< Mambo ya Walawi 20 >
1 Yahweh akazungumza na Musa, akasema,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
2 “Waambie watu wa Waisraeli, 'mtu yeyote miongoni mwa watu Israeli, au Mgeni yeyote anayeishi miongoni mwa Waisraeli atakayemtoa mtoto wake yeyote kwa Moleki, hakika atauawa. Ni lazima watu wa nchi wamponde kwa mawe.
“İsrail halkına de ki, ‘İsrailliler'den ya da aranızda yaşayan yabancılardan kim çocuklarından birini ilah Molek'e sunarsa, kesinlikle öldürülecek. Ülke halkı onu taşlayacak.
3 Pia nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumkatilia mbali kutoka miongoni mwa watu wake kwa sababu amemtoa mtoto wake kwa Moleki, ili kupatia unajisi mahali pangu patakatifu na kulinajisi jina langu takatifu.
Kim çocuğunu Molek'e sunarak tapınağımı kirletir, kutsal adıma leke sürerse, ona öfkeyle bakacağım. Onu halkımın arasından atacağım.
4 Na kama watu wa nchi watayafumba macho yao kwa mtu huyo anapomtoa mmoja wa watoto wake kwa Moleki, kama hawatamwua mtu huyo, ndipo Mimi mwenyewe nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na ukoo wake,
Adam çocuğunu Molek'e sunar da, ülke halkı bunu görmezden gelir, onu öldürmezse,
5 Nami nitamkatilia mbali pamoja na yeyote anayejifanya kahaba ili kufanya umalaya na Moleki.
adama ve ailesine öfkeyle bakacağım. Hem onu, hem de bana ihanet edip onu izleyerek Molek'e tapanların hepsini halkımın arasından atacağım.
6 Mtu yule anayewageukia wanaozungumza na wafu, au na wale wanaozungumza na roho ili kufanya ukahaba nao, Nitakaza uso wangu dhidi ya mtu huyo; Nami nitamkatilia mbali atoke miongoni mwa watu wake.
“‘Kim cincilere, ruh çağıranlara danışır, bana ihanet ederse, ona öfkeyle bakacak, halkımın arasından atacağım.
7 Kwa hiyo jitakaseni wenyewe na muwe watakatifu, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Kendinizi bana adayın, kutsal olun. Tanrınız RAB benim.
8 Mtazitunza amari zangu na kuzifuta. Mimi ndimi Yahweh anayewatenga ninyi muwe watakatifu.
Kurallarıma uyacak, onları yerine getireceksiniz. Sizi kutsal kılan RAB benim.
9 Yeyote amlaaniye baba yake au mama yake hakika mtu huyo atauawa. Amemlaani baba yake au mama yake, kwa hiyo ana hatia na anastahili kufa.
“‘Annesine ya da babasına lanet eden herkes kesinlikle öldürülecektir. Annesine ya da babasına lanet ettiği için ölümü hak etmiştir.
10 Mwanaume yeyote afanyaye uzinzi na mke wa mwanaume mwingine, yaani, yeyote anayezini na mke wa jirani yake—yule mwanaume mzinzi na mwanamke mzinzi ni lazima wote wawili wauawe.
“‘Biri başka birinin karısıyla, yani komşusunun karısıyla zina ederse, hem kendisi, hem de zina ettiği kadın kesinlikle öldürülecektir.
11 Mwanaume yeyote anayelala na mke wa baba yake ili kukutana naye kimwili amemfedhehesha baba yake mwenye. Wote wawili; mwana huyo na mke huyo wa baba yake kwa hakika watauawa. wanahatia na wanastahili kufa.
Babasının karısıyla yatan, babasının namusuna leke sürmüş olur. İkisi de kesinlikle öldürülecektir. Ölümü hak etmişlerdir.
12 Kama mwanaume atalala na mke wa mwanawe, wote wawili; mwanaume huyo na mke huyo wa mwanawe hakika watauawa. Wametenda upotovu. Wana hatia na wanastahili kufa.
Bir adam geliniyle yatarsa, ikisi de kesinlikle öldürülecektir. Rezillik etmişler, ölümü hak etmişlerdir.
13 Kama mwanaume analala na mwanaume mwingine kama alalavyo na mwanamke, wote wawili watakuwa wamefanya jambo lililo ovu. Hakika watauawa. Wana hatia na wanastahili kufa.
Bir erkek başka bir erkekle cinsel ilişki kurarsa, ikisi de iğrençlik etmiş olur. Kesinlikle öldürülecekler. Ölümü hak etmişlerdir.
14 Ikiwa mwanaume atamwoa mwanamke na pia akamwoa mama wa mwanamke huyo, huu ni uovu. Ni lazima wachomwe kwa moto, wote wawili, mwanaume huyo na manamke huyo, ili kwamba hapatakuwepo na uovu miongoni mwenu.
Bir adam hem bir kızla, hem de kızın annesiyle evlenirse, alçaklık etmiş olur. Aranızda böyle alçaklıklar olmasın diye üçü de yakılacaktır.
15 Ikiwa mwanaume analala na mnyama, hakika atauawa, ni lazima mumuue na mnyama huyo pia.
Bir hayvanla cinsel ilişki kuran adam kesinlikle öldürülecek, hayvansa kesilecektir.
