< Mambo ya Walawi 14 >

1 Yahwe alizungumza na Musa, akisema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Hii itakuwa sheria kwaajili ya mtu aliyekufa kwenye siku ya utakaso. Lazima aletwe kwa kuhani.
This it will be [the] legal [procedure] of the [one who] has a serious skin disease on [the] day of purification his and he will be brought to the priest.
3 Kuhani atakwenda nje ya kambi kumchunguza mtu kuona kama madhara ya ugonjwa wa ngozi yameponywa.
And he will go out the priest to from [the] outside of the camp and he will see the priest and there! it has been healed [the] plague of the serious skin disease from the [one who] had a serious skin disease.
4 Ndipo kuhani ataamuru kwamba mtu mwenye kutakaswa lazima achukue ndege safi wawili, waliohai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
And he will command the priest and someone will take for the [one] purifying himself two birds living pure and wood of cedar and scarlet of a worm and hyssop.
5 Kuhani atamwamuru kuua moja ya hao ndege juu ya maji safi yaliyo kwenye chungu cha udongo.
And he will command the priest and someone will cut [the] throat of the bird one into a vessel of earthenware over water living.
6 Ndipo kuhani atamchukua ndege aliyehai na mti wa mwerezi, na kitani nyekundu na hisopo, na vyote hivi, pamoja na ndege aliyehai atavichovya kwenye damu ya ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
The bird living he will take it and [the] wood of cedar and [the] scarlet of the worm and the hyssop and he will dip them and - the bird living in [the] blood of the bird [which] had the throat cut over the water living.
7 Ndipo kuhani atanyunyiza maji haya mara saba juu ya mtu anayetakaswa katika ugonjwa, na ndipo kuhani atamtangaza kuwa msafi. Ndipo kuhani atamwachia ndege aliyehai katika eneo wazi.
And he will spatter [it] on the [one] purifying himself from the serious skin disease seven times and he will declare pure him and he will let go the bird living over [the] surface of the field.
8 Mtu aliyetakaswa atafua nguo zake, atanyoa nywele zake zote, ataoga kwa maji, na ndipo atakuwa safi. Baada ya hayo lazima aje kwenye kambi, lakini ataishi nje ya hema lake kwa siku saba.
And he will wash the [one] purifying himself garments his and he will shave all hair his and he will wash with water and he will be pure and after he will come into the camp and he will remain from [the] outside of tent his seven days.
9 Katika siku ya saba lazima anyoe nywele za kichwa chake, na lazima pia anyoe ndevu zake na nyusi. Lazima anyoe nywele zake zote, na lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji; ndipo atakuwa safi.
And it will be on the day seventh he will shave all hair his head his and beard his and [the] eyebrows of eyes his and all hair his he will shave and he will wash garments his and he will wash body his with water and he will be pure.
10 Katika siku ya nane lazima achukue dume wa wana kondoo wawili wasio na lawama, mwana kondoo jike wa mwaka mmoja asiye na lawama, na tatu ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa mafuta kama sadaka ya nafaka, na kipimo kimoja cha mafuta.
And on the day eighth he will take two male lambs unblemished and a ewe-lamb one a daughter of year its unblemished and three tenths fine flour a grain offering mixed with oil and a log one oil.
11 Kuhani ambaye amemtakasa mtu atamsimamisha mtu ambaye aliyemtakasa, pamoja na vile vitu, mbele ya Yahwe mahali pa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
And he will station the priest who declares pure the person who is purifying himself and with them before Yahweh [the] entrance of [the] tent of meeting.
12 Kuhani atachukua mmoja wa wanakondoo dume na kumtoa kama sadaka ya hatia, pamoja na kipimo cha mafuta; atavitikisa kwa sadaka ya kutikiswa mbele ya Yahwe.
And he will take the priest the male lamb one and he will present it to a guilt offering and [the] log of oil and he will wave them a wave-offering before Yahweh.
13 Lazima aue mwana kondoo dume mahali ambapo wanapochinjia sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, katika eneo la hema, sababu sadaka ya dhambi ni ya kuhani, kama afanyavyo sadaka ya hatia, kwasababu ni takatifu zaidi.
And he will cut [the] throat of the male lamb in [the] place where someone cuts [the] throat of the sin offering and the burnt offering in [the] place of holiness for like the sin offering the guilt offering it [belongs] to the priest [is] a holy thing of holy things it.
