< Mambo ya Walawi 16 >

1 Yahwe alizungumza na Musa - hii ni baada vifo vya wana wawili wa Haruni, walipomkaribia Yahwe na ndipo wakafa.
And Yahweh spake unto Moses, after the death of the two sons of Aaron, —when they had offered strange fire before Yahweh and died.
2 Yahwe alimwambia Musa, “Ongea na Haruni kaka yako na umwambie hapana kuja tu wakati wowote katika patakatifu pa patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kifuniko cha upatanisho kilicho juu ya sanduku. Akifanya hivyo, anakufa, kwasababu naonekana katika wingu juu ya kifuniko cha upatanisho.
And Yahweh said unto Moses—Speak unto Aaron thy brother, that he do not come at all times into the holy place, within the veil, —into the presence of the propitiatory, which is upon the ark, so shall he not die, for, in the cloud, will I appear upon the propitiatory.
3 Hivi ndivyo jinsi Haruni lazima aje katika patakatifu pa patakatifu. Yeye lazima aingie pamoja na ndama kama sadaka ya dhambi, na kondoo dume kama sadaka ya dhambi.
Herewith, shall Aaron come into the holy place, —With a bullock the choice of the herd as a sin-bearer, and a ram as an ascending-sacrifice.
4 Ni lazima avae kanzu ya kitatani, na lazima avae ndani yake nguo ya kitani, na lazima avae mshipi wa kitani na kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu. Lazima aoge mwili wake katika maji na avae mavazi haya.
A holy tunic of linen, shall he put on and drawers of linen, shall be upon his flesh, and with a band of linen, shall he gird himself, and with a turban of linen, shall his head be wrapped about, —holy garments, they are, therefore shall he bathe in water his flesh, and so put them on.
5 Lazima achukue kwenye umati wa watu wa Israeli mbuzi wawili waume kama sadaka ya dhambi na kondoo dume moja ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa.
And, from the assembly of the sons of Israel, shall he receive two he-goats, for bearing sin, —and one ram, as an ascending-sacrifice.
6 Ndipo Haruni lazima alete ng'ombe kama sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake.
Then shall Aaron bring near the sin-bearing bullock which is for himself, —and put a propitiatory-covering about himself, and about his household.
7 Ndipo lazima achukue mbuzi wawili na kuwaweka mbele ya Yahwe katika mlango wa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
Then shall he take the two goats, —and cause them to stand before Yahweh, at the entrance of the tent of meeting.
8 Ndipo Haruni lazima apige kura kwaajili ya mbuzi hao wawili, kura moja kwaajili ya Yahwe, na kura nyingine kwaajili ya msingiziwa.
And Aaron shall cast lots over the two goats, —one lot for Yahweh, and one lot for Azazel.
9 Ndipo Haruni lazima awasilishe mbuzi ambaye kura imeangukia kwa Yahwe, na kumtoa mbuzi huyo kama sadaka ya dhambi.
Then shall Aaron bring near the goat over which came up the lot for Yahweh, —and shall make of him a sin-bearer;
10 Lakini mbuzi ambaye kura ya usingiziwa imemwangukia lazima aletwe kwa Yahwe akiwa hai, kufanya upatanisho kwa kumwachia aende porini kama, mbuzimsingiziwa.
but, the goat over which came up the lot for Azazel, shall he cause to stand alive—before Yahweh to put a propitiatory-covering over him, —to send him away unto Azazel, towards the desert.
11 Pia Haruni lazima alete ng'ombe kwaajili ya sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, lazima afanye upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake, hivyo lazima yeye amuue huyo ng'ombe kama sadaka ya dhambi kwaajili yake mwenyewe.
So Aaron shall bring near the sin-bearing bullock which is for himself, and shall put a propitiatory-covering about himself, and about his household, —and shall slay the sin-bearing bullock which is for himself;
12 Haruni lazima achukue chetezo iliyojaa mkaa wa moto kutoka kwenye madhabahu mbele ya Yahwe, na mikono imejaa ubani mzuri, na kuleta vitu hivi ndani ya pazia.
and shall take the censer-full of burning coals of fire from off the altar from before Yahweh, and his hands full of fragrant incense, beaten small, —and bring within the veil;
13 Hapo lazima aweke ubani juu ya moto mbele za Yahwe ili kwamba wingu kutoka kwenye ubani liweze kufunika kifuniko cha agano la imani ya upatanisho. Yeye afanye hivyo ili kwamba asife.
and shall put the incense upon the fire before Yahweh, —and the cloud of incense shall cover the propitiatory which is over the testimony, and he shall not die.
