< Mambo ya Walawi 13 >
1 Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
Yahvé parla à Moïse et à Aaron, et dit:
2 Mtu yeyote anayeonekana na uvimbe au pele au doa ling'aalo juu ya ngozi ya mwili wake, na likawa limeambukizwa ugonjwa wa ngozi mwilini mwake, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani mkuu au kwa mmoja wa wanawe makuhani.
« Lorsqu'un homme aura une tuméfaction sur la peau de son corps, ou une croûte, ou une tache brillante, et que cela deviendra dans la peau de son corps la plaie de la lèpre, on l'amènera au prêtre Aaron ou à l'un de ses fils, les prêtres.
3 Naye kuhanai atachunguza ugonjwa huo kwenye ngozi ya mwili wake. Iwapo malaika zilizopo eneo lenye ugonjwa zimegeuka kuwa nyeupe, na iwapo ugonjwa umejitokeza juu ya ngozi, huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Baada cha kuhani kumchunguza, atamtangaza kuwa ni najisi.
Le prêtre examinera la plaie sur la peau du corps. Si le poil de la plaie est devenu blanc, et si l'aspect de la plaie est plus profond que la peau du corps, c'est la plaie de la lèpre; le prêtre l'examinera donc et le déclarera impur.
4 Iwapo lile doa ling'aalo katika ngozi yake ni jeupe, na kuonekana kwake halikwenda chini zaidi ya ngozi, na iwapo malaika za eneo lenye ugonjwa hazijabadilika kuwa nyeupe, naye kuhani atamtenga mgonjwa kwa siku saba.
Si la tache brillante est blanche sur la peau de son corps, que son aspect n'est pas plus profond que la peau et que son poil n'est pas devenu blanc, le prêtre isolera la personne infectée pendant sept jours.
5 Katika siku ya saba, huyo kuhani itambidi kumchunguza tena ili kuona kama katika maamzi yake huo ugonjwa siyo mbaya, na kama haujaenea kwenye ngozi. Iwapo haujaenea, basi, kuhani atamtenga kwa siku saba zaidi.
Le prêtre l'examinera le septième jour. Si, à ses yeux, la plaie est arrêtée et que la plaie ne s'est pas propagée dans la peau, le prêtre l'isolera encore pendant sept jours.
6 Naye kuhani atamchunga tena katika siku ya saba ili kuona kama ugonjwa ubepona na haujasambaa zaidi kwenye ngozi. kama haujasambaa, basi, kuhani atamtangaza kuwa yeye ni safi. Ni upele tu. Naye atafua nguo zake, na kisha yeye yu safi.
Le prêtre l'examinera de nouveau le septième jour. Voici, si la plaie a disparu et que la plaie ne s'est pas propagée dans la peau, alors le prêtre le déclarera pur. C'est une gale. Il lavera ses vêtements et sera pur.
7 Lakini endapo ule upele utakuwa umishasambaa kwenye ngozi baada ya kuwa amejionyesha kwa kuhani kwa ajili kusafishwa kwake, itambidi kujionyesha tena kwa kuhani.
Mais si la gale s'étend sur la peau après qu'il s'est présenté au prêtre pour sa purification, il se présentera de nouveau au prêtre.
8 Naye kuhani atamchunguza ilikuona kama huo upele umsambaa zaidi ndani ya ngozi. Na endapo utakuwa umesambaa, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
Le prêtre l'examinera; et voici, si la gale s'est étendue sur la peau, le prêtre le déclarera impur. C'est la lèpre.
9 Iwapo ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza umo kwa mtu fulani, naye mtu huyo yapasa aletwe kwa kuhan.
« Lorsqu'un homme aura la plaie de la lèpre, on l'amènera au prêtre;
10 Kuhani atamchunguza ili kuona kama kunauvimbe mweupe katika ngozi yake, endapo malaika zitakuwa zimebadilika kuwa nyeupe, au kumekuwa na nyama mbichi kwenye uvimbe.
et le prêtre l'examinera. S'il y a une tuméfaction blanche sur la peau, si le poil est devenu blanc et s'il y a de la chair à vif dans la tuméfaction,
11 Kama ipo, basi, huo ni ugonjwa sugu wa ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga kwa kuwa yeye tayari ni najisi.
c'est une lèpre chronique sur la peau de son corps, et le prêtre le déclarera impur. Il ne l'isolera pas, car il est déjà impur.