14 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu yule wa kutakaswa, katika dole gumba la kulia, katika dole la mguu wa kulia.
And he will take the priest some of [the] blood of the guilt offering and he will put [it] the priest on [the] lobe of [the] ear of the [one] purifying himself right and on [the] thumb of hand his right and on [the] big toe of foot his right.
15 Ndipo kuhani atachukua mafuta kutoka chombo na kuyamimina katika kiganja cha mkono wake wa kushoto, na kuzamisha kidole chake katika mafuta hayo yaliyo kwenye mkono wa kushoto,
And he will take the priest some of [the] log of oil and he will pour [it] on [the] palm of the priest left.
16 na kunyunyiza baadhi ya mafuta kwa kidole mara saba mbele za Yahwe.
And he will dip the priest finger his right some of the oil which [is] on palm his left and he will spatter some of the oil with finger his seven times before Yahweh.
17 kuhani ataweka mafuta yaliyobaki kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu wa kutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wa kulia, na katika dole kubwa la mguu wa kulia. Lazima aweke mafuta haya juu ya damu kutoka kwenye sadaka ya hatia.
And some of [the] remainder of the oil which [is] on palm his he will put the priest on [the] lobe of [the] ear of the [one] purifying himself right and on [the] thumb of hand his right and on [the] big toe of foot his right on [the] blood of the guilt offering.
18 Kama kwa mafuta yaliyosalia kwamba katika mkono wa kuhani, atayaweka juu ya kichwa cha mtu ambaye atakaswaye, na kuhani atafanya utakaso kwaajili yake mbele za Yahwe.
And the remainder in the oil which [is] on [the] palm of the priest he will put on [the] head of the [one] purifying himself and he will make atonement on him the priest before Yahweh.
19 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwaajili yake atakaswaye kwa sababu ya kutokuwa safi kwake, na badaye ataua sadaka ya kuchomwa.
And he will offer the priest the sin offering and he will make atonement on the [one] purifying himself from uncleanness his and after he will cut [the] throat of the burnt offering.
20 Ndipo kuhani atatoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka juu ya madhabahu. Kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya mtu huyo, na ndipo atakuwa safi.
And he will offer up the priest the burnt offering and the grain offering the altar towards and he will make atonement on him the priest and he will be clean.
21 Kwa namna hiyo, kama mtu ni masikini na hawezi kumudu matoleo haya, ndipo anaweza kuchukua kondoo mmoja dume kama sadaka ya hatia ya kutikiswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe, na moja ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka, na chombo cha mafuta,
And if [is] poor he and not hand his [is] reaching and he will take a male lamb one a guilt offering to a wave-offering to make atonement on himself and a tenth of fine flour one mixed with oil to a grain offering and a log of oil.
22 pamoja na njiwa wawili au kinda mbili za njiwa, ambao anaweza kupata; ndege mmoja atakuwa sadaka ya dhambi na mwingine sadaka ya kuteketezwa.
And two turtle-doves or two young ones of a dove which it will reach hand his and it will be one [bird] a sin offering and the one a burnt offering.
23 Katika siku ya nane lazima awalete kwa kuhani kwaajili ya utakaso, pakuigilia katika hema ya mkutano, mbele ya Yahwe.
And he will bring them on the day eighth for purification his to the priest to [the] entrance of [the] tent of meeting before Yahweh.
24 Kuhani atachukua mwana kondoo kwaajili ya sadaka, na atachukua pamoja na kiasi cha mafuta ya mzeituni, na ataviinua juu kama anaviwasilisha kwa Yahwe.
And he will take the priest [the] male lamb of the guilt offering and [the] log of oil and he will wave them the priest a wave-offering before Yahweh.
25 Atamuua mwana kondoo kwaajili ya sadaka ya hatia, na atachukua baadhi ya ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka juu ya ncha ya sikio la kulia la yule wakutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye dole kubwa la mguu, wa kulia.
And he will cut [the] throat of [the] male lamb of the guilt offering and he will take the priest some of [the] blood of the guilt offering and he will put [it] on [the] lobe of [the] ear of the [one] purifying himself right and on [the] thumb of hand his right and on [the] big toe of foot his right.
26 Ndipo kuhani atamimina baadhi ya mafuta katika kiganja cha mkono wake wa kushoto,
And some of the oil he will pour the priest on [the] palm of the priest left.
27 na atanyunyiza kwa kidole chake cha kulia baadhi ya mafuta ambayo yako kwenye mkono wa kushoto mara saba mbele za Yahwe.
