< Mambo ya Walawi 18 >
1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
L'Eternel parla encore à Moïse, en disant:
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Parle aux enfants d'Israël, et leur dis: Je suis l'Eternel votre Dieu.
3 Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
Vous ne ferez point ce qui se fait au pays d'Egypte où vous avez habité, ni ce qui se fait au pays de Canaan, auquel je vous amène; et vous ne vivrez point selon leurs statuts.
4 Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
[Mais] vous ferez selon mes statuts, et vous garderez mes ordonnances pour marcher en elles; je suis l'Eternel votre Dieu.
5 Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
Vous garderez donc mes statuts, et mes ordonnances, lesquelles [si] l'homme accomplit, il vivra par elles; je suis l'Eternel.
6 Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
Que nul ne s'approche de celle qui [est] sa proche parente pour découvrir sa nudité; je suis l'Eternel.
7 Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
Tu ne découvriras point la nudité de ton père, ni la nudité de ta mère; c'[est] ta mère, tu ne découvriras point sa nudité.
8 Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
Tu ne découvriras point la nudité de la femme de ton père; c'est la nudité de ton père.
9 Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
Tu ne découvriras point la nudité de ta sœur, fille de ton père, ou fille de ta mère, née dans la maison, ou hors [de la maison]; tu ne découvriras point leur nudité.
10 Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
Quant à la nudité de la fille de ton fils, ou de la fille de ta fille, tu ne découvriras point leur nudité, car elles sont ta nudité.
11 Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
Tu ne découvriras point la nudité de la fille de la femme de ton père, née de ton père, c'est ta sœur.
12 Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
Tu ne découvriras point la nudité de la sœur de ton père; elle est proche parente de ton père.
13 Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
Tu ne découvriras point la nudité de la sœur de ta mère; car elle est proche parente de ta mère.
14 Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
Tu ne découvriras point la nudité du frère de ton père, [et] ne t'approcheras point de sa femme; elle est ta tante.
15 Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
Tu ne découvriras point la nudité de ta belle-fille; elle est la femme de ton fils, tu ne découvriras point sa nudité.
16 Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
Tu ne découvriras point la nudité de la femme de ton frère, c'est la nudité de ton frère.
17 Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
Tu ne découvriras point la nudité d'une femme et de sa fille, et ne prendras point la fille de son fils, ni la fille de sa fille pour découvrir leur nudité, elles sont tes proches parentes; c'est une énormité.
18 Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
Tu ne prendras point aussi une femme avec sa sœur pour l'affliger en découvrant sa nudité sur elle, pendant sa vie.
19 Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
Tu n'approcheras point de la femme durant la séparation de sa souillure, pour découvrir sa nudité.
20 Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
Tu n'auras point aussi la compagnie de la femme de ton prochain, te souillant avec elle.
21 Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
Tu ne donneras point de tes enfants pour les faire passer [par le feu] devant Molec, et tu ne profaneras point le Nom de ton Dieu; je suis l'Eternel.
22 Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
Tu n'auras point aussi la compagnie d'un mâle; c'est une abomination.
23 Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
Tu ne t'approcheras point aussi d'aucune bête pour te souiller avec elle; et la femme ne se prostituera point à une bête; c'est une confusion.
24 Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
Ne vous souillez point en aucune de ces choses; car les nations que je m'en vais chasser de devant vous, se sont souillées en toutes ces choses;
25 Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
Dont la terre a été souillée, et je m'en vais punir sur elle son iniquité, et la terre vomira ses habitants.
26 Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
Mais quant à vous, vous garderez mes ordonnances et mes jugements, et vous ne ferez aucune de ces abominations, tant celui qui est né au pays, que l'étranger qui fait son séjour parmi vous.
27 Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
Car les gens de ce pays-là qui ont été avant vous, ont fait toutes ces abominations, et la terre en a été souillée.
28 Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
La terre ne vous vomirait-elle point, si vous la souilliez, comme elle aura vomi les gens qui y ont été avant vous?
29 Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
Car quiconque fera aucune de toutes ces abominations, les personnes qui les auront faites seront retranchées du milieu de leur peuple.
30 Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Vous garderez donc ce que j'ai ordonné de garder, et vous ne pratiquerez aucune de ces coutumes abominables qui ont été pratiquées avant vous, et vous ne vous souillerez point par elles; je suis l'Eternel votre Dieu.