< Mambo ya Walawi 14 >

1 Yahwe alizungumza na Musa, akisema,
And the Lord spak to Moises, and seide, This is the custom of a leprouse man,
2 “Hii itakuwa sheria kwaajili ya mtu aliyekufa kwenye siku ya utakaso. Lazima aletwe kwa kuhani.
whanne he schal be clensid. He schal be brouyt to the preest,
3 Kuhani atakwenda nje ya kambi kumchunguza mtu kuona kama madhara ya ugonjwa wa ngozi yameponywa.
which preest schal go out of the castels, and whanne he schal fynde that the lepre is clensid,
4 Ndipo kuhani ataamuru kwamba mtu mwenye kutakaswa lazima achukue ndege safi wawili, waliohai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
he schal comaunde to the man which is clensid, that he offre for hym silf twei quyke sparewis, whiche it is leueful to ete, and a `tree of cedre, and vermylyoun, and isope.
5 Kuhani atamwamuru kuua moja ya hao ndege juu ya maji safi yaliyo kwenye chungu cha udongo.
And the preest schal comaunde that oon of the sparewes be offrid in `a vessel of erthe,
6 Ndipo kuhani atamchukua ndege aliyehai na mti wa mwerezi, na kitani nyekundu na hisopo, na vyote hivi, pamoja na ndege aliyehai atavichovya kwenye damu ya ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
on quyke watris; sotheli he schal dippe the tother sparewe quyk with the `tre of cedre, and with a reed threed and ysope, in the blood of the sparewe offrid,
7 Ndipo kuhani atanyunyiza maji haya mara saba juu ya mtu anayetakaswa katika ugonjwa, na ndipo kuhani atamtangaza kuwa msafi. Ndipo kuhani atamwachia ndege aliyehai katika eneo wazi.
with which he schal sprenge seuensithis hym that schal be clensid, that he be purgid riytfuli; and he schal delyuere the quyk sparewe, that it fle in to the feeld.
8 Mtu aliyetakaswa atafua nguo zake, atanyoa nywele zake zote, ataoga kwa maji, na ndipo atakuwa safi. Baada ya hayo lazima aje kwenye kambi, lakini ataishi nje ya hema lake kwa siku saba.
And whanne the man hath waische hise clothis, he schal schaue alle the heeris of the bodi, and he schal be waischun in watir, and he schal be clensid, and he schal entre in to the castels; so oneli that he dwelle without his tabernacle bi seuene daies;
9 Katika siku ya saba lazima anyoe nywele za kichwa chake, na lazima pia anyoe ndevu zake na nyusi. Lazima anyoe nywele zake zote, na lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji; ndipo atakuwa safi.
and that in the seuenthe dai he schaue the heeris of the heed, and the beerd, and brewis, and the heeris of al the bodi. And whanne the clothis and bodi ben waischun,
10 Katika siku ya nane lazima achukue dume wa wana kondoo wawili wasio na lawama, mwana kondoo jike wa mwaka mmoja asiye na lawama, na tatu ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa mafuta kama sadaka ya nafaka, na kipimo kimoja cha mafuta.
eft in the eiyetithe dai he schal take twei lambren without wem, and a scheep of o yeer without wem, and thre dymes of wheete flour, in to sacrifice, which be spreynte with oile, and bi it silf a sextarie of oyle.
11 Kuhani ambaye amemtakasa mtu atamsimamisha mtu ambaye aliyemtakasa, pamoja na vile vitu, mbele ya Yahwe mahali pa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
And whanne the preest, that purgith the man, hath set hym and alle hise thingis bifor the Lord, in the dore of the tabernacle of witnessyng, he schal take a lomb,
12 Kuhani atachukua mmoja wa wanakondoo dume na kumtoa kama sadaka ya hatia, pamoja na kipimo cha mafuta; atavitikisa kwa sadaka ya kutikiswa mbele ya Yahwe.
and schal offre it for trespas, and schal offre the sextarie of oyle; and whanne alle thingis ben offrid bifor the Lord,
13 Lazima aue mwana kondoo dume mahali ambapo wanapochinjia sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, katika eneo la hema, sababu sadaka ya dhambi ni ya kuhani, kama afanyavyo sadaka ya hatia, kwasababu ni takatifu zaidi.
he schal offre the lomb, where the sacrifice for synne and the brent sacrifice is wont to be offrid, that is, in the hooli place; for as for synne so and for trespas the offryng perteyneth to the preest; it is hooli of the noumbre of hooli thingis.
