< Mambo ya Walawi 22 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, kusema,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
2 “Ongea na Aroni na wanawe, waambie wajiepushe na vitu vitakatifu vya watu wa Israeli wanavyovitenga kwangu. Wasilinajisi jina langu. Mimi ndimi Yahweh.
Speak unto Aaron and to his sons, that they keep themselves away from the holy things of the children of Israel, [so that they profane not my holy name] which they hallow unto me: I am the Lord.
3 Waambie, 'Ikiwa mmoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote anakaribia vitu vitakatiifu vile ambavyo watu wa Israeli wamevitenga kwa Yahweh, wakati akiwa najisi, sharti mtu huyo akatiliwe mbali atoke mbele zangu. Mimi ndimi Yahweh.
Say unto them, In your generations, if there be any man of all your seed, that approacheth unto the holy things, which the children of Israel hallow unto the Lord, having his uncleanness upon him, that soul shall be cut off from my presence: I am the Lord.
4 Hatakuwapo yeyote wa uzao wa Aroni aliye na ungonjwa wa ngozi wa kuambukiza, au maambukizi yatirirkayo kutoka mwilini mwake, atakayekula sehemu yoyote ya dhabihu inatolewayo kwa Yahweh mpaka atakapotakasika. Yeyote agusaye kitu chochote kilichonajisi kwa njia ya kugusa maiti, au kwa kumgusa mtu yeyote aliyetokwa na shahawa,
Any man whatsoever of the seed of Aaron, that is a leper, or hath a running issue, shall not eat of the holy things, until he be clean; and whoso toucheth any thing that is unclean by the dead, or a man whose seed goeth from him;
5 au yeyote agusaye mnyama atakayemtia unajisi, au mtu yeyote atakayemfanya najisi, kwa hiyo unajisi wowote unaweza kuwa—
Or a man who toucheth any creeping thing, whereby he may be made unclean, or a man through whom he can be rendered unclean, through any kind of uncleanness which he hath:
6 kuhani yeyote agusaye kitu chochote kisichosafi atakuwa najisi hata jioni. Hatakula chochote cha vitu vitakatifu, isipokuwa ameuosha mwili wake katika maji.
The person that toucheth any such shall be unclean until the evening, and he shall not eat of the holy things, unless he have bathed his flesh in water.
7 Jua linapotua, ndipo atakuwa safi. Baada ya machweo anaweza kula kutoka katika vitu vitakatifu, kwasababu hivyo ni vyakuala vyake.
And when the sun hath set, he shall be clean; and afterward he may eat of the holy things; because it is his food.
8 Asile mzoga wowote uliookotwa au mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori, ambaye kwake atajitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh.
That which dieth of itself, or is torn by beasts, shall he not eat, to defile himself therewith: I am the Lord.
9 Ni lazima makuhani wafuate maagizo yangu, ama sivyo watakuwa na hatia ya dhambi na wangeweza kufa kwa kunitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh ninayewafanya wao watakatifu.
And they shall keep my charge, that they may not bear sin through it, and die therefore, if they profane it: I am the Lord who sanctify them.
10 Hakuna mtu kutoka nje ya familia ya kuahani, wakiwemo wageni wa kuhani au watumwa wake wa kuajiliwa, atakayeweza kula kitu chochote kilicho kitakatifu.
And no stranger shall eat of a holy thing: a sojourner of a priest, or a hired servant, shall not eat of a holy thing.
11 Lakini kama huyo kuhani amenunua mtumwa kwa fedha yake mwenyewe, mtumwa huyo anaweza kula kutoka katika vitu vilivyotengwa kwa Yahweh. Na watu wa familia ya kuhani na watumwa waliozaliwa nyumbani mwake, pia wanaweza kula pamoja naye kutoka katika vitu hivyo.
But if a priest buy a person with his money, then may he eat of it; and those that are born in his house, may eat of his bread.
12 Ikiwa binti wa kuhani ameolewa na mtu asiye kuhani, hataweza kula chochote cha mchango wa matoleo matakatifu.
And if the daughter of a priest be married unto a stranger, she may not eat of the offered part of holy things.
13 Lakini ikiwa huyo binti wa kuhani ni mjane au ametalikiwa, na ikiwa hana mtoto, na anarudi kuishi knyumbani kwa baba yake kama alivyokuwa wakati wa ujana wake, anaweza kula kutoka katika chakula cha baba yake. Lakini hakuna yeyote asiye wa familia ya kikuhani anatakayeruhusiwa kula kutoka katika chakula cha kuhani.
But the daughter of a priest, if she be a widow, or divorced, and have no child, and is returned unto her father's house, as in her youth, may eat of her father's bread; but no stranger shall eat thereof.
14 Kama mtu anakula chakula kitakatifu bila ya kukijua, naye atamlipa kuahani kwa ajili ya hicho; itampasa kuongeza moja ya tano juu yake na kukirejesha kwa kuhani.
And if a man eat a holy thing unwittingly, then shall he add the fifth part thereof unto it, and he shall make good unto the priest the holy thing.
15 Haiwapasi watu wa Israeli kutoheshimu vitu vitakatifu ambavyo vimeinuliwa juu na kuletwa kwa Yahweh,
And they shall not profane the holy things of the children of Israel, which they offer unto the Lord;
16 kisha wakajisababishia wenyewe kuchukua dhambi amabyo ingewafanya kuwa na hatia ya kula chakula kitakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Yahweh awafanyaye wao watakatifu.”