16 Ikiwa mwanamke anamkaribia mnyama ili kulala naye, ni lazima mmuuwe mwanamke huyo pamoja na mnyama. Kwa hakika ni lazima wauawe. wana hatia na wanastahili kufa.
Bir kadın cinsel ilişki kurmak amacıyla bir hayvana yaklaşırsa, kadını da hayvanı da kesinlikle öldüreceksiniz. Ölümü hak etmişlerdir.
17 Ikiwa mwanaume analala na dada yake, ama ni binti ya baba yake au binti ya mama yake—ikiwa wamelala pamoja, hilo ni jambo la aibu. Ni lazima wakatiliwe mbali watoke machoni pa watu wao, kwa sababu amelala na dada yake. Ni lazima aibebe hatia yake.
“‘Bir adam anne ya da baba tarafından üvey olan kızkardeşiyle evlenir, cinsel ilişki kurarsa, utançtır. Açıkça aşağılanıp halkın arasından atılacaklardır. Adam kızkardeşiyle ilişki kurduğu için suçunun cezasını çekecektir.
18 Kama mwanaume analala na mwanamke katika kipindi cha hedhi yake, na amekutana naye kimwili, atakuwa amefunua mtiririko wa damu yake, chanzo cha damu yake. Ni lizima wote wawili wakatiliwe mbali kutoka mingoni mwa watu wao.
Âdet gören bir kadınla yatıp cinsel ilişki kuran adam kadının akıntılı yerini açığa çıkarmış, kadın da buna katılmış olur. İkisi de halkın arasından atılacaktır.
19 Usilale na dada ya mama yako, au dada ya baba yako, kwa sababu ungeweza kumwaibisha jamaa yako wa karibu. Ni lazima utabeba hatia yako mwenyewe.
“‘Teyzenle ya da halanla cinsel ilişki kurmayacaksın. Çünkü yakın akrabanın namusudur. İkiniz de suçunuzun cezasını çekeceksiniz.
20 Ikiwa mwanaume analala na shangazi yake, atakuwa amemfedhehesha mjomba wake. Wanapokufa, nitawaadhibu wote wawili, na wanapokufa nitauondolea mbali urithi wa watoto wao ambao wangeliupokea kutoka kwa wazazi wao.
“‘Amcasının karısıyla cinsel ilişki kuran adam, amcasının namusuna leke sürmüş olur. İkisi de günahlarının cezasını çekecek ve çocuk sahibi olmadan öleceklerdir.
21 Ikiwa mwanaume anamwoa mke wa kaka yake wakati ambapo kaka yake angali hai, hilo ni jambo la aibu. Amemfedhehesha kaka yake, na nitaondolea mbali mali yoyote amabayo watoto wao wangerithi kutoka kwa wazazi wao.
Kardeşinin karısıyla evlenen adam rezillik etmiş olur. Kardeşinin namusunu lekelemiştir. Çocuk sahibi olmayacaklardır.
22 Kwa hiyo imewapasa kuzishika amri na sheria zangu zote; ni lazima mzitii ili kwamba ile nchi ambayo ninawaleta kuishi isiwatapike nyinyi.
“‘Bütün kurallarıma, ilkelerime uyacak, onları yerine getireceksiniz. Öyle ki, yaşamak üzere sizi götüreceğim ülke sizi dışarı kusmasın.
23 Msienende katika desturi za mataifa ambayo nitayafukuza mbele yenu, ni kwa sababu wamefanya mambo haya yote, nami mimewachukia wao.
Önünüzden kovacağım ulusların törelerine göre yaşamayacaksınız. Çünkü onlar bütün bu kötülükleri yaptılar. Bu yüzden onlardan nefret ettim.
24 Nami nikawaambia ninyi, “Mtaimiliki nchi yao, nitaitoa kwenu ili muimiliki, nchi itiririkayo amaziwa na asali. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu, aliyewatenga nyinyi kutoka kwa watu wengine.
Oysa, Siz onların topraklarını sahipleneceksiniz. Bal ve süt akan bu ülkeyi size mülk olarak vereceğim, dedim. Sizi öteki uluslardan ayrı tutan Tanrınız RAB benim.
25 Ni lazima pia mtofautishe kati ya wanya najisi na wale walio safi, na kati ya ndege walio najisi na walio safi. Msijichafue wenyewe kwa wanyama au ndege au kiumbe kitambaacho juu ya nchi kilicho najisi, ambacho nimekitenga kuwa najisi.
“‘Temiz hayvanlarla kuşları kirli olanlardan ayırt edeceksiniz. Sizin için kirli ilan ettiğim hayvanlarla, kuşlarla, küçük kara hayvanlarıyla kendinizi kirletmeyeceksiniz.
26 Mtakuwa watakatifu, kwa kuwa Mimi, Yahweh, ni mtakakatifu, nami nimewatenga nyinyi kutoka kwa watu wengine, kwa kuwa nyinyi ni wangu.
Benim için kutsal olacaksınız. Çünkü ben RAB kutsalım. Bana ait olmanız için sizi öbür halklardan ayrı tuttum.
27 Mwanaume au mwanamke anayeongea na wafu au anayeongea na roho hakika atauawa. Watu watawaponda kwa mawe. Wanayo hatia na wanastahili kufa.
“‘Cincilik yapan ve ruh çağıran ister erkek olsun, ister kadın olsun kesinlikle öldürülecektir. Onları taşlayacaksınız. Ölümlerinden kendileri sorumludur.’”