< Mambo ya Walawi 24 >

1 Yahweh akamwambia Musa, akisema,
I PAN powiedział do Mojżesza:
2 “Waamru watu wa Israeli wakuletee mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni ili yatumike kwenye taa, ili kwamba taa ziweze kuwaka daima na kuleta mwanga.
Rozkaż synom Izraela, aby przynieśli ci czystą, wyciśniętą oliwę z oliwek, na oświetlenie, aby lampy ciągle się paliły.
3 Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi ndani ya hema la kukutania, Aroni ataiwasha daima taa mbele za Yahweh, tangu asubuhi hata jioni. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu.
Aaron sporządzi je na zewnątrz zasłony Świadectwa, w Namiocie Zgromadzenia, [aby się paliły] od wieczora aż do poranka przed PANEM nieustannie. Będzie to wieczysta ustawa przez wszystkie wasze pokolenia.
4 Kuhani mkuu atazifanya taa ziwake daima mbele za Yahweh, taa hizo zilizo kwenye kinara cha dhahabu safi.
Będzie ustawiał lampy na czystym świeczniku przed PANEM nieustannie.
5 Yawapasa kuchukua unga laini na kuoka kwa huo mikate kumi na miwili. Ni lazima kuwe na mbili za kumi za efa za unga katika kila mkate.
Weźmiesz też mąki pszennej i upieczesz z niej dwanaście placków, każdy placek będzie z dwóch dziesiątych efy.
6 Kisha mtaipanga juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh katika safu mbili, mikate sita katika kila safu,
Potem ułożysz je w dwóch rzędach, po sześć w [każdym] rzędzie, na czystym stole przed PANEM.
7 Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu ya mikata kuwa sadaka ya kuwakilisha. Uvumba huo utachomwa kwa moto kwa ajili ya Yahweh.
Na [każdy] rząd położysz czystego kadzidła, aby było pamiątką na chlebie, ofiarą spaloną dla PANA.
8 Kila siku ya Sabato kuhani mkuu sharti aipange kwa utaratibu hiyo mikate mbele za Yahweh kwa niaba ya watu wa Israeli, iwe ishara ya agano la milele.
W każdy dzień szabatu [kapłan] będzie je nieustannie układać przed PANEM, biorąc je od synów Izraela jako wieczne przymierze.
9 Sadaka hii itakuwa kwa ajili ya Aroni na wanawe, na ni lazima waile mahali palipo patakatifu, kwa kuwa ni sehemu ya matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto.”
I będą [należały] do Aarona i jego synów: będą je jeść w miejscu świętym, gdyż jest to dla nich najświętsza rzecz ze spalanych ofiar PANA jako wieczysta ustawa.
10 Sasa ilitokea kwamba mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye baba yake alikuwa Mmisri, alikwenda miongoni mwa watu wa Israeli. Huyu mwana wa mwanamke Mwisraeli akagombana na mwanume Mwisraeli kambini.
W tym czasie syn Izraelitki, którego ojcem był Egipcjanin, wyszedł między synów Izraela. I pokłócił się w obozie syn [tej] Izraelitki z pewnym Izraelitą.
11 Mwana wa mwanamke Mwisraeli akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu, kwa hiyo watu wakamleta kwa Musa. Jina la mama yake aliitwa Shelomithi, binti wa Dibri, kutoka kabila la Dani.
I syn Izraelitki bluźnił imieniu [PANA] i przeklinał. Przyprowadzono go więc do Mojżesza. A jego matce było na imię Szelomit, [była] córką Dibriego, z pokolenia Dana.
12 Wakamweka kizuizini mpaka Yahweh mwenyewe atakapotangaza mapenzi yake kwao.
I osadzili go pod strażą, żeby im oznajmiono, co PAN rozkaże uczynić.
13 Kisha Yahweh akamwambia Musa,
Wtedy PAN powiedział do Mojżesza:
14 “Mchukue nje ya kambi huyo aliyemlaani Mungu. Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake, na kisha kusanyiko lote watamponda kwa mawe.
Wyprowadź bluźniercę poza obóz i niech wszyscy, którzy to słyszeli, położą swoje ręce na jego głowie i niech ukamienuje go całe zgromadzenie.
15 Ni lazima uwaeleze watu wa Israeli na kusema, 'Yeyote anayemlaani Mungu wake imempasa kubeba hatia yake mwenyewe.
A synom Izraela powiedz tak: Ktokolwiek przeklnie swego Boga, obciąży się swym grzechem.
16 Yeye anayelikufuru jina la Yahweh kwa hakika ni lazima auawe. Hakika, kusanyiko lote litampiga mawe, ama awe mgeni au Mwisraeli mwenyeji mzaliwa. Ikiwa yeyote analikufuru jina la Yahweh, ni lazima auawe.
Ten również, kto zbluźnił imieniu PANA, poniesie śmierć: Ukamienuje go całe zgromadzenie. Zarówno przybysz, jak i rodowity mieszkaniec, jeśli zbluźni imieniu PANA, poniesie śmierć.
17 Naye amuuaye mtu mwingine ni lazima kwa hakika auewa.
Każdy, kto zabije jakiegokolwiek człowieka, poniesie śmierć.
18 Yeye anayemuua mnyama wa mwingine sharti amfidie, uhai kwa uhai.
A kto zabije zwierzę, zwróci inne: zwierzę za zwierzę.
19 Iwapo mtu anamjeruhi jirani yake, ni lazima atendewe vivyo hivyo alivyomtendea jirani yake:
Kto też ranił swego bliźniego, niech mu uczynią tak, jak on uczynił.
20 Mvunjiko kwa mvunjiko, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama amesababisha jeraha kwa mtu, ndivyo ipasavyo kutendwa kwake.
Złamanie za złamanie, oko za oko, ząb za ząb; jak ranił człowieka, tak niech mu oddadzą.
21 Yeyote auaye mnyama ni lazima amfidie, na yeyote auaye mtu ni lazima auawe.
Kto zabije zwierzę, zwróci inne; lecz kto zabije człowieka, poniesie śmierć.
22 Ni lazima mwe na sheria moja kwa wote, mgeni na Mwisraeli mwenyeji mzaliwa, kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wanu.”
Będziecie mieli jedno prawo zarówno dla przybysza, jak i dla rodowitego mieszkańca, gdyż ja jestem PAN, wasz Bóg.
23 Kwa hiyo Musa akazungumza na watu wa Israeli, nao watu wakamleta mwanaume huyo nje ya kambi, yule ambaye alikuwa amemlaani Yahweh. Wakampiga kwa mawe. Watu waisraeli wakaitekeleza amri ya Yahweh aliyoitoa kupitia Musa.
I Mojżesz przemówił do synów Izraela, a wyprowadzili bluźniercę poza obóz i ukamienowali go. I synowie Izraela uczynili tak, jak PAN przykazał Mojżeszowi.

< Mambo ya Walawi 24 >