< Mambo ya Walawi 14 >
1 Yahwe alizungumza na Musa, akisema,
Yahvé parla à Moïse, et dit,
2 “Hii itakuwa sheria kwaajili ya mtu aliyekufa kwenye siku ya utakaso. Lazima aletwe kwa kuhani.
« Voici la loi du lépreux, le jour de sa purification: On l'amènera au sacrificateur,
3 Kuhani atakwenda nje ya kambi kumchunguza mtu kuona kama madhara ya ugonjwa wa ngozi yameponywa.
et le sacrificateur sortira du camp. Le prêtre l'examinera. Si la plaie de la lèpre est guérie chez le lépreux,
4 Ndipo kuhani ataamuru kwamba mtu mwenye kutakaswa lazima achukue ndege safi wawili, waliohai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
le sacrificateur ordonnera de prendre pour celui qui doit être purifié deux oiseaux vivants et purs, du bois de cèdre, du cramoisi et de l'hysope.
5 Kuhani atamwamuru kuua moja ya hao ndege juu ya maji safi yaliyo kwenye chungu cha udongo.
Le prêtre leur ordonnera de tuer l'un des oiseaux dans un vase de terre, au-dessus de l'eau courante.
6 Ndipo kuhani atamchukua ndege aliyehai na mti wa mwerezi, na kitani nyekundu na hisopo, na vyote hivi, pamoja na ndege aliyehai atavichovya kwenye damu ya ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
Il prendra l'oiseau vivant, le bois de cèdre, le cramoisi et l'hysope, et les trempera avec l'oiseau vivant dans le sang de l'oiseau tué au-dessus de l'eau courante.
7 Ndipo kuhani atanyunyiza maji haya mara saba juu ya mtu anayetakaswa katika ugonjwa, na ndipo kuhani atamtangaza kuwa msafi. Ndipo kuhani atamwachia ndege aliyehai katika eneo wazi.
Il fera sept fois l'aspersion sur celui qui doit être purifié de la lèpre, et le déclarera pur, puis il laissera l'oiseau vivant aller en plein champ.
8 Mtu aliyetakaswa atafua nguo zake, atanyoa nywele zake zote, ataoga kwa maji, na ndipo atakuwa safi. Baada ya hayo lazima aje kwenye kambi, lakini ataishi nje ya hema lake kwa siku saba.
« Celui qui veut se purifier lavera ses vêtements, rasera tous ses cheveux et se baignera dans l'eau, et il sera pur. Après cela, il entrera dans le camp, mais il restera sept jours hors de sa tente.
9 Katika siku ya saba lazima anyoe nywele za kichwa chake, na lazima pia anyoe ndevu zake na nyusi. Lazima anyoe nywele zake zote, na lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji; ndipo atakuwa safi.
Le septième jour, il rasera tous les cheveux de sa tête, sa barbe et ses sourcils. Il rasera tous ses cheveux. Il lavera ses vêtements et se lavera le corps dans l'eau. Il sera alors pur.
10 Katika siku ya nane lazima achukue dume wa wana kondoo wawili wasio na lawama, mwana kondoo jike wa mwaka mmoja asiye na lawama, na tatu ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa mafuta kama sadaka ya nafaka, na kipimo kimoja cha mafuta.
« Le huitième jour, il prendra deux agneaux mâles sans défaut, une agnelle d'un an sans défaut, trois dixièmes d'un épha de fleur de farine pour l'offrande de farine, mélangée à de l'huile, et un log d'huile.
11 Kuhani ambaye amemtakasa mtu atamsimamisha mtu ambaye aliyemtakasa, pamoja na vile vitu, mbele ya Yahwe mahali pa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
Le prêtre qui l'aura purifié présentera l'homme à purifier et ces objets devant Yahvé, à l'entrée de la tente de la Rencontre.
12 Kuhani atachukua mmoja wa wanakondoo dume na kumtoa kama sadaka ya hatia, pamoja na kipimo cha mafuta; atavitikisa kwa sadaka ya kutikiswa mbele ya Yahwe.
« Le prêtre prendra l'un des agneaux mâles et l'offrira en sacrifice de culpabilité, avec le log d'huile, et il les agitera en signe d'offrande devant l'Éternel.
13 Lazima aue mwana kondoo dume mahali ambapo wanapochinjia sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, katika eneo la hema, sababu sadaka ya dhambi ni ya kuhani, kama afanyavyo sadaka ya hatia, kwasababu ni takatifu zaidi.
Il égorgera l'agneau mâle dans le lieu où l'on égorge le sacrifice pour le péché et l'holocauste, dans le lieu du sanctuaire; car si le sacrifice pour le péché appartient au prêtre, il en est de même du sacrifice de culpabilité. Elle est très sainte.