12 Iwapo huo ugonjwa unajitokeza na kupanuka zaidi kwenye ngozi, na kuifunika ngozi ya mtu kwa ugonjwa tangu kichwani pake hata miguuni, maadamu anajitokeza kwa kuhani,
« Si la lèpre se déclare sur toute la peau, et si la lèpre couvre toute la peau de la personne infectée, depuis sa tête jusqu'à ses pieds, selon ce qui apparaît au prêtre,
13 naye kuhani atamchunguza ili kuona kama huo ugonjwa umeshaenea mwili wake wote. Ikiwa imetokeo hivyo, kuhani atamtangaza mtu huyo aliye na ugonjwa kuwa ni safi. Ikiwa amebadilika kuwa mweupe, huyo ni safi.
alors le prêtre l'examinera. Voici, si la lèpre a couvert toute sa chair, il le déclarera pur de la plaie. Tout est devenu blanc: il est pur.
14 Lakini ikiwa nyama mbichi imeonekana juu yake, atakuwa najisi.
Mais si de la chair crue apparaît en lui, il sera impur.
15 Kuhani ataiangalia hiyo nyama mbichi na kumtanga kuwa najisi kwa sababu hiyo nyama mbichi ni najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
Le prêtre examinera la chair crue et le déclarera impur: la chair crue est impure. C'est la lèpre.
16 Lakini endapo hiyo nyama mbichi inageuka kuwa nyeupe tena, naye huyo mtu hana budi kwenda kwa kuhani.
Ou bien, si la chair crue se transforme et devient blanche, il se présentera au sacrificateur.
17 Kuhani atamchunguza ili kuona kama hiyo nyama imebadilika kuwa nyeupe. Kama imekuwa hivyo naye kuhani atatangaza kwamba mtu huyo kuwa ni safi.
Le prêtre l'examinera. Si la plaie est devenue blanche, le prêtre le déclarera pur de la plaie. Il est pur.
18 Mtu anapokuwa na jipu juu yangozi yake na limishapona,
« Lorsque le corps a un furoncle sur la peau, qu'il est guéri,
19 na mahali pa jipu pamekuwa na uvimbe au doa lenye kung'aa, wekundu unaochanganyikana na weupe, yapasa kuonyeshwa kwa kuhani.
et qu'à la place du furoncle il y a une tuméfaction blanche, ou une tache brillante, d'un blanc rougeâtre, on le montrera au prêtre.
20 Naye kuhani atalichunguza ili kuona kama linaonekana limekwenda chini ya ngozi, na kama hizo malaika zimebadilika kuwa nyeupe, kama ni hivyo, kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza, endapo utakuwa umezalishwa mahali lilipokuwa jipu hilo.
Le prêtre l'examinera. Si son aspect est plus profond que la peau, et si son poil est devenu blanc, le prêtre le déclarera impur. C'est la plaie de la lèpre. Elle s'est déclarée dans le furoncle.
21 Lakini endapo kuhani atakuwa amelichunguza na haoni malaika nyeupe ndani yake, na kwamba iliko chini ya ngozi bali limefifia, kisha kuhani atamtenga kwa siku saba.
Mais si le prêtre l'examine, et qu'il n'y ait pas de poils blancs, et que la plaie ne soit pas plus profonde que la peau, mais qu'elle soit pâle, le prêtre l'isolera pendant sept jours.
22 Kama linaenea kwa kupanuka kwenye ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
Si elle se propage dans la peau, le prêtre la déclarera impure. C'est une plaie.
23 Lakini kama hilo doa lenye kung'ara linabaki mahali pake na halijasambaa, basi hilo ni kovu la jipu, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
Mais si la tache brillante reste à sa place, et ne s'est pas étendue, c'est la cicatrice de l'ulcère; et le prêtre le déclarera pur.
24 Ngozi inapoungua na nyama mbichi ya inamekuwa na wekundu uliochanganyika na weupe au doa jeupe,
« Ou lorsque le corps a sur la peau une brûlure par le feu, et que la chair crue de la brûlure devient une tache brillante, d'un blanc rougeâtre ou blanc,
25 kisha kuhani ataichunguza kuona kama malaika zilizoko kwenye doa hilo zimebadilika na kuwa nyeupe, na kama limeonekana kwenda chini zaidi ya ngozi, kama limekuwa hivyo, basi huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Umejitokeza kwenye jeraha la moto, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
le prêtre l'examinera; et voici, si le poil de la tache brillante est devenu blanc, et si son aspect est plus profond que la peau, c'est la lèpre. Elle s'est déclarée chez le brûlé, et le prêtre le déclarera impur. C'est la plaie de la lèpre.
