< Mambo ya Walawi 18 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
וידבר יהוה אל משה לאמר
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
דבר אל בני ישראל ואמרת אלהם אני יהוה אלהיכם
3 Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
כמעשה ארץ מצרים אשר ישבתם בה לא תעשו וכמעשה ארץ כנען אשר אני מביא אתכם שמה לא תעשו ובחקתיהם לא תלכו
4 Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
את משפטי תעשו ואת חקתי תשמרו ללכת בהם אני יהוה אלהיכם
5 Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
ושמרתם את חקתי ואת משפטי אשר יעשה אתם האדם וחי בהם אני יהוה
6 Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
איש איש אל כל שאר בשרו לא תקרבו לגלות ערוה אני יהוה
7 Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
ערות אביך וערות אמך לא תגלה אמך הוא לא תגלה ערותה
8 Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
ערות אשת אביך לא תגלה ערות אביך הוא
9 Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
ערות אחותך בת אביך או בת אמך מולדת בית או מולדת חוץ--לא תגלה ערותן
10 Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
ערות בת בנך או בת בתך לא תגלה ערותן כי ערותך הנה
11 Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
ערות בת אשת אביך מולדת אביך אחותך הוא--לא תגלה ערותה
12 Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
ערות אחות אביך לא תגלה שאר אביך הוא
13 Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
ערות אחות אמך לא תגלה כי שאר אמך הוא
14 Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
ערות אחי אביך לא תגלה אל אשתו לא תקרב דדתך הוא
15 Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
ערות כלתך לא תגלה אשת בנך הוא לא תגלה ערותה
16 Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
ערות אשת אחיך לא תגלה ערות אחיך הוא
17 Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
ערות אשה ובתה לא תגלה את בת בנה ואת בת בתה לא תקח לגלות ערותה--שארה הנה זמה הוא
18 Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
ואשה אל אחתה לא תקח לצרר לגלות ערותה עליה--בחייה
19 Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
ואל אשה בנדת טמאתה--לא תקרב לגלות ערותה
20 Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
ואל אשת עמיתך--לא תתן שכבתך לזרע לטמאה בה
21 Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
ומזרעך לא תתן להעביר למלך ולא תחלל את שם אלהיך אני יהוה
22 Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
ואת זכר--לא תשכב משכבי אשה תועבה הוא
23 Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
ובכל בהמה לא תתן שכבתך לטמאה בה ואשה לא תעמד לפני בהמה לרבעה--תבל הוא
24 Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
אל תטמאו בכל אלה כי בכל אלה נטמאו הגוים אשר אני משלח מפניכם
25 Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
ותטמא הארץ ואפקד עונה עליה ותקא הארץ את ישביה
26 Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
ושמרתם אתם את חקתי ואת משפטי ולא תעשו מכל התועבת האלה האזרח והגר הגר בתוככם
27 Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
כי את כל התועבת האל עשו אנשי הארץ אשר לפניכם ותטמא הארץ
28 Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
ולא תקיא הארץ אתכם בטמאכם אתה כאשר קאה את הגוי אשר לפניכם
29 Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
כי כל אשר יעשה מכל התועבת האלה--ונכרתו הנפשות העשת מקרב עמם
30 Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
ושמרתם את משמרתי לבלתי עשות מחקות התועבת אשר נעשו לפניכם ולא תטמאו בהם אני יהוה אלהיכם

< Mambo ya Walawi 18 >