14 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu yule wa kutakaswa, katika dole gumba la kulia, katika dole la mguu wa kulia.
Le prêtre prendra du sang du sacrifice de culpabilité, et il en mettra sur le bout de l'oreille droite de celui qui doit être purifié, sur le pouce de sa main droite et sur le gros orteil de son pied droit.
15 Ndipo kuhani atachukua mafuta kutoka chombo na kuyamimina katika kiganja cha mkono wake wa kushoto, na kuzamisha kidole chake katika mafuta hayo yaliyo kwenye mkono wa kushoto,
Le prêtre prendra un peu de la bûche d'huile et la versera dans la paume de sa main gauche.
16 na kunyunyiza baadhi ya mafuta kwa kidole mara saba mbele za Yahwe.
Le prêtre trempera son doigt droit dans l'huile qui est dans sa main gauche, et il fera sept fois l'aspersion de l'huile avec son doigt devant Yahvé.
17 kuhani ataweka mafuta yaliyobaki kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu wa kutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wa kulia, na katika dole kubwa la mguu wa kulia. Lazima aweke mafuta haya juu ya damu kutoka kwenye sadaka ya hatia.
Le prêtre mettra une partie du reste de l'huile qui est dans sa main sur le bout de l'oreille droite de celui qui doit être purifié, sur le pouce de sa main droite et sur le gros orteil de son pied droit, sur le sang du sacrifice de culpabilité.
18 Kama kwa mafuta yaliyosalia kwamba katika mkono wa kuhani, atayaweka juu ya kichwa cha mtu ambaye atakaswaye, na kuhani atafanya utakaso kwaajili yake mbele za Yahwe.
Le reste de l'huile qui est dans la main du prêtre, il en mettra sur la tête de celui qui doit être purifié, et le prêtre fera pour lui l'expiation devant Yahvé.
19 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwaajili yake atakaswaye kwa sababu ya kutokuwa safi kwake, na badaye ataua sadaka ya kuchomwa.
« Le prêtre offrira le sacrifice pour le péché et fera l'expiation pour celui qui doit être purifié à cause de sa souillure. Ensuite, il égorgera l'holocauste;
20 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka juu ya madhabahu. Kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya mtu huyo, na ndipo atakuwa safi.
puis le prêtre offrira l'holocauste et l'offrande sur l'autel. Le prêtre fera l'expiation pour lui, et il sera pur.
21 Kwa namna hiyo, kama mtu ni masikini na hawezi kumudu matoleo haya, ndipo anaweza kuchukua kondoo mmoja dume kama sadaka ya hatia ya kutikiswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe, na moja ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka, na chombo cha mafuta,
« S'il est pauvre et qu'il n'a pas les moyens d'en acheter autant, il prendra un agneau mâle en sacrifice de culpabilité, pour faire l'expiation pour lui, et un dixième d'épha de fleur de farine mélangée à de l'huile, pour l'offrande de farine, et un log d'huile;
22 pamoja na njiwa wawili au kinda mbili za njiwa, ambao anaweza kupata; ndege mmoja atakuwa sadaka ya dhambi na mwingine sadaka ya kuteketezwa.
et deux tourterelles ou deux jeunes pigeons, selon ce qu'il pourra se permettre; l'un sera un sacrifice pour le péché, et l'autre un holocauste.
23 Katika siku ya nane lazima awalete kwa kuhani kwaajili ya utakaso, pakuigilia katika hema ya mkutano, mbele ya Yahwe.
« Le huitième jour, il les apportera au sacrificateur, à l'entrée de la tente d'assignation, devant Yahvé, pour sa purification.
24 Kuhani atachukua mwana kondoo kwaajili ya sadaka, na atachukua pamoja na kiasi cha mafuta ya mzeituni, na ataviinua juu kama anaviwasilisha kwa Yahwe.
Le sacrificateur prendra l'agneau du sacrifice de culpabilité et le log d'huile, et il les agitera en sacrifice par agitation devant Yahvé.
25 Atamuua mwana kondoo kwaajili ya sadaka ya hatia, na atachukua baadhi ya ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka juu ya ncha ya sikio la kulia la yule wakutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye dole kubwa la mguu, wa kulia.
Il égorgera l'agneau du sacrifice de culpabilité. Le prêtre prendra un peu du sang du sacrifice de culpabilité et en mettra sur le bout de l'oreille droite de celui qui doit être purifié, sur le pouce de sa main droite et sur le gros orteil de son pied droit.
26 Ndipo kuhani atamimina baadhi ya mafuta katika kiganja cha mkono wake wa kushoto,
Le prêtre versera une partie de l'huile dans la paume de sa main gauche;
27 na atanyunyiza kwa kidole chake cha kulia baadhi ya mafuta ambayo yako kwenye mkono wa kushoto mara saba mbele za Yahwe.
et le prêtre fera avec son doigt droit sept aspersions de l'huile qui est dans sa main gauche, devant Yahvé.
