< Mambo ya Walawi 25 >

1 Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
And the LORD spoke to Moses in mount Sinai, saying,
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
Speak to the children of Israel, and say to them, When you come into the land which I give you, then shall the land keep a sabbath to the LORD.
3 Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
Six years you shall sow your field, and six years you shall prune your vineyard, and gather in the fruit thereof;
4 Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
But in the seventh year shall be a sabbath of rest to the land, a sabbath for the LORD: you shall neither sow your field, nor prune your vineyard.
5 Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
That which grows of its own accord of your harvest you shall not reap, neither gather the grapes of your vine undressed: for it is a year of rest to the land.
6 Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
And the sabbath of the land shall be meat for you; for you, and for your servant, and for your maid, and for your hired servant, and for your stranger that sojourns with you.
7 Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
And for your cattle, and for the beast that are in your land, shall all the increase thereof be meat.
8 Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
And you shall number seven sabbaths of years to you, seven times seven years; and the space of the seven sabbaths of years shall be to you forty and nine years.
9 Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
Then shall you cause the trumpet of the jubilee to sound on the tenth day of the seventh month, in the day of atonement shall you make the trumpet sound throughout all your land.
10 Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
And you shall hallow the fiftieth year, and proclaim liberty throughout all the land to all the inhabitants thereof: it shall be a jubilee to you; and you shall return every man to his possession, and you shall return every man to his family.
11 Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
A jubilee shall that fiftieth year be to you: you shall not sow, neither reap that which grows of itself in it, nor gather the grapes in it of your vine undressed.
12 Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
For it is the jubilee; it shall be holy to you: you shall eat the increase thereof out of the field.
13 Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
In the year of this jubilee you shall return every man to his possession.
14 Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
And if you sell something to your neighbor, or buy something of your neighbor’s hand, you shall not oppress one another:
15 Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
According to the number of years after the jubilee you shall buy of your neighbor, and according to the number of years of the fruits he shall sell to you:
16 Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
According to the multitude of years you shall increase the price thereof, and according to the fewness of years you shall diminish the price of it: for according to the number of the years of the fruits does he sell to you.
17 Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
You shall not therefore oppress one another; but you shall fear your God: for I am the LORD your God.
18 Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
Why you shall do my statutes, and keep my judgments, and do them; and you shall dwell in the land in safety.
19 Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
And the land shall yield her fruit, and you shall eat your fill, and dwell therein in safety.
20 Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
And if you shall say, What shall we eat the seventh year? behold, we shall not sow, nor gather in our increase:
21 Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
Then I will command my blessing on you in the sixth year, and it shall bring forth fruit for three years.
22 Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
And you shall sow the eighth year, and eat yet of old fruit until the ninth year; until her fruits come in you shall eat of the old store.
23 Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
The land shall not be sold for ever: for the land is mine, for you are strangers and sojourners with me.
24 Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
And in all the land of your possession you shall grant a redemption for the land.
25 Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
If your brother be waxen poor, and has sold away some of his possession, and if any of his kin come to redeem it, then shall he redeem that which his brother sold.
26 Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
And if the man have none to redeem it, and himself be able to redeem it;
27 kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
Then let him count the years of the sale thereof, and restore the remainder to the man to whom he sold it; that he may return to his possession.
28 Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
But if he be not able to restore it to him, then that which is sold shall remain in the hand of him that has bought it until the year of jubilee: and in the jubilee it shall go out, and he shall return to his possession.
29 Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
And if a man sell a dwelling house in a walled city, then he may redeem it within a whole year after it is sold; within a full year may he redeem it.
30 Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
And if it be not redeemed within the space of a full year, then the house that is in the walled city shall be established for ever to him that bought it throughout his generations: it shall not go out in the jubilee.
31 Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
But the houses of the villages which have no wall round about them shall be counted as the fields of the country: they may be redeemed, and they shall go out in the jubilee.
32 Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
Notwithstanding the cities of the Levites, and the houses of the cities of their possession, may the Levites redeem at any time.
33 Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
And if a man purchase of the Levites, then the house that was sold, and the city of his possession, shall go out in the year of jubilee: for the houses of the cities of the Levites are their possession among the children of Israel.
34 Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
But the field of the suburbs of their cities may not be sold; for it is their perpetual possession.
35 Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
And if your brother be waxen poor, and fallen in decay with you; then you shall relieve him: yes, though he be a stranger, or a sojourner; that he may live with you.
36 Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
Take you no usury of him, or increase: but fear your God; that your brother may live with you.
37 Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
You shall not give him your money on usury, nor lend him your victuals for increase.
38 Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
I am the LORD your God, which brought you forth out of the land of Egypt, to give you the land of Canaan, and to be your God.
39 Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
And if your brother that dwells by you be waxen poor, and be sold to you; you shall not compel him to serve as a bondservant:
40 Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
But as an hired servant, and as a sojourner, he shall be with you, and shall serve you to the year of jubilee.
41 Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
And then shall he depart from you, both he and his children with him, and shall return to his own family, and to the possession of his fathers shall he return.
42 Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
For they are my servants, which I brought forth out of the land of Egypt: they shall not be sold as slaves.
43 Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
You shall not rule over him with rigor; but shall fear your God.
44 Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
Both your slaves, and your bondmaids, which you shall have, shall be of the heathen that are round about you; of them shall you buy slaves and bondmaids.
45 Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
Moreover of the children of the strangers that do sojourn among you, of them shall you buy, and of their families that are with you, which they begat in your land: and they shall be your possession.
46 Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
And you shall take them as an inheritance for your children after you, to inherit them for a possession; they shall be your slaves for ever: but over your brothers the children of Israel, you shall not rule one over another with rigor.
47 Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
And if a sojourner or stranger wax rich by you, and your brother that dwells by him wax poor, and sell himself to the stranger or sojourner by you, or to the stock of the stranger’s family:
48 baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
After that he is sold he may be redeemed again; one of his brothers may redeem him:
49 Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
Either his uncle, or his uncle’s son, may redeem him, or any that is near of kin to him of his family may redeem him; or if he be able, he may redeem himself.
50 Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
And he shall reckon with him that bought him from the year that he was sold to him to the year of jubilee: and the price of his sale shall be according to the number of years, according to the time of an hired servant shall it be with him.
51 Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
If there be yet many years behind, according to them he shall give again the price of his redemption out of the money that he was bought for.
52 Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
And if there remain but few years to the year of jubilee, then he shall count with him, and according to his years shall he give him again the price of his redemption.
53 Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
And as a yearly hired servant shall he be with him: and the other shall not rule with rigor over him in your sight.
54 Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
And if he be not redeemed in these years, then he shall go out in the year of jubilee, both he, and his children with him.
55 Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
For to me the children of Israel are servants; they are my servants whom I brought forth out of the land of Egypt: I am the LORD your God.

< Mambo ya Walawi 25 >