< Mambo ya Walawi 13 >
1 Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
And the Lord spoke unto Moses and unto Aaron, saying,
2 Mtu yeyote anayeonekana na uvimbe au pele au doa ling'aalo juu ya ngozi ya mwili wake, na likawa limeambukizwa ugonjwa wa ngozi mwilini mwake, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani mkuu au kwa mmoja wa wanawe makuhani.
If a man shall have in the skin of his flesh a swelling, a rising, or a bright spot, and it might become in the skin of his flesh the plague of leprosy: then shall he be brought unto Aaron the priest, or unto one of his sons the priests.
3 Naye kuhanai atachunguza ugonjwa huo kwenye ngozi ya mwili wake. Iwapo malaika zilizopo eneo lenye ugonjwa zimegeuka kuwa nyeupe, na iwapo ugonjwa umejitokeza juu ya ngozi, huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Baada cha kuhani kumchunguza, atamtangaza kuwa ni najisi.
And if the priest shall see the plague in the skin of the flesh, and the hair in the plague be turned white, and the appearance of the plague be deeper than the skin of his flesh: it is a plague of leprosy; and [so soon as] the priest shall see him, he shall pronounce him unclean.
4 Iwapo lile doa ling'aalo katika ngozi yake ni jeupe, na kuonekana kwake halikwenda chini zaidi ya ngozi, na iwapo malaika za eneo lenye ugonjwa hazijabadilika kuwa nyeupe, naye kuhani atamtenga mgonjwa kwa siku saba.
But if it be a white bright spot in the skin of his flesh, and its appearance be not deeper than the skin, and the hair be not turned white: then shall the priest shut up the plague seven days.
5 Katika siku ya saba, huyo kuhani itambidi kumchunguza tena ili kuona kama katika maamzi yake huo ugonjwa siyo mbaya, na kama haujaenea kwenye ngozi. Iwapo haujaenea, basi, kuhani atamtenga kwa siku saba zaidi.
And the priest shall see him on the seventh day; and, behold, if the plague have remained unchanged in its appearance, the plague have not spread in the skin: then shall the priest shut him up seven days more.
6 Naye kuhani atamchunga tena katika siku ya saba ili kuona kama ugonjwa ubepona na haujasambaa zaidi kwenye ngozi. kama haujasambaa, basi, kuhani atamtangaza kuwa yeye ni safi. Ni upele tu. Naye atafua nguo zake, na kisha yeye yu safi.
And the priest shall see him again on the seventh day; and, behold, if the plague be somewhat pale, and the plague have not spread in the skin: then shall the priest pronounce him clean; it is a rising, and he shall wash his clothes, and be clean.
7 Lakini endapo ule upele utakuwa umishasambaa kwenye ngozi baada ya kuwa amejionyesha kwa kuhani kwa ajili kusafishwa kwake, itambidi kujionyesha tena kwa kuhani.
But if the rising should spread abroad in the skin, after he hath been seen by the priest for his cleansing, he shall be seen again by the priest.
8 Naye kuhani atamchunguza ilikuona kama huo upele umsambaa zaidi ndani ya ngozi. Na endapo utakuwa umesambaa, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
And if the priest see that, behold, the rising have spread abroad in the skin, then shall the priest pronounce him unclean: it is leprosy.
9 Iwapo ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza umo kwa mtu fulani, naye mtu huyo yapasa aletwe kwa kuhan.
If the plague of leprosy happen to be on a man, then shall he be brought unto the priest;
10 Kuhani atamchunguza ili kuona kama kunauvimbe mweupe katika ngozi yake, endapo malaika zitakuwa zimebadilika kuwa nyeupe, au kumekuwa na nyama mbichi kwenye uvimbe.
And the priest shall see, and, behold, if there be a white swelling in the skin, and the hair in it have turned white, or there be a trace of healthy flesh in the swelling:
11 Kama ipo, basi, huo ni ugonjwa sugu wa ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga kwa kuwa yeye tayari ni najisi.