28 Ndipo kuhani ataweka kiasi cha mafuta ambayo yako kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la yule mtu wa kutakaswa, katika dole gumba lake la mkono wa kulia, na dole kubwa la mguu wa kulia, maeneo yale yale ambayo kaweka damu ya sadaka ya hatia.
Puis le prêtre mettra un peu de l'huile qui est dans sa main sur le bout de l'oreille droite de celui qui doit être purifié, sur le pouce de sa main droite et sur le gros orteil de son pied droit, à la place du sang du sacrifice de culpabilité.
29 Ataweka mafuta yaliyobaki yaliyo mkononi mwake juu ya yule wakutakaswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe.
Il mettra le reste de l'huile qui est dans la main du prêtre sur la tête de celui qui doit être purifié, afin de faire pour lui l'expiation devant Yahvé.
30 Lazima atoe sadaka ya njiwa au makinda ya njiwa, yale ambayo mtu ameweza kupata -
Il offrira l'une des tourterelles ou l'un des jeunes pigeons qu'il pourra se procurer,
31 moja kama ya sadaka ya dhambi na nyingine kama sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya yule ambaye atatakaswa mbele za Yahwe.
de l'espèce qu'il pourra se procurer, l'un pour le sacrifice pour le péché, l'autre pour l'holocauste, avec l'offrande de gâteau. Le prêtre fera l'expiation pour celui qui doit être purifié devant Yahvé. »
32 Hii ni sheria kwaajili ya mtu kwake kuna athari za ugonjwa wa ngozi, ambaye hawezi kumudu kiwango cha sadaka kwaajili ya utakaso wake.”
Telle est la loi pour celui qui a la plaie de la lèpre et qui n'a pas les moyens de payer le sacrifice pour sa purification.
33 Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
Yahvé parla à Moïse et à Aaron, et dit:
34 “Wakati mtakuja katika nchi ya Kanaani ambayo nimewapa kama miliki, na kama naweka ukungu unaenea ndani ya nyumba katika nchi ya miliki yenu,
Lorsque vous serez entrés dans le pays de Canaan, dont je vous donne la possession, et que j'aurai mis de la moisissure dans une maison du pays dont vous avez la possession,
35 ndipo yeye ambaye anamiliki nyumba ile lazima aje na kumwambia kuhani. Lazima aseme 'Inaonekana kwangu kuna kitu fulani kama ukungu ndani ya nyumba yangu.'”
le propriétaire de la maison viendra dire au prêtre: « Il me semble qu'il y a une sorte de plaie dans la maison ».
36 Ndipo kuhani ataamuru kwamba watoe vitu vyote ndani kabla hajaenda ndani kuona uthibitisho wa ukungu, kiasi kwamba hakuna ndani ya nyumba kitakachofanywa najisi. Badaye kuhani lazima aende ndani kuona humo ndani.
Le prêtre ordonnera que l'on vide la maison, avant que le prêtre n'entre pour examiner la plaie, afin que tout ce qui se trouve dans la maison ne soit pas rendu impur. Ensuite, le prêtre entrera pour examiner la maison.
37 Yeye lazima achunguze ukungu kuona kama umo katika kuta za nyumba, na kuona ikiwa kunaonekana ukijani au wekundu katika bonde za mwonekano wa kuta.
Il examinera la plaie; et voici, si la plaie est dans les murs de la maison, avec des stries creuses, verdâtres ou rougeâtres, et qu'elle paraisse plus profonde que le mur,
38 Kama nyumba inao ukungu, ndipo kuhani atatoka nje ya nyuma na kufunga mlango wa nyumba kwa siku saba.
le prêtre sortira de la maison, à la porte de la maison, et il fermera la maison pendant sept jours.
39 Ndipo kuhani atarudi tena katika siku ya saba na kuichunguza kuona kama ukungu umeenea katika kuta za nyumba.
Le prêtre reviendra le septième jour et regardera. Si la plaie s'est étendue dans les murs de la maison,
40 Kama hivyo, ndipo kuhani ataamuru kwamba wayaondoe mawe ambayo ukungu umepatikana na yatupwe katika sehemu najisi nje ya mji.
le prêtre ordonnera qu'on enlève les pierres dans lesquelles se trouve la plaie, et qu'on les jette dans un lieu impur hors de la ville.
41 Yeye atataka kuta zote za ndani ya nyumba zikwanguliwe, na lazima achukue vitu vilivyochafuliwa na hivyo vilivyokwanguliwa nje ya mji na kuvitupa kwenye eneo lisilosafi.
