< Mambo ya Walawi 24 >

1 Yahweh akamwambia Musa, akisema,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
2 “Waamru watu wa Israeli wakuletee mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni ili yatumike kwenye taa, ili kwamba taa ziweze kuwaka daima na kuleta mwanga.
Command the children of Israel, that they bring unto thee pure beaten olive-oil, for the lighting, to cause the lamp to burn continually.
3 Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi ndani ya hema la kukutania, Aroni ataiwasha daima taa mbele za Yahweh, tangu asubuhi hata jioni. Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu.
Without the vail of the testimony, in the tabernacle of the congregation, shall Aaron put it in order [for] from evening unto morning before the Lord continually; as a statute for ever in your generations.
4 Kuhani mkuu atazifanya taa ziwake daima mbele za Yahweh, taa hizo zilizo kwenye kinara cha dhahabu safi.
Upon the pure candlestick shall be put in order the lamps, before the Lord, continually.
5 Yawapasa kuchukua unga laini na kuoka kwa huo mikate kumi na miwili. Ni lazima kuwe na mbili za kumi za efa za unga katika kila mkate.
And thou shalt take fine flour, and bake thereof twelve cakes: of two tenth parts shall each one cake be.
6 Kisha mtaipanga juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh katika safu mbili, mikate sita katika kila safu,
And thou shalt place them in two rows, six in a row, upon the pure table before the Lord.
7 Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu ya mikata kuwa sadaka ya kuwakilisha. Uvumba huo utachomwa kwa moto kwa ajili ya Yahweh.
And thou shalt put upon each row pure frankincense, that it may be unto the bread for a memorial, as a fire-offering unto the Lord.
8 Kila siku ya Sabato kuhani mkuu sharti aipange kwa utaratibu hiyo mikate mbele za Yahweh kwa niaba ya watu wa Israeli, iwe ishara ya agano la milele.
On every and each sabbath day shall he place it in order before the Lord continually, [obtained] from the children of Israel as an everlasting covenant.
9 Sadaka hii itakuwa kwa ajili ya Aroni na wanawe, na ni lazima waile mahali palipo patakatifu, kwa kuwa ni sehemu ya matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto.”
And it shall belong to Aaron and to his sons; and they shall eat it in a holy place; for it is most holy unto him, from the fire-offerings of the Lord, as a perpetual fixed portion.
10 Sasa ilitokea kwamba mwana wa mwanamke Mwisraeli, ambaye baba yake alikuwa Mmisri, alikwenda miongoni mwa watu wa Israeli. Huyu mwana wa mwanamke Mwisraeli akagombana na mwanume Mwisraeli kambini.
And there went forth a son of an Israelitish woman, but who was the son of an Egyptian man, among the children of Israel; and there quarrelled together in the camp this son of the Israelitish woman and an Israelitish man.
11 Mwana wa mwanamke Mwisraeli akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu, kwa hiyo watu wakamleta kwa Musa. Jina la mama yake aliitwa Shelomithi, binti wa Dibri, kutoka kabila la Dani.
And the son of the Israelitish woman pronounced the [holy] Name, and blasphemed; and they brought him unto Moses: [and his mother's name was Shelomith, the daughter of Dibri, of the tribe of Dan; ]
12 Wakamweka kizuizini mpaka Yahweh mwenyewe atakapotangaza mapenzi yake kwao.
And they placed him in ward, until the decision of the Lord could be explained to them.
13 Kisha Yahweh akamwambia Musa,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
14 “Mchukue nje ya kambi huyo aliyemlaani Mungu. Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake, na kisha kusanyiko lote watamponda kwa mawe.
Lead forth the blasphemer to without the camp; and all that have heard him shall lay their hands upon his head; and all the congregation shall stone him.
15 Ni lazima uwaeleze watu wa Israeli na kusema, 'Yeyote anayemlaani Mungu wake imempasa kubeba hatia yake mwenyewe.
And unto the children of Israel shalt thou speak, saying, Whatsoever man that blasphemeth his God shall bear his sin.
16 Yeye anayelikufuru jina la Yahweh kwa hakika ni lazima auawe. Hakika, kusanyiko lote litampiga mawe, ama awe mgeni au Mwisraeli mwenyeji mzaliwa. Ikiwa yeyote analikufuru jina la Yahweh, ni lazima auawe.
But he that pronounced the name of the Lord [with blasphemy] shall be put to death, all the congregation shall stone him; be he a stranger, or be he one that is born in the land, when he pronounceth the [holy] Name [with blasphemy, ] he shall be put to death.
17 Naye amuuaye mtu mwingine ni lazima kwa hakika auewa.
And he that taketh the life of any man shall surely be put to death.
18 Yeye anayemuua mnyama wa mwingine sharti amfidie, uhai kwa uhai.
And he that taketh the life of a beast shall make it good: beast for beast.
19 Iwapo mtu anamjeruhi jirani yake, ni lazima atendewe vivyo hivyo alivyomtendea jirani yake:
And if a man cause a bodily defect in his neighbor, as he hath done, so shall be done to him;
20 Mvunjiko kwa mvunjiko, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kama amesababisha jeraha kwa mtu, ndivyo ipasavyo kutendwa kwake.
Breach for breach, eye for eye, tooth for tooth: in the manner as he hath caused a bodily defect in a man, so shall it be done to him.
21 Yeyote auaye mnyama ni lazima amfidie, na yeyote auaye mtu ni lazima auawe.
And he that killeth a beast, shall make restitution for it; and he that killeth a man, shall be put to death.
22 Ni lazima mwe na sheria moja kwa wote, mgeni na Mwisraeli mwenyeji mzaliwa, kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wanu.”
One manner of judicial law shall ye have, the stranger shall be equal with one of your own country; for I am the Lord your God.
23 Kwa hiyo Musa akazungumza na watu wa Israeli, nao watu wakamleta mwanaume huyo nje ya kambi, yule ambaye alikuwa amemlaani Yahweh. Wakampiga kwa mawe. Watu waisraeli wakaitekeleza amri ya Yahweh aliyoitoa kupitia Musa.
And Moses spoke to the children of Israel; and they led forth the blasphemer to without the camp, and they stoned him with stones; and the children of Israel did as the Lord had commanded Moses.

< Mambo ya Walawi 24 >