It is an inveterate leprosy in the skin of his flesh, and the priest shall pronounce him unclean; he shall not shut him up, for he is unclean.
12 Iwapo huo ugonjwa unajitokeza na kupanuka zaidi kwenye ngozi, na kuifunika ngozi ya mtu kwa ugonjwa tangu kichwani pake hata miguuni, maadamu anajitokeza kwa kuhani,
And if the leprosy break out abroad in the skin, and the leprosy cover all the skin of [him that hath] the plague from his head even to the feet, so far as the eyes of the priest can see:
13 naye kuhani atamchunguza ili kuona kama huo ugonjwa umeshaenea mwili wake wote. Ikiwa imetokeo hivyo, kuhani atamtangaza mtu huyo aliye na ugonjwa kuwa ni safi. Ikiwa amebadilika kuwa mweupe, huyo ni safi.
If now the priest should see, that, behold, the leprosy have covered all his flesh, he shall pronounce the plague clean; it is all turned white, he is clean.
14 Lakini ikiwa nyama mbichi imeonekana juu yake, atakuwa najisi.
But on the day that healthy flesh appeareth therein, he shall be unclean.
15 Kuhani ataiangalia hiyo nyama mbichi na kumtanga kuwa najisi kwa sababu hiyo nyama mbichi ni najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
And the priest shall see the healthy flesh, and pronounce him to be unclean; the healthy flesh is unclean, it is the leprosy.
16 Lakini endapo hiyo nyama mbichi inageuka kuwa nyeupe tena, naye huyo mtu hana budi kwenda kwa kuhani.
Or if the healthy flesh turn again, and be changed unto white, he shall come unto the priest;
17 Kuhani atamchunguza ili kuona kama hiyo nyama imebadilika kuwa nyeupe. Kama imekuwa hivyo naye kuhani atatangaza kwamba mtu huyo kuwa ni safi.
And if the priest see him, and, behold, the plague be turned into white: then shall the priest pronounce the plague clean, he is clean.
18 Mtu anapokuwa na jipu juu yangozi yake na limishapona,
And if there be a person who hath had in his skin an inflammation, and hath been healed,
19 na mahali pa jipu pamekuwa na uvimbe au doa lenye kung'aa, wekundu unaochanganyikana na weupe, yapasa kuonyeshwa kwa kuhani.
And if there be on the place of the inflammation a white swelling, or a white and dark red bright spot, he shall be shown to the priest;
20 Naye kuhani atalichunguza ili kuona kama linaonekana limekwenda chini ya ngozi, na kama hizo malaika zimebadilika kuwa nyeupe, kama ni hivyo, kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza, endapo utakuwa umezalishwa mahali lilipokuwa jipu hilo.
And if the priest see, and, behold, its appearance be lower than the skin, and the hair thereof have been turned white: then shall the priest pronounce him unclean, it is the plague of leprosy broken out in the inflammation.
21 Lakini endapo kuhani atakuwa amelichunguza na haoni malaika nyeupe ndani yake, na kwamba iliko chini ya ngozi bali limefifia, kisha kuhani atamtenga kwa siku saba.
But if the priest see it, and, behold, there be no white hair therein, and if it be not lower than the skin, and it be pale: then shall the priest shut him up seven days.
22 Kama linaenea kwa kupanuka kwenye ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
And if it now spread abroad in the skin, then shall the priest pronounce him unclean: it is the plague [of leprosy].
23 Lakini kama hilo doa lenye kung'ara linabaki mahali pake na halijasambaa, basi hilo ni kovu la jipu, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
But if the bright spot remain in its place, and spread not, it is a scar of the inflammation; and the priest shall pronounce him clean.
