the number of years after the Jubilee; he sells to you by the number of the years of increase;
16 Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
you multiply its price according to the multitude of the years, and you diminish its price according to the fewness of the years; for [it is] a number of increases [that] he is selling to you;
17 Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
and you do not oppress one another, and you have been afraid of your God; for I [am] your God YHWH.
18 Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
And you have done My statutes, and you keep My judgments, and have done them, and you have dwelt on the land confidently,
19 Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
and the land has given its fruit, and you have eaten to satiety, and have dwelt confidently on it.
20 Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
And when you say, What do we eat in the seventh year, behold, do we not sow, nor gather our increase?
21 Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
Then I have commanded My blessing on you in the sixth year, and it has made the increase for three years;
22 Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
and you have sown [in] the eighth year, and have eaten of the old increase; you eat the old until the ninth year, until the coming in of its increase.
23 Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
And the land is not sold—to extinction, for the land [is] Mine, for you [are] sojourners and settlers with Me;
24 Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
and in all the land of your possession you give a redemption for the land.
25 Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
When your brother becomes poor, and has sold his possession, then his redeemer who is near to him has come, and he has redeemed the sold thing of his brother;
26 Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
and when a man has no redeemer, and his own hand has attained [means], and he has found [it] as sufficient [for] its redemption,
27 kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
then he has reckoned the years of its sale, and has given back that which is over to the man to whom he sold [it], and he has returned to his possession.
28 Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
And if his hand has not found sufficiency to give back to him, then his sold thing has been in the hand of him who buys it until the Year of Jubilee; and it has gone out in the Jubilee, and he has returned to his possession.
29 Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
And when a man sells a dwelling-house [in] a walled city, then his right of redemption has been until the completion of a year from its selling; his right of redemption is [during these] days;
30 Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
and if it is not redeemed to him until the fullness of a perfect year, then the house which [is] in a walled city has been established to extinction to him buying it, throughout his generations; it does not go out in the Jubilee.
31 Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
And a house of the villages which have no surrounding wall is reckoned on the field of the country; there is redemption for it, and it goes out in the Jubilee.
32 Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
As for cities of the Levites—houses of the cities of their possession—continuous redemption is for the Levites;
33 Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
as for him who redeems from the Levites, then the sale of a house (and [in] the city of his possession) has gone out in the Jubilee, for the houses of the cities of the Levites are their possession in the midst of the sons of Israel.
34 Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
And a field, a outskirt of their cities, is not sold; for it [is] a continuous possession for them.
35 Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
And when your brother has become poor, and his hand has failed with you, then you have kept hold on him, sojourner and settler, and he has lived with you;
36 Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
you take no usury or increase from him; and you have been afraid of your God; and your brother has lived with you;
37 Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
you do not give your money to him in usury, and you do not give your food for increase.
38 Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
I [am] your God YHWH, who has brought you out of the land of Egypt to give the land of Canaan to you, to become your God.
39 Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
And when your brother becomes poor with you, and he has been sold to you, you do not lay servile service on him;
40 Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
he is as a hired worker [and] as a settler with you; he serves with you until the Year of the Jubilee—
41 Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
then he has gone out from you, he and his sons with him, and has turned back to his family; and he turns back to the possession of his fathers.
42 Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
For they [are] My servants, whom I have brought out from the land of Egypt: they are not sold [with] the sale of a servant;
43 Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
you do not rule over him with rigor, and you have been afraid of your God.
44 Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
And your manservant and your handmaid whom you have [are] from the nations who [are] around you; you buy manservant and handmaid from them,
45 Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
and also from the sons of the settlers who are sojourning with you, you buy from them, and from their families who [are] with you, which they have begotten in your land, and they have been to you for a possession;
46 Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
and you have taken them for an inheritance for your sons after you, to inherit [for] a possession; you lay service on them for all time, but on your brothers, the sons of Israel, each with his brother—you do not rule over him with rigor.
47 Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
And when the hand of a sojourner or settler with you attains [riches], and your brother with him has become poor, and he has been sold to a sojourner, a settler with you, or to the root of the family of a sojourner,
48 baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
after he has been sold, there is a right of redemption for him; one of his brothers redeems him,
49 Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
or his uncle or a son of his uncle redeems him, or any of the relations of his flesh, of his family, redeems him, or [if] his own hand has attained [means] then he has been redeemed.
50 Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
And he has reckoned with his buyer from the year of his being sold to him until the Year of Jubilee, and the money of his sale has been by the number of years; it is with him as the days of a hired worker.
51 Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
If many years still [remain], he gives back his redemption [money] according to them, from the money of his purchase.
52 Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
And if few are left of the years until the Year of Jubilee, then he has reckoned with him [and] he gives back his redemption [money] according to his years;
53 Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
as a hired worker, year by year, he is with him, and he does not rule him with rigor before your eyes.
54 Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
And if he is not redeemed in these [years], then he has gone out in the Year of Jubilee, he and his sons with him.
55 Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
For the sons of Israel [are] servants to Me; they [are] My servants whom I have brought out of the land of Egypt; I [am] your God YHWH.”