26 Lakini endapo kuahani analichunguza na naona kwamba hakuna malaika nyeupe kwenye doa, na kwamba halikuenda chini ya ngozi bali linafifia, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
Mais si le prêtre l'examine, et que voici, il n'y a pas de poil blanc dans la tache brillante, et qu'elle n'est pas plus profonde que la peau, mais qu'elle s'est effacée, alors le prêtre l'isolera sept jours.
27 Kisha yapasa kuahani kumchunguza tena katika siku ya saba. Iwapo litakuwa limesambaa kwa upana kwenye ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugojwa wa kuambukiza.
Le prêtre l'examinera le septième jour. Si la tache s'est étendue sur la peau, le prêtre le déclarera impur. C'est la plaie de la lèpre.
28 Iwapo hilo doa lisalia mahali pake na halitakuwa limesambaa kwenye ngozi bali limefifia, ni uvimbe tu kutokana na kuungua moto, naye kuhani atamtangaza kuwa safi, kwa kuwa siyo zaidi ya jeraha la kuungua.
Si la tache brillante reste à sa place, ne s'est pas étendue dans la peau, mais s'est estompée, c'est l'enflure de la brûlure, et le prêtre le déclarera pur, car c'est la cicatrice de la brûlure.
29 Iwapo mwanaume au mwanamke ana ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni pake,
« Lorsqu'un homme ou une femme aura une plaie sur la tête ou sur la barbe,
30 kisha kuhani atamchunguza mtu huyo kwa ajili ya ugonjwa wa kuambukiza ili kuona kama unakwenda ndani zaidi ya ngozi, na kama kuna nywele za manjano, nyembamba ndani yake. endapo zinaonekana, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni mwasho, ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni.
le prêtre examinera la plaie; et voici, si son aspect est plus profond que la peau, et que les poils qui la composent sont jaunes et fins, le prêtre le déclarera impur. C'est une démangeaison. C'est une lèpre de la tête ou de la barbe.
31 Iwapo kuhani anachunguza ugonjwa wa mwasho na anagundu kuwa hauko chini ya ngozi, na kama hakuna nywele nyeusi ndani yake, kisha kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
Si le prêtre examine la plaie de démangeaison, et que son aspect n'est pas plus profond que la peau, et qu'il n'y a pas de poil noir, alors le prêtre isolera la personne atteinte de démangeaison pendant sept jours.
32 Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena huo ugonjwa ili kuona kama umesambaa, Endapo hakuna malaika za manjano, na iwapo ugonjwa uko usawa ngozi tu,
Le septième jour, le prêtre examinera la plaie; et voici, si la démangeaison ne s'est pas étendue, s'il n'y a pas de poil jaune et si l'aspect de la démangeaison n'est pas plus profond que la peau,
33 basi, yapasa mtu huyo kunyolewa., lakini sehemu yenye ugonjwa haitanyolewa, naye kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
alors il sera rasé, mais il ne rasera pas la démangeaison. Ensuite, le prêtre isolera celui qui a la démangeaison pendant sept jours encore.
34 Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena ugonjwa ili kuona kama umacha kusambaa ndani ya ngozi. Iwapo unaonekana kuwa hukwenda chini zaidi ya ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa safi. Mtu huyo yapasa kufua nguo zake, na kisha atakuwa safi.
Le septième jour, le prêtre examinera la démangeaison; et voici, si la démangeaison ne s'est pas étendue dans la peau, et si son aspect n'est pas plus profond que la peau, alors le prêtre le déclarera pur. Il lavera ses vêtements et sera pur.
35 Lakini ikiwa ugonjwa wa mwasho umeenea kwa sehemu kubwa kwenye ngozi baada ya kuhani kutangaza kuwa alikuwa safi,
Mais si la démangeaison s'étend sur la peau après sa purification,
36 naye kuhani itabidi amchunguze tena. Iwapo ugonjwa utakuwa umesambaa katika ngozi, kuhani hahitajiki kutafuta nywele za manjano. Mtu huyo ni najisi.
le prêtre l'examinera; et voici, si la démangeaison s'est étendue sur la peau, le prêtre ne cherchera pas le poil jaune: il est impur.