24 Ngozi inapoungua na nyama mbichi ya inamekuwa na wekundu uliochanganyika na weupe au doa jeupe,
Or if there be a person in whose skin there is a place burnt by fire, and the mark of the burning become a bright spot, white and dark red, or white;
25 kisha kuhani ataichunguza kuona kama malaika zilizoko kwenye doa hilo zimebadilika na kuwa nyeupe, na kama limeonekana kwenda chini zaidi ya ngozi, kama limekuwa hivyo, basi huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Umejitokeza kwenye jeraha la moto, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
And if the priest see it, and, behold, the hair in the bright spot have been turned white, and its appearance be deeper than the skin: it is leprosy, broken out in the fire-wound; and the priest shall pronounce him unclean, it is the plague of leprosy.
26 Lakini endapo kuahani analichunguza na naona kwamba hakuna malaika nyeupe kwenye doa, na kwamba halikuenda chini ya ngozi bali linafifia, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
But if the priest see it, and, behold, there be in the bright spot no white hair, and it be not lower than the skin, and it be pale: then shall the priest shut him up seven days.
27 Kisha yapasa kuahani kumchunguza tena katika siku ya saba. Iwapo litakuwa limesambaa kwa upana kwenye ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugojwa wa kuambukiza.
And the priest shall see him on the seventh day: if now it have spread abroad in the skin, then shall the priest pronounce him unclean: it is the plague of leprosy.
28 Iwapo hilo doa lisalia mahali pake na halitakuwa limesambaa kwenye ngozi bali limefifia, ni uvimbe tu kutokana na kuungua moto, naye kuhani atamtangaza kuwa safi, kwa kuwa siyo zaidi ya jeraha la kuungua.
And if the bright spot remain in its place, [and] it have not spread abroad in the skin, and it be pale: it is a swelling of the fire-wound; and the priest shall pronounce him clean; for it is a scar of the fire-wound.
29 Iwapo mwanaume au mwanamke ana ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni pake,
And if there be a man or woman on whom there arise a plague, on the head or on the beard;
30 kisha kuhani atamchunguza mtu huyo kwa ajili ya ugonjwa wa kuambukiza ili kuona kama unakwenda ndani zaidi ya ngozi, na kama kuna nywele za manjano, nyembamba ndani yake. endapo zinaonekana, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni mwasho, ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni.
Then shall the priest see the plague; and, behold, if its appearance be deeper than the skin, and there be in it a yellow thin hair: then shall the priest pronounce him unclean, it is a dry scall, it is the leprosy of the head or of the beard.
31 Iwapo kuhani anachunguza ugonjwa wa mwasho na anagundu kuwa hauko chini ya ngozi, na kama hakuna nywele nyeusi ndani yake, kisha kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
And if the priest see the plague of the scall, and, behold, its appearance be not deeper than the skin, and there be no black hair in it: then shall the priest shut up the plague of the scall seven days.
32 Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena huo ugonjwa ili kuona kama umesambaa, Endapo hakuna malaika za manjano, na iwapo ugonjwa uko usawa ngozi tu,
And the priest shall see the plague on the seventh day; and, behold, if the scall have not spread, and there be in it no yellow hair, and the appearance of the scall be not deeper than the skin:
33 basi, yapasa mtu huyo kunyolewa., lakini sehemu yenye ugonjwa haitanyolewa, naye kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
Then shall he be shaved, but the scall he shall not shave; and the priest shall shut up the scall seven days more.
34 Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena ugonjwa ili kuona kama umacha kusambaa ndani ya ngozi. Iwapo unaonekana kuwa hukwenda chini zaidi ya ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa safi. Mtu huyo yapasa kufua nguo zake, na kisha atakuwa safi.
And the priest shall see the scall on the seventh day; and, behold, if the scall have not spread in the skin, and its appearance be not deeper than the skin: then shall the priest pronounce him clean, and he shall wash his clothes, and be clean.
35 Lakini ikiwa ugonjwa wa mwasho umeenea kwa sehemu kubwa kwenye ngozi baada ya kuhani kutangaza kuwa alikuwa safi,
But if the scall should spread abroad in the skin after his being pronounced clean:
36 naye kuhani itabidi amchunguze tena. Iwapo ugonjwa utakuwa umesambaa katika ngozi, kuhani hahitajiki kutafuta nywele za manjano. Mtu huyo ni najisi.