And he will spatter the priest with finger his right some of the oil which [is] on palm his left seven times before Yahweh.
28 Ndipo kuhani ataweka kiasi cha mafuta ambayo yako kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la yule mtu wa kutakaswa, katika dole gumba lake la mkono wa kulia, na dole kubwa la mguu wa kulia, maeneo yale yale ambayo kaweka damu ya sadaka ya hatia.
And he will put the priest some of the oil - which [is] on palm his on [the] lobe of [the] ear of the [one] purifying himself right and on [the] thumb of hand his right and on [the] big toe of foot his right on [the] place of [the] blood of the guilt offering.
29 Ataweka mafuta yaliyobaki yaliyo mkononi mwake juu ya yule wakutakaswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe.
And the remainder of the oil which [is] on [the] palm of the priest he will put on [the] head of the [one] purifying himself to make atonement on him before Yahweh.
30 Lazima atoe sadaka ya njiwa au makinda ya njiwa, yale ambayo mtu ameweza kupata -
And he will offer the one of the turtle-doves or of [the] young ones of the dove from [that] which it will reach hand his.
31 moja kama ya sadaka ya dhambi na nyingine kama sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya yule ambaye atatakaswa mbele za Yahwe.
[that] which It will reach hand his the one [bird] a sin offering and the one a burnt offering with the grain offering and he will make atonement the priest on the [one] purifying himself before Yahweh.
32 Hii ni sheria kwaajili ya mtu kwake kuna athari za ugonjwa wa ngozi, ambaye hawezi kumudu kiwango cha sadaka kwaajili ya utakaso wake.”
This [is] [the] legal [procedure] of [one] whom [was] in him a plague of a serious skin disease who not it will reach hand his for purification his.
33 Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
And he spoke Yahweh to Moses and to Aaron saying.
34 “Wakati mtakuja katika nchi ya Kanaani ambayo nimewapa kama miliki, na kama naweka ukungu unaenea ndani ya nyumba katika nchi ya miliki yenu,
That you will go into [the] land of Canaan which I [am] about to give to you to a possession and I will put a plague of a serious disease in [the] house of [the] land of possession your.
35 ndipo yeye ambaye anamiliki nyumba ile lazima aje na kumwambia kuhani. Lazima aseme 'Inaonekana kwangu kuna kitu fulani kama ukungu ndani ya nyumba yangu.'”
And he will come [the one] whom [belongs] to him the house and he will tell to the priest saying like a plague it has appeared to me in the house.
36 Ndipo kuhani ataamuru kwamba watoe vitu vyote ndani kabla hajaenda ndani kuona uthibitisho wa ukungu, kiasi kwamba hakuna ndani ya nyumba kitakachofanywa najisi. Badaye kuhani lazima aende ndani kuona humo ndani.
And he will command the priest and people will make clear the house before he will go the priest to see the plague and not it will be unclean all that [is] in the house and after thus he will go the priest to see the house.
37 Yeye lazima achunguze ukungu kuona kama umo katika kuta za nyumba, na kuona ikiwa kunaonekana ukijani au wekundu katika bonde za mwonekano wa kuta.
And he will see the plague and there! the plague [is] in [the] walls of the house depressions greenish or reddish and appearance their [is] deep more than the wall.
38 Kama nyumba inao ukungu, ndipo kuhani atatoka nje ya nyuma na kufunga mlango wa nyumba kwa siku saba.
And he will go out the priest from the house to [the] entrance of the house and he will shut up the house seven days.
39 Ndipo kuhani atarudi tena katika siku ya saba na kuichunguza kuona kama ukungu umeenea katika kuta za nyumba.
And he will return the priest on the day seventh and he will see and there! it has spread the plague in [the] walls of the house.
40 Kama hivyo, ndipo kuhani ataamuru kwamba wayaondoe mawe ambayo ukungu umepatikana na yatupwe katika sehemu najisi nje ya mji.
And he will command the priest and people will tear out the stones which [is] in them the plague and they will throw them to from [the] outside of the city to a place unclean.
41 Yeye atataka kuta zote za ndani ya nyumba zikwanguliwe, na lazima achukue vitu vilivyochafuliwa na hivyo vilivyokwanguliwa nje ya mji na kuvitupa kwenye eneo lisilosafi.
And the house he will scrape from inside all around and they will pour out the dust which they have scraped off to from [the] outside of the city to a place unclean.