37 Lakini iwapo katika mtazamo wa kuhani inaonekana kuwa huo ugonjwa wa mwasho umekoma kusambaa, basi huo ugonjwa umekwisha pona. Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
Mais si, à ses yeux, la démangeaison est arrêtée et qu'un poil noir y a poussé, alors la démangeaison est guérie. Il est pur. Le prêtre le déclarera pur.
38 Iwapo mwanume au mwanamke ana madoa juu ya ngozi,
« Lorsqu'un homme ou une femme aura sur la peau de son corps des taches brillantes, d'un blanc éclatant,
39 kisha kuhani atamchunguza mtu huyo ili kuona kama hayo madoa ni meupe kwa kufiifia, ambalo ni kovu tu lililojitokeza kwenye ngozi. Yeye yu safi.
le prêtre les examinera. Si les taches brillantes sur la peau de leur corps sont d'un blanc terne, c'est une éruption cutanée inoffensive. La peau a éclaté. Il est pur.
40 Iwapo nywele za mtu zimenyonyoka kichwani, yeye ni kipara lakini yu safi.
« Si les cheveux d'un homme sont tombés de sa tête, il est chauve. Il est pur.
41 Na iwapo nywele zake zimenyonyoka upande wa mbele wa kichwa chake, na iwapo paji lake la uso lina kipara, yeye yu safi.
Si ses cheveux sont tombés de la partie antérieure de sa tête, il est chauve du front. Il est pur.
42 Lakini endapo kuna kidonda chenye wekundu uliochanganyika na weupe, juu ya kipara chake au paji lake la uso, huo ni ugonjwa wa kuambukiza uliojitokeza.
Mais s'il y a une plaie d'un blanc rougeâtre dans la tête chauve ou sur le front chauve, c'est la lèpre qui éclate dans sa tête chauve ou sur son front chauve.
43 Naye kuhani atamchunguza ili kuona iwapo uvimbe wa eneo linaugua juu ya upara wake au paji lake la uso lina wekundu uliochanganyika na weupe, kama kuonekana kwa ugonjwa wa kuambukiza kwenye ngozi.
Le prêtre l'examinera. Voici, si l'enflure de la plaie est d'un blanc rougeâtre dans sa tête chauve ou dans son front chauve, comme l'apparence de la lèpre sur la peau du corps,
44 Ikionekana hivyo, basi huyo ana ugonjwa wa kuambukiza naye ni najisi. Hakika kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya ugonjwa wake kichwani pake.
c'est un homme lépreux. Il est impur. Le prêtre le déclarera impur. Sa plaie est sur sa tête.
45 Mtu aliye na ugojwa wa kuambukiza atavaa nguo zilizochanika, ni lazima nywele zake ziachwe wazi, na yampasa kufunika uso wake mpaka puani na kupiga kelele, 'Najisi, najisi.'
« Le lépreux qui a la plaie portera des vêtements déchirés, et les cheveux de sa tête seront détachés. Il se couvrira la lèvre supérieure et criera: 'Impur! Impur!
46 Naye atakuwa najisi siku zote za ugonjwa wake wa kuambukiza. Kwa sababu anao ugonjwa unaosambaa, yapasa kuishi peke yake nje ya kambi.
Pendant tout le temps que durera la plaie, il sera impur. Il est impur. Il habitera seul. Sa demeure sera en dehors du camp.
47 Kuna wakati fulani vazi la mtu hupata ukungu juu yake. Laweza kuwa vazi, ama la sufu au kitani,
Le vêtement dans lequel se trouve la plaie de la lèpre, soit un vêtement de laine ou un vêtement de lin,
48 au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi.
soit un vêtement de chaîne ou de trame, de lin ou de laine, soit un vêtement de cuir ou un objet en cuir,
49 Iwapo sehemu iliyochafuliwa ina rangi ya kijani au nyekundu katika vazi, ngozi, kifaa kilichosukwa au kufumwa, basi huo ni ukungu uanasambaa, ni lazima uonyeshwe kwa kuhani.
si la plaie est verdâtre ou rougeâtre dans le vêtement, dans le cuir, dans la chaîne ou la trame, ou dans un objet en cuir, c'est la plaie de la lèpre; on la montrera au sacrificateur.