Then shall the priest see him; and, behold, if the scall have spread in the skin, the priest shall not seek for the yellow hair; he is unclean.
37 Lakini iwapo katika mtazamo wa kuhani inaonekana kuwa huo ugonjwa wa mwasho umekoma kusambaa, basi huo ugonjwa umekwisha pona. Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
But if the scall have remained stationary in its color, and black hair have grown up therein: the scall is then healed, he is clean; and the priest shall pronounce him clean.
38 Iwapo mwanume au mwanamke ana madoa juu ya ngozi,
And if there be a man or a woman having in the skin of their flesh bright spots, white bright spots;
39 kisha kuhani atamchunguza mtu huyo ili kuona kama hayo madoa ni meupe kwa kufiifia, ambalo ni kovu tu lililojitokeza kwenye ngozi. Yeye yu safi.
And if the priest do see, and, behold, there are in the skin of their flesh bright spots, pale and white: it is a freckly eruption grown in the skin; he is clean.
40 Iwapo nywele za mtu zimenyonyoka kichwani, yeye ni kipara lakini yu safi.
And if there be a man whose hair of the head fall off, he is a bald head; he is clean.
41 Na iwapo nywele zake zimenyonyoka upande wa mbele wa kichwa chake, na iwapo paji lake la uso lina kipara, yeye yu safi.
And if from the side of his face his hair fall off, he is forehead-bald; he is clean.
42 Lakini endapo kuna kidonda chenye wekundu uliochanganyika na weupe, juu ya kipara chake au paji lake la uso, huo ni ugonjwa wa kuambukiza uliojitokeza.
But if there be on the bald head, or the bald forehead, an eruption, white and dark red: it is the leprosy sprung up on his bald head, or his bald forehead.
43 Naye kuhani atamchunguza ili kuona iwapo uvimbe wa eneo linaugua juu ya upara wake au paji lake la uso lina wekundu uliochanganyika na weupe, kama kuonekana kwa ugonjwa wa kuambukiza kwenye ngozi.
And the priest shall see him; and, behold, if the swelling of the eruption be white and dark red on his bald head, or on his bald forehead, like the appearance of the leprosy on the [other parts of the] skin of the flesh:
44 Ikionekana hivyo, basi huyo ana ugonjwa wa kuambukiza naye ni najisi. Hakika kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya ugonjwa wake kichwani pake.
He is a leprous man, he is unclean; the priest shall pronounce him unclean; his plague is on his head.
45 Mtu aliye na ugojwa wa kuambukiza atavaa nguo zilizochanika, ni lazima nywele zake ziachwe wazi, na yampasa kufunika uso wake mpaka puani na kupiga kelele, 'Najisi, najisi.'
And the leper on whom the plague is, his clothes shall be rent, and his head shall be bare, and he shall cover himself up to his upper lip, and, Unclean, unclean, shall he call out.
46 Naye atakuwa najisi siku zote za ugonjwa wake wa kuambukiza. Kwa sababu anao ugonjwa unaosambaa, yapasa kuishi peke yake nje ya kambi.
All the days whereon the plague which rendereth unclean is on him, he shall be unclean; alone shall he dwell; without the camp shall his habitation be.
47 Kuna wakati fulani vazi la mtu hupata ukungu juu yake. Laweza kuwa vazi, ama la sufu au kitani,
And if there be a garment on which there arise a plague of leprosy, whether it be on a woollen garment, or on a linen garment;
48 au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi.
Whether it be on the warp, or on the woof; of linen, or of woollen; whether on a skin, or on any thing made of skin;
49 Iwapo sehemu iliyochafuliwa ina rangi ya kijani au nyekundu katika vazi, ngozi, kifaa kilichosukwa au kufumwa, basi huo ni ukungu uanasambaa, ni lazima uonyeshwe kwa kuhani.
