< Mambo ya Walawi 17 >
1 Yahweh akamwambia Musa,
And the Lord spake vnto Moses, saying,
2 “Zungumza na Aroni na wanawe, na watu wote wa Israeli. Waambie mambo ambayo ameamru Yahweh:
Speake vnto Aaron, and to his sonnes, and to all the children of Israel, and say vnto them, This is the thing which the Lord hath commanded, saying,
3 Mtu yeyote wa Isreli anayeua fahali au mwana—kondoo au mbuzi kambini, au amuuaye nje ya kambi, ili kumtoa dhabihu—
Whosoeuer he be of the house of Israel that killeth a bullocke, or lambe, or goate in the hoste, or that killeth it out of the hoste,
4 kama hamleti katika ingilio la hema la kukutania ili kumtoa dhabihu kwa Yahweh mbele za hema lake la kukutania, mtu huyo ana hatia ya damu iliyomwagika. Amemwaga damu, na mtu huyo ni sharti akatiliwe mabali kutoka miongoni mwa watu wake.
And bringeth it not vnto the doore of the Tabernacle of the Congregation to offer an offring vnto the Lord before the Tabernacle of the Lord, blood shalbe imputed vnto that man: he hath shed blood, wherefore that man shall be cut off from among his people.
5 Kusudi la amri hii ni kwamba watu wa Israeli wataleta dhabihu zao kwa Yahweh kwenye ingilio la hema la kukutania, watazileta kwa kuhani ziweze kutolewa kuwa matoleo ya shukrani kwa Yahweh, badala ya kutoa dhabihu hadharani katika shamba.
Therefore the children of Israel shall bring their offrings, which they would offer abroad in the fielde, and present the vnto ye Lord at the doore of the Tabernacle of ye Congregation by ye Priest, and offer them for peace offrings vnto the Lord.
6 Kuhani atainyunyiza damu juu ya madhabahu ya Yahweh kwenye ingilio la hema la kukutania; atayachoma mafuta yake ili kutoa harufu ya kupendeza mbele za Yahweh.
Then the Priest shall sprinkle the blood vpon the Altar of the Lord before the doore of the Tabernacle of the Congregation, and burne the fat for a sweete sauour vnto the Lord.
7 Ni lazima watu wasitoe tena dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi, ambazo kwazo hutenda kama makahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yao katika vizazi vya watu wao vyote.
And they shall no more offer their offerings vnto deuils, after whom they haue gone a whoring: this shalbe an ordinance for euer vnto them in their generations.
8 Ni lazima uwaambie, 'Mtu yeyote wa Israeli, au Mgeni yeyote aishiye miongoni mwao, atoweye dhabihu
Also thou shalt say vnto them, whosoeuer he be of the house of Israel, or of the strangers which soiourne among them, that offreth a burnt offring or sacrifice,
9 na asiilete kwenye ingilio la hema la kukutania ili kuitoa kwa Yahweh, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'
And bringeth it not vnto ye doore of the Tabernacle of the Congregation to offer it vnto the Lord, euen that man shall be cut off from his people.
10 Na Mtu yeyote wa Israeli, au yeyote wa Wageni anayeishi miongoni mwao, ambaye hunywa damu; nitamkatilia mbali atoke miongoni mwa watu wake.
Likewise whosoeuer he be of the house of Israel, or of the strangers that soiourne among them, that eateth any blood, I will euen set my face against that person that eateth blood, and will cut him off from among his people.
11 Kwa kuwa uhai wa mnyama yeyote umo katika damu yake. Nimeitoa damu yake kwenu kufanya upatanisho juu ya madhabahu kwa ajili ya uhai wenu, kwa sababu ni damu ndiyo ifanyayo upatanisho, kwa kuwa ni damu ipatanishayo kwa ajili ya uhai
For the life of the flesh is in the blood, and I haue giuen it vnto you to offer vpon the altar, to make an atonement for your soules: for this blood shall make an atonement for the soule.
12 Kwa hiyo Niliwaambia Watu wa Israeli kwamba hayupo miongoni mwenu impasaye kula damu, wala yeyote wa Wageni aishiye miongoni mwenu atakaye kula damu.
Therefore I saide vnto ye children of Israel, None of you shall eate blood: neither the stranger that soiourneth among you, shall eate blood.
13 Na yeyote miongoni mwa watu wa Israeli, au yeyote wa Wageni aishiye miongoni mwenu ni lazima aimwage damu ya mnyama na kuifukia hiyo damu kwa mafumbi.
Moreouer whosoeuer he be of the children of Israel, or of the strangers that soiourne among the, which by hunting taketh any beast or foule that may be eaten, he shall powre out the blood thereof, and couer it with dust:
14 Kwa kuwa uhai wa kila kiumbe umo katika damu yake. Ni kwa sababu hii niliwaambia watu wa Israeli, ni lazima msile damu ya kiumbe cho chote, kwa kuwa maisha ya kila kiumbe chenye uhai ni damu yake. Yeyeote ailaye ni lazima akatiliwe mbali.
For ye life of all flesh is his blood, it is ioyned with his life: therefore I sayd vnto the children of Israel, Ye shall eate the blood of no flesh: for the life of al flesh is the blood thereof: whosoeuer eateth it, shalbe cut off.
15 Mtu yeyote alaye mnyama aliyekufa au ambaye amelaruliwa na wanyama pori, ama yule mtu ni mwenyeji wa kuzaliwa au ni mgeni aishiye miongoni mwenu, ni lazima atazifua nguo zake na kujiosha katika maji, naye atakuwa najisi hata jioni. Kisha atakuwa safi.
And euery person that eateth it which dyeth alone, or that which is torne with beastes, whether it be one of the same countrey or a stranger, he shall both wash his clothes, and wash himselfe in water, and be vncleane vnto the euen: after he shalbe cleane.
16 Lakini kama hazifui nguo zake au kuosha mwili wake, ni lazima aichukue hatia yake”.
But if he wash them not, nor wash his flesh, then he shall beare his iniquitie.