< Mambo ya Walawi 24 >
1 Yahweh akamwambia Musa, akisema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Waamru watu wa Israeli wakuletee mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni ili yatumike kwenye taa, ili kwamba taa ziweze kuwaka daima na kuleta mwanga.
Command [the] people of Israel so they may bring to you oil of olive[s] pure pressed for the light to lift up a lamp continually.
3 Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi ndani ya hema la kukutania, Aroni ataiwasha daima taa mbele za Yahweh, tangu asubuhi hata jioni. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu.
From [the] outside of [the] curtain of the testimony in [the] tent of meeting he will arrange it Aaron from evening until morning before Yahweh continually a statute of perpetuity to generations your.
4 Kuhani mkuu atazifanya taa ziwake daima mbele za Yahweh, taa hizo zilizo kwenye kinara cha dhahabu safi.
On the lampstand pure he will arrange the lamps before Yahweh continually.
5 Yawapasa kuchukua unga laini na kuoka kwa huo mikate kumi na miwili. Ni lazima kuwe na mbili za kumi za efa za unga katika kila mkate.
And you will take fine flour and you will bake it two [plus] ten round perforated breads two tenths it will be the round perforated bread one.
6 Kisha mtaipanga juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh katika safu mbili, mikate sita katika kila safu,
And you will place them two rows six the row on the table pure before Yahweh.
7 Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu ya mikata kuwa sadaka ya kuwakilisha. Uvumba huo utachomwa kwa moto kwa ajili ya Yahweh.
And you will put on the row frankincense pure and it will belong to the bread to a memorial offering a fire offering to Yahweh.
8 Kila siku ya Sabato kuhani mkuu sharti aipange kwa utaratibu hiyo mikate mbele za Yahweh kwa niaba ya watu wa Israeli, iwe ishara ya agano la milele.
On [the] day of the sabbath on [the] day of the sabbath he will arrange it before Yahweh continually from with [the] people of Israel a covenant of perpetuity.
9 Sadaka hii itakuwa kwa ajili ya Aroni na wanawe, na ni lazima waile mahali palipo patakatifu, kwa kuwa ni sehemu ya matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto.”
And it will belong to Aaron and to sons his and they will eat it in a place holy for [is] a holy thing of holy things it for him from [the] fire offerings of Yahweh a prescribed portion of perpetuity.
10 Sasa ilitokea kwamba mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye baba yake alikuwa Mmisri, alikwenda miongoni mwa watu wa Israeli. Huyu mwana wa mwanamke Mwisraeli akagombana na mwanume Mwisraeli kambini.
And he went out a son of a woman Israelite and he [was] a son of a man Egyptian in among [the] people of Israel and they struggled together in the camp [the] son of the Israelite [woman] and [the] man of the Israelite[s].
11 Mwana wa mwanamke Mwisraeli akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu, kwa hiyo watu wakamleta kwa Musa. Jina la mama yake aliitwa Shelomithi, binti wa Dibri, kutoka kabila la Dani.
And he slandered [the] son of the woman Israelite the name and he cursed and people brought him to Moses and [the] name of mother his [was] Shelomith [the] daughter of Dibri of [the] tribe of Dan.
12 Wakamweka kizuizini mpaka Yahweh mwenyewe atakapotangaza mapenzi yake kwao.
And they placed him in custody to decide for themselves on [the] mouth of Yahweh.
13 Kisha Yahweh akamwambia Musa,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
14 “Mchukue nje ya kambi huyo aliyemlaani Mungu. Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake, na kisha kusanyiko lote watamponda kwa mawe.
Bring out the [one who] cursed to from [the] outside of the camp and they will lean all those [who] heard hands their on head his and they will stone him all the congregation.
15 Ni lazima uwaeleze watu wa Israeli na kusema, 'Yeyote anayemlaani Mungu wake imempasa kubeba hatia yake mwenyewe.
And to [the] people of Israel you will speak saying a person a person if he will curse God his and he will bear sin his.
16 Yeye anayelikufuru jina la Yahweh kwa hakika ni lazima auawe. Hakika, kusanyiko lote litampiga mawe, ama awe mgeni au Mwisraeli mwenyeji mzaliwa. Ikiwa yeyote analikufuru jina la Yahweh, ni lazima auawe.
And [one who] slanders [the] name of Yahweh certainly he will be put to death certainly they will stone him all the congregation as the sojourner as the native-born when slanders he [the] name he will be put to death.
17 Naye amuuaye mtu mwingine ni lazima kwa hakika auewa.
And anyone if he will strike down any life of humankind certainly he will be put to death.
18 Yeye anayemuua mnyama wa mwingine sharti amfidie, uhai kwa uhai.
And [one who] strikes down [the] life of an animal he will repay it a life for a life.
19 Iwapo mtu anamjeruhi jirani yake, ni lazima atendewe vivyo hivyo alivyomtendea jirani yake:
And anyone if he will make a blemish on fellow citizen his just as he has done so it will be done to him.
20 Mvunjiko kwa mvunjiko, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama amesababisha jeraha kwa mtu, ndivyo ipasavyo kutendwa kwake.
A fracture for a fracture an eye for an eye a tooth for a tooth just as he will make a blemish on person so it will be made on him.
21 Yeyote auaye mnyama ni lazima amfidie, na yeyote auaye mtu ni lazima auawe.
And [one who] strikes down an animal he will repay it and [one who] strikes down a person he will be put to death.
22 Ni lazima mwe na sheria moja kwa wote, mgeni na Mwisraeli mwenyeji mzaliwa, kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wanu.”
Judgment one it will belong to you as the sojourner as the native-born it will be for I [am] Yahweh God your.
23 Kwa hiyo Musa akazungumza na watu wa Israeli, nao watu wakamleta mwanaume huyo nje ya kambi, yule ambaye alikuwa amemlaani Yahweh. Wakampiga kwa mawe. Watu waisraeli wakaitekeleza amri ya Yahweh aliyoitoa kupitia Musa.
And he spoke Moses to [the] people of Israel and they brought out the [one who] had cursed to from [the] outside of the camp and they stoned him stone[s] and [the] people of Israel they did just as he had commanded Yahweh Moses.