And load on themselves the iniquity of trespass, when they eat their holy things; for I am the Lord who sanctify them.
17 Yahweh akazungumza na Musa, akasema,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
18 “Sema na Aroni na wanawe, na kwa watu wa Israeli wote. Waambie, Mwisraeli yeyote, au Mgeni anayeishi katika Israeli, waletapo dhabihu—iwe ni kutimiza kiapo, au iwe ni sadaka ya hiari, au wanaleta kwa Yahweh sadaka ya kuteketezwa kwa moto,
Speak unto Aaron, and unto his sons, and unto all the children of Israel, and say unto them, If there be any man of the house of Israel, or of the strangers in Israel, that offereth his oblation, be it for any manner of vows, or for any manner of freewill-offerings, which they may offer unto the Lord for a burnt-offering:
19 ikiwa wanataka ikubalike, ni lazima watowe mnyama dume asiye na dosari, kutoka kwenye kundi la ng'ombe, kondoo au mbuzi
Then shall it be, that it may be favorably received for you, a male without blemish, of the oxen, of the sheep, or of the goats.
20 Lakini hamtatoa chochote kilicho na dosari. Sitakipokea kwa niaba yenu.
Whatsoever on which there is a blemish shall ye not offer; for it will not be favorably received for you.
21 Yeyote atoae dhabihu ya sadaka ya ushirika kutoka katika kundi la ng'ombe au la kondoo kwa Yahweh ili kutimiza kiapo, au kama sadaka ya hiari, ili ikubalike, ni lazima isiwe na kilema. Ni lazima pasiweko na kasoro katika mnyama.
And when a man offereth a sacrifice of peace-offering unto the Lord as a vow, or a freewill-offering of the herds or of the flocks: it shall be without blemish to be favorably received; no kind of bodily defect shall be thereon.
22 Msitoe kabisa wanyama waliovipofu, waliojeruhiwa, wala walio na kilema, wenye upele, vidonda vitokavyo usaha, wala wenye vigaga. Msiwatoe hawa kuwa dhabihu ya kuteketezwa kwa moto iliyotolewa kwa Yahweh juu ya madhabahu.
A blind, or broken-limbed, or maimed animal, or one having a wen, or itch, or scurvy, —ye shall not offer these unto the Lord, and a fire-offering shall ye not make of them upon the altar unto the Lord.
23 Unaweza kumleta makisai au mwana-kondoo mlemavu au aliyedumaa kuwa sadaka ya hiari, lakini sadaka kama hiyo kwa ajili kutimiza kiapo, haitapokelewa.
And an ox or a lamb that hath a limb too long or too short, that mayest thou offer for a freewill-offering; but for a vow it shall not be favorably received.
24 Usitoe kwa Yahweh mnyama yeyote aliyetiwa jeraha, kupondwa, au kukatwa korodani zake.
And one that is bruised, or crushed, or broken, or cut in the testicles, shall ye not offer unto the Lord; and in your land shall ye not make the like.
25 Usifanye haya katika nchi yako. Usilete mkate wa Mungu wako kutoka mkononi mwa mgeni. Hao wanyama wenye vilema na dosari ndani yao, hawatapokelewa kabisa kwa ajili yako.
And from a stranger's hand shall ye not offer the bread of your God from any of these; because their corruption is on them, a bodily defect is on them: they shall not be favorably received for you.
26 Yahweh akamwambia Musa na akasema,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
27 “Wakati ndama, mwana—kondo au mwana—mbuzi azaliwapo, sharti abaki na mama yake kwa muda wa siku saba. Ndipo kuanzia siku ya nane na kuendelea, anaweza kupokelewa kuwa dhabihu iliyofanywa kwa moto kwa Yahweh.
When a bullock, or a sheep, or a goat, is brought forth, then shall it remain seven days by its mother; and from the eighth day and thenceforth shall it be favorably received for an offering made by fire unto the Lord.
28 Usimchinje ng'ombe jike pamoja na ndama wake au mbuzi jike pamoja na kitoto chake kwa siku moja.
And whether it be ox or sheep, ye shall not kill it and its young both in one day.
29 Utoapo sadaka ya shukrani kwa Yahweh utaitoa kwa njia iliyokubalika.
And when ye offer a sacrifice of thanksgiving unto the Lord, offer it so that it may be favorably received of you.
30 Ni lazima iliwe siku iyo hiyo inayotolewa. Hutakiwi kubakiza chochote hata asubuhi. Mimi ndimi Yahweh.
On the same day shall it be eaten up; ye shall leave none of it until the morning: I am the Lord.
31 Kwa hiyo imewapasa kuzishika amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Yahweh.
And ye shall keep my commandments and do them: I am the Lord.
32 Msiliabishe jina langu takatifu. Ni lazima nitambuliwe kuwa ni mtakatifu na watu wa Israeli. Mimi ndimi Yahweh niwafanyaye ninyi watakatifu,
And ye shall not profane my holy name; so that I may be sanctified among the children of Israel; I am the Lord who sanctify you,
33 ambaye amewaleta kutoka katika nchi ya Misri ili niwe Mungu wenu: Mimi ndimi Yahweh.”
That brought you out of the land of Egypt, to be unto you a God: I am the Lord.

< Mambo ya Walawi 22 >