14 Ndipo lazima achukue kiasi cha damu ya ng'ombe na kuinyunyiza kwa kidole chake mbele ya kifuniko cha upatanisho. Lazima anyunyize kiasi cha damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko cha upatanisho.
Then shall he take of the blood of the bullock, and shall sprinkle with his finger upon the face of the propitiatory, eastwards, —and before the propitiatory, shall he sprinkle seven times, of the blood, with his finger.
15 Ndipo lazima aue mbuzi kwaajili ya sadaka ya dhambi ambayo ni kwaajili ya watu na kuileta damu yake ndani kwenye pazi. Hapo lazima aifanyie damu kama alivyofanya kwenye damu ya fahali: lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho.
Then shall he slay the sin-bearing goat which is for the people, and bring in its blood, within the veil, —and do with its blood, as he did to the blood of the bullock, and shall sprinkle it, upon the propitiatory and before the propitiatory:
16 Yeye lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli, na kwa sababu ya uasi na dhambi zao zote. Yeye pia lazima afanye haya kwaajili ya hema ya mkutano, ambapo Yahwe anaishi kati yao, katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.
so shall he put a propitiatory-covering, over the holy place because of the uncleanness of the sons of Israel, and because of their transgressions to the extent of all their sins, —and, so, shall he do for the tent of meeting which abideth with them, in the midst of their uncleanness.
17 Hakuna mtu anayetakiwa kuwepo katika hema ya mkutano wakati Haruni anaingia kufanya upatanisho katika mahali patakatifu pa patakatifu, na mpaka atoke nje na amemaliza kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya familia yake, na kwaajili umati wa Israeli.
And no human being, shall be in the tent of meeting, when he cometh in to make a covering by propitiation in the holy place, until he goeth out, —so shall he put a propitiatory-covering about himself and about his household and about all the convocation of Israel.
18 Yeye lazima aende nje kwenye madhabahu hapo mbele za Yahwe na kufanya upatanisho kwaajili ya hiyo, na lazima achukue kiasi cha damu ya mbuzi na kuiweka juu ya pembe za madhabahu yote kuzunguka.
Then shall he go out unto the altar which is before Yahweh and shall put a propitiatory-covering thereupon, —and shall take of the blood of the bullock, and of the blood of the goat, and put upon the horns of the altar, round about;
19 Anatakiwa anyunyize kiasi cha damu juu yake kwa kidole chake mara saba kuitakasa na kuitenga maalumu kwa Yahwe, mbali kutoka matendo ya unajisi wa watu wa Israeli.
and shall sprinkle upon it, of the blood with his finger seven times, —and shall cleanse it and hallow it, from the uncleannesses of the sons of Israel.
20 Atakapo maliza kupatanisha kwaajili ya mahali patakatifu sana, hema la mkutano, na madhabahu, lazima amlete mbuzi aliyehai.
And, when he hath made an end of covering by propitiation the holy place, and the tent of meeting, and the altar, then shall he bring near the living goat.
21 Haruni lazima aweke mikono yake yote juu ya kichwa cha mbuzi huyu aliyehai na akiri juu yake maovu yote ya watu wa Israeli, uasi wao wote, dhambi zao zote. Ndipo lazima aweke dhambi hizo juu ya kichwa cha mbuzi na amwachie katika uangalizi wa mtu aliyetari kumwongoza mbuzi huyo porini.
And Aaron shall lean his two hands upon the head of the living goat, and confess over him, all the iniquities of the sons of Israel, and all their transgressions, to the extent of all their sins, —and shall put them upon the head of the goat, and then send him away, by the hand of a man appointed towards the desert:
22 Mbuzi lazima abebe juu yake mwenyewe uovu wote kwenda mahali pakiwa. Kule msituni, huyo mtu amwache mbuzi aende huru.
so shall the goat bear upon him all their iniquities into a lone land, —and he shall set the goat free, in the desert.
