< Mambo ya Walawi 24 >

1 Yahweh akamwambia Musa, akisema,
Et l'Éternel parla à Moïse, en disant:
2 “Waamru watu wa Israeli wakuletee mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni ili yatumike kwenye taa, ili kwamba taa ziweze kuwaka daima na kuleta mwanga.
Ordonne aux enfants d'Israël qu'ils t'apportent de l'huile pure, d'olives broyées, pour le luminaire, afin de tenir les lampes continuellement allumées.
3 Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi ndani ya hema la kukutania, Aroni ataiwasha daima taa mbele za Yahweh, tangu asubuhi hata jioni. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu.
Aaron les arrangera, en dehors du voile du Témoignage, dans le tabernacle d'assignation, afin qu'elles brûlent du soir au matin, devant l'Éternel, continuellement; c'est une ordonnance perpétuelle dans vos générations.
4 Kuhani mkuu atazifanya taa ziwake daima mbele za Yahweh, taa hizo zilizo kwenye kinara cha dhahabu safi.
Il arrangera les lampes sur le chandelier d'or pur, devant l'Éternel, continuellement.
5 Yawapasa kuchukua unga laini na kuoka kwa huo mikate kumi na miwili. Ni lazima kuwe na mbili za kumi za efa za unga katika kila mkate.
Tu prendras aussi de la fleur de farine, et tu la cuiras en douze gâteaux; chaque gâteau sera de deux dixièmes;
6 Kisha mtaipanga juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh katika safu mbili, mikate sita katika kila safu,
Et tu les placeras en deux rangées, six par rangée, sur la table d'or pur devant l'Éternel.
7 Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu ya mikata kuwa sadaka ya kuwakilisha. Uvumba huo utachomwa kwa moto kwa ajili ya Yahweh.
Et tu mettras de l'encens pur sur chaque rangée, et il sera un mémorial pour le pain, comme un sacrifice fait par le feu à l'Éternel:
8 Kila siku ya Sabato kuhani mkuu sharti aipange kwa utaratibu hiyo mikate mbele za Yahweh kwa niaba ya watu wa Israeli, iwe ishara ya agano la milele.
Chaque jour de sabbat on rangera ces pains devant l'Éternel continuellement de la part des enfants d'Israël; c'est une alliance perpétuelle.
9 Sadaka hii itakuwa kwa ajili ya Aroni na wanawe, na ni lazima waile mahali palipo patakatifu, kwa kuwa ni sehemu ya matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto.”
Et ils appartiendront à Aaron et à ses fils, qui les mangeront dans un lieu saint; car ce sera pour eux une chose très sainte, provenant des sacrifices de l'Éternel faits par le feu; c'est une ordonnance perpétuelle.
10 Sasa ilitokea kwamba mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye baba yake alikuwa Mmisri, alikwenda miongoni mwa watu wa Israeli. Huyu mwana wa mwanamke Mwisraeli akagombana na mwanume Mwisraeli kambini.
Or, le fils d'une femme israélite, qui était fils d'un homme égyptien, sortit au milieu des enfants d'Israël; et ce fils d'une femme israélite se querella dans le camp avec un homme israélite.
11 Mwana wa mwanamke Mwisraeli akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu, kwa hiyo watu wakamleta kwa Musa. Jina la mama yake aliitwa Shelomithi, binti wa Dibri, kutoka kabila la Dani.
Et le fils de la femme israélite blasphéma le nom de l'Éternel, et le maudit; et on l'amena à Moïse. Or sa mère s'appelait Shelomith, fille de Dibri, de la tribu de Dan.
12 Wakamweka kizuizini mpaka Yahweh mwenyewe atakapotangaza mapenzi yake kwao.
Et on le mit en prison, jusqu'à ce qu'il y eût décision, selon l'ordre de l'Éternel.
13 Kisha Yahweh akamwambia Musa,
Or l'Éternel parla à Moïse, en disant:
14 “Mchukue nje ya kambi huyo aliyemlaani Mungu. Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake, na kisha kusanyiko lote watamponda kwa mawe.
Fais sortir du camp celui qui a maudit, et que tous ceux qui l'ont entendu posent leurs mains sur sa tête, et toute l'assemblée le lapidera.
15 Ni lazima uwaeleze watu wa Israeli na kusema, 'Yeyote anayemlaani Mungu wake imempasa kubeba hatia yake mwenyewe.
Et parle aux enfants d'Israël, et dis-leur: Quiconque maudira son Dieu portera la peine de son péché;
16 Yeye anayelikufuru jina la Yahweh kwa hakika ni lazima auawe. Hakika, kusanyiko lote litampiga mawe, ama awe mgeni au Mwisraeli mwenyeji mzaliwa. Ikiwa yeyote analikufuru jina la Yahweh, ni lazima auawe.
Et celui qui blasphémera le nom de l'Éternel sera puni de mort; toute l'assemblée le lapidera; aussi bien l'étranger que celui qui est né au pays, quand il blasphémera le nom de l'Éternel, il sera mis à mort.
17 Naye amuuaye mtu mwingine ni lazima kwa hakika auewa.
Celui qui frappera mortellement un homme, quel qu'il soit, sera puni de mort.
18 Yeye anayemuua mnyama wa mwingine sharti amfidie, uhai kwa uhai.
Celui qui frappera une bête mortellement, la remplacera; vie pour vie.
19 Iwapo mtu anamjeruhi jirani yake, ni lazima atendewe vivyo hivyo alivyomtendea jirani yake:
Et quand un homme aura fait une blessure à son prochain, on lui fera comme il a fait;
20 Mvunjiko kwa mvunjiko, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama amesababisha jeraha kwa mtu, ndivyo ipasavyo kutendwa kwake.
Fracture pour fracture, œil pour œil, dent pour dent; il lui sera fait le même mal qu'il aura fait à un autre homme.
21 Yeyote auaye mnyama ni lazima amfidie, na yeyote auaye mtu ni lazima auawe.
Celui qui aura tué une bête, la remplacera; mais celui qui aura tué un homme, sera mis à mort.
22 Ni lazima mwe na sheria moja kwa wote, mgeni na Mwisraeli mwenyeji mzaliwa, kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wanu.”
Vous n'aurez qu'une même loi; l'étranger sera comme celui qui est né au pays; car je suis l'Éternel votre Dieu.
23 Kwa hiyo Musa akazungumza na watu wa Israeli, nao watu wakamleta mwanaume huyo nje ya kambi, yule ambaye alikuwa amemlaani Yahweh. Wakampiga kwa mawe. Watu waisraeli wakaitekeleza amri ya Yahweh aliyoitoa kupitia Musa.
Moïse parla donc aux enfants d'Israël, et ils firent sortir du camp celui qui avait maudit, et ils le lapidèrent. Ainsi les enfants d'Israël firent comme l'Éternel avait commandé à Moïse.

< Mambo ya Walawi 24 >