Il fera gratter l'intérieur de la maison sur toute sa surface. Ils jetteront le mortier qu'ils auront gratté hors de la ville, dans un lieu impur.
42 Lazima wayachukue mawe mengine na kuyaweka katika sehemu ya mawe yaliyoondolewa, na lazima watumie udongo mpya kupigia lipu nyumba.
On prendra d'autres pierres et on les mettra à la place de ces pierres; on prendra un autre mortier et on crépitera la maison.
43 Kama ukungu unakuja tena na unaingia katika nyumba ambayo mawe yameondolewa na kuta zimekwanguliwa na kupigwa lipu upya,
« Si la plaie revient et se déclare dans la maison, après qu'on a enlevé les pierres, qu'on a gratté la maison et qu'on l'a plâtrée,
44 ndipo kuhani lazima aje aingie ndani na kuchunguza nyumba kuona kama ukungu umeenea ndani ya nyumba. Kama hivyo, huo ni ukungu mbaya, na nyumba ni najisi.
le prêtre entrera et regardera; et voici, si la plaie s'est répandue dans la maison, c'est un mildiou destructeur dans la maison. Elle est impure.
45 Nyumba hiyo lazima iangushwe chini. Hayo mawe, mbao, na lipu yote ndani ya nyumba lazima vibebwe kupelekwa nje ya mji kwenye sehemu najisi.
Il démolira la maison, ses pierres et son bois, et tout le mortier de la maison. Il les emportera hors de la ville, dans un lieu impur.
46 Kwa nyongeza, yeyote anaenda ndani ya nyumba wakati imefungwa atakuwa najisi mpaka jioni.
De plus, celui qui entrera dans la maison pendant qu'elle sera fermée sera impur jusqu'au soir.
47 Na yeyote aliyelala ndani ya nyumba lazima afue nguo zake, na yeyote aliyekula ndani ya nyumba lazima afue nguo zake.
Celui qui se couchera dans la maison lavera ses vêtements, et celui qui mangera dans la maison lavera ses vêtements.
48 Kama kuhani akaingia hiyo kuichunguza kuona ikiwa ukungu umeenea katika nyumba baada ya nyumba kupigwa lipu, ndipo, kama ukungu umetoweka, ataitangaza nyumba hiyo kuwa ni safi.
« Si le prêtre entre et l'examine, et que la plaie ne se soit pas répandue dans la maison, après que la maison a été enduite, le prêtre déclarera la maison pure, parce que la plaie est guérie.
49 Ndipo kuhani lazima achukue ndege wawili kuitakasa nyumba, na mti wa mwelezi, na sufu nyekundu, na hisopo.
Pour purifier la maison, il prendra deux oiseaux, du bois de cèdre, du cramoisi et de l'hysope.
50 Atamuua ndege mmojawapo katika maji masafi kwenye dumu la udongo.
Il tuera l'un des oiseaux dans un vase de terre, au-dessus de l'eau courante.
51 Atachukua mti wa mwerezi, hisopo, sufu nyekundu na ndege aliyehai, na kuvichovya kwenye damu ya ndege aliyekufa, kwenye maji safi, na kunyunyizia nyumba mara saba.
Il prendra le bois de cèdre, l'hysope, le cramoisi et l'oiseau vivant; il les trempera dans le sang de l'oiseau tué et dans l'eau courante, et il fera sept aspersions sur la maison.
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya ndege na maji safi, pamoja na ndege aliyehai, mti wa mwerezi, hisopo, na sufu nyekundu. Lakini atamwachia ndege aliyehai aende nje ya mji mashambani.
Il purifiera la maison avec le sang de l'oiseau, avec l'eau courante, avec l'oiseau vivant, avec le bois de cèdre, avec l'hysope et avec le cramoisi;
53 Kwa njia hii lazima afanye upatanisho kwaajili ya nyumba, na itakuwa safi.
mais il laissera l'oiseau vivant sortir de la ville dans les champs. Il fera ainsi l'expiation de la maison, et elle sera pure. »
54 Hii ni sheria kwa aina zote za athari ya ugonjwa wa ngozi na vitu vyote vinavyosababisha ugonjwa kama huo, na kwaajili ya kuwashwa,
Telle est la loi pour toute plaie de lèpre, pour une démangeaison,
55 na kwa ukungu kwenye mavazi na nyumba,
pour la moisissure destructrice d'un vêtement, et pour une maison,
56 kwaajili ya uvimbe, kwaajili ya vipele, madoa,
pour un gonflement, une croûte, et une tache brillante;
57 kutambua wakati wowote tatizo hili ni najisi au lini limetakaswa. Hii ni sheria kwaajili ya athari za ugonjwa wa ukungu.
pour enseigner quand c'est impur, et quand c'est pur. C'est la loi de la lèpre.