50 Yapasa kuhani akichunguze hicho kifaa kwa ajili ya ukungu; ni lazima akitenge kitu chochote kilicho na ukungu kwa siku saba.
Le prêtre examinera la plaie et l'isolera pendant sept jours.
51 Naye atauchunguza tena huo ukungu katika siku ya saba. Endapo utakuwa umesambaa katika kifaa hicho, basi ni wazi kwamba huo ni ukungu wenye kuangamiza, na hicho kifaa ni najisi.
Le septième jour, il examinera la plaie. Si la plaie s'est étendue dans le vêtement, soit dans la chaîne, soit dans la trame, soit dans la peau, quel que soit l'usage auquel la peau est destinée, la plaie est une moisissure destructrice. Il est impur.
52 Na mwenye kukimiliki atalazimika kukichoma na kukiteketeza kabisa hicho kifaa kilichoonekana na ukungu ndani yake, haijalishi kiwe ni kifaa cha aina gani, kwani huo ukungu unaweza kusababisha ugonjwa.
Il brûlera le vêtement, qu'il s'agisse de la chaîne ou de la trame, de laine ou de lin, ou de tout ce qui est en cuir, dans lequel se trouve la plaie, car c'est une moisissure destructrice. Il le brûlera au feu.
53 Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa na kuona kwamba ukungu haujaenea kwenye vazi au chombo kilichosukwa au kusokotwa kutokana na sufu, kitani au ngozi,
« Si le prêtre l'examine et que la plaie ne s'est pas étendue dans le vêtement, ni dans la chaîne, ni dans la trame, ni dans aucune partie de la peau,
54 basi atawaagiza wakisafishe hicho kifaa kilichopatikana na ukungu, naye yampasa kukitenga kwa siku saba zaidi.
le prêtre ordonnera qu'on lave l'objet dans lequel se trouve la plaie, et il l'isolera encore sept jours.
55 Kisha kuhani atakichunguza tena hicho kifaa chenye ukungu baada ya kuwa kimesafinshwa. Kama ukungu haukubadilika rangi yake, hata kama haukusambaa, kifaa hicho ni najisi. Yapasa kichomwe, haijalishi ni wapi ukungu huo utakuwa umekichafua.
Puis le prêtre l'examinera, après que la plaie aura été lavée; et voici, si la plaie n'a pas changé de couleur, et si la plaie ne s'est pas étendue, elle est impure; vous la brûlerez au feu. C'est une tache de moisissure, que la plaie soit en dedans ou en dehors.
56 Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa, na kama ukungu umefifia baada ya kuwa umeoshwa, basi atakirarua kile kipande kilichochaufuliwa kutoka kwenye vazi au kutoka kwenye ngozi, au kutoka kwenye chombo kilichosukwa au kusokotwa.
Si le prêtre regarde, et que la plaie ait pâli après avoir été lavée, il l'arrachera du vêtement, ou de la peau, ou de la chaîne, ou de la trame;
57 Ikiwa ukungu unazidi kuonekana katika vazi, ama katika chombo kilichosukwa au kufumwa, au katika kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi, basi, ukungu utakuwa unasambaa. Kifaa chochote kilicho na ukungu ni lazima kichomwe.
et si elle reparaît dans le vêtement, soit dans la chaîne, soit dans la trame, ou dans quoi que ce soit de peau, elle se propage. Vous brûlerez au feu ce qui contient la plaie.
58 Vazi au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi—iwapo unakisafisha kifaa nao ukungu ukawa umetoka, nacho kifaa lazima kisafishwe mara ya pili, kisha kitakuwa safi.
Le vêtement, soit la chaîne, soit la trame, soit tout ce qui est de peau, que vous laverez, si la plaie en est sortie, vous le laverez une seconde fois, et il sera pur. »
59 Hii ndiyo sheria ihusuyo ukungu katika vazi la sufu au kitani, au kwenye kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au kitu chochote kilichotengenewa kwa ngozi, ili kwamba mweze kuvitangaza kuwa safi au najisi.
Voici la loi concernant la plaie de la moisissure dans un vêtement de laine ou de lin, soit dans la chaîne, soit dans la trame, soit dans tout ce qui est en peau, pour le déclarer pur ou pour le déclarer impur.