< Mambo ya Walawi 17 >

1 Yahweh akamwambia Musa,
Yahweh also said to Moses/me,
2 “Zungumza na Aroni na wanawe, na watu wote wa Israeli. Waambie mambo ambayo ameamru Yahweh:
“Speak to Aaron and his sons and to all the other Israeli people, and say this to them: ‘This is what Yahweh has commanded:
3 Mtu yeyote wa Isreli anayeua fahali au mwana—kondoo au mbuzi kambini, au amuuaye nje ya kambi, ili kumtoa dhabihu—
If you sacrifice an ox or a lamb or a goat, you must bring it [to the priest] at the entrance of the Sacred Tent [area], to present/offer it to me there.
4 kama hamleti katika ingilio la hema la kukutania ili kumtoa dhabihu kwa Yahweh mbele za hema lake la kukutania, mtu huyo ana hatia ya damu iliyomwagika. Amemwaga damu, na mtu huyo ni sharti akatiliwe mabali kutoka miongoni mwa watu wake.
If you slaughter it to be a sacrifice anywhere else in the camp or outside the camp, you will be guilty of killing an animal [in an unacceptable place]. As a result you will no longer be allowed to be/associate with my people.
5 Kusudi la amri hii ni kwamba watu wa Israeli wataleta dhabihu zao kwa Yahweh kwenye ingilio la hema la kukutania, watazileta kwa kuhani ziweze kutolewa kuwa matoleo ya shukrani kwa Yahweh, badala ya kutoa dhabihu hadharani katika shamba.
That rule is in order that you Israeli people, instead of offering sacrifices in the open fields, will offer them to me by taking them to the priest at the entrance of the Sacred Tent [area], to be offerings to maintain fellowship [with me].
6 Kuhani atainyunyiza damu juu ya madhabahu ya Yahweh kwenye ingilio la hema la kukutania; atayachoma mafuta yake ili kutoa harufu ya kupendeza mbele za Yahweh.
[After the animal is slaughtered], the priest must sprinkle some of its blood against the altar at the entrance of the Sacred Tent, and burn its fat to be an aroma that is pleasing to me.
7 Ni lazima watu wasitoe tena dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi, ambazo kwazo hutenda kama makahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yao katika vizazi vya watu wao vyote.
You people must no longer give sacrifices to the demons that resemble goats which you are worshiping. You people must obey this command forever.’
8 Ni lazima uwaambie, 'Mtu yeyote wa Israeli, au Mgeni yeyote aishiye miongoni mwao, atoweye dhabihu
“And tell this to the people: ‘If any Israeli or any foreigner who is living among them brings an offering that is to be completely burned [on the altar], or any other sacrifice,
9 na asiilete kwenye ingilio la hema la kukutania ili kuitoa kwa Yahweh, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'
and does not bring it to the entrance of the Sacred Tent [area] to be a sacrifice to me, that person will no longer be allowed to associate with my people.
10 Na Mtu yeyote wa Israeli, au yeyote wa Wageni anayeishi miongoni mwao, ambaye hunywa damu; nitamkatilia mbali atoke miongoni mwa watu wake.
‘I will reject [IDM] any Israeli or any foreigner who is living among you who eats any blood, and I [will command that he] no longer be allowed to associate with my people.
11 Kwa kuwa uhai wa mnyama yeyote umo katika damu yake. Nimeitoa damu yake kwenu kufanya upatanisho juu ya madhabahu kwa ajili ya uhai wenu, kwa sababu ni damu ndiyo ifanyayo upatanisho, kwa kuwa ni damu ipatanishayo kwa ajili ya uhai
That is because the life of every creature is in its blood; I have declared that it is blood that is to be offered on the altar to enable people to be forgiven for their sins.
12 Kwa hiyo Niliwaambia Watu wa Israeli kwamba hayupo miongoni mwenu impasaye kula damu, wala yeyote wa Wageni aishiye miongoni mwenu atakaye kula damu.
That is why I say that you Israelis must not eat blood, and the foreigners who live among you must also not eat blood.
13 Na yeyote miongoni mwa watu wa Israeli, au yeyote wa Wageni aishiye miongoni mwenu ni lazima aimwage damu ya mnyama na kuifukia hiyo damu kwa mafumbi.
‘Any Israeli or any foreigner who is living among you who hunts any animal or bird that is permitted for you to eat, must drain out the blood [of the animal or bird that he kills], and cover the blood with dirt.
14 Kwa kuwa uhai wa kila kiumbe umo katika damu yake. Ni kwa sababu hii niliwaambia watu wa Israeli, ni lazima msile damu ya kiumbe cho chote, kwa kuwa maisha ya kila kiumbe chenye uhai ni damu yake. Yeyeote ailaye ni lazima akatiliwe mbali.
This is because the life of every creature is in its blood. And that is why I have said [DOU] to you Israelis that anyone who eats blood must no longer [be allowed to associate with my people].
15 Mtu yeyote alaye mnyama aliyekufa au ambaye amelaruliwa na wanyama pori, ama yule mtu ni mwenyeji wa kuzaliwa au ni mgeni aishiye miongoni mwenu, ni lazima atazifua nguo zake na kujiosha katika maji, naye atakuwa najisi hata jioni. Kisha atakuwa safi.
‘Anyone in Israel, including foreigners, who eats any of the meat of any creature that is found dead, or that had been killed by wild animals, must wash his clothes and bathe. Then he must not touch anyone until that evening.
16 Lakini kama hazifui nguo zake au kuosha mwili wake, ni lazima aichukue hatia yake”.
If he does not do those things, he will be punished for what he did.’”

< Mambo ya Walawi 17 >