< Mambo ya Walawi 18 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
Then the LORD said to Moses,
2 “Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
“Speak to the Israelites and tell them: I am the LORD your God.
3 Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
You must not follow the practices of the land of Egypt, where you used to live, and you must not follow the practices of the land of Canaan, into which I am bringing you. You must not walk in their customs.
4 Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
You are to practice My judgments and keep My statutes by walking in them. I am the LORD your God.
5 Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
Keep My statutes and My judgments, for the man who does these things will live by them. I am the LORD.
6 Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
None of you are to approach any close relative to have sexual relations. I am the LORD.
7 Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
You must not expose the nakedness of your father by having sexual relations with your mother. She is your mother; you must not have sexual relations with her.
8 Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
You must not have sexual relations with your father’s wife; it would dishonor your father.
9 Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
You must not have sexual relations with your sister, either your father’s daughter or your mother’s daughter, whether she was born in the same home or elsewhere.
10 Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
You must not have sexual relations with your son’s daughter or your daughter’s daughter, for that would shame your family.
11 Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
You must not have sexual relations with the daughter of your father’s wife, born to your father; she is your sister.
12 Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
You must not have sexual relations with your father’s sister; she is your father’s close relative.
13 Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
You must not have sexual relations with your mother’s sister, for she is your mother’s close relative.
14 Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
You must not dishonor your father’s brother by approaching his wife to have sexual relations with her; she is your aunt.
15 Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
You must not have sexual relations with your daughter-in-law. She is your son’s wife; you are not to have sexual relations with her.
16 Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
You must not have sexual relations with your brother’s wife; that would shame your brother.
17 Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
You must not have sexual relations with both a woman and her daughter. You are not to marry her son’s daughter or her daughter’s daughter and have sexual relations with her. They are close relatives; it is depraved.
18 Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
You must not take your wife’s sister as a rival wife and have sexual relations with her while your wife is still alive.
19 Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
You must not approach a woman to have sexual relations with her during her menstrual period.
20 Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
You must not lie carnally with your neighbor’s wife and thus defile yourself with her.
21 Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
You must not give any of your children to be sacrificed to Molech, for you must not profane the name of your God. I am the LORD.
22 Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
You must not lie with a man as with a woman; that is an abomination.
23 Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
You must not lie carnally with any animal, thus defiling yourself with it; a woman must not stand before an animal to mate with it; that is a perversion.
24 Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
Do not defile yourselves by any of these practices, for by all these things the nations I am driving out before you have defiled themselves.
25 Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
Even the land has become defiled, so I am punishing it for its sin, and the land will vomit out its inhabitants.
26 Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
But you are to keep My statutes and ordinances, and you must not commit any of these abominations—neither your native-born nor the foreigner who lives among you.
27 Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
For the men who were in the land before you committed all these abominations, and the land has become defiled.
28 Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
So if you defile the land, it will vomit you out as it spewed out the nations before you.
29 Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
Therefore anyone who commits any of these abominations must be cut off from among his people.
30 Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
You must keep My charge not to practice any of the abominable customs that were practiced before you, so that you do not defile yourselves by them. I am the LORD your God.”

< Mambo ya Walawi 18 >