42 Lazima wayachukue mawe mengine na kuyaweka katika sehemu ya mawe yaliyoondolewa, na lazima watumie udongo mpya kupigia lipu nyumba.
And they will take stones other and they will bring [them] to in place of the stones and dust other he will take and he will plaster the house.
43 Kama ukungu unakuja tena na unaingia katika nyumba ambayo mawe yameondolewa na kuta zimekwanguliwa na kupigwa lipu upya,
And if it will return the plague and it will break out in the house after tears out the stones and after has scraped the house and after was plastered.
44 ndipo kuhani lazima aje aingie ndani na kuchunguza nyumba kuona kama ukungu umeenea ndani ya nyumba. Kama hivyo, huo ni ukungu mbaya, na nyumba ni najisi.
And he will come the priest and he will see and there! it has spread the plague in the house [is] a serious disease malignant it in the house [is] unclean it.
45 Nyumba hiyo lazima iangushwe chini. Hayo mawe, mbao, na lipu yote ndani ya nyumba lazima vibebwe kupelekwa nje ya mji kwenye sehemu najisi.
And he will pull down the house stones its and wood its and all [the] dust of the house and he will take [them] out to from [the] outside of the city to a place unclean.
46 Kwa nyongeza, yeyote anaenda ndani ya nyumba wakati imefungwa atakuwa najisi mpaka jioni.
And the [one who] goes into the house all [the] days [which] he has shut up it he will be unclean until the evening.
47 Na yeyote aliyelala ndani ya nyumba lazima afue nguo zake, na yeyote aliyekula ndani ya nyumba lazima afue nguo zake.
And the [one who] lies down in the house he will wash garments his and the [one who] eats in the house he will wash garments his.
48 Kama kuhani akaingia hiyo kuichunguza kuona ikiwa ukungu umeenea katika nyumba baada ya nyumba kupigwa lipu, ndipo, kama ukungu umetoweka, ataitangaza nyumba hiyo kuwa ni safi.
And if indeed he will come the priest and he will see and there! not it has spread the plague in the house after was plastered the house and he will declare pure the priest the house for it has been healed the plague.
49 Ndipo kuhani lazima achukue ndege wawili kuitakasa nyumba, na mti wa mwelezi, na sufu nyekundu, na hisopo.
And he will take to cleanse from sin the house two birds and wood of cedar and scarlet of a worm and hyssop.
50 Atamuua ndege mmojawapo katika maji masafi kwenye dumu la udongo.
And he will cut [the] throat of the bird one into a vessel of earthenware over water living.
51 Atachukua mti wa mwerezi, hisopo, sufu nyekundu na ndege aliyehai, na kuvichovya kwenye damu ya ndege aliyekufa, kwenye maji safi, na kunyunyizia nyumba mara saba.
And he will take [the] wood of cedar and the hyssop and - [the] scarlet of the worm and the bird living and he will dip them in [the] blood of the bird [which] had the throat cut and in the water living and he will spatter [it] to the house seven times.
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya ndege na maji safi, pamoja na ndege aliyehai, mti wa mwerezi, hisopo, na sufu nyekundu. Lakini atamwachia ndege aliyehai aende nje ya mji mashambani.
And he will cleanse from sin the house with [the] blood of the bird and with the water living and with the bird living and with [the] wood of cedar and with the hyssop and with [the] scarlet of the worm.
53 Kwa njia hii lazima afanye upatanisho kwaajili ya nyumba, na itakuwa safi.
And he will let go the bird living to from [the] outside of the city to [the] surface of the field and he will make atonement on the house and it will be pure.
54 Hii ni sheria kwa aina zote za athari ya ugonjwa wa ngozi na vitu vyote vinavyosababisha ugonjwa kama huo, na kwaajili ya kuwashwa,
This [is] the legal [procedure] to every plague of serious skin disease and to scall.
55 na kwa ukungu kwenye mavazi na nyumba,
And to [the] serious disease of clothing and to house.
56 kwaajili ya uvimbe, kwaajili ya vipele, madoa,
And to swelling and to flaking skin and to bright spot.
57 kutambua wakati wowote tatizo hili ni najisi au lini limetakaswa. Hii ni sheria kwaajili ya athari za ugonjwa wa ukungu.
To teach on [the] day of the unclean [thing] and on [the] day of the pure [thing] this [is] [the] legal [procedure] of serious skin disease.

< Mambo ya Walawi 14 >