And the plague be dark green or dark red, on the garment, or on the skin, or on the warp, or on the woof, or on any article made of skin: it is the plague of leprosy; and it shall be shown unto the priest.
50 Yapasa kuhani akichunguze hicho kifaa kwa ajili ya ukungu; ni lazima akitenge kitu chochote kilicho na ukungu kwa siku saba.
And the priest shall see the plague, and shut up the plague seven days.
51 Naye atauchunguza tena huo ukungu katika siku ya saba. Endapo utakuwa umesambaa katika kifaa hicho, basi ni wazi kwamba huo ni ukungu wenye kuangamiza, na hicho kifaa ni najisi.
And if he see the plague on the seventh day, that the plague have spread in the garment, either in the warp, or in the woof, or in the skin, or in any article that is made of skin: the plague is a corroding leprosy; it is unclean.
52 Na mwenye kukimiliki atalazimika kukichoma na kukiteketeza kabisa hicho kifaa kilichoonekana na ukungu ndani yake, haijalishi kiwe ni kifaa cha aina gani, kwani huo ukungu unaweza kusababisha ugonjwa.
And he shall then burn that garment, whether warp or woof, in woollen or in linen, or any article of skin, whereon the plague is; for it is a corroding leprosy, in fire shall it be burnt.
53 Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa na kuona kwamba ukungu haujaenea kwenye vazi au chombo kilichosukwa au kusokotwa kutokana na sufu, kitani au ngozi,
And if the priest shall see, and, behold, the plague have not spread on the garment, either on the warp, or on the woof, or on any article of skin:
54 basi atawaagiza wakisafishe hicho kifaa kilichopatikana na ukungu, naye yampasa kukitenga kwa siku saba zaidi.
Then shall the priest command that they wash the thing whereon the plague is, and he shall shut it up seven days more.
55 Kisha kuhani atakichunguza tena hicho kifaa chenye ukungu baada ya kuwa kimesafinshwa. Kama ukungu haukubadilika rangi yake, hata kama haukusambaa, kifaa hicho ni najisi. Yapasa kichomwe, haijalishi ni wapi ukungu huo utakuwa umekichafua.
And if the priest see, after the plague hath been washed, and, behold, the plague have not changed its color, and the plague have not spread: it is unclean, in fire shalt thou burn it; it is a decay on its inside or on its outside.
56 Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa, na kama ukungu umefifia baada ya kuwa umeoshwa, basi atakirarua kile kipande kilichochaufuliwa kutoka kwenye vazi au kutoka kwenye ngozi, au kutoka kwenye chombo kilichosukwa au kusokotwa.
And if the priest see, and, behold, the plague have become pale after its having been washed: then shall he tear it out from the garment, or from the skin, or from the warp, or from the woof.
57 Ikiwa ukungu unazidi kuonekana katika vazi, ama katika chombo kilichosukwa au kufumwa, au katika kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi, basi, ukungu utakuwa unasambaa. Kifaa chochote kilicho na ukungu ni lazima kichomwe.
And if it appear again on the garment, either on the warp, or on the woof, or on any instrument of skin: it is a growing plague; with fire shalt thou burn that whereon the plague is.
58 Vazi au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi—iwapo unakisafisha kifaa nao ukungu ukawa umetoka, nacho kifaa lazima kisafishwe mara ya pili, kisha kitakuwa safi.
And the garment, either the warp or the woof, or every instrument of skin, which thou shalt wash, and the plague depart therefrom, shall be washed the second time, when it shall be clean.
59 Hii ndiyo sheria ihusuyo ukungu katika vazi la sufu au kitani, au kwenye kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au kitu chochote kilichotengenewa kwa ngozi, ili kwamba mweze kuvitangaza kuwa safi au najisi.
This is the law of the plague of leprosy on a garment of woollen or linen, either in the warp, or the woof, or any article of skin, to pronounce it clean, or unclean.