23 Ndipo Haruni anapaswa kwenda tena humo kwenye hema ya mkutano na kuvua mavazi ya kitani ambayo amayavaa kabla hajaenda mahali patakatifu sana, na anatakiwa kuyaacha mavazi hayo pale.
Then shall Aaron come into the tent of meeting, and put off the linen garments which he put on when he came into the holy place, —and shall leave them there;
24 Anapaswa aoshe mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na avae nguo zake za kawaida; pia lazima atoke nje kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa kwaajili ya wale watu, na kwa njia hii anafanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya watu.
and shall bathe his flesh in water in a holy place, and put on his [other] garments, —and go forth, and offer his own ascending-sacrifice, and the ascending-sacrifice of the people, so shall he put a propitiatory-covering about himself, and about the people;
25 Lazima yeye achome mafuta ya sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
and, with the fat of the sin-bearer, shall he make a perfume at the altar.
26 Huyu mtu anayemwacha mbuzi msingiziwa aende huru anafua nguo zake na kuosha mwili wake katika maji; baada ya hayo, anaweza kurudi tena kambini.
And he that sent away the goat unto Azazel, shall wash—his clothes, and bathe his flesh in water, —and, after that, shall he come into the camp.
27 Yule fahali kwaajili ya sadaka ya dhambi na mbuzi kwaajili ya sadaka za dhambi, ambaye damu yake ililetwa kufanya upatanisho katika mahali patakatifu, lazima ipelekwe nje ya kambi. kule lazima wachome, ngozi zao, nyama yao na kinyesi chao.
And the, sin-bearing bullock, and the sin-bearing goat whose blood was brought in to make a propitiatory-covering in the holy place, shall be carried forth outside the camp, —and they shall burn up, in fire, their skins and their flesh, and their dung;
28 Huyu anayechoma sehemu hizo lazima afue nguo zake na aoge mwili wake katika maji; baada ya hapo, anaweza kurudi tena kwenye kambi.
and he that hath burned them, shall wash his clothes, and bathe his flesh in water, —and, after that, shall he come into the camp.
29 Hii itakuwa sharti kwaajili yenu kwamba katika mwezi wa saba, kwenye siku ya kumi ya mwezi, mtanyenyekea wenyewe na msifanye kazi, iwe mwenyeji wa kuzaliwa au mgeni anayeishi kati yenu.
And it shall become unto you, a statute age-abiding, —In the seventh month on the tenth of the month, Shall ye humble you souls And, no work, shall ye do, The home-born, Or the sojourner that sojourneth in your midst;
30 Hii ni kwasababu katika siku hii ya upatanisho utafanywa kwaajili yenu, kuwatakasa ninyi kutoka dhambi zenu zote ili mwe safi mbele za Yahwe.
For on this day, shall a propitiatory-covering, be put over you, to cleanse you, —From all your sins before Yahweh, shall ye be clean.
31 Hii ni maalumu kwa Sabato ya kupumzika kwaajili yenu, na lazima mnyenyekee wenyewe na msifanye kazi. Hili litakuwa sharti kati yenu.
A sabbath of sacred rest, it is unto you, Therefore shall ye humble your souls, A statute age-abiding.
32 Kuhani mkuu, ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu kuwa kuhani mkuu katika nafasi ya baba yake, lazima afanye upatanisho huu na kuvaa mavazi ya kitani, hayo ni mavazi matakatifu.
Therefore shall the priest who shall be anointed, and installed, to minister as priest in the stead of his father make propitiation, —So then he shall put on the linen garments the holy garments;
33 Lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu sana; lazima afanye upatanisho kwaajili ya hema ya mkutano na madhabahu, na lazima afanye upatanisho kwaajili ya makuhani na kwaajili ya kusanyiko la watu.
And make propitiation for the holy sanctuary, And for the tent of meeting, and for the altar, shall he make propitiation, —Over the priests also and over all the people of the convocation, shall he put a covering by propitiation.
34 Hii daima itakuwa sharti kwaajili yako, kufanya upatanisho kwaajili ya watu wa Israeli kwasababu ya dhambi zao zote, mara moja kwa kila mwaka.” Na ilikuwa ikifanika kama Yahwe alivyomwamuru Musa.
So shall this become unto you an age-abiding statute, —to put a propitiatory-covering over the sons of Israel because of all their sins, Once in the year. And he did, As Yahweh commanded Moses.

< Mambo ya Walawi 16 >