< Mambo ya Walawi 18 >
1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
« Parle aux enfants d’Israël, et dis-leur: Je suis Yahweh, votre Dieu.
3 Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
Vous ne ferez point ce qui se fait dans le pays d’Égypte où vous avez habité, et vous ne ferez point ce qui se fait dans le pays de Chanaan où je vous conduis: vous ne suivrez pas leurs lois.
4 Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Vous pratiquerez mes ordonnances et vous observerez mes lois: vous les suivrez. Je suis Yahweh votre Dieu.
5 Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
Vous observerez mes Lois et mes ordonnances; l’homme qui les mettra en pratique vivra par elles. Je suis Yahweh.
6 Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
Aucun de vous ne s’approchera d’une femme qui est sa proche parente, pour découvrir sa nudité: je suis Yahweh.
7 Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
Tu ne découvriras pas la nudité de ton père et la nudité de ta mère. C’est ta mère, tu ne découvriras pas sa nudité.
8 Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
Tu ne découvriras pas la nudité de la femme de ton père: c’est la nudité de ton père.
9 Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
Tu ne découvriras pas la nudité de ta sœur, fille de ton père ou fille de ta mère, née dans la maison ou née hors de la maison; tu ne découvriras pas leur nudité.
10 Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
Tu ne découvriras pas la nudité de la fille de ton fils ou de la fille de ta fille: car c’est ta nudité.
11 Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
Tu ne découvriras pas la nudité de la fille de la femme de ton père, née de ton père: c’est ta sœur.
12 Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
Tu ne découvriras pas la nudité de la sœur de ton père: c’est la chair de ton père.
13 Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
Tu ne découvriras pas la nudité de la sœur de ta mère: c’est la chair de ta mère.
14 Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
Tu ne découvriras pas la nudité du frère de ton père, en t’approchant de sa femme: c’est ta tante.
15 Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
Tu ne découvriras pas la nudité de ta belle-fille: c’est la femme de ton fils, tu ne découvriras pas sa nudité.
16 Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
Tu ne découvriras pas la nudité de la femme de ton frère: c’est la nudité de ton frère.
17 Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
Tu ne découvriras pas la nudité d’une femme et de sa fille: tu ne prendras pas la fille de son fils ni la fille de sa fille, pour découvrir leur nudité: elles sont proches parentes, c’est un crime.
18 Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
Tu ne prendras pas la sœur de ta femme, pour en faire une rivale, en découvrant sa nudité avec celle de ta femme, de son vivant.
19 Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
Tu ne t’approcheras pas d’une femme pendant son impureté menstruelle, pour découvrir sa nudité.
20 Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
Tu n’auras pas commerce avec la femme de ton prochain, pour te souiller avec elle.
21 Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
Tu ne donneras aucun de tes enfants pour le faire passer par le feu en l’honneur de Moloch, et tu ne profaneras pas le nom de ton Dieu. Je suis Yahweh.
22 Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
Tu ne coucheras pas avec un homme comme on fait avec une femme: c’est une abomination.
23 Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
Tu ne coucheras pas avec une bête, pour te souiller avec elle. La femme ne se tiendra pas devant une bête pour se prostituer à elle: c’est une honte.
24 Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
Ne vous souillez par aucune de ces choses, car c’est par elles que se sont souillées les nations que je vais chasser devant vous.
25 Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
Le pays a été souillé; je punirai ses iniquités, et le pays vomira ses habitants.
26 Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
Mais vous, vous observerez mes lois et mes ordonnances, et vous ne commettrez aucune de ces abominations, ni l’indigène, ni l’étranger qui séjourne au milieu de vous.
27 Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
Car toutes ces abominations, les hommes du pays, qui y ont été avant vous, les ont commises, et le pays en a été souillé.
28 Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
Et le pays ne vous vomira pas pour l’avoir souillé, comme il a vomi les nations qui y étaient avant vous.
29 Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
Car tous ceux qui commettront quelqu’une de ces abominations seront retranchés du milieu de leur peuple.
30 Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
Vous observerez mes commandements, afin de ne pratiquer aucun des usages abominables qui se pratiquaient avant vous, et vous ne vous souillerez point par eux. Je suis Yahweh, votre Dieu. »