14 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu yule wa kutakaswa, katika dole gumba la kulia, katika dole la mguu wa kulia.
And the preest schal take of the blood of sacrifice which is offrid for trespas, and schal putte on the laste part of the riyt eere `of hym which is clensid, and on the thumbis of the riyt hond and foot.
15 Ndipo kuhani atachukua mafuta kutoka chombo na kuyamimina katika kiganja cha mkono wake wa kushoto, na kuzamisha kidole chake katika mafuta hayo yaliyo kwenye mkono wa kushoto,
And he schal putte of the sextarie of oyle in to his left hond,
16 na kunyunyiza baadhi ya mafuta kwa kidole mara saba mbele za Yahwe.
and he schal dippe the riyt fyngur therynne, and schal sprynge seuensithis bifor the Lord.
17 kuhani ataweka mafuta yaliyobaki kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu wa kutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wa kulia, na katika dole kubwa la mguu wa kulia. Lazima aweke mafuta haya juu ya damu kutoka kwenye sadaka ya hatia.
Sotheli he schal schede that that is residue of the oile in the left hond, on the laste part of the riyt eere `of hym which is clensid, and on the thombis of the riyt hond and foot, and on the blood which is sched for trespas,
18 Kama kwa mafuta yaliyosalia kwamba katika mkono wa kuhani, atayaweka juu ya kichwa cha mtu ambaye atakaswaye, na kuhani atafanya utakaso kwaajili yake mbele za Yahwe.
and on the heed `of hym.
19 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwaajili yake atakaswaye kwa sababu ya kutokuwa safi kwake, na badaye ataua sadaka ya kuchomwa.
And the preest schal preye for hym bifor the Lord, and schal make sacrifice for synne; thanne he schal offre brent sacrifice,
20 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka juu ya madhabahu. Kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya mtu huyo, na ndipo atakuwa safi.
and schal putte it in the auter with hise fletynge sacrifices, and the man schal be clensid riytfuli.
21 Kwa namna hiyo, kama mtu ni masikini na hawezi kumudu matoleo haya, ndipo anaweza kuchukua kondoo mmoja dume kama sadaka ya hatia ya kutikiswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe, na moja ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka, na chombo cha mafuta,
That if he is pore, and his hoond may not fynde tho thingis that ben seid, he schal take for trespas a lomb to offryng, that the preest preie for him, and the tenthe part of wheete flour spreynt togidire with oile in to sacrifice, and a sextarie of oile,
22 pamoja na njiwa wawili au kinda mbili za njiwa, ambao anaweza kupata; ndege mmoja atakuwa sadaka ya dhambi na mwingine sadaka ya kuteketezwa.
and twei turtlis, ethir twei `briddis of culueris, of whiche oon be for synne, and the tothir in to brent sacrifice;
23 Katika siku ya nane lazima awalete kwa kuhani kwaajili ya utakaso, pakuigilia katika hema ya mkutano, mbele ya Yahwe.
and he schal offre tho in the eiytthe dai of his clensyng to the preest, at the dore of tabernacle of witnessyng bifor the Lord.
24 Kuhani atachukua mwana kondoo kwaajili ya sadaka, na atachukua pamoja na kiasi cha mafuta ya mzeituni, na ataviinua juu kama anaviwasilisha kwa Yahwe.
And the preest schal take the lomb for trespas, and the sextarie of oile, and schal reise togidere;
25 Atamuua mwana kondoo kwaajili ya sadaka ya hatia, na atachukua baadhi ya ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka juu ya ncha ya sikio la kulia la yule wakutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye dole kubwa la mguu, wa kulia.
and whanne the lomb is offrid, he schal putte of the blood therof on the laste part of the riyt eere `of hym that is clensid, and on the thumbis of his riyt hond and foot.
