< Mambo ya Walawi 24 >
1 Yahweh akamwambia Musa, akisema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
2 “Waamru watu wa Israeli wakuletee mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni ili yatumike kwenye taa, ili kwamba taa ziweze kuwaka daima na kuleta mwanga.
“Enjoin the children of Israel [God prevails], that they bring to you pure olive oil beaten for the light, to cause a menorah ·lamp· to burn continually.
3 Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi ndani ya hema la kukutania, Aroni ataiwasha daima taa mbele za Yahweh, tangu asubuhi hata jioni. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu.
Outside of the veil of the Testimony, in the Tent of Meeting, shall Aaron [Light-bringer] keep it in order from evening to morning before Adonai continually: it shall be a statute forever throughout all your generations.
4 Kuhani mkuu atazifanya taa ziwake daima mbele za Yahweh, taa hizo zilizo kwenye kinara cha dhahabu safi.
He shall keep in order the menorah ·lamp· candles on the pure gold menorah ·lamp· before Adonai continually.
5 Yawapasa kuchukua unga laini na kuoka kwa huo mikate kumi na miwili. Ni lazima kuwe na mbili za kumi za efa za unga katika kila mkate.
“You shall take fine flour, and bake twelve cakes of it: one tenth of an ephah [two omers; 4.6 q; 4.4 L] shall be in one cake.
6 Kisha mtaipanga juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh katika safu mbili, mikate sita katika kila safu,
You shall set them in two rows, six on a row, on the pure gold table before Adonai.
7 Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu ya mikata kuwa sadaka ya kuwakilisha. Uvumba huo utachomwa kwa moto kwa ajili ya Yahweh.
You shall put pure frankincense on each row, that it may be to the bread for a memorial, even an offering made by fire to Adonai.
8 Kila siku ya Sabato kuhani mkuu sharti aipange kwa utaratibu hiyo mikate mbele za Yahweh kwa niaba ya watu wa Israeli, iwe ishara ya agano la milele.
Every Shabath ·Intermission· day he shall set it in order before Adonai continually. It is on the behalf of the children of Israel [God prevails] an everlasting covenant.
9 Sadaka hii itakuwa kwa ajili ya Aroni na wanawe, na ni lazima waile mahali palipo patakatifu, kwa kuwa ni sehemu ya matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto.”
It shall be for Aaron [Light-bringer] and his sons; and they shall eat it in a holy place: for it is most holy to him of the offerings of Adonai made by fire by a perpetual statute.”
10 Sasa ilitokea kwamba mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye baba yake alikuwa Mmisri, alikwenda miongoni mwa watu wa Israeli. Huyu mwana wa mwanamke Mwisraeli akagombana na mwanume Mwisraeli kambini.
The son of an Israelite [Descendant of God prevails] woman, whose father was an Egyptian [person from Abode of slavery], went out among the children of Israel [God prevails]; and the son of the Israelite [Descendant of God prevails] woman and a man of Israel [God prevails] strove together in the camp.
11 Mwana wa mwanamke Mwisraeli akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu, kwa hiyo watu wakamleta kwa Musa. Jina la mama yake aliitwa Shelomithi, binti wa Dibri, kutoka kabila la Dani.
The son of the Israelite [Descendant of God prevails] woman blasphemed HaShem [The Name], and cursed; and they brought him to Moses [Drawn out]. His mother’s name was Shelomith, the daughter of Dibri, of the tribe of Dan [He judged].
12 Wakamweka kizuizini mpaka Yahweh mwenyewe atakapotangaza mapenzi yake kwao.
They put him in custody, until Adonai’s will should be declared to them.
13 Kisha Yahweh akamwambia Musa,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
14 “Mchukue nje ya kambi huyo aliyemlaani Mungu. Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake, na kisha kusanyiko lote watamponda kwa mawe.
“Bring out of the camp him who cursed; and let all who sh'ma ·heard obeyed· him lay their hands on his head, and let all the congregation stone him.
15 Ni lazima uwaeleze watu wa Israeli na kusema, 'Yeyote anayemlaani Mungu wake imempasa kubeba hatia yake mwenyewe.
You shall speak to the children of Israel [God prevails], saying, ‘Whoever curses his God shall bear his crime deserving penalty, sin ·missing the goal·.
16 Yeye anayelikufuru jina la Yahweh kwa hakika ni lazima auawe. Hakika, kusanyiko lote litampiga mawe, ama awe mgeni au Mwisraeli mwenyeji mzaliwa. Ikiwa yeyote analikufuru jina la Yahweh, ni lazima auawe.
He who blasphemes Adonai’s name, he shall surely be put to death. All the congregation shall certainly stone him. The foreigner as well as the native-born, when he blasphemes HaShem [The Name], shall be put to death.
17 Naye amuuaye mtu mwingine ni lazima kwa hakika auewa.
“‘He who strikes any man mortally shall surely be put to death.
18 Yeye anayemuua mnyama wa mwingine sharti amfidie, uhai kwa uhai.
He who strikes an animal mortally shall make it good, life for life.
19 Iwapo mtu anamjeruhi jirani yake, ni lazima atendewe vivyo hivyo alivyomtendea jirani yake:
If anyone injures his neighbor; as he has done, so shall it be done to him:
20 Mvunjiko kwa mvunjiko, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama amesababisha jeraha kwa mtu, ndivyo ipasavyo kutendwa kwake.
fracture for fracture, eye for eye, tooth for tooth; as he has injured someone, so shall it be done to him.
21 Yeyote auaye mnyama ni lazima amfidie, na yeyote auaye mtu ni lazima auawe.
He who kills an animal shall make it good; and he who kills a man shall be put to death.
22 Ni lazima mwe na sheria moja kwa wote, mgeni na Mwisraeli mwenyeji mzaliwa, kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wanu.”
You shall have one kind of judgment for the foreigner as well as the native-born; for I am Adonai your God.’”
23 Kwa hiyo Musa akazungumza na watu wa Israeli, nao watu wakamleta mwanaume huyo nje ya kambi, yule ambaye alikuwa amemlaani Yahweh. Wakampiga kwa mawe. Watu waisraeli wakaitekeleza amri ya Yahweh aliyoitoa kupitia Musa.
Moses [Drawn out] spoke to the children of Israel [God prevails]; and they brought out him who had cursed out of the camp, and stoned him with stones. The children of Israel [God prevails] did as Adonai enjoined Moses [Drawn out].