26 Ndipo kuhani atamimina baadhi ya mafuta katika kiganja cha mkono wake wa kushoto,
Sotheli the preest putte the part of oile in to his left hond,
27 na atanyunyiza kwa kidole chake cha kulia baadhi ya mafuta ambayo yako kwenye mkono wa kushoto mara saba mbele za Yahwe.
in which he schal dippe the fyngur of the riyt hond, and schal sprynge seuensithes ayens the Lord;
28 Ndipo kuhani ataweka kiasi cha mafuta ambayo yako kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la yule mtu wa kutakaswa, katika dole gumba lake la mkono wa kulia, na dole kubwa la mguu wa kulia, maeneo yale yale ambayo kaweka damu ya sadaka ya hatia.
and the preest schal touche the laste part of the riyt eere `of hym that is clensid, and the thombe of the riyt hond and foot, in the place of blood which is sched out for trespas.
29 Ataweka mafuta yaliyobaki yaliyo mkononi mwake juu ya yule wakutakaswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe.
Sotheli he schal putte the tother part of oile, which is in the left hond, on the `heed of the man clensid, that he plese the Lord for hym.
30 Lazima atoe sadaka ya njiwa au makinda ya njiwa, yale ambayo mtu ameweza kupata -
And he schal offre a turtle, ethir a culuer brid,
31 moja kama ya sadaka ya dhambi na nyingine kama sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya yule ambaye atatakaswa mbele za Yahwe.
oon for trespas, and the tothir in to brent sacrifice, with her fletynge offryngis.
32 Hii ni sheria kwaajili ya mtu kwake kuna athari za ugonjwa wa ngozi, ambaye hawezi kumudu kiwango cha sadaka kwaajili ya utakaso wake.”
This is the sacrifice of a leprouse man, that may not haue alle thingis in to the clensyng of hym silf.
33 Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
And the Lord spak to Moises and Aaron, and seide,
34 “Wakati mtakuja katika nchi ya Kanaani ambayo nimewapa kama miliki, na kama naweka ukungu unaenea ndani ya nyumba katika nchi ya miliki yenu,
Whanne ye han entrid in to the lond of Canaan, which lond Y schal yyue to you in to possessioun, if the wounde of lepre is in the housis,
35 ndipo yeye ambaye anamiliki nyumba ile lazima aje na kumwambia kuhani. Lazima aseme 'Inaonekana kwangu kuna kitu fulani kama ukungu ndani ya nyumba yangu.'”
he schal go, whos the hous is, `and schal telle to the preest, and schal seie, It semeth to me, that as a wound of lepre is in myn hous.
36 Ndipo kuhani ataamuru kwamba watoe vitu vyote ndani kabla hajaenda ndani kuona uthibitisho wa ukungu, kiasi kwamba hakuna ndani ya nyumba kitakachofanywa najisi. Badaye kuhani lazima aende ndani kuona humo ndani.
And the preest schal comaunde, `that thei bere out of the hous alle thingis bifore that he entre in to it, `and me se where it be lepre, lest alle thingis that ben in the hows, be maad vnclene; and the preest schal entre aftirward, that he se the lepre of the hows.
37 Yeye lazima achunguze ukungu kuona kama umo katika kuta za nyumba, na kuona ikiwa kunaonekana ukijani au wekundu katika bonde za mwonekano wa kuta.
And whanne he seeth in the wallis therof as litle valeis `foule bi palenesse, ethir bi reednesse, and lowere than the tother hiyere part,
38 Kama nyumba inao ukungu, ndipo kuhani atatoka nje ya nyuma na kufunga mlango wa nyumba kwa siku saba.
he schal go out at the dore of the hows, and anoon he schal close it bi seuene daies.
39 Ndipo kuhani atarudi tena katika siku ya saba na kuichunguza kuona kama ukungu umeenea katika kuta za nyumba.
And he schal turne ayen in the seuenthe day, and schal se it; if he fyndith that the lepre encreesside,
40 Kama hivyo, ndipo kuhani ataamuru kwamba wayaondoe mawe ambayo ukungu umepatikana na yatupwe katika sehemu najisi nje ya mji.
he schal comaunde that the stoonys be cast out, in whyche the lepre is, and that tho stonys be cast out of the citee in an vncleene place.
41 Yeye atataka kuta zote za ndani ya nyumba zikwanguliwe, na lazima achukue vitu vilivyochafuliwa na hivyo vilivyokwanguliwa nje ya mji na kuvitupa kwenye eneo lisilosafi.
Sotheli he schal comaunde that thilke hows be rasid with ynne bi cumpas, and that the dust of the rasyng be spreynt without the citee, in an vnclene place,
42 Lazima wayachukue mawe mengine na kuyaweka katika sehemu ya mawe yaliyoondolewa, na lazima watumie udongo mpya kupigia lipu nyumba.
and that othere stoonys be put ayen for these, that ben takun awey, and that the hows be daubid with othir morter.
43 Kama ukungu unakuja tena na unaingia katika nyumba ambayo mawe yameondolewa na kuta zimekwanguliwa na kupigwa lipu upya,
But if aftir that the stoonus ben takun awey, and the dust is borun out,
44 ndipo kuhani lazima aje aingie ndani na kuchunguza nyumba kuona kama ukungu umeenea ndani ya nyumba. Kama hivyo, huo ni ukungu mbaya, na nyumba ni najisi.
and othere erthe is daubid, the preest entrith, and seeth the lepre turned ayen, and the wallis spreynt with spottis, the lepre is stidfastly dwellynge, and the hows is vnclene;
45 Nyumba hiyo lazima iangushwe chini. Hayo mawe, mbao, na lipu yote ndani ya nyumba lazima vibebwe kupelekwa nje ya mji kwenye sehemu najisi.
which hows thei schulen destrye anoon, and thei schulen caste out of the citee, in an vnclene place, the stoonys therof, and the trees, and al the dust.
46 Kwa nyongeza, yeyote anaenda ndani ya nyumba wakati imefungwa atakuwa najisi mpaka jioni.
He that entrith in to the hous, whanne it is schit, schal be vnclene `til to euentid,
47 Na yeyote aliyelala ndani ya nyumba lazima afue nguo zake, na yeyote aliyekula ndani ya nyumba lazima afue nguo zake.
and he that slepith and etith ony thing therynne, schal waische hise clothis.
48 Kama kuhani akaingia hiyo kuichunguza kuona ikiwa ukungu umeenea katika nyumba baada ya nyumba kupigwa lipu, ndipo, kama ukungu umetoweka, ataitangaza nyumba hiyo kuwa ni safi.
That if the preest entrith, and seeth that the lepre encreesside not in the hows, aftir that it was daubid the secounde tyme, he schal clense it; for heelthe is yoldun.
49 Ndipo kuhani lazima achukue ndege wawili kuitakasa nyumba, na mti wa mwelezi, na sufu nyekundu, na hisopo.
And in the clensyng therof he schal take twey sparewis, and `a tre of cedre, and `a reed threed, and isope.
50 Atamuua ndege mmojawapo katika maji masafi kwenye dumu la udongo.
And whanne o sparewe is offrid in a vessel of erthe, on quyk watris,
51 Atachukua mti wa mwerezi, hisopo, sufu nyekundu na ndege aliyehai, na kuvichovya kwenye damu ya ndege aliyekufa, kwenye maji safi, na kunyunyizia nyumba mara saba.
he schal take the `tre of cedre, and ysope, and reed threed, and the quyk sparewe, and he schal dippe alle thingis in the blood of the sparewe offrid, and in lyuynge watris;
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya ndege na maji safi, pamoja na ndege aliyehai, mti wa mwerezi, hisopo, na sufu nyekundu. Lakini atamwachia ndege aliyehai aende nje ya mji mashambani.
and he schal sprynge the hows seuen sithis; and he schal clense it as wel in the blood of the sparewe as in lyuynge watris, and in the quyk sparewe, and in the `tre of cedre, and in ysope, and `reed threed.
53 Kwa njia hii lazima afanye upatanisho kwaajili ya nyumba, na itakuwa safi.
And whanne he hath left the sparewe to fle in to the feeld frely, he schal preye for the hows, and it schal be clensid riytfuli.
54 Hii ni sheria kwa aina zote za athari ya ugonjwa wa ngozi na vitu vyote vinavyosababisha ugonjwa kama huo, na kwaajili ya kuwashwa,
This is the lawe of al lepre,
55 na kwa ukungu kwenye mavazi na nyumba,
and of smytyng, of lepre of clothis, and of housis,
56 kwaajili ya uvimbe, kwaajili ya vipele, madoa,
of syngne of wounde, and of litle whelkis brekynge out, of spotte schynynge, and in colours chaungid in to dyuerse spices,
57 kutambua wakati wowote tatizo hili ni najisi au lini limetakaswa. Hii ni sheria kwaajili ya athari za ugonjwa wa ukungu.
that it may be wist, what is cleene, ether uncleene.

< Mambo ya Walawi 14 >